Zombe: Sitishiki!

3296882.jpg

Friday, October 09, 2009 4:36 PM
ALIYEKUWA Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe ameandika barua ya kuacha kazi katika jeshi hilo baada ya Serikali kukata Rufaa dhidi yake.

Jeshi la Polisi limethibitisha kupokea barua ya Zombe inayoeleza kutotaka tena kuendelea na ajira ya jeshi hilo.


Maamuzi ya Zombe yamekuja kwa kudai kuwa baada ya kuona amefikia hatua hiyo ya hofu ya kwa kutengenezewa kesi nyingine na kulazimika kuandika barua ya kuomba kuacha kazi.


Kamishna wa utawala na rasilimali watu wa Jeshi la Polisi, CP Clodwig Mtweve, amesema barua hiyo imepokelewa na imekabidhiwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ambaye kiutaratibu ndiye mwajiri wa Zombe.

Mtwere alisema kuwa katibu huyo ndiye mwenye mamlaka ya kujibu barua hiyo ya kuacha kazi ama kuendelea nay eye ndiye atakayekuwa na mamlaka juu ya maombi hayo.


Hatua ya Zombe imekuja baada Juzi Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) alikata rufani dhidi ya Zombe na wenzake wanaotuhumiwa kwa mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro, na dereva teksi mmoja.


Rufani hiyo ina sababu 11 zinazopinga kuachiwa huru kwa washitakiwa hao wanaodaiwa kuwaua kwa makusudi wafanyabiashara hao.



Sababu hizo zilizowasilishwa na DPP ni pamoja na Jaji Salum Massati, ambaye ndiye alikuwa akisikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu ya kuwaachia huru washitakiwa hao, kufanya makosa katika kujielekeza, kujenga na kutoa tafsiri katika kanuni za kosa.


Rufani hiyo inadai kuwa Jaji Massati alifanya makosa katika kumwachia huru mshitakiwa wa kwanza, ambaye ni Zombe, pamoja na kuwapo ushahidi wa kutosha wa kimazingira ambao ungeweza kumtia hatiani.


Rufani hiyo pia inadai kuwa Jaji alishindwa kutoa sababu za washitakiwa wa WP Jane na D.2300 D/CPL Sarro kwa kuathirika kwao kimazingira kama alivyoeleza kwenye hukumu yake.

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3296882&&Cat=1
 
Zombe kuomba kustaafu mara baada ya kesi amehisi mafao yake yatakuwa hatarini endapo atashindwa rufaa?
 
3. Ushauri wangu ni kwamba kama mwananchi wa kawaida usiyesoma Sheria darasani, jitahidi kuhudhuria Mahakamani mara kwa mara ili kuona jinsi kesi zinavyoendeshwa, usione kama kuhudhuria Mahakamani unajitafutia nuksi! La hasha. Unaweza kujikuta umeshtakiwa au unatakiwa (unalazimika) kutoa ushahidi siku moja Mahakamani, who knows!

Ni kweli mkuu Buchanan unayosema,ni muhimu kwenda mahakamani kuona na kujifunza jinsi kesi zinavyoendeshwa,nakumbuka kuna rafiki yangu mmoja alishawahi pia kunishauri hilo kuwa tusione ni kupoteza muda tunapoenda mahakama kusikiliza na kujifunza pia kesi zinavyoendeshwa.
 
Zombe kuomba kustaafu mara baada ya kesi amehisi mafao yake yatakuwa hatarini endapo atashindwa rufaa?
ukisoma vizuri maelezo ya Zombe utagundua hio kesi jamaa amebambikiwa ili wamkomoe.KUNA SIRI NZITO HUMO.
SWALI LA MSINGI- Ni vipi Zombe alielitumikia jeshi la polisi kwa muda mrefu aje ababaike kuuwa watu ili wakwibe Tshs.5m???? Ina katika muda wote ni hao majambazi tuu walioshikwa baada ya ujambazi kutokea????
Hapa kuna visasi na inavyoonekana ni vya kisiasa zaidi....ref uchaguzi wa 2005!!!
- Iweje real washiriki wa uuaji wapotee kimiujiza????
 
ukisoma vizuri maelezo ya Zombe utagundua hio kesi jamaa amebambikiwa ili wamkomoe.KUNA SIRI NZITO HUMO.
SWALI LA MSINGI- Ni vipi Zombe alielitumikia jeshi la polisi kwa muda mrefu aje ababaike kuuwa watu ili wakwibe Tshs.5m???? Ina katika muda wote ni hao majambazi tuu walioshikwa baada ya ujambazi kutokea????
Hapa kuna visasi na inavyoonekana ni vya kisiasa zaidi....ref uchaguzi wa 2005!!!
- Iweje real washiriki wa uuaji wapotee kimiujiza????

Mimi naona kwa haraka haraka kama Zombe alikuwa organizer wa tukio la mauaji ya wale wafanyabiashara ila siye aliyeua, kwa nini? Baada ya kupewa taarifa kwamba baada ya kuwaua "majambazi" fedha iliyopatikana ni TSh 5m/- alizira fedha hizo na kudai eti ni kidogo! Kumbuka kuwa wale wafanyabiashara walikuwa na zaidi ya 5m/- na Zombe alijua in advance! Suala jingine litialo shaka ni kwa nini Zombe hakuenda eneo la tukio kama Police General Orders (PGO) inavyomtaka hasa kwenye tukio kubwa kama hilo? All in all, kwa namna moja au nyingine Zombe alijua kilichokuwa kinaendelea na alikuwa masterminder wa tukio zima, lakini hakuua yeye mwenyewe (hakuna 'actus reus')!
 
Zombe anapolalamika kuwa watu wanabambikizwa kesi...akiwa kama polisi mwandamizi ina maana anakiri kuwa POLISI wanawabambikizia wananchi wasio na hatia kesi?
 
Zombe sitaki tena ajira

photos
pix.gif
1255171432_zombe_asepa.jpg

Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe ameandika barua ya kuacha kazi katika jeshi la Polisi baada ya Serikali kukata rufaa ya kupinga kuachiwa huru.

Tayari jeshi la Polisi limethibitisha kupokea barua ya Zombe inayoeleza sababu za yeye kutoendelea na ajira ya jeshi hilo na imekabidhiwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ambaye kiutaratibu ndiye mwajiri wa Zombe..

Hivi karibuni, Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) alikata rufani dhidi ya Zombe na wenzake wanaotuhumiwa kwa mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro, na dereva teksi mmoja ikiwa na sababu 11 zinazopinga kuachiwa huru kwa washitakiwa hao.
 
Zombe sitaki tena ajira

photos
pix.gif
1255171432_zombe_asepa.jpg

Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe ameandika barua ya kuacha kazi katika jeshi la Polisi baada ya Serikali kukata rufaa ya kupinga kuachiwa huru.

Tayari jeshi la Polisi limethibitisha kupokea barua ya Zombe inayoeleza sababu za yeye kutoendelea na ajira ya jeshi hilo na imekabidhiwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ambaye kiutaratibu ndiye mwajiri wa Zombe..

Hivi karibuni, Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) alikata rufani dhidi ya Zombe na wenzake wanaotuhumiwa kwa mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro, na dereva teksi mmoja ikiwa na sababu 11 zinazopinga kuachiwa huru kwa washitakiwa hao.

Poor Zombe!
 
Back
Top Bottom