Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Watanzania walio wengi ikiwa ni pamoja na Wabunge, Viongozi wa ngazi mbali mbali Serikalini, Viongozi wa dini na watu wengine wa kada mbalimbali walitegemea na walikuwa na matumaini chanya katika hotuba ya Waziri Mkuu wakati akilihitimisha Bunge la 10 katika Mkutano wake wa 7 na Kikao chake cha 10 tarehe 23.04.2012, matumaini ambayo yamekuwa tofauti kabisa na mategemeo yao hivyo kupelekea walio wengi kubaki kujiuliza ni nini hatma yaTaifa letu.
Nitaomba nianzie mbali kidogo, ukiacha ile Ibara ya 64(1) ya Katiba (1977) inayoipa Bunge mamlaka na madaraka ya kutunga Sheria, Ibara ya 63(2) ya Katiba inatamka wazi nanukuu "Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."
Katiba hiyo hiyo Chini ya Ibara ya 96(1) inaipa Bunge nguvu ama uwezo, wa kuunda Kamati mbali mbali kwa ajili ya ufanisi wa kazi za Bunge kazi ambazo zimeshatajwa hapo juu. Na bila ya kuathiri masharti ya Ibara 96(1), Kanuni za Kudumu za Bunge (2007), Kanuni ya 115 pia inatambua uwepo wa Kamati za Kudumu za Bunge. Vile vile Kanuni hiyo ya 115 ndiyo inayotambua na kuipa nguvu Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge.
Nyongeza ya Nane ya Kanuni, katika Sehemu yake ya Kwanza inatambua Kamati za Kudumu zisizo za Sekta, Sehemu ya Pili inatambua Kamati za Kudumu za Bunge za Sekta na sehemu ya Mwisho ni ile inayotambua Kamati ya Kudumu za Bunge zinazosimamia Fedha za umma. Ni sehemu ile ya Pili pamoja na ya Tatu ambayo Kamati ya Zitto Zuberi ambaye ni Mwenyekiti pamoja na Wenyeviti wengine wa Kamati mbali mbali za Kudumu za Bunge wamo. Kamati hizi zote chini ya Nyongeza hii ya Nane zimepewa majukumu mahususi juu ya ama Wizara au Sekta mbali mbali ambazo zinapaswa kuzisimamia ipasavyo.
Ni vyema ikatambulika kwamba kazi zinazopewa kamati ni katika kuhakikisha kuwa ile Ibara ya 63(2) ya Katiba inasimamiwa ipasavyo katika kuhakikisha kuwa Bunge inaishauri na kuisimamia Serikali.Wananchi tumeona namna ambavyo Kamati husika zimekuwa zikifanya kazi kwa niaba ya Wananchi waliowatuma humo Bungeni kwa ufanisi na uzalendo mkubwa ila cha kustaajabisha Serikali ambayo inapaswa kusimamiwa na kushauriwa na Bunge kwa kupitia Kamati husika ama imekuwa ikipuuza ushauri utolewao au kulidharau Bunge kwa ujumla wake na hivyo kudhihirisha kutotambua kazi ya Mhimili huu mwingine hivyo kupelekea kuvunja Katiba ambayo Serikali imeapa kuilinda na kuitetea.
Binafsi ningependa kutoa wito, kwa kuwa hata Spika anaonekana kutoona kuwa Bunge linadharauliwa basi Wenyeviti na Wanakamati wao wafanye maamuzi ya kujivua nyadhifa zao Bungeni mara moja ili kulinda heshima zao na za wale waliowatuma. Haiwezekani watu wakafanya kazi nzito namna ile na kutoa ushauri wenye nia njema kwa Taifa lakini hakuna hatua zozote za kutia matumaini zilizo ama zinazoonesha kuchukuliwa. Niwaulize wanakamati;
1. Kuna haja gani ya kuwa na hizo Kamati ambazo ni rubberstamp ??
2. Kuna haja gani wanakamati kukutana Dar es Salaam kwa shughuli ambazo Serikali inaziona ni batili ??
3. Kuna haja gani ya kutoa ushauri na maelekezo ambayo yataendelea kuwekwa kapuni ??
4. Kuna haja gani ya kuendelea kuvumilia Kanuni na Katiba zikivunjwa wazi wazi ??
5. Kuna haja gani ya kuendelea kulidhalilisha na kulidharau Bunge ??
6. Kuna haja gani ya kuendelea kuitwa mwanakamati ilihali kazi uifanyayo inapuuzwa ??
7. Kuna haja gani ya kuendelea kutumia kodi za Watanzania ilihali mafanikio hayaonekani ??
8. Kuna haja gani ya kuendelea kutukanwa na kunyooshewa vidole kwa sababu tu wewe ni mwanakamati uliyeamua kuwasaidia watanzania lakini Serikali isiyowajali Watanzania inakung'ata na kukupuliza ??
9. Kuna haja gani ya kuendelea kuishauri Serikali inayoongozwa kwa Upepo wa Kisiasa ??
10. Kuna haja gani ya kusema Bunge lina Haki na Madaraka ??
SASA BASI;KAMA Anne Semamba Makinda haoni Bunge likidhalilishwa na kudharauliwa, KAMA Anne Semamba Makinda haoni wanakamati wake wakipuuzwa kwa kiwango cha juu, KAMA Anne Semamba Makinda haoni Katiba na Kanuni za Bunge zikivunjwa kwa uhodari na kishujaa BASI NINYI Wanakamati na Wenyeviti wenu oneni hilo na mwonyesheni pia Anne Semamba Makinda hilo mwachieni hizo nafasi ili tuone kama ataweza kuliongoza Bunge pasipo hizo Kamati.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki JF
MEITINYIKU L. Robinson
Nitaomba nianzie mbali kidogo, ukiacha ile Ibara ya 64(1) ya Katiba (1977) inayoipa Bunge mamlaka na madaraka ya kutunga Sheria, Ibara ya 63(2) ya Katiba inatamka wazi nanukuu "Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."
Katiba hiyo hiyo Chini ya Ibara ya 96(1) inaipa Bunge nguvu ama uwezo, wa kuunda Kamati mbali mbali kwa ajili ya ufanisi wa kazi za Bunge kazi ambazo zimeshatajwa hapo juu. Na bila ya kuathiri masharti ya Ibara 96(1), Kanuni za Kudumu za Bunge (2007), Kanuni ya 115 pia inatambua uwepo wa Kamati za Kudumu za Bunge. Vile vile Kanuni hiyo ya 115 ndiyo inayotambua na kuipa nguvu Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge.
Nyongeza ya Nane ya Kanuni, katika Sehemu yake ya Kwanza inatambua Kamati za Kudumu zisizo za Sekta, Sehemu ya Pili inatambua Kamati za Kudumu za Bunge za Sekta na sehemu ya Mwisho ni ile inayotambua Kamati ya Kudumu za Bunge zinazosimamia Fedha za umma. Ni sehemu ile ya Pili pamoja na ya Tatu ambayo Kamati ya Zitto Zuberi ambaye ni Mwenyekiti pamoja na Wenyeviti wengine wa Kamati mbali mbali za Kudumu za Bunge wamo. Kamati hizi zote chini ya Nyongeza hii ya Nane zimepewa majukumu mahususi juu ya ama Wizara au Sekta mbali mbali ambazo zinapaswa kuzisimamia ipasavyo.
Ni vyema ikatambulika kwamba kazi zinazopewa kamati ni katika kuhakikisha kuwa ile Ibara ya 63(2) ya Katiba inasimamiwa ipasavyo katika kuhakikisha kuwa Bunge inaishauri na kuisimamia Serikali.Wananchi tumeona namna ambavyo Kamati husika zimekuwa zikifanya kazi kwa niaba ya Wananchi waliowatuma humo Bungeni kwa ufanisi na uzalendo mkubwa ila cha kustaajabisha Serikali ambayo inapaswa kusimamiwa na kushauriwa na Bunge kwa kupitia Kamati husika ama imekuwa ikipuuza ushauri utolewao au kulidharau Bunge kwa ujumla wake na hivyo kudhihirisha kutotambua kazi ya Mhimili huu mwingine hivyo kupelekea kuvunja Katiba ambayo Serikali imeapa kuilinda na kuitetea.
Binafsi ningependa kutoa wito, kwa kuwa hata Spika anaonekana kutoona kuwa Bunge linadharauliwa basi Wenyeviti na Wanakamati wao wafanye maamuzi ya kujivua nyadhifa zao Bungeni mara moja ili kulinda heshima zao na za wale waliowatuma. Haiwezekani watu wakafanya kazi nzito namna ile na kutoa ushauri wenye nia njema kwa Taifa lakini hakuna hatua zozote za kutia matumaini zilizo ama zinazoonesha kuchukuliwa. Niwaulize wanakamati;
1. Kuna haja gani ya kuwa na hizo Kamati ambazo ni rubberstamp ??
2. Kuna haja gani wanakamati kukutana Dar es Salaam kwa shughuli ambazo Serikali inaziona ni batili ??
3. Kuna haja gani ya kutoa ushauri na maelekezo ambayo yataendelea kuwekwa kapuni ??
4. Kuna haja gani ya kuendelea kuvumilia Kanuni na Katiba zikivunjwa wazi wazi ??
5. Kuna haja gani ya kuendelea kulidhalilisha na kulidharau Bunge ??
6. Kuna haja gani ya kuendelea kuitwa mwanakamati ilihali kazi uifanyayo inapuuzwa ??
7. Kuna haja gani ya kuendelea kutumia kodi za Watanzania ilihali mafanikio hayaonekani ??
8. Kuna haja gani ya kuendelea kutukanwa na kunyooshewa vidole kwa sababu tu wewe ni mwanakamati uliyeamua kuwasaidia watanzania lakini Serikali isiyowajali Watanzania inakung'ata na kukupuliza ??
9. Kuna haja gani ya kuendelea kuishauri Serikali inayoongozwa kwa Upepo wa Kisiasa ??
10. Kuna haja gani ya kusema Bunge lina Haki na Madaraka ??
SASA BASI;KAMA Anne Semamba Makinda haoni Bunge likidhalilishwa na kudharauliwa, KAMA Anne Semamba Makinda haoni wanakamati wake wakipuuzwa kwa kiwango cha juu, KAMA Anne Semamba Makinda haoni Katiba na Kanuni za Bunge zikivunjwa kwa uhodari na kishujaa BASI NINYI Wanakamati na Wenyeviti wenu oneni hilo na mwonyesheni pia Anne Semamba Makinda hilo mwachieni hizo nafasi ili tuone kama ataweza kuliongoza Bunge pasipo hizo Kamati.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki JF
MEITINYIKU L. Robinson