Mtanzanika
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 2,389
- 1,131
Jamaa mmoja alituma M pesa kwa bahati mbaya akamtumi Zuzu.
Zuzu aliposhtukia katumiwa na mtu asiyemjua harakaharaka akaituma kwa Janja rafiki yake ili kuwapiga chenga wenye mtandao.
Baada ya muda mfupi akapokea simu na kupewa shukrani nyingi na ahsante kwa kitendo cha kiungwana alichofanya.
Alipomaliza kuongea na simu akagundua kuwa zile shukrani hazikutoka kwa Janja rafiki yake bali zilitoka kwa yule jamaa aliyetuma pesa kwa makosa.
ndipo Zuzu alipobaini kuwa hakuzifoward zile pesa kwa rafiki yake Janja na badala yake alikosea na kuzirudisha zilipotoka.
Zuzu aliposhtukia katumiwa na mtu asiyemjua harakaharaka akaituma kwa Janja rafiki yake ili kuwapiga chenga wenye mtandao.
Baada ya muda mfupi akapokea simu na kupewa shukrani nyingi na ahsante kwa kitendo cha kiungwana alichofanya.
Alipomaliza kuongea na simu akagundua kuwa zile shukrani hazikutoka kwa Janja rafiki yake bali zilitoka kwa yule jamaa aliyetuma pesa kwa makosa.
ndipo Zuzu alipobaini kuwa hakuzifoward zile pesa kwa rafiki yake Janja na badala yake alikosea na kuzirudisha zilipotoka.