Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.
Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.
Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.
Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.
Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.
Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.
Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.
Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.
Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Mkuu huu ushauri wako na ulichokifanya nimekipenda na ntatekeleza kwa kukuiga ili kudumisha ushauri wako
Vipi kuhusu soko la mbao dar ? Nachotaka kujua ni kuhusu soko kama ni kubwa
Kwa kweli soko la mbao ni kubwa sana hapa hapa nchini na nje ya nchi. Kwa sasa mbao za Tanzania zinauzwa Kenya, Uganda, Sudan ya Kusini, Somalia hadi uarabuni. Ukitaka kujua ukubwa wa soko hili nenda Morogoro uhesabu malori yanayoleta mbao kutoka nyanda za juu kusini. Mbao nyingine zinatoka mpaka Malawi.
Kwa maoni yangu soko la mbao litazidi kupanuka ingawaje uzalishaji kwa miaka kadhaa ijayo utakuwa chini kutokana na kuisha kwa miti hasa huko vijijini. Hivyo bei itazidi kupanda na siyo kushuka. Mahitaji ya mbao yatazidi kwenda juu kwani wengi siku hizi wanajitahidi kujenga nyumba bora, mpaka huko vijijini. Mbao za asili kama mninga, mvule, n.k haziwezi tena kutumika kwenye kazi za kuezekea majumba kutokana na bei zake kuwa kubwa mno.
Kwa kweli soko la mbao ni kubwa sana hapa hapa nchini na nje ya nchi. Kwa sasa mbao za Tanzania zinauzwa Kenya, Uganda, Sudan ya Kusini, Somalia hadi uarabuni. Ukitaka kujua ukubwa wa soko hili nenda Morogoro uhesabu malori yanayoleta mbao kutoka nyanda za juu kusini. Mbao nyingine zinatoka mpaka Malawi.
Kwa maoni yangu soko la mbao litazidi kupanuka ingawaje uzalishaji kwa miaka kadhaa ijayo utakuwa chini kutokana na kuisha kwa miti hasa huko vijijini. Hivyo bei itazidi kupanda na siyo kushuka. Mahitaji ya mbao yatazidi kwenda juu kwani wengi siku hizi wanajitahidi kujenga nyumba bora, mpaka huko vijijini. Mbao za asili kama mninga, mvule, n.k haziwezi tena kutumika kwenye kazi za kuezekea majumba kutokana na bei zake kuwa kubwa mno.
mkuu mninga unachukua muda gani mpaka kuuvuna? mimi huwa naiona vijijini lakini nikiuliza una umri gani huwa sipati majibu yenye uhakika. Mninga ni utajiri.
Pia niliona kwenye maonesho ya kilimo mwaka fulani.. kuna gereza moja huko kilimanjaro wanatengeneza furniture (nyeupe) nzuri sana kwa kutumia muarobaini.
"Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)
mkuu mninga unachukua muda gani mpaka kuuvuna? mimi huwa naiona vijijini lakini nikiuliza una umri gani huwa sipati majibu yenye uhakika. Mninga ni utajiri.
Pia niliona kwenye maonesho ya kilimo mwaka fulani.. kuna gereza moja huko kilimanjaro wanatengeneza furniture (nyeupe) nzuri sana kwa kutumia muarobaini.
Mninga/Mvule ili uvunwe unahitaji miaka isiyopungua sabini.Kwa hiyo ukipanda wewe atavuna mjukuu wako.
Jamani maeneo ya chalinze -- lugoba ni miti gani inastawi vizuri..........
Maeneo yale ni makame sana,miarobaini inaweza kustawi ila jamii nyingine ni ngumu sana kukua kibiashara. kama unaingia Chalinze ukitokea huku Dar,kuna mitiki upande wa kushoto,ipo na haiongezeki kimo wala unene. Sijui Msederela kama unaweza kumea na kukua kibiashara.
Maeneo yale ni makame sana,miarobaini inaweza kustawi ila jamii nyingine ni ngumu sana kukua kibiashara. kama unaingia Chalinze ukitokea huku Dar,kuna mitiki upande wa kushoto,ipo na haiongezeki kimo wala unene. Sijui Msederela kama unaweza kumea na kukua kibiashara.
Hivi miarobaini inafaa kwa mbao? Mbona kama vile huwa haikui sana kwenda juu?
Hivi miarobaini inafaa kwa mbao? Mbona kama vile huwa haikui sana kwenda juu?
Miarobaini inatoa mbao nzuri sana. Sasa kama mnazi unachongwa mbao, itakuwa muarobaini. Waulize mafundi fenicha mjini Dar wakuambie miguu ya makochi na vitanda iliyobora kabisa wanachonga mti gani.
KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!
Wenger...!!! Nadhani wewe tunaweza kwenda pamoja jamaa yangu, Ebana unaweza kunidokeza kidogo acre moja maeneo ya huko inauzwaje...???/
Mninga/Mvule ili uvunwe unahitaji miaka isiyopungua sabini.Kwa hiyo ukipanda wewe atavuna mjukuu wako.
miaka 70! sipo tayari kwa hili. Ngoja niendelee kufanya utaratibu wa kumiliki ardhi kisheria maana hizi projects za muda mrefu ni lazima uwashirikishe watu wa ardhi kikamilifu kabla ya kuanza kupanda miti. Tuliangalie kwa umakini hili swala, watu wengi wamepoteza ardhi kwa kutofuata taratibu za umiliki
miaka 70! sipo tayari kwa hili. Ngoja niendelee kufanya utaratibu wa kumiliki ardhi kisheria maana hizi projects za muda mrefu ni lazima uwashirikishe watu wa ardhi kikamilifu kabla ya kuanza kupanda miti. Tuliangalie kwa umakini hili swala, watu wengi wamepoteza ardhi kwa kutofuata taratibu za umiliki
well said mkuu, hivi ule utaratibu wa hati za kimila uliishia wapi? nasikia ilikuwa 20,000 tu , au hauwahusu wanunuzi wa ardhi yaani mpaka uwe umerithi?
Nichangie kwa kuleta nyongeza za hapa na pale ili kujazia mjadala wetu. Maeneo ya kupanda miti yaliyosahaulika ni Kilolo, Mfindi,Mby vijijini, Makonde plateau.
Tumetaja sana pines, cyprus, teak,eucalyptus, tumesahau acrocarpus kwa ukanda wa baridi na Msederela kwa kanda za joto kiasi.
Hatujazungumzia mbegu, mbegu bora za Pines kwa sasa ni Tatizo sugu.Tangu mwaka jana kituo cha Iringa wameshindwa kuzalisha, kwa hiyo pines/cyprus zinaandaliwa kienyeji na vijana huko vijijini.Kwa sasa pines za uhakika zinapatikana Nairobi, ila bei imesimama.
Mwaka jana tulipata taabu sana ya tubes, ila mwaka huu walau zipo pale TFA Iringa, bei iko juu. Ukiwa na usafiri wako, ni bora kununua Dar ukasafirisha. Dar ni Tsh 5000/ kwa kilo na TFA Iringa ni 6500/ kwa kilo.
Ili kupunguza gharama za kitalu, watika miche mapema, miezi mitano kabla ya msimu wa kupanda haujafika.
Kama unataka ardhi kubwa,Makete usiende, ni kazi ngumu kupata eka 50 za pamoja zinazofikiwa na miundo mbinu. Utapanda milimani ambako utashindwa kuvuna. Na maeneo mazuri yaliyobaki bei iko juu. Ludewa/Wino/Lupembe/Mfindi kusini huko bei poa.Kilolo bei inaanza kupanda.
Kwa wale wanaonunua miti na ardhi, wawe waangalifu, vijijini unaweza kuta miti ni mtu mwingine na ardhi ni ya mtu mwingine.
Asante, tuendelee kukata issue.
Kiongozi unaonekana unafahamu mengi juu ya miti hapo aithee, NAOMBA KUJOIN naamini nitafamu mengi nitakapopata mawasiliano yako... Email yangu ni [email protected]
Kiongozi unaonekana unafahamu mengi juu ya miti hapo aithee, NAOMBA KUJOIN naamini nitafamu mengi nitakapopata mawasiliano yako... Email yangu ni wag[email protected]
well said mkuu, hivi ule utaratibu wa hati za kimila uliishia wapi? nasikia ilikuwa 20,000 tu , au hauwahusu wanunuzi wa ardhi yaani mpaka uwe umerithi?
Utaratibu ule bado upo na kuna maeneo wanaendelea kugawa hata sasa. Sehemu zingine hakuna kinachoendelea kwa sababu ya ulegelege wa serikali za maeneo hayo.
OOh!!! Mkuu hilo tu? mi nipo huku Iringa. kuhusu shamba la miti ya mbao hususani pine naweza kukusaidia kwa kukuunganisha na kikundi kimoja kinacho jihusisha na uhamasishaji wa upandaji miti hasa mipaine: Yaani wao watakutafutia shamba, watapanda, na kukumilikisha chinni ya serikali ya kijiji na utakabidhiwa hati ya umiliki wa shamba hilo. Na jumla ya gharama zote ni SH;250000 Kwa eka moja.Pia kipo kikundi kingine ambacho unaweza kuingia mkataba juu ya utunzaji wa miti yako hasa issue ya moto na mambo mengine ambayo ni hatarishi kwa ustawi na ukuaji wa miti yako. hii ni serious issue kama upo Interested ninyongee kupitia 0768953122 or via [email protected];Japo mi ni mdau mpya so nimeipenda sana topic ya kimaendeleo zaidi.
KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!
Nipo Iringa kama utakuwa tayari naomba tuwasiliane. Nina ekari 20 Kidabaga - Kilolo naona hazitoshi na huku bei kwa ekari moja imepanda sana. Nahitaji shamba huko Njombe.
Nipo Iringa kama utakuwa tayari naomba tuwasiliane. Nina ekari 20 Kidabaga - Kilolo naona hazitoshi na huku bei kwa ekari moja imepanda sana. Nahitaji shamba huko Njombe.
Kidabaga vijiji gani mkuu? Uko karibu na hawa New Forest kule Magome au Ng`ang`ange? Maeneo hayo bei iko juu sana sababu ya hawa NF. Jaribu kwenda Ng`ingula au Masisiwe, kule bado ardhi ipo, ila Lupilo bei iko juu sana.
Kidabaga vijiji gani mkuu? Uko karibu na hawa New Forest kule Magome au Ng`ang`ange? Maeneo hayo bei iko juu sana sababu ya hawa NF. Jaribu kwenda Ng`ingula au Masisiwe, kule bado ardhi ipo, ila Lupilo bei iko juu sana.
Njombe mambo bado hayajaharibika sana. Wahi wahi.
Ni katika vijiji vya Idete maeneo ya hao New Forest lakini kwa mbele.
KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!
Follow Us Here