Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 117
    1. KVM
      #1
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

      Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

      Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

      Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

      Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Wenger's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 143
      Rep Power : 461
      Likes Received
      20
      Likes Given
      69

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Hiyo biashara Mufindi, Njombe na Makete inalipa sana. Kule Njombe vijijini kwa sasa mti mmoja wa kupasua mbao ukiuza jumla unakwenda kwa bei kati 10,000 mpaka 15,000 kutemegea na size yake na wateja wapo sio wakutafuta wanakufuata wenyewe, sasa ukiwa na miti 100,000 tayari milionea. mwenye nimenunua mashamba huko kwaajili ya kupanda Pines .

    4. #3
      collezione's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd October 2010
      Posts : 347
      Rep Power : 505
      Likes Received
      132
      Likes Given
      3

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      pia kuna mpango wa kimataifa unakuja. Utakuwa unalipwa hela kutokana na idadi ya miti unayotunza...

      This has been started by international organisations, concerning with environment and global warming.

      Nia kubwa ni Ku_promote upandaji na utunzaji wa mazingira. So ukiwa na shamba la miti, utakuwa unalipwa kila mwezi hela kadhaa.

      Mradi umeanza nchi za ulaya na asia. Kwa africa bado. Sina uhakika kwa nn kwa africa, bado haujaja.
      Kivumah and Adharusi like this.

    5. KVM
      #4
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Quote By Wenger
      Hiyo biashara Mufindi, Njombe na Makete inalipa sana. Kule Njombe vijijini kwa sasa mti mmoja wa kupasua mbao ukiuza jumla unakwenda kwa bei kati 10,000 mpaka 15,000 kutemegea na size yake na wateja wapo sio wakutafuta wanakufuata wenyewe, sasa ukiwa na miti 100,000 tayari milionea. mwenye nimenunua mashamba huko kwaajili ya kupanda Pines .
      Kwa mti unaoweza kutoa angalau mbao tatu ndefu za 2" x6" hiyo bei ni ndogo sana ukilinganisha na atakachopata mnunuzi. Ubao mrefu wa 2x6 na uliopakwa dawa DSM una siyo chini ya Shs 17,000. Bei ya mti moja pale Mafinga (Sao Hill) ni zaidi ya Shs. 50 000. Tatizo kule vijijini watu wananunua vimiti vichanga sana.
      Adharusi likes this.

    6. #5
      kakaamiye's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th August 2009
      Posts : 28
      Rep Power : 504
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Ninashukuru sana kwa hii topic, hata mimi nipo interested sana na kupanda miti na ni idea ya muda sasa, issue kwangu ni namna ya kuanza especially kupata shamba kwa ajili ya kupanda. Ningeomba kupata japo idea kama ninaweza kupata eneo huko njombe na kwingineko ukizingatia mimi ninaishi dar. Na price inakuwaje, pia gharama za miche kwa sasa ni kiasi gani na kuotesha plus kutunza. Please please mwenye data ninaomba

    7. Miaka 50

    8. #6
      Kamuzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2008
      Location : Vigwaza
      Posts : 716
      Rep Power : 684
      Likes Received
      122
      Likes Given
      48

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      QUOTE=kakaamiye;3629943]Ninashukuru sana kwa hii topic,hata mimi nipo interested sana na kupanda miti na ni idea ya muda sasa, issuekwangu ni namna ya kuanza especially kupata shamba kwa ajili ya kupanda.Ningeomba kupata japo idea kama ninaweza kupata eneo huko njombe na kwinginekoukizingatia mimi ninaishi dar. Na price inakuwaje, pia gharama za miche kwasasa ni kiasi gani na kuotesha plus kutunza. Please please mwenye dataninaomba[/QUOTE]

      Wasiliana na Malila, ni memba humu, mtafute
      All the best mkuu.


    9. #7
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Enaboishu-Umenyeni
      Posts : 11,929
      Rep Power : 5064
      Likes Received
      3203
      Likes Given
      2661

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Kuna miti inaitwa mitiki,hii vipi kupanda mpaka kuvuna inachukua miaka mingapi? Je hizo pines na eucalyptus nikipanda kwenye heka 10 ninunue miche mingapi? Au unaweza kunisaidia kupanda miche ya hekari kumi?
      Maundumula likes this.

    10. #8
      Kamuzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2008
      Location : Vigwaza
      Posts : 716
      Rep Power : 684
      Likes Received
      122
      Likes Given
      48

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Halafu mkubwa KVM umelete uzi mzuri ila mwaga maujuziyako zaidi kwenye hii habari ya miti ili na wengine tupate nguvu au mwamko,pengine tukatoka kiaina. Mfano miti hiyo uliyoitaja inachukua muda gani kutunzampaka kuvuna, je yaweza kutoa mbao ngapi n.k

    11. KVM
      #9
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Quote By Kamuzu
      Halafu mkubwa KVM umelete uzi mzuri ila mwaga maujuziyako zaidi kwenye hii habari ya miti ili na wengine tupate nguvu au mwamko,pengine tukatoka kiaina. Mfano miti hiyo uliyoitaja inachukua muda gani kutunzampaka kuvuna, je yaweza kutoa mbao ngapi n.k
      Subiri kidogo nitakupa data/hadithi ya upandaji miti.

    12. KVM
      #10
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Quote By Kamuzu
      Halafu mkubwa KVM umelete uzi mzuri ila mwaga maujuziyako zaidi kwenye hii habari ya miti ili na wengine tupate nguvu au mwamko,pengine tukatoka kiaina. Mfano miti hiyo uliyoitaja inachukua muda gani kutunzampaka kuvuna, je yaweza kutoa mbao ngapi n.k
      Kazi ya kupanda miti inachukua muda mrefu kidogo. Hesabia siyo chini ya miaka kumi na mbili hivi
      toka upande ndiyo unaanza kuvuna. Unatakiwa kwenda nayo taratibu. Kila mwaka panda miti kiasi
      fulani ili utakapoanza kuvuna uendelee kuvuna kila mwaka na kupanda ulikovuna.
      Kuhusu gharama za kupanda zinatofautiana kufuatana na kijiji. Kijijini kwangu kwa sasa nadhani ni
      aghali kidogo kwani ni watu wengi wanopanda miti. Muamko umekuwa mkubwa sana. Ni mimi niliwastua
      baada ya kuona kazi niliyokuwa naifanya. Kwa sasa nadhani mche mmoja upo chini ya Sh 100 nakuupanda
      ni Shs 30. Mimi nilianza kwa kununua mche Shs 30 na kupanda Shs 20. Hiyo ilikuwa miaka kumi iliyopita
      lakini leo mti huo naweza kuuza siyo chini ya Shs 10,000 mpaka 20,000.

      Kiasi cha mbao utakazopata inategemea na aina ya miti, matunzo,umri wa mti, na ulipanda
      kwa nafasi gani (distance between trees). Mazungumzo yangu hapa yanahusu zaidi miti aina ya Pines.
      Kwa kawaida tegemea kupata kati ya mbao tano za 2x6 kama ukiharakisha kuvuna lakini mtihuo
      kama umekomaa (miaka 25 hivi) umetunzwa vizuri na ulipandwa kwa nafasi nzuri unaweza kutoa hadi
      mbao 30. Wengi wetu ikifika miaka 12 tunavuna, na kinachopatikana siyo haba lakini nadhani ni
      nzuri zaidi kuvuna kuanzia miaka 15 au 16 hivi kwani utakuwa na uhakika wa kupata pingili siyo
      chini ya mbili na mbao ndefu za 2x6 angalau 6 nakwenda juu . Ubao mmoja wa 2x6 uliopakwa dawa
      hapo DSM unauzwa siyo chini ya Shs 17,000 na kule Mafinga kiwandani bila dawa ni Shs 10,000
      bila kupungua senti tano.

      Maeneo Mazuri za Kupanda Miti

      Miti ninayozungumzia hapa ni Pines, Cypress na Eucalyptus. Miti hii inaota na kustawi vizuri sana
      nyanda za juu kusini. Ukitaka kupanda miti nakushauri uende Njombe halafu kutoka hapo fuata barabara
      nne: Kwenda Makete, Kwenda Ludewa, Kwenda Songea na Kwenda Lupembe. Utakapopita sehemu hizo zote
      utaoona maeneo mazuri sana ya kupanda miti. Kupata eneo unaweza kununua kijijini au kwa wananchi.
      Nakushauri usikubali kukodishiwa. Bei inategemea na eneo. Kuna sehemu upandaji wa miti umeshika kasi
      sana kwa hiyo maeneo hayo ardhi itakuwa aghali kidogo japokuwa ndiyo sehemu nzuri kwani wananchi
      wake watakuwa na uzoefu wa upandaji miti na hutakuwa peke yako kwenye kuhangaika kudhibiti moto.

      Matunzo ya Miti

      Baada ya kupanda unaweza kufyekelea mara moja au mbili mpaka mti ukomae. Pruning nayo unaweza kufanya
      mara mbili. Njia za kuzuia moto (Fire Lines) unatakiwa utengeneze kila mwaka bila kukosa. Kwa vile
      mimi nimepanda eneo kubwa basi niliamua kununua ng'ombe ambao wananisaidia kupunguza majani
      pembezoni mwa shamba.

      Ili uweze kumudu vizuri upandaji wa miti mingi, hasa kama utapanda kila mwaka, na nakushauri upande
      kila mwaka kwa kweli inabidi uajiri kijana, kama siyo mwanzoni basi baada ya miaka kadhaa kupita.
      Yeye ndiye atakayekuwa ndiyo wa kwanza kujua shamba linakabiliwa na matatizo gani na namna ya kuyatatua
      haraka iwezekanavyo. Mimi shamba langu ni kubwa (siyo chini ya ekari 1500) nimeajiri vijana watatu.
      Mmoja wao anaishi ndani ya shamba na ndiye anayetunza ng'ombe. Pamoja na ukubwa wa shamba lakini
      nimelipanda polepole kwa miaka kama kumi hivi.

      Nimeamua kuambatanisha picha chache za mradi wangu nashindwa kuleta nyingi zaidi kwa vile zinatumia muda mrefu mno kuload.
      Attached Thumbnails            
      JokaKuu, Koba, kkiwango and 14 others like this.

    13. #11
      Ameir's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Posts : 83
      Rep Power : 434
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Biashara ya mbao inalipa sana aisee ndungu. Namjua jamaa yangu mmoja anafanya na rafiki yake. Nimeongea nae jana tu aliniambia wanaenda kijijini.

    14. #12
      Narubongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 1,886
      Rep Power : 811
      Likes Received
      842
      Likes Given
      680

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      mkuu safi sana nimeipenda sana project yako pamoja na ng'ombe wazuri wa kienyeji. Karibu sana hapo juu kwenye jukwaa la ujasiriamali kuna nondo za kutosha, NB kuna thread yetu initwa "Kwenu kinaota/kinamea au kustawi kitu gani?" tulijadili pia miti ya mbao karibu kwenye mjadala
      Maundumula and Adharusi like this.
      "Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)

    15. #13
      Pakawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 1,151
      Rep Power : 750
      Likes Received
      168
      Likes Given
      171

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Kilimo Kwanza in the move...nimeipenda sana hii topic. Alijisemea Mwalimu Kilimo ni uti wa mgongo ni kweli kabisa. Shukrani mkuu kwa mada hii
      Hata itakuwa kwa kila mtu atakayeliita jina la bwana atampokea roho wa mungu' 'Niiteni nami nitaitika anasema bwana wa majeshi.'

    16. #14
      Kamuzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2008
      Location : Vigwaza
      Posts : 716
      Rep Power : 684
      Likes Received
      122
      Likes Given
      48

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Mkubwa, umetisha sana kwa kweli. Haya ndiyo mambo tunapaswa kufanya ili kujinasua na pingu za ajira, na kwa wale tunaoanza kuchungulia anga hizo za ujasiriamali basi wewe ni mmoja wa WAALIMU wetu.
      Ahsante sana kwa mchango wako na usiishie hapo, endelea kutoa darasa based on your experience.

    17. #15
      TIQO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 4,615
      Rep Power : 6856
      Likes Received
      1040
      Likes Given
      131

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Mi hii biashara nimeishtukia ila tatizo nikupata maeneo ya kupanda miti maeneo mengi yameshwa panda mi nacho kifanya sasa nanua maeneo kwa wenyeji wanauza pamoja na miti.
      Mwisho wa Ubaya Aibu.

    18. #16
      Red Giant's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 730
      Rep Power : 3611
      Likes Received
      233
      Likes Given
      282

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Quote By King Kong III
      Kuna miti inaitwa mitiki,hii vipi kupanda mpaka kuvuna inachukua miaka mingapi? Je hizo pines na eucalyptus nikipanda kwenye heka 10 ninunue miche mingapi? Au unaweza kunisaidia kupanda miche ya hekari kumi?
      hii mitiki(teak) inachukua muda mrefu sana kuwa na bei nzuri ni ya miaka 15 na kuendelea, ila ukiwa unafanya thining ya shamba unaanza kuuza kuanzia miaka saba, na ina hela mti unaweza fika hadi milioni moja(wanatumia kwa nguzo za umeme ,kujenga meli na fenicha za gharama) , kuhusu mbegu sifahamu ila european union wanafadhili mradi huko kilombero nasikia tayari wana hekta 3000
      King Kong III likes this.
      COAL UNDER PRESSURE BECOMES DIAMOND

    19. #17
      Mopalmo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2010
      Posts : 425
      Rep Power : 518
      Likes Received
      51
      Likes Given
      43

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Aisee hizi taarifa ni za muhimu sana,tuna eneo moshi karibu heka kumi sijajua naweza kupata wapi taarifa za miti itakayochukua muda wa wastani chini ya miaka kumi ili nipande,miti baadhi iliyopo ni cyprus ila naona kama inachukua miaka mingi mno,kama naweza kunisaidia ushauri

    20. KVM
      #18
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Cypresses kwa kawaida zinachukua muda mrefu kidogo. Pines watu wanaweza kuvuna zikiwa na miaka hata kumi lakini kwa kweli ni vizuri kuvumilia kidogo angalau ifikie miaka kama 15 hivi kwani hapo kipato chake kinaweza kuwa maradufu. Sina uhakika na hali ya hewa ya Moshi kama Pines zinastawi vizuri.

    21. KVM
      #19
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 472
      Rep Power : 514
      Likes Received
      178
      Likes Given
      70

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      Ardhi ya kupanda miti kama pines bado ni nyingi sana hasa kwenye karibu ya mkoa wote wa Njombe has kwenye wilaya za Njombe, Ludewa na Makete. Nadhani kuna sehemu za mkoa wa Rukwa na mbeya miti hii hustawi vizuri pia.

      Mimi nawatia moyo nyote ambao mnataka kupanda miti kufanya hivyo. siyo lazima uwe na kipato kikubwa sana. Huu ni mradi mzuri kwa wafanyakazi. Mimi nimepanda miti kutumia mshahara wangu tu. Tunaweza kupishana kipato lakini panda angalau eka 10 au 20 kwa mwaka. Ni gharama ndogo tu. Hata mimi mshahara wangu siyo mkubwa sana lakini kwa uvumilivu sana nimeweza kupanda miti ya kutosha.

      Kazi ya kupanda inafanyika mwezi wa 12 kwa mikoa ya kusini. Ukishapanda huo mti unasubiri miaka ya kustaafu basi unaanza kuvuna. Ni kiunua mgongo kizuri kwa wafanyakazi. Lakini ukiwa kijana bado ni kipato tosha na cha uhakika kwa kila mwaka. Mbao za Tanzania zinauzwa Kenya, Uganda, South Sudan, Somalia na Uarabuni. Kwa sasa hivi mbao za Tanzania hazitoshi kwa hiyo wapasuaji wanakwenda mpaka Malawi kununua miti huko.

      Uzuri mwingine wa kupanda mti ni kuwa unawatia hamasa wenyeji wa eneo utakalopanda miti. Wakati naanza kupanda miti pale kijijini nilikuwa karibu peke yangu tu. Baada ya kuwashauri wanakijiji nao kufanya kile nilichokuwa nafanya nao wakaanza kupanda miti. Leo hii kijiji kimezungukwa na mashamba mengi ya miti ya wanakijiji. Baada ya miaka mitano uchumi wa kile kijiji utapaa sana kwani nitakuwepo kuhakikisha hawalaliwi na walanguzi wa miti.
      Malila, Kivumah and Adharusi like this.

    22. #20
      Wenger's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 143
      Rep Power : 461
      Likes Received
      20
      Likes Given
      69

      Default Re: Biashara ya Upandaji wa Miti Ya Mbao

      KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!
      Maundumula and Adharusi like this.

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...