Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Unataka kuwa tajiri?

    Report Post
    Page 5 of 7 FirstFirst ... 34567 LastLast
    Results 81 to 100 of 137
    1. #1
      GAZETI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2011
      Location : ILALA
      Posts : 1,621
      Rep Power : 1302
      Likes Received
      644
      Likes Given
      1173

      Default Mwongozo kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji

      Pengine umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Yako mambo mengi ya kufanya mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.Viko vitabu vingi na tena siku hizi zinatolewa DVD za jinsi ya kufanikiwa katika maisha. Utashangaa mpaka unamaliza kusoma au kutazama DVD hizo hujapata njia ya wazi sana sana utajilaumu tu kwa kuendelea kupoteza fedha kwa kuchangia miradi ya wajanja hao. Wengine wanakuambia "amini tu kuwa wewe ni tajiri na utafanikiwa" mh! INAWEZEKANA? Afadhali hao, balaa zaidi ni wale ambao wanayanadi mafanikikio na utajiri kwa mizizi, hirizi na hata roho za binadamu wenzao!

      Somo langu ni dogo lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana. Sasas kuwa makini zaidi. Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo. Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4 . Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri. Wale vifaranga tunakadiria kuwa makoo(majike) watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga. Utakuwa na kuku 200 + 25 =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700. Ndugu mwanajamvi hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku 1,000. Mwaka 2. 750(majike) x 10 = 7500 (uza wengine) 3000 x 10 = 30,000. Kutegemea na uwezo wako mpaka mwisho wa mwaka wa pili utakuwa umefanikiwa sana. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi huku ukiacha kando uzushi wa vitabu vya wasanii na DVD zao pia. NB. Kumbuka kuku ninao wazungumzia hapa ni wale wa kawaida sio wale mataahira (wa kisasa).Fuatilia zaidi kuhusu matibabu na matunzo mengineyo.

      MAELEZO ZAIDI
      UFUGAJI BORA WA KUKU WA KIENYEJI



      SEHEMU YA KWANZA

      UTANGULIZI

      Napenda kumshukuru mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kwa namna moja au nyingine kutoa mchango wangu kwa mtindo huu. Huu ni kama mwongozo tu wa nini utakabiliana nacho au unatakiwa kufanya katika zoezi zima la ufugaji wa kuku wa kienyeji. Nimeamua kuuleta kwenu wana JF ili kwa mtu mwenye malengo ya kufanikiwa kupitia ufugaji wa kuku ajue mlolongo mzima na changamoto ambazo atakabiliana nazo.

      A.KWA NINI KUKU WA KIENYEJI?

      1. Wastahimilivu wa magonjwa lakini ni muhimu wakikingwa na magonjwa ya kuku kama mdondo, ndui ya kuku n.k ili kuweza kuwaendeleza.
      2. Wana uwezo wa kujitafutia chakula ardhini.
      3. Wana uwezo wa kuatamia mayai, kutotoa na kulea vifaranga na ustahimilivu wa mazingira magumu kama ukame, baridi n.k
      4.Nyama na mayai yake vina ladha nzuri kuliko kuku wa kisasa.(PATA SUPU YA KUKU WA KIENYEJI ILI UTHIBITISHE)
      5. Wana uwezo wa kujilinda na maadui kama mwewe n.k . Pamoja na sifa hizi ni muhimu muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri, wakawekwa kwenye mabanda mazuri, wakapewa maji na chakula cha kutosha.

      B.FAIDA ZA KUKU WA KIENYEJI.

      Faida ni nyingi na zinafahamika lakini nitaeleza zile ambazo kwa wengine huenda zikawa ni ngeni kwao.
      - Mayai huweza kutumika kwa tiba. (Pata maelezo jinsi yai la kuku wa kienyeji linavyoweza kutumika kwa tiba kutoka kwa wataalam wa tiba mbadala)
      - Kiini cha njano cha yai kinaweza kutumika kutengenezea mafuta ya nywele (shampoo)
      - Manyoya yake yanaweza kutumika kama mapambo.
      Fuga kuku upate faida kwa kuzingatia:
      Chanjo ya mdondo kila baada ya miezi mitatu na chanjo ya ndui mara mbili kwa mwaka
      Zuia viroboto, utitiri na minyoo.
      Chagua mayai bora kwa ajili ya kuatamiza
      Panga kuuza kuku kwa makundi uongeze kipato
      Kula mayai na kuku kadri uzalishaji unavyoongezeka.
      Kipato unachokipata utenge pia na kiasi kwa ajili ya uendelezaji wa kuku

      C:MAPUNGUFU

      Yako mapungufu mengi yanayofahamika lakini hapa naomba niweke lile la muhimu zaidi. MAGONJWA kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku kutokana na kutokuzingatia kuchanja kuku kwa wakati.


      D: KABILA ZA KUKU WA KIENYEJI

      Kuna maelezo ya kusisimua sana kuhusu makabila ya kuku wa kienyeji, hata hivyo kuna ugumu kidogo kuweza kuyachanganua makabila hayo kutokana na muingiliano mkubwa wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Hata hivyo kuku hawa wana tofauti za kimaumbile zinazosaidia kwa kiasi fulani kutambua uwepo wa baadhi ya makabila ya kuku. Kabila hizi pia zinahusishwa kwa kiasi kikubwa na eneo kuku wanakotoka. Baadhi ya kuku wa kienyeji wanaweza kutambuliwa kwa maumbile yao Mfano:
      a. Kishingo - kuku wasio na manyoya shingoni
      b. Njachama au Nungunungu - Hawa ni wale wenye manyoya yaliyosimama.
      c. Kibwenzi - Ni wale wenye manyoya mengi kichwani.
      d. Kibutu- Hawa hawana manyoya mkiani
      Mwingiliano wa vizazi unaweza ukasababisha kuku kuwa na aina ya maumbile mchanganyiko. Mfano kuku aina ya kuchi anaweza kuwa na alama ya kishingo, Njachama, Kibwenzi au Kibutu.
      Hivyo kabila za kuku zifuatazo zinaweza kutambuliwa kama ndiyo kabila za kuku wa kienyeji kulingana na maumbile yao na maeneo wanakotoka.

      (i) KUCHI

      Ni kuku warefu kwa umbo na wenye kusimama mgongo ukiwa wima. Wana manyoya machache mwilinini na hasa kifuani, vilemba vyao ni vidogo. Majogoo huwa na wastani wa uzito wa Kg. 2.5 na mitetea kg 1.5 mayai ya kuchi yana uzito wa wastani wa gm 45. Kuku hawa hupatikana kwa wingi maeneo ya Mwanza, Shinyanga, Tabora na Zanzibar.

      (ii) CHING'WEKWE

      Kuku hawa ambao jina lao ni gumu kidogo kwa mtu asiyekuwa na meno kulitamka wana sifa zifuatazo.
      Majogoo wana wastani wa kg 1.6, Mitetea wastani kg 1.2, mayai wastani wa gm 37. Kuku hawa wenye umbo dogo hupatikana zaidi maeneo ya CHAKWALE mkoani Morogoro na pia sehemu za umasaini. Kuku hawa hutaga mayai mengi sana kuliko aina nyingine ya kuku wa kienyeji waliopo Tanzania, kwa hiyo wanafaa sana kwa biashara ya mayai.

      (iii)UMBO LA KATI

      Majogoo wana uzito wa wastani wa kg. 1.9, Mitetea kg. 1.1, Kuku hawa ndio hasa wanaoitwa wa kienyeji(wa kawaida) Wana rangi tofauti. Utafiti umeonyesha kuwa kuku hawa hukua upesi na hupata kinga upesi baada ya kuwachanja dhidi ya ugonjwa wa mdondo (Castle desease)
      Muhimu - Mfugaji akifanya uchaguzi kutoka kwenye aina hii ya kuku na kutoa matunzo mazuri kwa hao kuku waliochaguliwa, Hakika anaweza kupata kuku walio bora na wenye uzito wa kutosha pia kutaga mayai mengi na makubwa.

      (iv) SINGAMAGAZI

      Ni aina ya kuku wakubwa wa kienyeji wanaopatikana zaidi TABORA, kuku hawa wana utambulisho maalum kutokana na rangi zao. Majogoo huwa na rangi ya moto na mitetea huwa na rangi ya nyuki. Uzito - Majogoo uzito wa wastani wa kg 2.9, mitetea wastani wa kilo 2 mayai gramu 56.

      (iiv) MBEYA

      Kuku hawa wanapatikana Ileje mkoani mbeya. Asili hasa ya kuku hawa ni kutoka nchi ya jirani ya Malawi na si wa kienyeji asilia bali wana damu ya kuku wa Kizungu "Black Australop". Majogoo Kg 3 mitetea kg 2 mayai gram 49

      (iiiv)PEMBA

      Hupatikana zaidi Pemba. Majogoo Kg.1.5 Mitetea Kg 1 mayai wastani gm 42

      (xi) UNGUJA.

      Majogoo Kg 1.6,mitetea kg 1.2 mayai gm 42. Kuku hawa wa Unguja na Pemba wanashabihiana sana na Kuchi isipokuwa hawa ni wadogo.


      SEHEMU YA PILI

      1. MIFUMO YA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI.

      A. MFUMO HURIA
      Katika mfumo huu kuku huachiwa wakitembea toka asubuhi wakijitafutia chakula na maji na kufungiwa kwenye vibanda visivyo rasmi wakati wa usiku. Huu ni mfumo rahisi lakini si nzuri kwa mfugaji wa kuku wengi kwani atahitaji eneo kubwa la ardhi.

      FAIDA.
      Mfumo huu una faida za gharama ndogo za uendeshaji kiujumla.

      HASARA
      Uwezekano mkubwa wa kuku kuliwa na vicheche, kuibiwa mitaani n.k
      Kuku huweza kutaga popote na kusababisha upotevu mkubwa wa mayai.
      Ni rahisi kuku kuambukizwa magonjwa
      Utagaji unakuwa si nzuri kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa.
      Uwekaji kumbukumbu si nzuri.
      Ni vigumu kugundua kuku wagonjwa hivyo kusababisha ugumu katika utoaji wa tiba.

      UTUMIAJI NZURI WA MFUMO HUU
      Kuku wajengewe banda kwa ajili ya kulala nyakati za usiku na liwasaidie wakati mwingine wowote hali ya hewa inapokuwa si nzuri.
      Kuku wapatiwe chakula cha ziada na maji.
      Kuku waandaliwe kwa viota vya kutagia.
      Kuku 100 ni vizuri wakitumia eneo la ardhi la ekari 1.


      B.MFUMO NUSU HURIA
      Huu ni mfumo ambao kuku hujengewa banda rasmi na banda hilo huzungushiwa uzio/ wigo. Mfumo huu ni ghari kiasi ukilinganisha na mfumo huria lakini huweza kumpatia mfugaji faida haraka sana.

      FAIDA
      Sehemu ndogo ya kufugia hutumika kuliko ufugaji huria, utunzaji wa kuku ni rahisi ukilinganisha na mfumo huria, Ni rahisi kutibu magonjwa ya mlipuka kama mdondo (Newcastle desease), Upotevu wa kuku na mayai ni mdogo sana ukilinganisha na mfumo huria.


      C. MFUMO WA NDANI
      Kuku hujengewa banda rasmi na hufugwa wakiwa ndani. Mfumo huu kuku huwekwa kwenye mabanda ambayo sakafu hufunikwa kwa matandiko ya makapi ya mpunga, takataka za mbao(randa), maganda ya karanga au majani makavu yaliyokatwa katwa.

      FAIDA
      Mfumo huu unahitaji eneo dogo la kufugia, uangalizi mzuri na rahisi wa kuku, Joto litokanalo na matandiko lina uwezo wa kuua vimelea vya maradhi, kuku wanakingwa na hali ya hewa mbaya na maadui wengine.

      HASARA
      Uwezekano wa kuku kudonoana ni mkubw na pia Gharama za ujenzi wa mabanda

      UTUMIAJI MZURI WA MFUMO HUU.
      1. Matandiko yageuzwe kila siku
      2. Kila mara matandiko yawe makavu kwa kuwa na madirisha yanayopitisha hewa ya kutosha, ambayo yatatoa unyevunyevu hewa chafu ikiwemo ammonia.
      4. Mita mraba moja hutosha kuku 5 hadi 8.



      UTATUZI WA KUKABILIANA NA VIKWAZO KATIKA UFUGAJI.
      Mambo ya kuzingatia:

      Mabanda bora - Fuatilia kwa wataalamu wa mifugo walio karibu nawe.
      Sifa za banda bora (Waone wataalam wa mifugo)
      Kuchagua kuku wa kuendeleza kizazi
      Kuwa makini na aina ya mitetea na majogoo unatakiwa kuchagua ili kuwa na kizazi bora.


      UTAGAJI WA MAYAI
      Kwa kawaida kuku huanza kutetea(Kutoa mlio wa ishara ya kutaga) anapofikisha miezi sita hadi minane. Hivyo ni vyema viota viandaliwe mapema wakiwa na umri wa miezi mitano. Kuku anapoanza kutaga akifikisha mayai matatu mfugaji anashauriwa kuondoa kila yai linalozidi hayo matatu kila siku linapotagwa na kuliweka alama ya tarehe au namba kwa kutumia penseli ili kumfanya kuku aendelee kutaga kwa lengo la kufikisha mayai 15 mpaka 20. Mayai yanayoondolewa yawekwe kwenye chombo kikavu kinachopitisha hewa ni vizuri pia kuweka mchanga ndani ya chombo hicho.

      Hakikisha ya fuatayo.
      Sehemu iliyochongoka iwe chini na pana iwe juu.
      Hifadhi sehemu yenye hewa ya kutosha na isiyohifadhi joto
      Mayai yasikae kwenye hifadhi hiyo zaidi ya wiki mbili toka siku ya kuanza kutagwa.

      UATAMIAJI WA MAYAI NA UANGUAJI WA VIFARANGA
      Uatamiaji na uanguaji wa kubuni - Mfumo huu hutumia mashine za kutotoleshea vifaranga (Incubators) hutumika kuangua mayai mengi kati ya 50 hadi 500 kwa wakati mmoja Mashine zinazotumika kutotoleshea vifaranga wa kisasa zinaweza kutumika pia kutotoleshea wa kienyeji.
      Uatamiaji na uanguaji wa asili

      KUCHAGUA MAYAI YA KUANGUA.
      Hili nalo ni muhimu kuzingatia. Ni vizuri kuchagua mayai ya kuatamia ili mayai yasiyofaa yaweze kuuzwa au kutumiwa nyumbani kwa chakula. Mayai ya kuatamia yawe na sifa zifuatazo
      Yasiwe na uchafu yawe masafi
      Yasiwe na nyufa
      Yatokane na kuku aliyepandwa na jogoo
      Yasiwe madogo wala makubwa bali yawe na ukubwa wa wastani kulingana na umbile la kuku.
      Yasiwe mviringo kama mpira pia yasiwe na ncha kali sana.
      Yasiwe yamekaa muda mrefu zaidi ya wiki mbili toka yalipotagwa
      Yasiwe yaliyohifadhiwa kwenye sehemu yenye joto.

      KUMTAYARISHA KUKU WA KUATAMIA
      Pamoja na matayarisho hayo zingatia kumuwekea mayai yasiyozidi 15 pia ni vizuri yasipungue 12. Kuku wanaotazamiwa kuatamia ni lazima wachunguzwe kwa makini kabla ya kuatamia ili kuhakikisha kwamba hawana chawa, utitiri n.k. Kuwepo kwa wadudu hao huwafanya kuku wakose raha na kutotulia kwenye viota vyao. Hali hii husababisha kuanguliwa kwa Vifaranga wachache.
      Sasa unatakiwa kufanya yafuatayo:-
      Nyunyiza dawa ya kuua wadudu ndani ya kiota
      Pia mnyunyuzie dawa kuku anayetarajia kuatamia
      Weka mayai kwenye kiota huku mikono yako ikiwa imepakwa jivu ili kuepuka kuwa na harufu kwani kuku anaweza kuyasusa.

      Ni vizuri kuifanya kazi hii ya kumuandaa kuku anayetaka kuatamia wakati wa usiku. Pia ifahamike kuwa kwa kawaida kuku huatamia mayai yake siku 21.

      PIA JIFUNZE MBINU ZA KUATAMIA MAYAI MENGI KWA NJIA ZA ASILI
      Iwapo una kuku wengi wanaotaga kwa wakati mmoja ni vema ukawafanya wakaatamia na kutotoa pamoja.
      Unachotakiwa kufanya ni kuchagua mayai ya kuatamia ukianzia na yai la mwisho kutaga.
      Unaweza kuwaandaa kuku wako zaidi ya mmoja ili waanze kuatamia kwa pamoja na kupata vifaranga vingi kwa mara moja kuku wa kwanza anapoanza kuatamia. Mwekee mayai viza au ya kuku wa kisasa kwani kuku huatamia hadi mayai yanapoanguliwa hivyo ukimuwekea mayai yasiyo na mbegu atakaa hapo muda mrefu hadi vifaranga watoke.

      UTEKELEZAJI WAKE
      Kuku anapotaga kila siku weka alama ya namba au tarehe kulinganisha na siku anayotaga
      Yanapofika mayai matatu yaondoe na muwekee mayai viza au ya kisasa huku ukiendelea kuweka alama mayai yanayotagwa kila siku.
      Mara kuku anapoanza kuatamia muongezee mayai ya uongo yafikie 8 hadi 10
      Fanya hivyo kwa kila kuku anayetaga hadi utakapoweza kupata idadi itakayoweza kukupatia vifaranga wengi kwa wakati mmoja.
      Wawekee kuku wote mayai siku moja kwa kuondoa mayai ya uongo na kuwawekea mayai ya ukweli wakati wa usiku.

      MUHIMU
      Mayai ya kuatamia yasishikwe kwa mkono ulio wazi na wala yasipate harufu za mafuta ya taa, manukato n.k.

      JIFUNZE PIA KUTAMBUA MAYAI YALIYO NA MBEGU NA YALE YASUYO NA MBEGU.
      Mfugaji anaweza kutambua mayai yaliyo na mbegu na yale yasiyo na mbegu siku ya saba baada ya kuanza kuatamia iwapo atapima mayai kwa kutumia box lililotengenezwa maalum pamoja na tochi yenye mwanga mkali ndani ya chumba chenye kiza. Hii itamuwezesha mfugaji ayatumie mayai yasiyo na mbegu kwa chakula cha familia au kuyauza.

      TAMBUA VYAKULA NA UZALISHAJI WA KUKU - Sitalielezea hili naomba ufuatilie mwenyewe.

      JIFUNZE MBINU ZA KUZALISHA KUKU WENGI KWA MUDA MFUPI
      Zoezi hili linawezekana iwapo uleaji wa vifaranga kwa njia ya kubuni utatumika. Kuku mmoja anaweza kutotoa zaidi ya mara saba kwa mwaka.
      Taz.
      Hesabu ya uzalishaji wa kuku wengi kwa mwaka kwa kutumia mtetea mmoja tu.
      Mpaka mwisho wa mwaka unaweza kuwa na idadi ya vifaranga 252 kwa kadirio la vifaranga 8 kila mzao. Hivyo kama una kuku 10 wanaotunzwa vizuri utakuwa umezalisha jumla ya vifaranga 2520.

      Fuatilia kwa wataalamu wa mifugo ili ufundishwe zaidi kuhusu mbinu hiyo ya kuzalisha kuku wengi.

      ULEAJI WA VIFARANGA
      NJIA YA KUBUNI
      NJIA YA ASILI
      Njia zote mbili zinafahamika kama huzifahamu tafadhali fuatilia kwa mtaalamu aliye karibu nawe.


      MAGONJWA NA WADUDU WANAOSHAMBULIA KUKU WA KIENYEJI NA JINSI YA KUKINGA.

      A. MAGONJWA.
      Ugonjwa hatari - Mdondo/ Kideri (Newcastle desease) Hapo nyuma dawa ya kukinga ugonjwa huu ilikuwepo lakini ilikuwa inahitaji kuhifadhiwa kwenye hali ya ubaridi (Friji) Hali hiyo ilisababisha iwe ngumu kutumika vijijini kwa dawa hiyo. Hivi sasa kumepatikana chanjoa ambayo inastahimili joto ambayo inaweza kutumika hata vijijini.

      Pamoja na mdondo yapo pia magonjwa yanayoshambulia kuku hapa nchini

      Ndui ya kuku(Fowl pox)
      Mafua ya kuku(Infectious coryza)
      Homa ya matumbo (Cocciodiosis)
      Minyoo na wadudu kama viroboto, chawa, utitiri na kupe wa kuku.

      DALILI ZA KUKU MGONJWA.

      Huzubaa
      Hali chakula/maji vizuri
      Hujitenga na wenzake
      Hujikunyata au kuinama
      Hutetemeka
      Hutembea kwa shida
      Utagaji wa mayai hupungua au hukoma kabisa


      MAGONJWA YA KUKU HUSABABISHWA NA NINI?
      Yako mambo mengi yanayosababisha lakini matunzo hafifu pia huchangia.

      ATHARI ZA MAGONJWA.
      Hili liko wazi

      Maelezo haya ya magonjwa ni mengi hivyo tuwe wafuatiliaji kwa wataalam.



      MATIBABU

      KIDERI - Sifahamu tiba ya kitaalam ya ugonjwa huu kama kuna ambaye anafahamu tunaomba atufahamishe lakini ziko dawa za asili na za kitaalam ambazo zinafaa zaidi kwa chanjo.
      Ugonjwa huu unaweza kuukinga kwa kuwapa kuku chanjo ya Mdondo. Pia usichanganye kuku wako na kuku ambao huna taarifa zao za chanjo.

      KUMBUKA
      Mdondo au kideri ni ugonjwa tishio ambao huweza kuua kuku wote
      Mdondo ukitokea vifo huwa vingi pia kuku hupumua kwa taabu, hupooza na wengine huzunguka na huzungusha vichwa.
      Mdondo unaweza kuzuilika kwa chanjo kila baada ya miezi 3

      NDUI YA KUKU
      HOMA YA MATUMBO (Fowly typhoid)
      MAFUA YA KUKU(Infectious coryzya)
      KUHARISHA DAMU(Coccidiosis)
      Minyoo na wadudu wanaoshambulia kuku kama viroboto n.k

      Kwa magonjwa na wadudu tuliowataja hapo juu please wasiliana na mtaalamu wa mifugo aliye karibu nawe Kwani siwezi kueleza kila kitu hapa wataalamu tunao naamini watatusaidia.

      TIBA ZA ASILI
      Kuna madawa ya asili ambayo hutokana na mimea ambayo hukinga kuku.

      BAADHI YA MIMEA INAYOTIBU NA KUKINGA MARADHI YA KUKU.

      MWAROBAINI - Typhoid, kuhara, kideri, kifua na vidonda
      ALOEVERA - Typhoid, kuhara, kideri, kifua na vidonda,ngozi na Cholera. Tutaelekezana zaidi namna ya kuandaa dawa hii.

      Hapa nataka niorodheshe baadhi ya madawa ya asili ambayo yanasaidia kutibu na kukinga kuku.
      Mwarobaini, Aloevera, Mtakalang'onyo(Euphorbia),Mbar ika, mlonge, Ndulele/dungurusi/tura/ndura, Majani ya mpapai, Mwembe, Minyaa na Pilipili kichaa.

      NAWASHUKURU PIA NAOMBA MWENYE MCHANGO ZAIDI AENDELEE KUONGEZEA TUSIWE WACHOYO WA MAARIFA KIDOGO GAWANA NA MWENZIO
      Last edited by GAZETI; 4th December 2011 at 18:04.

    2. FemaTV & Radio

    3. #81
      Washawasha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : jo'burg
      Posts : 4,004
      Rep Power : 1455
      Likes Received
      456
      Likes Given
      891

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Quote By GAZETI
      Nitatoa maelezo ya banda baadae kidogo!
      sawa mkuu,nitaendelea kusubiri.Nalog off

      shuka halina mfuko



    4. #82
      Tutor B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : Bukoba Municipal
      Posts : 1,966
      Rep Power : 1187
      Likes Received
      594
      Likes Given
      41

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Nimejaribu kupiga gharama za kutunza kuku kwa miezi sita zimekuwa juu; sijui mtoa mada unashauri nini kuhusu hilo?
      Masikini_Jeuri likes this.
      "Ukipendwa - penda, ipo siku utapenda - usipendwe"

    5. #83
      Masikini_Jeuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Location : Igangidung'u
      Posts : 5,953
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      698
      Likes Given
      5029

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Gazeti waweza kuja na idadi fulani ya kuku kutoka kwenye kila kundi ambao yafa kuanza nao katika ukubwa fulani wa banda ili kupima uwezo kiuzalishaji na faida kwa mfugaji?
      Papizo and GAZETI like this.
      24 hours in a day! 24 beers in a case, Coincidence? I think not!

    6. #84
      Drake's Avatar
      Member Array
      Join Date : 12th December 2010
      Posts : 52
      Rep Power : 438
      Likes Received
      17
      Likes Given
      15

      Default Re: Mwongozo kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji

      asante, sasa gazeti hizi breed tunaweza zipataje bila safari ndeefu za tabora , pemba, morogoro, etc ?
      GAZETI likes this.
      Efficiency is in the manner which the job is being done!

    7. #85
      kanyagio's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2009
      Location : shambani
      Posts : 801
      Rep Power : 665
      Likes Received
      194
      Likes Given
      27

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Quote By Tutor B
      Nimejaribu kupiga gharama za kutunza kuku kwa miezi sita zimekuwa juu; sijui mtoa mada unashauri nini kuhusu hilo?
      Tutor ni kweli kabisa gharama ipo juu. kwa mfano mimi nina kuku 1000 ambapo 600 wapo wiki ya 18 na 400 wiki ya 10 na so far nimetumia milioni 11. hawa wakubwa ambao ni 600 waaanza kutaga (naona wataanza wiki ijayo). kama anayetaka breakdown aniambie nitamtumia. ni kweli unahitaji mtaji.
      kama mtaji mdogo anza na kuku wa nyama.
      Papizo and GAZETI like this.
      CDM wasipokuwa makini, watawapokea fisi ngomani badala ya binadamu- by Collezione

    8. Miaka 50

    9. #86
      GAZETI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2011
      Location : ILALA
      Posts : 1,621
      Rep Power : 1302
      Likes Received
      644
      Likes Given
      1173

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Nimekuwa Busy na kazi nyingi, lakini kuna hoja ambazo inabidi nirudi kuzijibu sina jinsi
      kwani inaweza kuwa waliopost wanaanza kukata tamaa au pengine kutokana na mimi
      kutoweka hapa jukwaani mbinu zote za jinsi ya kuuendesha mradi huu.

      Kama mmefuatilia vizuri post zangu kuna sehemu nimesema mradi huu ni nzuri zaidi
      kwa mtu aliyeko kijijini\, naomba niongezee tu kuwa kwa mwenye shamba pia mradi huu
      ni nzuri sana. Ninajua wapi mnakosea katika hesabu zenu lakini sitafika huko. Ukianza tu
      huo mradi utagundua nini ulikuwa unakosea katika hizo hesabu.

      Naomba nieleze kitu kimoja kikubwa ambacho nilikifanya nilipoanza kufuga. Bila shaka
      itakuwa ni faida kubwa kwa watu wenye nia ya dhati. Nilianza kulima mtama, karanga,
      mahindi na mpunga. Nilipata eneo kubwa la kupanda kiasi kikubwa cha vitu nilivyoeleza
      kwa sababu ni kijijini ambako kuna maeneo ya kutosha. Wakati vile vitu vinakaribia kukomaa
      ndo nikaanza kufuga kuku. Wakati vyakula vimekomaa nilikuwa na chakula cha kutosha kwa
      ajili ya mifugo yangu hiyo. Samahani nafikiri nimejitahidi kutoa ufafanuzi kwani nashindwa kuendelea kuna kazi naifanya.
      Malila, Papizo and Masikini_Jeuri like this.
      NI SISI TWAWEZA

    10. #87
      Sunshow's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2011
      Posts : 689
      Rep Power : 517
      Likes Received
      95
      Likes Given
      2

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Next time summarize your post. Its too long especially for mobile users.

    11. #88
      GAZETI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2011
      Location : ILALA
      Posts : 1,621
      Rep Power : 1302
      Likes Received
      644
      Likes Given
      1173

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Quote By Sunshow
      Next time summarize your post. Its too long especially for mobile users.
      Duh yani we sijui unafikiria nini! Hapo ilipo tu bado inahitaji ufafanuzi nikisummarize si
      ndo itakuwa balaa!
      Liz Senior and Masikini_Jeuri like this.
      NI SISI TWAWEZA

    12. #89
      kanyagio's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2009
      Location : shambani
      Posts : 801
      Rep Power : 665
      Likes Received
      194
      Likes Given
      27

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      mkuu Gazeti unafugia wapi hao kuku.
      nimependa approach yako ya kulima mazao fulani fulani kwanza
      GAZETI likes this.
      CDM wasipokuwa makini, watawapokea fisi ngomani badala ya binadamu- by Collezione

    13. #90
      Masikini_Jeuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Location : Igangidung'u
      Posts : 5,953
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      698
      Likes Given
      5029

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Quote By Sunshow
      Next time summarize your post. Its too long especially for mobile users.

      Find a PC and do your stuff...............mobile connection is meant to expedite things and not a total solution for everything you want to communicate!
      GAZETI and Excellent like this.
      24 hours in a day! 24 beers in a case, Coincidence? I think not!

    14. #91
      Nyuki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th July 2009
      Location : D'salaam
      Posts : 375
      Rep Power : 577
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwongozo kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji

      Quote By GAZETI
      Pengine umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Yako mambo mengi ya kufanya mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.Viko vitabu vingi na tena siku hizi zinatolewa DVD za jinsi ya kufanikiwa katika maisha. Utashangaa mpaka unamaliza kusoma au kutazama DVD hizo hujapata njia ya wazi sana sana utajilaumu tu kwa kuendelea kupoteza fedha kwa kuchangia miradi ya wajanja hao. Wengine wanakuambia "amini tu kuwa wewe ni tajiri na utafanikiwa" mh! INAWEZEKANA? Afadhali hao, balaa zaidi ni wale ambao wanayanadi mafanikikio na utajiri kwa mizizi, hirizi na hata roho za binadamu wenzao!

      Somo langu ni dogo lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana. Sasas kuwa makini zaidi. Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo. Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4 . Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri. Wale vifaranga tunakadiria kuwa makoo(majike) watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga. Utakuwa na kuku 200 + 25 =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700. Ndugu mwanajamvi hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku 1,000. Mwaka 2. 750(majike) x 10 = 7500 (uza wengine) 3000 x 10 = 30,000. Kutegemea na uwezo wako mpaka mwisho wa mwaka wa pili utakuwa umefanikiwa sana. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi huku ukiacha kando uzushi wa vitabu vya wasanii na DVD zao pia. NB. Kumbuka kuku ninao wazungumzia hapa ni wale wa kawaida sio wale mataahira (wa kisasa).Fuatilia zaidi kuhusu matibabu na matunzo mengineyo.

      MAELEZO ZAIDI
      UFUGAJI BORA WA KUKU WA KIENYEJI



      SEHEMU YA KWANZA

      UTANGULIZI

      Napenda kumshukuru mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kwa namna moja au nyingine kutoa mchango wangu kwa mtindo huu. Huu ni kama mwongozo tu wa nini utakabiliana nacho au unatakiwa kufanya katika zoezi zima la ufugaji wa kuku wa kienyeji. Nimeamua kuuleta kwenu wana JF ili kwa mtu mwenye malengo ya kufanikiwa kupitia ufugaji wa kuku ajue mlolongo mzima na changamoto ambazo atakabiliana nazo.

      A.KWA NINI KUKU WA KIENYEJI?

      1. Wastahimilivu wa magonjwa lakini ni muhimu wakikingwa na magonjwa ya kuku kama mdondo, ndui ya kuku n.k ili kuweza kuwaendeleza.
      2. Wana uwezo wa kujitafutia chakula ardhini.
      3. Wana uwezo wa kuatamia mayai, kutotoa na kulea vifaranga na ustahimilivu wa mazingira magumu kama ukame, baridi n.k
      4.Nyama na mayai yake vina ladha nzuri kuliko kuku wa kisasa.(PATA SUPU YA KUKU WA KIENYEJI ILI UTHIBITISHE)
      5. Wana uwezo wa kujilinda na maadui kama mwewe n.k . Pamoja na sifa hizi ni muhimu muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri, wakawekwa kwenye mabanda mazuri, wakapewa maji na chakula cha kutosha.

      B.FAIDA ZA KUKU WA KIENYEJI.

      Faida ni nyingi na zinafahamika lakini nitaeleza zile ambazo kwa wengine huenda zikawa ni ngeni kwao.
      - Mayai huweza kutumika kwa tiba. (Pata maelezo jinsi yai la kuku wa kienyeji linavyoweza kutumika kwa tiba kutoka kwa wataalam wa tiba mbadala)
      - Kiini cha njano cha yai kinaweza kutumika kutengenezea mafuta ya nywele (shampoo)
      - Manyoya yake yanaweza kutumika kama mapambo.
      Fuga kuku upate faida kwa kuzingatia:
      Chanjo ya mdondo kila baada ya miezi mitatu na chanjo ya ndui mara mbili kwa mwaka
      Zuia viroboto, utitiri na minyoo.
      Chagua mayai bora kwa ajili ya kuatamiza
      Panga kuuza kuku kwa makundi uongeze kipato
      Kula mayai na kuku kadri uzalishaji unavyoongezeka.
      Kipato unachokipata utenge pia na kiasi kwa ajili ya uendelezaji wa kuku

      C:MAPUNGUFU

      Yako mapungufu mengi yanayofahamika lakini hapa naomba niweke lile la muhimu zaidi. MAGONJWA kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku kutokana na kutokuzingatia kuchanja kuku kwa wakati.


      D: KABILA ZA KUKU WA KIENYEJI

      Kuna maelezo ya kusisimua sana kuhusu makabila ya kuku wa kienyeji, hata hivyo kuna ugumu kidogo kuweza kuyachanganua makabila hayo kutokana na muingiliano mkubwa wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Hata hivyo kuku hawa wana tofauti za kimaumbile zinazosaidia kwa kiasi fulani kutambua uwepo wa baadhi ya makabila ya kuku. Kabila hizi pia zinahusishwa kwa kiasi kikubwa na eneo kuku wanakotoka. Baadhi ya kuku wa kienyeji wanaweza kutambuliwa kwa maumbile yao Mfano:
      a. Kishingo - kuku wasio na manyoya shingoni
      b. Njachama au Nungunungu - Hawa ni wale wenye manyoya yaliyosimama.
      c. Kibwenzi - Ni wale wenye manyoya mengi kichwani.
      d. Kibutu- Hawa hawana manyoya mkiani
      Mwingiliano wa vizazi unaweza ukasababisha kuku kuwa na aina ya maumbile mchanganyiko. Mfano kuku aina ya kuchi anaweza kuwa na alama ya kishingo, Njachama, Kibwenzi au Kibutu.
      Hivyo kabila za kuku zifuatazo zinaweza kutambuliwa kama ndiyo kabila za kuku wa kienyeji kulingana na maumbile yao na maeneo wanakotoka.

      (i) KUCHI

      Ni kuku warefu kwa umbo na wenye kusimama mgongo ukiwa wima. Wana manyoya machache mwilinini na hasa kifuani, vilemba vyao ni vidogo. Majogoo huwa na wastani wa uzito wa Kg. 2.5 na mitetea kg 1.5 mayai ya kuchi yana uzito wa wastani wa gm 45. Kuku hawa hupatikana kwa wingi maeneo ya Mwanza, Shinyanga, Tabora na Zanzibar.

      (ii) CHING'WEKWE

      Kuku hawa ambao jina lao ni gumu kidogo kwa mtu asiyekuwa na meno kulitamka wana sifa zifuatazo.
      Majogoo wana wastani wa kg 1.6, Mitetea wastani kg 1.2, mayai wastani wa gm 37. Kuku hawa wenye umbo dogo hupatikana zaidi maeneo ya CHAKWALE mkoani Morogoro na pia sehemu za umasaini. Kuku hawa hutaga mayai mengi sana kuliko aina nyingine ya kuku wa kienyeji waliopo Tanzania, kwa hiyo wanafaa sana kwa biashara ya mayai.

      (iii)UMBO LA KATI

      Majogoo wana uzito wa wastani wa kg. 1.9, Mitetea kg. 1.1, Kuku hawa ndio hasa wanaoitwa wa kienyeji(wa kawaida) Wana rangi tofauti. Utafiti umeonyesha kuwa kuku hawa hukua upesi na hupata kinga upesi baada ya kuwachanja dhidi ya ugonjwa wa mdondo (Castle desease)
      Muhimu - Mfugaji akifanya uchaguzi kutoka kwenye aina hii ya kuku na kutoa matunzo mazuri kwa hao kuku waliochaguliwa, Hakika anaweza kupata kuku walio bora na wenye uzito wa kutosha pia kutaga mayai mengi na makubwa.

      (iv) SINGAMAGAZI

      Ni aina ya kuku wakubwa wa kienyeji wanaopatikana zaidi TABORA, kuku hawa wana utambulisho maalum kutokana na rangi zao. Majogoo huwa na rangi ya moto na mitetea huwa na rangi ya nyuki. Uzito - Majogoo uzito wa wastani wa kg 2.9, mitetea wastani wa kilo 2 mayai gramu 56.

      (iiv) MBEYA

      Kuku hawa wanapatikana Ileje mkoani mbeya. Asili hasa ya kuku hawa ni kutoka nchi ya jirani ya Malawi na si wa kienyeji asilia bali wana damu ya kuku wa Kizungu "Black Australop". Majogoo Kg 3 mitetea kg 2 mayai gram 49

      (iiiv)PEMBA

      Hupatikana zaidi Pemba. Majogoo Kg.1.5 Mitetea Kg 1 mayai wastani gm 42

      (xi) UNGUJA.

      Majogoo Kg 1.6,mitetea kg 1.2 mayai gm 42. Kuku hawa wa Unguja na Pemba wanashabihiana sana na Kuchi isipokuwa hawa ni wadogo.


      SEHEMU YA PILI

      1. MIFUMO YA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI.

      A. MFUMO HURIA
      Katika mfumo huu kuku huachiwa wakitembea toka asubuhi wakijitafutia chakula na maji na kufungiwa kwenye vibanda visivyo rasmi wakati wa usiku. Huu ni mfumo rahisi lakini si nzuri kwa mfugaji wa kuku wengi kwani atahitaji eneo kubwa la ardhi.

      FAIDA.
      Mfumo huu una faida za gharama ndogo za uendeshaji kiujumla.

      HASARA
      Uwezekano mkubwa wa kuku kuliwa na vicheche, kuibiwa mitaani n.k
      Kuku huweza kutaga popote na kusababisha upotevu mkubwa wa mayai.
      Ni rahisi kuku kuambukizwa magonjwa
      Utagaji unakuwa si nzuri kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa.
      Uwekaji kumbukumbu si nzuri.
      Ni vigumu kugundua kuku wagonjwa hivyo kusababisha ugumu katika utoaji wa tiba.

      UTUMIAJI NZURI WA MFUMO HUU
      Kuku wajengewe banda kwa ajili ya kulala nyakati za usiku na liwasaidie wakati mwingine wowote hali ya hewa inapokuwa si nzuri.
      Kuku wapatiwe chakula cha ziada na maji.
      Kuku waandaliwe kwa viota vya kutagia.
      Kuku 100 ni vizuri wakitumia eneo la ardhi la ekari 1.


      B.MFUMO NUSU HURIA
      Huu ni mfumo ambao kuku hujengewa banda rasmi na banda hilo huzungushiwa uzio/ wigo. Mfumo huu ni ghari kiasi ukilinganisha na mfumo huria lakini huweza kumpatia mfugaji faida haraka sana.

      FAIDA
      Sehemu ndogo ya kufugia hutumika kuliko ufugaji huria, utunzaji wa kuku ni rahisi ukilinganisha na mfumo huria, Ni rahisi kutibu magonjwa ya mlipuka kama mdondo (Newcastle desease), Upotevu wa kuku na mayai ni mdogo sana ukilinganisha na mfumo huria.


      C. MFUMO WA NDANI
      Kuku hujengewa banda rasmi na hufugwa wakiwa ndani. Mfumo huu kuku huwekwa kwenye mabanda ambayo sakafu hufunikwa kwa matandiko ya makapi ya mpunga, takataka za mbao(randa), maganda ya karanga au majani makavu yaliyokatwa katwa.

      FAIDA
      Mfumo huu unahitaji eneo dogo la kufugia, uangalizi mzuri na rahisi wa kuku, Joto litokanalo na matandiko lina uwezo wa kuua vimelea vya maradhi, kuku wanakingwa na hali ya hewa mbaya na maadui wengine.

      HASARA
      Uwezekano wa kuku kudonoana ni mkubw na pia Gharama za ujenzi wa mabanda

      UTUMIAJI MZURI WA MFUMO HUU.
      1. Matandiko yageuzwe kila siku
      2. Kila mara matandiko yawe makavu kwa kuwa na madirisha yanayopitisha hewa ya kutosha, ambayo yatatoa unyevunyevu hewa chafu ikiwemo ammonia.
      4. Mita mraba moja hutosha kuku 5 hadi 8.



      UTATUZI WA KUKABILIANA NA VIKWAZO KATIKA UFUGAJI.
      Mambo ya kuzingatia:

      Mabanda bora - Fuatilia kwa wataalamu wa mifugo walio karibu nawe.
      Sifa za banda bora (Waone wataalam wa mifugo)
      Kuchagua kuku wa kuendeleza kizazi
      Kuwa makini na aina ya mitetea na majogoo unatakiwa kuchagua ili kuwa na kizazi bora.


      UTAGAJI WA MAYAI
      Kwa kawaida kuku huanza kutetea(Kutoa mlio wa ishara ya kutaga) anapofikisha miezi sita hadi minane. Hivyo ni vyema viota viandaliwe mapema wakiwa na umri wa miezi mitano. Kuku anapoanza kutaga akifikisha mayai matatu mfugaji anashauriwa kuondoa kila yai linalozidi hayo matatu kila siku linapotagwa na kuliweka alama ya tarehe au namba kwa kutumia penseli ili kumfanya kuku aendelee kutaga kwa lengo la kufikisha mayai 15 mpaka 20. Mayai yanayoondolewa yawekwe kwenye chombo kikavu kinachopitisha hewa ni vizuri pia kuweka mchanga ndani ya chombo hicho.

      Hakikisha ya fuatayo.
      Sehemu iliyochongoka iwe chini na pana iwe juu.
      Hifadhi sehemu yenye hewa ya kutosha na isiyohifadhi joto
      Mayai yasikae kwenye hifadhi hiyo zaidi ya wiki mbili toka siku ya kuanza kutagwa.

      UATAMIAJI WA MAYAI NA UANGUAJI WA VIFARANGA
      Uatamiaji na uanguaji wa kubuni - Mfumo huu hutumia mashine za kutotoleshea vifaranga (Incubators) hutumika kuangua mayai mengi kati ya 50 hadi 500 kwa wakati mmoja Mashine zinazotumika kutotoleshea vifaranga wa kisasa zinaweza kutumika pia kutotoleshea wa kienyeji.
      Uatamiaji na uanguaji wa asili

      KUCHAGUA MAYAI YA KUANGUA.
      Hili nalo ni muhimu kuzingatia. Ni vizuri kuchagua mayai ya kuatamia ili mayai yasiyofaa yaweze kuuzwa au kutumiwa nyumbani kwa chakula. Mayai ya kuatamia yawe na sifa zifuatazo
      Yasiwe na uchafu yawe masafi
      Yasiwe na nyufa
      Yatokane na kuku aliyepandwa na jogoo
      Yasiwe madogo wala makubwa bali yawe na ukubwa wa wastani kulingana na umbile la kuku.
      Yasiwe mviringo kama mpira pia yasiwe na ncha kali sana.
      Yasiwe yamekaa muda mrefu zaidi ya wiki mbili toka yalipotagwa
      Yasiwe yaliyohifadhiwa kwenye sehemu yenye joto.

      KUMTAYARISHA KUKU WA KUATAMIA
      Pamoja na matayarisho hayo zingatia kumuwekea mayai yasiyozidi 15 pia ni vizuri yasipungue 12. Kuku wanaotazamiwa kuatamia ni lazima wachunguzwe kwa makini kabla ya kuatamia ili kuhakikisha kwamba hawana chawa, utitiri n.k. Kuwepo kwa wadudu hao huwafanya kuku wakose raha na kutotulia kwenye viota vyao. Hali hii husababisha kuanguliwa kwa Vifaranga wachache.
      Sasa unatakiwa kufanya yafuatayo:-
      Nyunyiza dawa ya kuua wadudu ndani ya kiota
      Pia mnyunyuzie dawa kuku anayetarajia kuatamia
      Weka mayai kwenye kiota huku mikono yako ikiwa imepakwa jivu ili kuepuka kuwa na harufu kwani kuku anaweza kuyasusa.

      Ni vizuri kuifanya kazi hii ya kumuandaa kuku anayetaka kuatamia wakati wa usiku. Pia ifahamike kuwa kwa kawaida kuku huatamia mayai yake siku 21.

      PIA JIFUNZE MBINU ZA KUATAMIA MAYAI MENGI KWA NJIA ZA ASILI
      Iwapo una kuku wengi wanaotaga kwa wakati mmoja ni vema ukawafanya wakaatamia na kutotoa pamoja.
      Unachotakiwa kufanya ni kuchagua mayai ya kuatamia ukianzia na yai la mwisho kutaga.
      Unaweza kuwaandaa kuku wako zaidi ya mmoja ili waanze kuatamia kwa pamoja na kupata vifaranga vingi kwa mara moja kuku wa kwanza anapoanza kuatamia. Mwekee mayai viza au ya kuku wa kisasa kwani kuku huatamia hadi mayai yanapoanguliwa hivyo ukimuwekea mayai yasiyo na mbegu atakaa hapo muda mrefu hadi vifaranga watoke.

      UTEKELEZAJI WAKE
      Kuku anapotaga kila siku weka alama ya namba au tarehe kulinganisha na siku anayotaga
      Yanapofika mayai matatu yaondoe na muwekee mayai viza au ya kisasa huku ukiendelea kuweka alama mayai yanayotagwa kila siku.
      Mara kuku anapoanza kuatamia muongezee mayai ya uongo yafikie 8 hadi 10
      Fanya hivyo kwa kila kuku anayetaga hadi utakapoweza kupata idadi itakayoweza kukupatia vifaranga wengi kwa wakati mmoja.
      Wawekee kuku wote mayai siku moja kwa kuondoa mayai ya uongo na kuwawekea mayai ya ukweli wakati wa usiku.

      MUHIMU
      Mayai ya kuatamia yasishikwe kwa mkono ulio wazi na wala yasipate harufu za mafuta ya taa, manukato n.k.

      JIFUNZE PIA KUTAMBUA MAYAI YALIYO NA MBEGU NA YALE YASUYO NA MBEGU.
      Mfugaji anaweza kutambua mayai yaliyo na mbegu na yale yasiyo na mbegu siku ya saba baada ya kuanza kuatamia iwapo atapima mayai kwa kutumia box lililotengenezwa maalum pamoja na tochi yenye mwanga mkali ndani ya chumba chenye kiza. Hii itamuwezesha mfugaji ayatumie mayai yasiyo na mbegu kwa chakula cha familia au kuyauza.

      TAMBUA VYAKULA NA UZALISHAJI WA KUKU - Sitalielezea hili naomba ufuatilie mwenyewe.

      JIFUNZE MBINU ZA KUZALISHA KUKU WENGI KWA MUDA MFUPI
      Zoezi hili linawezekana iwapo uleaji wa vifaranga kwa njia ya kubuni utatumika. Kuku mmoja anaweza kutotoa zaidi ya mara saba kwa mwaka.
      Taz.
      Hesabu ya uzalishaji wa kuku wengi kwa mwaka kwa kutumia mtetea mmoja tu.
      Mpaka mwisho wa mwaka unaweza kuwa na idadi ya vifaranga 252 kwa kadirio la vifaranga 8 kila mzao. Hivyo kama una kuku 10 wanaotunzwa vizuri utakuwa umezalisha jumla ya vifaranga 2520.

      Fuatilia kwa wataalamu wa mifugo ili ufundishwe zaidi kuhusu mbinu hiyo ya kuzalisha kuku wengi.

      ULEAJI WA VIFARANGA
      NJIA YA KUBUNI
      NJIA YA ASILI
      Njia zote mbili zinafahamika kama huzifahamu tafadhali fuatilia kwa mtaalamu aliye karibu nawe.


      MAGONJWA NA WADUDU WANAOSHAMBULIA KUKU WA KIENYEJI NA JINSI YA KUKINGA.

      A. MAGONJWA.
      Ugonjwa hatari - Mdondo/ Kideri (Newcastle desease) Hapo nyuma dawa ya kukinga ugonjwa huu ilikuwepo lakini ilikuwa inahitaji kuhifadhiwa kwenye hali ya ubaridi (Friji) Hali hiyo ilisababisha iwe ngumu kutumika vijijini kwa dawa hiyo. Hivi sasa kumepatikana chanjoa ambayo inastahimili joto ambayo inaweza kutumika hata vijijini.

      Pamoja na mdondo yapo pia magonjwa yanayoshambulia kuku hapa nchini

      Ndui ya kuku(Fowl pox)
      Mafua ya kuku(Infectious coryza)
      Homa ya matumbo (Cocciodiosis)
      Minyoo na wadudu kama viroboto, chawa, utitiri na kupe wa kuku.

      DALILI ZA KUKU MGONJWA.

      Huzubaa
      Hali chakula/maji vizuri
      Hujitenga na wenzake
      Hujikunyata au kuinama
      Hutetemeka
      Hutembea kwa shida
      Utagaji wa mayai hupungua au hukoma kabisa


      MAGONJWA YA KUKU HUSABABISHWA NA NINI?
      Yako mambo mengi yanayosababisha lakini matunzo hafifu pia huchangia.

      ATHARI ZA MAGONJWA.
      Hili liko wazi

      Maelezo haya ya magonjwa ni mengi hivyo tuwe wafuatiliaji kwa wataalam.



      MATIBABU

      KIDERI - Sifahamu tiba ya kitaalam ya ugonjwa huu kama kuna ambaye anafahamu tunaomba atufahamishe lakini ziko dawa za asili na za kitaalam ambazo zinafaa zaidi kwa chanjo.
      Ugonjwa huu unaweza kuukinga kwa kuwapa kuku chanjo ya Mdondo. Pia usichanganye kuku wako na kuku ambao huna taarifa zao za chanjo.

      KUMBUKA
      Mdondo au kideri ni ugonjwa tishio ambao huweza kuua kuku wote
      Mdondo ukitokea vifo huwa vingi pia kuku hupumua kwa taabu, hupooza na wengine huzunguka na huzungusha vichwa.
      Mdondo unaweza kuzuilika kwa chanjo kila baada ya miezi 3

      NDUI YA KUKU
      HOMA YA MATUMBO (Fowly typhoid)
      MAFUA YA KUKU(Infectious coryzya)
      KUHARISHA DAMU(Coccidiosis)
      Minyoo na wadudu wanaoshambulia kuku kama viroboto n.k

      Kwa magonjwa na wadudu tuliowataja hapo juu please wasiliana na mtaalamu wa mifugo aliye karibu nawe Kwani siwezi kueleza kila kitu hapa wataalamu tunao naamini watatusaidia.

      TIBA ZA ASILI
      Kuna madawa ya asili ambayo hutokana na mimea ambayo hukinga kuku.

      BAADHI YA MIMEA INAYOTIBU NA KUKINGA MARADHI YA KUKU.

      MWAROBAINI - Typhoid, kuhara, kideri, kifua na vidonda
      ALOEVERA - Typhoid, kuhara, kideri, kifua na vidonda,ngozi na Cholera. Tutaelekezana zaidi namna ya kuandaa dawa hii.

      Hapa nataka niorodheshe baadhi ya madawa ya asili ambayo yanasaidia kutibu na kukinga kuku.
      Mwarobaini, Aloevera, Mtakalang'onyo(Euphorbia),Mbar ika, mlonge, Ndulele/dungurusi/tura/ndura, Majani ya mpapai, Mwembe, Minyaa na Pilipili kichaa.

      NAWASHUKURU PIA NAOMBA MWENYE MCHANGO ZAIDI AENDELEE KUONGEZEA TUSIWE WACHOYO WA MAARIFA KIDOGO GAWANA NA MWENZIO
      mkuu saafi sana
      Lets become a change thats we want to see in the world

    15. #92
      GAZETI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2011
      Location : ILALA
      Posts : 1,621
      Rep Power : 1302
      Likes Received
      644
      Likes Given
      1173

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Quote By kanyagio
      mkuu Gazeti unafugia wapi hao kuku.
      nimependa approach yako ya kulima mazao fulani fulani kwanza
      Nilikuwa nafuga, kwa kuwa nilikuwa nimesomea uhasibu nikashawishika
      kuajiriwa hapo ndipo nilipoharibu. Najipanga kurudi tena na nimeshaanza maandalizi
      kwani nimepata shamba maeneo ya JARIBU MPAKANI. Nauli ni Tsh 3000 kutoka
      Mbagala.
      NI SISI TWAWEZA

    16. #93
      blea's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : URU ONGOMA MAMBA
      Posts : 239
      Rep Power : 427
      Likes Received
      48
      Likes Given
      145

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Ni kweli mkuu ufugaji wa kuku unalipa cha kuzingatia ni taratibu za ufugaji bora pia kuwa karibu na wazoefu ili wakupe mbinu za kukabiliana na changamoto za ufugaji pindi zitakapojitokeza
      GAZETI likes this.

    17. #94
      Relief's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th August 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 255
      Rep Power : 1359
      Likes Received
      44
      Likes Given
      83

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Somo zuri sana.
      GAZETI likes this.
      " The main thing is to keep the main thing the main thing"

    18. #95
      kihodombi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd January 2012
      Posts : 27
      Rep Power : 375
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      I will take this
      GAZETI likes this.

    19. #96
      khashdz's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th July 2011
      Posts : 10
      Rep Power : 399
      Likes Received
      2
      Likes Given
      2

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Kwa nyaongeza ni bora ukanza na kuku wachache ili ukasoma mazingira na kuepuka garama za pamoja then ukawa unaongezea kidogokidogo kulingana na halihalisi unavyoiona. lakini wengi wetu huwa tunapiga maesabu makubwa hapo ndipo tunapo fail kufikia malengo coz ukichemsha kidogo tu unaona hiyo plan haifai kabisa na kama unaimani ndogo unaweza sema umelogwa lakini ni kutokujiandaa tu.
      alsaidy and GAZETI like this.

    20. #97
      Hkeen's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th August 2011
      Posts : 97
      Rep Power : 411
      Likes Received
      4
      Likes Given
      3

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Asante, kwa msaada. Muda huu ninaoelekea kumalza mtihan wa advc kesho, niwakati muhafaka kufikiri kugusa hili, na kulfanyia uchungu kulingana maeneo ninayo ya KDC - MOSHI. Mwanzo mwema kwangu . . .

    21. #98
      lola's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th December 2011
      Posts : 18
      Rep Power : 376
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      good idea

    22. #99
      satellite's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th November 2010
      Location : HOMELAND SECURITY
      Posts : 546
      Rep Power : 540
      Likes Received
      94
      Likes Given
      60

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Mkuu thanx a lot hapo umesomeka sana

    23. #100
      lumbagengata's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th May 2011
      Posts : 25
      Rep Power : 411
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Re: Unataka kuwa tajiri?

      Thankx bwana Gazeti ,wazo lako nimelipata. Binafsi saizi niko ktk kilimo cha Mpunga kuishia mwezi mei 2012 nitakuwa ktk mavuno then nataraji kulima kitunguu maji mwezi July-October 2012 .Hivyo kutokana na wazo lako nimeona mazao mengine(yale uliyosema ulilima awali) itabidi niyafanyie kz ili kupunguza cost za mradi kuku kwa 2013 mazao hayo yatakapokuwa tayari. Nimeipenda idia yako kwani inatekelezeka ila structure ya mabanda sijaipata. Basi tuzidi shauriana wa jf
      GAZETI likes this.

    Page 5 of 7 FirstFirst ... 34567 LastLast

    Similar Topics

    1. Siri ya kuwa tajiri!
      By Maswa in forum Business & Economic Forum
      Replies: 0
      Last Post: 7th October 2011, 20:01
    2. Jinsi ya kuwa TAJIRI..........
      By El Toro in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 7
      Last Post: 22nd November 2010, 19:27
    3. Kuwa na akili nyingi sio kuwa tajiri!
      By Mtambuzi in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 28th August 2009, 09:44
    4. Kwani ni haramu kwa Kiongozi wa nchi kuwa Tajiri?
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 21st August 2007, 13:42

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...