Sir R
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 2,175
- 298
Leo mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro aliamua kukutana na walimu wa Sekondari manispaa ya Moshi katika ukumbi wa shule ya sekondari Majengo kwa ajili ya kusikiliza kero za walimu.
Mkutano uliaanza kwa mkurugenzi kutambulisha meza kuu. Baada ya utambulisho aliamkaribisha mkuu wa wilaya Ibrahimu Msengi kusema machache na kumkaribisha Rc Gama.
Mkuu huyo aliaanza kwa kuwasifu walimu kwa kusema walimu wanafanya kazi nzuri mfano walimu wengi walishiriki katika zoezi la uandikishaji wa sensa, hatua hiyo ilikumbana na kelele za kuzomea, kwani walimu wengi walikosa nafasi ya kushiriki katika zoezi hilo kwa kuwa walishiriki katika mgomo wa walimu. DC aliamua kumkaribisha mkuu wa Mkoa.
Wakati wa utambulisho watumisho wote wa halmashauri wakupigiwa makofi isipokuwa viongozi wa CWT waliokuwa meza kuu.
Mkuu wa mkoa aliongea kwa ufupi kuwa alikuja kusikiliza kero za walimu halafu akawakaibisha walimu kutaja kero zao. Baada ya kero kutajwa, Rc aliwakaribisha wakuu wa idara mbalimbali kujibu na kutoa ufafanuzi wa hoja za walimu.
Idara iliyokumbwa na zomea zomea ni idara ya utumishi. Walimu walikuwa wakali mno.
Bwana Gama alijitahidi sana kuwatuliza walimu na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa. Mkurugenzi na watumishi wake walikuwa kimya muda wote.
Rc alisema kuwa itakuwa ni utaratibu wake wa kukutana na walimu ili kuboresha sekta ya elimu mkoa wa Kilimanjaro.
Mkutano ulianza saa 4:15 asbuhi na kumalizika saa 10 jioni.
Mkutano uliaanza kwa mkurugenzi kutambulisha meza kuu. Baada ya utambulisho aliamkaribisha mkuu wa wilaya Ibrahimu Msengi kusema machache na kumkaribisha Rc Gama.
Mkuu huyo aliaanza kwa kuwasifu walimu kwa kusema walimu wanafanya kazi nzuri mfano walimu wengi walishiriki katika zoezi la uandikishaji wa sensa, hatua hiyo ilikumbana na kelele za kuzomea, kwani walimu wengi walikosa nafasi ya kushiriki katika zoezi hilo kwa kuwa walishiriki katika mgomo wa walimu. DC aliamua kumkaribisha mkuu wa Mkoa.
Wakati wa utambulisho watumisho wote wa halmashauri wakupigiwa makofi isipokuwa viongozi wa CWT waliokuwa meza kuu.
Mkuu wa mkoa aliongea kwa ufupi kuwa alikuja kusikiliza kero za walimu halafu akawakaibisha walimu kutaja kero zao. Baada ya kero kutajwa, Rc aliwakaribisha wakuu wa idara mbalimbali kujibu na kutoa ufafanuzi wa hoja za walimu.
Idara iliyokumbwa na zomea zomea ni idara ya utumishi. Walimu walikuwa wakali mno.
Bwana Gama alijitahidi sana kuwatuliza walimu na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa. Mkurugenzi na watumishi wake walikuwa kimya muda wote.
Rc alisema kuwa itakuwa ni utaratibu wake wa kukutana na walimu ili kuboresha sekta ya elimu mkoa wa Kilimanjaro.
Mkutano ulianza saa 4:15 asbuhi na kumalizika saa 10 jioni.