Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Nilikuwa nazungumza na rafiki yangu mmoja juu ya suala hili na mara moja tukawa na matatizo kadhaa; kwanza, linakusanya taarifa nyingi sana za mtu kiasi cha kutishia privacy ya mtu. Hizi taarifa zinasaidia vipi kuzuia money laundering? Hivi ni launderers wanaoutumia benki na kujanza taarifa zao zote muhimu? Vipi wanaotumia simu kulaunder money? Je makampuni ya simu yanayofanya shughuli za kibenki yanahitajiwa kufanya zoezi hili au ni mabenki tu?
Tatizo la pili ni kuwa inaonekana inatafutwa njia ya kuzidi kuwakamua na kuwabana law abiding citizens kwa ajili ya kodi na mapato kwa sababu serikali imegundua kuwa tax base yake haikui kwa kiasi kikubwa.
Jamaa yangu huyo alinidokeza (sijaweza kuthibitisha) kuwa VAT registered tax payers hawafiki 20,000 na wale wenye TIN hawazidi milioni moja. Sasa, hawa ndio ambao wanataka kuzidi kukamuliwa na TRA badala ya kufikiria namna ya kuexpand tax base yao na kuhakikisha kodi inalipwa ipasavyo na kwa wakati. Kwa mfano, mtu anayelipa kodi tayari taarifa zake nyingi zipo tayari kwanini benki nayo ijue hadi mtu anafanya kazi wapi? na hata kuhoji "estimated gross annual income"! Well, kama mtu akiandika EAGI halafu ikaonekana anapata fedha nyingi zaidi na akawa target ya TRA si itakuwa mtu kujichongea na badala yake watu wanaweza waka underpresent wanachokipata...
Hili zoezi hasa lina lengo gani kwa mwananchi anayetumia benki katika mazingira ya kawaida? Maana, wapo watu - kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali - wanaobadilisha kiasi kikubwa sana cha fedha nje ya mfumo wa mabenki na hawa hawaguswi!
Tatizo la pili ni kuwa inaonekana inatafutwa njia ya kuzidi kuwakamua na kuwabana law abiding citizens kwa ajili ya kodi na mapato kwa sababu serikali imegundua kuwa tax base yake haikui kwa kiasi kikubwa.
Jamaa yangu huyo alinidokeza (sijaweza kuthibitisha) kuwa VAT registered tax payers hawafiki 20,000 na wale wenye TIN hawazidi milioni moja. Sasa, hawa ndio ambao wanataka kuzidi kukamuliwa na TRA badala ya kufikiria namna ya kuexpand tax base yao na kuhakikisha kodi inalipwa ipasavyo na kwa wakati. Kwa mfano, mtu anayelipa kodi tayari taarifa zake nyingi zipo tayari kwanini benki nayo ijue hadi mtu anafanya kazi wapi? na hata kuhoji "estimated gross annual income"! Well, kama mtu akiandika EAGI halafu ikaonekana anapata fedha nyingi zaidi na akawa target ya TRA si itakuwa mtu kujichongea na badala yake watu wanaweza waka underpresent wanachokipata...
Hili zoezi hasa lina lengo gani kwa mwananchi anayetumia benki katika mazingira ya kawaida? Maana, wapo watu - kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali - wanaobadilisha kiasi kikubwa sana cha fedha nje ya mfumo wa mabenki na hawa hawaguswi!