Zitto umewadhalilisha Wabunge wa Viti Maalum CDM; Waombe Radhi

Hata mimi sioni ubaya wa maneno ya Zitto..
Watanzania tuna ustaarabu wetu wa lugha na matumizi yake. Majibu yalikuwa safi kabisa kwa mhusika kwani aloanza maneno haya sii Zitto. Nachopenda na kufurahia ni uwezo wa viongozi wa Chadema kuwa mbele ktk kujibu maswali na unapoleta uhuni unapewa dawa! Na nampenda Zitto kwaq kutomung'unya maneno. Ujasiri na kiburi chake kinahitajika sana na hakika tunamuhitaji mtu kama yeye ktk nafasi muhimu.

Mbunge wa viti maalum ni kuzawadiwa hilo halina ubishi tena kama umejiunga hivi karibuni ndio kabisa inatakiwa ukae kimyaa maanake hujui! na kutojua sii tusi bali ni usia mzuri kwa viongozi wageni wapate kujifunza kuheshimu viongozi wao. Zitto ni naibu katibu wa chama, na lugha inayotumiwa na baadhi ya vijana wa Chadema hapa JF nadhani inavuka mpaka wa heshima wakati wao wamemkabidhi mamlaka hayo..

Kwa hiyo mtu akijiunga na CDM kwa mara ya kwanza ni sawa kumwita wa kuja? Unaona ni sawa kwa Naibu Katibu wa Chama Kukuu cha upinzani kuwaita wanachama wake wapya ni wa kuja? Ingekuwaje hapa kama Pius Msekwa amewaita wanachama wapya wa CCM wa kuja. I am sure hii thread ingekuwa na pages 30 by now. Nilidhani Chadema ni wanachama bila kubaguana. Kumbe chama kilikuwa kina recruit wanachama wa kuja huko mikoani. Kwa hiyo wanachama wa siku nyingi wanakuwa treated tofauti na wanachama wa kuja? Huku sio kubaguana na kujenga matabaka ya wanachama? Wanachama wa zamani na wale wa kuja? Kwa vile umesema Mh Zitto hajamung'unya maneno, ina mana aliyosema ni kweli sio. Siungi mkono kuwepo kwa wabunge sijui wa viti maalumu, lakini the way Mh Zitto alivyoiandika hili suala, well I will better keep my mouth shut.
 
Ukipiga hesabu ya wabunge wanaoteuliwa na wengine kupita kupingwa utashangaa aian ya democracy tuliyo nayo.Ndiyo maana kuna post moja nilikuwa nimetoa suggestion kwamba kama tukiwa na federal system basi Bicameral parliament haitaepukika na pengine hapo tunaweza kuunda structure nzuri ya uwakilishi na ya demokrasia ya kweli kama INDIA,US,Switzerland etc.

Najaribu kutafakari aina hii ya Demokrasia ambayo Executive kama mhimili wa Dola unapata mwanya mkubwa wa kuingilia bunge kwa teuzi holela tu za wabunge,unategemea nini kutoka kwenye mhimili wa mmoja kuuwajibisha mwingine na kuusimamia?Kwa hiyo sisi kama Taifa huu mjadla unaweza kuwa mpana zaidi

Hilo fungu la wabunge wengi wa viti maalumu ambao hata kazi yao haipo consistent na dhumuni la kuwa na bunge au dhana nzima ya parliamentary system ni bora lingetumika vizuri kwa kupanua wigo wa uwakilishi kwa kuunda Rotating pyrammid like structure of representative kwa kusogeza uwakilishi zaidi kwa councillors/madiwani ili tuwe na Demokrasia ya pekee,vinginevyo tutaishia kuwa na udikteta wa mhimili(pillar dictatorship or totalitarian).Wale disadvateged group wataweza kuwakilishwa vizuri zaidi na kujenga uwakilishi uliokusudiwa kwa haki ya walipa kodi na katika utekelezaji wa dhamira ya kweli ya uhuru wa mawazo na uwakilishi uliotukuka kwa wananchi wake. nPengine tungeweza kuwa mfano wa kuandiaka theory mpya ya uwakilishi

 
Mkuu nadhani hukunielewa mantiki ya matumizi ya neno Kiburi kama nilivyolielezea.

Sii viongozi wote wana kiburi kwa nia njema lakini wapo wachache na Zitto ni mmojawapo. Kama unakumbuka Zitto ktk kiburi chake aliwahi fukuzwa bungeni kwa kuhoji mkataba wa Buzwagi na akasema UKWELI ambao spika na wabunge hawakuupenda, ya kwamba waziri Karamagi aliweka mkataba huo hotelini London kinyume cha sheria! pamoja na yote hayo mwisho wa siku ukweli ulikuwa bayana na kumlazimu Karamagi kujiuzuru. Majuzi pia Zitto tena ktk kiburi chake akiwakilisha hoja ya Posho umeliona sakata lake. Na unakumbuka vitisho vya spika Kilango dhidi ya Zitto, na Zitto akasema yuko tayari kurudishwa Kigoma akavue dagaa, na kwa kuthibitisha hayo - Zitto alikuwa mtu wa kwanza kuachia Posho hizi hata kama watamsema vibaya.

Uthubutu wa kijasiri na kiburi cha kuweza kuwakilisha hoja na ukaweza kuisimamia hata kama utapigwa vita ndio sifa nayoizungumzia kwa sababu sii rahisi kuwapata watu kama Zitto ktk bunge letu. Wengi wanathubutu kukosoa lakini wepesi wa kupokea maamuzi dhidi ya hoja zao kwa sababu hawana nia haswa ya kuhakikisha hoja zao zinachukuliwa maanani..

Kwangu ningependa kutumia maneno kama 'ujasiri na uthubutu' au 'ujasiri na msimamo' kuliko kutumia neno 'kiburi' ambalo lazima nilitolee maelezo ya ziada kueleweka kuwa linamaanisha positively.

Zitto kama binaadamu ana mapungufu yake, na moja kubwa ninaloliona ni ukosefu wa kiasi na uwezo wa kupima cha kusema anapozungumza kwenye hadhira zisizokuwa rasmi. Maneno yake kwenye FB, JF, Vipindi vya burudani kwenye redio, yamekuwa yakileta utata mara kwa mara. Ni wakati wa kujifunza kuwa Ubunge hauvuliwi akitoka 'mjengoni' na anachokisema chochote wakati wowote kitapimwa kwa mizania ile ile ya bungeni. Na kwake ni zaidi kwa sabau ni kiongozi wa ngazi ya juu kwenye chama.

Hata kama alimjibu Marytina ambae alimprovoke, jibu alilolitoa kwake limejeruhi wengine wa wanaoamini kwenye mfumo wa viti maalum pia. Tutasema watu wako too sensitive, hiyo ni kweli, lakini he should know better, mengine ni kujitafutia sababu za kulaumiwa tu.
 
Haya mada imehamia ktk viti maalum...
Hili kweli ni donda na linatakiwa kupatiwa dawa lakini sii kwa vigezo vya kuondoa viti hivi kwa sababu wamepewa wanawake. haya yatakuwa ni makosa kwa sababu zipo sababu muhimu za kuwawezesha wanawake ambao kwa muda mrefu wameachwa nyuma ktk kupewa nafasi za uwakilishi yaani kukaa meza moja na wanaume.

Makosa yapo ktk idadi na wanawakilisha vitengo gani? haya maswala ya kuwa na wabunge vivuli kwa sababu tu tunatazama idadi ya wabunge wanaume bungeni ni kuwadhalilisha zaidi wanawake. Ila idaid ipunguzwe na wateuliwe wabunge toka Taasisi tofauti kuwakilisha pengine taasisi za kijumuiya ambako itawafanya wanawake wengi wakijiunge na taasisi hizi iwe uzazi wa majira, HIV, malezi ya watoto, Lishe, elimu ya vidudu na kadhalika yaani vitu ambavyo ktk mila na desturi zetu wanawake wamekuwa wakiachwa nje ya mijadala hiyo hali wao ndio wako karibu zaidi ya matatizo hayo.
Kama rais anaweza kuchagua wabunge 10 ambao anajua atawatumia ktk utendaji kazi wake basi na wabunge wa viti maalum pia watoke ktk sekta ambazo tunajua watasimama kuzitetea au kuziboresha.
 
Duh!! Tatizo watu wanapenda kuchekewa ckewa tu!!!
Napenda watu wasio mung'unya maneno kama Zitto!!!

Hiyo sio kumung'unya maneno bali ni kiburi. Kama unaona ni sawa kuwaita wanachama wake wapya wa kuja then, you may probably be right.
 
Nimefuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea hapa JF uliokuwa ukijadili kuhusu Zitto,JK VS gazeti la tanzania daima na mmiliki wa gazeti hilo amabye ni Mbowe. Kuna mengi yamesemwa lakini lililoniku na hili la huyu Naibu Katibu Mkuu wa CDM Zitto Kabwe.Katika kujitetea na kuhamishia lawama kwa wenzake kiongozi huyu ninayemuamini miaka yote tangu nimemfahamu amewadhalilisha na kuwadharau wanachama wapya wa CDM.Naomba ninukuhuu maneno yake hapa chini wakati akimjibu mchangiaji mmoja kwenye ile thread.

[Ha ha ha ha ha ha. Kwi kwi kwi! Unanifanya nicheke kijuha juha na maneno yako.Chadema ni chama cha kidemokrasia na kitabaki hivyo. Sisi tulio ndani ya chama hiki toka kianze ndio tunajua utamaduni wa chadema. Wewe kwa kuwa ni wa kuja na ukazawadiwa ba Ubunge lazima useme hayo unayosema.Napenda nirudie kusema sina umri wa kugombea Urais kwa sasa. Nitamwunga mkono mgombea Urais wa CHADEMA atakayepitishwa ba vikao vya chama wakati utakapofika. Kwa sasa hakuna mgombea Urais CHADEMA na mie wala sioti kuwa mgombea. Kama uropokaji huu unatokana na Urais, mie simo. Kwamba sitaweza kuwa kama ningekuwa nina vigezo, unajidanganya tu na unajua unajidanganya. Chadema ni wanachama. Bring a free and fair election uone! ]

maneno haya ni ya dhihaka kubwa na hayakupaswa kuongelewa na kiongozi kama yeye tegemeo la taifa kwasababu zifuatazo
1. Zitto unaposema kuwa yeye ni mwananchama wa siku nyingi na wenzake ni wakuja ni dharau kubwa kwa wanachama wapya.Anamaanisha kuwa wanachama wazamani ndio wanajua zaidi utamaduni wa chama kuliko wapya na hawastahili kuhoji ukiukwaji wa tamaduni hizo zinapofanywa na wanachama wa zamani.Zitto unapaswa kuwaomba radhi wanachama hawa wapya.

2. Zitto unaposema kwa huyo aliyekujibu kuwa ni wakuja na amezawadiwa Ubunge ndio maana akaksema livyosema unamaanisha kuwa Wabunge wa CDM wamezawadiwa viti maalum-kauli hii ikitoka kwa kiongozi kama wewe maana yake ni kuwa vitimaalum CDM ni zawadi na hivyo waliopata wamepewa zawadi.Unatumaanisha nini sisi tuliogombea nahatukabahtaika kupata nafasi hizo?kuwa kumbe wenzetu walipewa zawadi?nilikuwa mgombea kwenye mchakato ule na baadaye tulitangaziwa vigezo kuwekwa ili watu wapite kwa vigezo ili kuepusha rushwa iliyotaka kufanyika aabayo iliasisiwa na wewe ndani ya chama,ulitumia pesa nyingi sana ili watu wako washinde. Zitto acha kupotosha umma,usikiharibu chama chako unapaswa kukijenga.Maneno kama hayo hayapawsi kusemwa na mtu kama wewe,ulishiriki kwenye mchakato wa kuwapata,unajua vigezo,mama yako alikuwepo kwenye kamati,rafiki yako Dk Kitilla alikuwa Mwenyekiti wa Kamati.Tueleze hawa wabunge walizawadiwaje?je ni mama yako,ni wewe,ni Kitilla,ni Dk Slaa,ni Mbowe tuambieni na sisi ambao hatkupata ili mwaka 2015 tujipange vizuri.

Zitto unapaswa kuomba radhi wabunge hawa waliopita kihalali kwa vigezo.

Nawasilisha.

Firstlady kumbuka unaandika mada itakayosomwa na ma-great thinkers na si watu wa vijiweni. Great thinker yeyote atakayeperuzi kwa makini thread yako atagundua uchochezi na ushari uliojificha kwa lengo la kuwachonganisha wana CHADEMA. Umeanza kwa kusema ati gazeti la Tanzania Daima ni la Mbowe(Tazama kwenye red), una ushahidi wowote? Kama unao uuwasilishe; maana tumeshachunguza mpaka kwa msajili wa magazeti na kuwafahamu wamiliki wa gazeti hilo na si Mbowe. Pili mtu yeyote makini atabaini hakuna lolote la kuwadhalilisha wabunge wa viti maalum wa CHADEMA hapo, kwani wabunge wa viti maalum si wa CHADEMA peke yao, wapo pia wa vyama vingine CCM ikiongoza kwa uwingi. Halafu kuna ubaya gani kwa Zito kujitambulisha kama mwanachama wa siku nyingi na kunadi kwamba hana ndoto za kugombea urais na kwamba wanaonadi hivyo ni wakuja? Kwani wewendiye msemaji wa waliotajwa hapo? au una maslahi yepi zaidi ya ukuwadi wa kijana mdogo asiye hata na adabu mbele ya wazee yule wa magamba magamba mlevi wa mvinyo wa ufisadi? Mwisho kabisa umeshindwa kufafanua alikuwa akiongea katika mazingira yepi na alimlenga nani katika statement hiyo kama ni kweli aliitamka zaidi ya generalized statement yenye kila dalili ya umbeya, uchonganishi na ushambenga kama ilivyo desturi ya CCM. Kawaambie waliokutuma kwamba umebainika na kamwe hawadanganyiki.
Mungu ibariki Tanzania, laana na kifo kwa mafisadi wote.
 
Hiyo sio kumung'unya maneno bali ni kiburi. Kama unaona ni sawa kuwaita wanachama wake wapya wa kuja then, you may probably be right.


EMT dawa ya moto sometime ni moto. Mfano mi nakujua wewe au gajin, au mushi na wengine kutokana na michango yao. Ikitokea siku ukanimbia neno baya nitaelewa kuwa EMT kateleza au I will take it easy sababu ni EMT. Lakini kuna na watu hapa JF kwa tathmini zangu nakuhakikishia peaceful diplomacy dont work to them . bila kuwajibu kwa style yao wanayoilewa hawakuelewi.........

So am giving benefit of the duoubt zitto. kuwa za japo kuna waunge wakuja wengi tuuu CDm sio wote ziito anaweza kuwaita hivyo. Huyo amuita hivyo sababu anamjua na bila kumpa majibu ya kiburi basi hawaelewi. Am trying trying to walk in zitto's shoes. sioni kama kuna tatizo.

Yes ziito ana mapugufu yake kama wote tulivyo. But i dont expect ziito awe angel kwa kila mwana CDM. I dont expect ziito awe na static characteristics kwa kila mtu wakati watu wewnyewe tuko tofauti tfauti.

I dont expect mwan cha chadema anatumia alias kuja kumachambua ziito au ana mu expose ziito in a negative way. Mind you ni mwana CDM na zito inawezekana anamjua. watu tunaanza akumshambulia zito. Then yeye ziito eti akae kimya akayamalize kwenye chama . Duh kama kuwa kiongozi wa CDM ndio hivi basi ni sawa na kuwa kifungoni.

Hao wanamshambulia na kumkosoa na umkanya na kutisha openly hamuangaliiii syntax na semantics zao but ziito akijibu ndio tunachambua sarufi na vivumishi vyote alivyotumia.

Chadema Kuna tatizo thanks mzigo wa hilo tatizo kwa sasa umejificha nyuma ya kivuli cha ziito but................

Sisi hapa ni kama yule dr ricky machumbuzi wa football unaweza kuelezea mpira vizuri baada ya mapunziko au baada ya mpira kwisha. but bila kujiweka kwenye position, pressure na mazigira ya wachezaji huwezi kuwa fair katika uchambuzi wa football.
 
Ukipiga hesabu ya wabunge wanaoteuliwa na wengine kupita kupingwa utashangaa aian ya democracy tuliyo nayo.Ndiyo maana kuna post moja nilikuwa nimetoa suggestion kwamba kama tukiwa na federal system basi Bicameral parliament haitaepukika na pengine hapo tunaweza kuunda structure nzuri ya uwakilishi na ya demokrasia ya kweli kama INDIA,US,Switzerland etc.

Najaribu kutafakari aina hii ya Demokrasia ambayo Executive kama mhimili wa Dola unapata mwanya mkubwa wa kuingilia bunge kwa teuzi holela tu za wabunge,unategemea nini kutoka kwenye mhimili wa mmoja kuuwajibisha mwingine na kuusimamia?Kwa hiyo sisi kama Taifa huu mjadla unaweza kuwa mpana zaidi

Hilo fungu la wabunge wengi wa viti maalumu ambao hata kazi yao haipo consistent na dhumuni la kuwa na bunge au dhana nzima ya parliamentary system ni bora lingetumika vizuri kwa kupanua wigo wa uwakilishi kwa kuunda Rotating pyrammid like structure of representative kwa kusogeza uwakilishi zaidi kwa councillors/madiwani ili tuwe na Demokrasia ya pekee,vinginevyo tutaishia kuwa na udikteta wa mhimili(pillar dictatorship or totalitarian).Wale disadvateged group wataweza kuwakilishwa vizuri zaidi na kujenga uwakilishi uliokusudiwa kwa haki ya walipa kodi na katika utekelezaji wa dhamira ya kweli ya uhuru wa mawazo na uwakilishi uliotukuka kwa wananchi wake. nPengine tungeweza kuwa mfano wa kuandiaka theory mpya ya uwakilishi

Mkuu how would you write a new theory of representative wakati our politicians are branding the people they would be representing wa kuja? Lets stick to the thread. Kuna issue mbili hapa. Issue ya kwanza ni ile ya ubngue wa kuzawadiwa. Hili halina mjadala. Issue ya pili ni ile Mh Zitto kawaita wanachama wapya wa Chadema wa kuja. Ana create matabaka kati ya according to him "sisi tulio ndani ya chama hiki toka kianze"na wale "wa kuja". kwa hito yeye kajiweka kwenye kundi la walio ndani ya Chadema toka kianze na wanachama wapya kama akina Pro Safari na wale wote walijiunga na Chadema hivi karibuni kama watu wa kuja. Is that right?

We all know that a multi-tiered level of parties has been created, with those at the top continually enhancing and protecting their position of privilege and power. This is exactly what Hon Zitto is trying acknowledging by calling new party members wa kuja. What he has said is not unlocking new party members. He is not unguesting new party members. he trying to lock them out.

We have been complaining here about unequal treatment of political parties in the country. The unequal treatment of political parties is one of several methods used by the ruling elite to obstruct and discourage the participation of Tanzanina in political affairs beyond that of casting a vote. What Hon. Zitto is trying to unveil is that this happens even within a particular political party like Chadema. That there those members who control the party and the so called "wakuja".

Hon Zitto's remarks is just another reflection of the marginalization of the electors within political parties. The current state of political party affairs and the discrimination faced by new members makes a mockery of the text-book teachings that tell civic-minded individuals they should join political parties if they want to have a say in how the country is being run or form their own if they don't like the existing parties.

So, whilst we complain that opposition parties are marginalised, party members within the parties are also totally marginalized. They do not even exercise control over the decisions taken by their own party conventions. I believe Chadema's support comes particularly from its new followers who want the party represent them in fighting for their visions of how this country should be governed. But if one of its top leader brands them as "wakuja" then I don't think even the writing of the new representative theory will ever be achieved.
 
zitto hata kama umri ungeruhusu hana sifa za kugombea urais kupitia CDM LABDA ccm au NCCR.zitto anataka kumaanisha KITILIA NKUMBO alitoa upendeleo ???? Zitto,Zitto kuna siku utauza watanzania
Majibu yako c ya mtu aliyekomaa kisiasa, una kurupuka na huna subira. Ndio maana Zitto kasema umezawadiwa Ubunge, hebu 2ambie sifa za mgombea urahisi CDM ambazo Zitto hana? Au lazima atoke upande fulani wa nchi hii?
 
Haya mada imehamia ktk viti maalum...
Hili kweli ni donda na linatakiwa kupatiwa dawa lakini sii kwa vigezo vya kuondoa viti hivi kwa sababu wamepewa wanawake. haya yatakuwa ni makosa kwa sababu zipo sababu muhimu za kuwawezesha wanawake ambao kwa muda mrefu wameachwa nyuma ktk kupewa nafasi za uwakilishi yaani kukaa meza moja na wanaume.
Makosa yapo ktk idadi na wanawakilisha vitengo gani? haya maswala ya kuwa na wabunge vivuli kwa sababu tu tunatazama idadi ya wabunge wanaume bungeni ni kuwadhalilisha zaidi wanawake. Ila idaid ipunguzwe na wateuliwe wabunge toka Taasisi tofauti kuwakilisha pengine taasisi za kijumuiya ambako itawafanya wanawake wengi wakijiunge na taasisi hizi iwe uzazi wa majira, HIV, malezi ya watoto, Lishe, elimu ya vidudu na kadhalika yaani vitu ambavyo ktk mila na desturi zetu wanawake wamekuwa wakiachwa nje ya mijadala hiyo
Hili la Zitto kutoa kauli zisizo na ulinganifu, zenye utata na wakati mwingine kusahau nafasi yake katika jamii linamletea matatizo na litakuwa na matatizo mbele ya safari. Nadhani communication skills zake zinahitaji review, na anahitaji ushauri zaidi kumsaidia. Ni ushauri tu!!!!

Kuhusu viti maalumu, nashangaa bunge la 320+, 1/3 ni wabunge wa viti maalumu!! Sijui wanamwakilisha nani. Dhana ya viti maalumu tunaiga kutoka nchi za Scandinavia na imepigiwa upatu sana na Kikwete kwasababu wanawake ni electorate college yake kubwa. Hakuwa na sababu yoyote ile ya msingi bali kutojiamini ukizangia aliingia Ikulu kwa misaada ya mrafiki n.k

Kama tulihitaji viti maalumu vingi kiasi hicho basi wakati wa mwalimu tungeona. Nchi kama Marekani pamoja na maendeleo yake hakuna hiki kitu vitu maalumu halikadhali UK, na kama vipo basi ni kwa mantiki iliyo dhahiri. Sisi tunadhani tumekuwa kidemokrasia kuliko India, Brazil au Ujerumani.

Kama wangekuwa wanasimamia masilahi ya akina mama tungewasikia wakigomea bajeti na posho za hovyo ili pesa zielekezwe kwenye shule na hospitali. Badala yake Mbunge kama Zarina Madabida CCM anasema posho ziongezwe.Wao wapo kwa ajili ya vyama vyao, lakini kura zao zina athari kubwa kwa mustakabali wa nchi. Katika mambo ninayotaka yafutiliwe mbali ni haya ya viti maalumu na uteuzi wa wabunge utokanao na rais.

Kuhusu maeneo maalumu, Mukandara nakubaliana kuwa bado tunaweza kuwa na wabunge wawakilishi wa makundi yenye interest kwa utaratibu wa ushindani na sio kuteuliwa , idadi yao iwe kitaifa, mfano mbunge wa walemavu mmoja kwa taifa.

Nina amini kabisa wanawake wanaweza, mbona akina Mdee, Kilango, Shelukindo,Makinda n.k wamepambana na wameshindawamewanaume? Si tumeona akina Regia walivyopambana na kubadili mwelekeo wa siasa za Kilombero, ngome ya CCM!! Hivi kuna jimbo hot kuzidi kawe ! Wengi wanabweteka wakijua kuna viti maalumu.
Njia ya kumkomboa mwanamke ni Elimu. Tuhakikishe wanapata elimu na kuhakikisha wanapata fursa sawa ya ushindani.

Hakuna mahali positive affirmative action imeleta matokeo yaliyokusudiwa haraka na kuna wakati kutotokea kabisa. Miaka ya 60 Wamasai /Wabarebeig n.k walipewa upendeleo kielimu, leo miaka 40 bado hali yao si nzuri. Kuondoa mtihani wa taifa kulilenga kutoa fursa sawa na kutoa upendeleo kwa baadhi ya sehemu, miaka 30 baadaye bado mikoa iliyokuwa mbele ipo mbele.

Wapiga kura wengi ni wanawake na nadhani wanatumia haki yao ya kuchagua kiongozi na si jinsia. Kutoa upendeleo ni kuwadhalilisha kwani hakuna utaifiti wowote unaoonyesha kuwa wanaume wana uwezo wa kufikiri kuliko wanawake kimantiki.

Hivi tatizo letu ni umasikini,ujinga njaa na maradhi au ni jinisia!! Je baada ya kuwa na wabunge 100 wa viti maalumu, wamewezaje au wamethibitishaje kuwa uwepo wao na wingi wao umeleta mabadiliko kwa mwanamke anayejifungulia sakafuni pale Temeke, anayebeba ndoo ya maji Km 10 Namtumbo, asiyeweza kupeleka watoto shule ili wakalime kule Handeni n.k
 
Viti maalum havina tija, Mwanamke anaetaka ubunge aende majimboni akagombee, badala ya kutetea maslahi ya Taifa wapo pale kupiga kelele za kutetea maslahi ya waliowaweka na hasa 'waliozawadiwa' huo ubunge.
Alichosema Zitto ni ukweli na utabaki kuwa hivyo, whatever u choose 2judge him ila ndiye Mbunge pekee aliyesimamia kauli yake hata alipoona tishio la ban mbele yake hakukwepesha msimamo juu ya sitting allowance za wabunge, wala kufuta kauli juu ya Buzwagi, na ni hoja zake za Msingi zilizochangia kwa kiasi kikubwa CHADEMA kupata kura nyingi kwenye uchaguzi Mkuu, kura zilizowasaidia hata hao 'wazawadiwa kupata ubunge'.
 
Hata mimi sioni ubaya wa maneno ya Zitto..
Watanzania tuna ustaarabu wetu wa lugha na matumizi yake. Majibu yalikuwa safi kabisa kwa mhusika kwani aloanza maneno haya sii Zitto. Nachopenda na kufurahia ni uwezo wa viongozi wa Chadema kuwa mbele ktk kujibu maswali na unapoleta uhuni unapewa dawa! Na nampenda Zitto kwaq kutomung'unya maneno. Ujasiri na kiburi chake kinahitajika sana na hakika tunamuhitaji mtu kama yeye ktk nafasi muhimu.

Mbunge wa viti maalum ni kuzawadiwa hilo halina ubishi tena kama umejiunga hivi karibuni ndio kabisa inatakiwa ukae kimyaa maanake hujui! na kutojua sii tusi bali ni usia mzuri kwa viongozi wageni wapate kujifunza kuheshimu viongozi wao. Zitto ni naibu katibu wa chama, na lugha inayotumiwa na baadhi ya vijana wa Chadema hapa JF nadhani inavuka mpaka wa heshima wakati wao wamemkabidhi mamlaka hayo..

Baba/babu misimamo yako huwa haieleweki whe it comes to Zitto.Unatetea makosa ya wazi aliyoyafanya ambayo jana ulikuwa unaona amekosea.Duu huna haya baba mzima hueleweki.
 
EMT dawa ya moto sometime ni moto. Mfano mi nakujua wewe au gajin, au mushi na wengine kutokana na michango yao. Ikitokea siku ukanimbia neno baya nitaelewa kuwa EMT kateleza au I will take it easy sababu ni EMT. Lakini kuna na watu hapa JF kwa tathmini zangu nakuhakikishia peaceful diplomacy dont work to them . bila kuwajibu kwa style yao wanayoilewa hawakuelewi.........

So am giving benefit of the duoubt zitto. kuwa za japo kuna waunge wakuja wengi tuuu CDm sio wote ziito anaweza kuwaita hivyo. Huyo amuita hivyo sababu anamjua na bila kumpa majibu ya kiburi basi hawaelewi. Am trying trying to walk in zittos his shoes. sioni kama kuna tatizo

Yes ziito ana mapugufu yake kama wote tulivyo. But i dont expect ziito awe angel kwa kila mwana CDM. I dont expect ziito awe na static characteristics kwa kila mtu wakati watu wewnyewe tuko tofauti tfauti.

I dont expect mwan cha chadema anatumia alias kuja kumachambua ziito au ana mu expose ziito in a negative way. Mind you ni mwana CDM na zito inawezekana anamjua. watu tunaanza akumshambulia zito. Then yeye ziito eti akae kimya akayamalize kwenye chama . Duh kama kuwa kiongozi wa CDM ndio hivi basi ni sawa na kuwa kifungoni.

Hao wanamshambulia na kumkosoa na umkanya na kutisha openly hamuangaliiii syntax na semantics zao but ziito akijibu ndio tunachambua sarufi na vivumishi vyote alivyotumia.

Chadema Kuna tatizo thanks mzigo wa hilo tatizo kwa sasa umejificha nyuma ya kivuli cha ziito kutokana but................

Sisi hapa ni kama yule dr ricky machumbuzi wa football unaweza kuelezea mpira vizuri baada ya mapunziko au baada ya mpira kwisha. but bila kujiweka kwenye position, pressure na mazigira ya wachezaji huwezi kuwa fair katika uchambuzi wa football.

Mkuu,

I have great respect for Hon. Zitto lakini kwa hili kuita wanachama wapya wa CDM wa kuja sitamuunga mkono. Never. Nakubali dawa ya moto ni moto na sometimes inabidi utumie force lakini kuna repercussion zake. Mh Zitto, wewe, Gainjin na mimi tunaweza kuwa level moja hapa JF, lakini Mh Zitto ni public figure. As a public figure one would expect some form of behaviors hasa pale anapokuwa kwenye public domain.

Kweli kama binadamu wengine Mh Zitto ana mapungufu yake lakini does this excuse him kuita wanachama wapya wa Chadema wa kuja? Kama anamjua si angeenda kumwambia tuu in private? Unakumbuka yaliyomkuta Gordon Brown baada ya kumwita mwanachama mwanamke wa chama chke a "bigot"? Tena alisema hili in private lakini huenda ndio iliyomcost kwenye uchaguzi. I am sure kama tungekuwa na tabloid media hapa Bongo, front pages zingekuwa na headings "Zitto amwita mwanachama wa Chadema wa kuja".

Imagine kama kulikuwa na mtu analiyetaka kujiunga na Chadema because of being impressed na Mh Zitto bungeni apitie hapa, amkute huyo huyo Zitto anaita wanachama wapya wa kuja. Atajiunga na Chadema kweli? Inawezekana kabisa kuwa alichokuwa anaonyesha Zitto ni matabaka ya wanachama ndani ya Chadema wakati chama kinatambuka kama chama cha wanachama.

Juzi juzi tuu hapa watu walikuwa wanamuunga mkono Mh Mbowe kwa kutokwenda mahakani japokuwa alikuwa amefanya kosa. Leo hii Mh Zitto ana brand wanachama wapya wa kuja na tunataka kuumunga mkono on the ground kuwa ana mapungufu yake, nk. Mkuu hapana. Hata siku moja wrong plus wrong haiwezi kuwa right na haitakuwa.
 
CHADEMA is not a political party, it is rather a clique of lawbreakers organised by gangster leaders. Its ways and ideologies virtually resemble those of TALIBAN. The sole difference between the two is, while Taliban lives on drug trafficking and double dealing, CHADEMA's survival relies on VANDALISM.
 
Si condone maneno ya kiburi aliyoyatoa Zitto na wala sikubaliani na Mkandara kupongeza kiburi cha viongozi.

Lakini ukweli unasimama kuwa viti maalum ni zawadi za chama kwa wapenzi wao. Na kama ni mfuatiliaji mzuri suala la vigezo lilikwisha jadiliwa hapa sana. Kuwa model iliyotumiwa na Kitila, kulikuwa na uwezekano wa kutizama wanaotakiwa "kuzawadiwa" kwanza, kisha akaweka vigezo, ili kuhakikisha hao wanaotakiwa kuzawadiwa wanafanikiwa kwenye hilo. Kwa hiyo uliposhindwa vigezo inaweza kumaanisha kuwa hukuwa na vigezo stahili kuzawadiwa.

Lakini FirstLady unanishangaza kumpinga Zitto kwa kuhujumu chama lakini wewe kufanya kile kile. Hapo kwenye maelezo ya Zitto alitoa rushwa unadhani upo katika kukijenga chama? Kuwa Zitto alitoa rushwa ili watu wake wapite na ikajuulikana wazi mpaka mfumo kubadilishwa lakini bado anaendelea kuwa nafasi ya juu kwenye chama, hii inakipa chama credibility ya aina gani?

Acha wivu wewe,vaa sketi nawewe ili uzawadiwe Ubunge kama ubunge unazawadiwa.Wacha Vitimaalum viwepo ili nasisi tunaotaka kuingia tuupate.Abarkiwe aliyeleta wazo la vitimaalum.Mtapiga kelele habari ndio hiyo.Hilo ni takwa la SADC.Wivu tu..
 
Mkuu,I have great respect for Hon. Zitto lakini kwa hili kuita wanachama wapya wa CDM wa kuja sitamuunga mkono. Never. Nakubali dawa ya moto ni moto na sometimes inabidi utumie force lakini kuna repercussion zake. Mh Zitto, wewe, Gainjin na mimi tunaweza kuwa level moja hapa JF, lakini Mh Zitto ni public figure. As a public figure one would expect some form of behaviors hasa pale anapokuwa kwenye public domain. Kweli kama binadamu wengine Mh Zitto ana mapungufu yake lakini does this excuse him kuita wanachama wapya wa Chadema wa kuja? Kama anamjua si angeenda kumwambia tuu in private? Unakumbuka yaliyomkuta Gordon Brown baada ya kumwita mwanachama mwanamke wa chama chke a "bigot"? Tena alisema hili in private lakini huenda ndio iliyomcost kwenye uchaguzi. I am sure kama tungekuwa na tabloid media hapa Bongo, front pages zingekuwa na headings "Zitto amwita mwanachama wa Chadema wa kuja". Imagine kama kulikuwa na mtu analiyetaka kujiunga na Chadema because of being impressed na Mh Zitto bungeni apitie hapa, amkute huyo huyo Zitto anaita wanachama wapya wa kuja. Atajiunga na Chadema kweli? Inawezekana kabisa kuwa alichokuwa anaonyesha Zitto ni matabaka ya wanachama ndani ya Chadema wakati chama kinatambuka kama chama cha wanachama. Juzi juzi tuu hapa watu walikuwa wanamuunga mkono Mh Mbowe kwa kutokwenda mahakani japokuwa alikuwa amefanya kosa. Leo hii Mh Zitto ana brand wanachama wapya wa kuja na tunataka kuumunga mkono on the ground kuwa ana mapungufu yake, nk. Mkuu hapana. Hata siku moja wrong plus wrong haiwezi kuwa right na haitakuwa.
I agree, two wrongs dont make it right, but tuangalie pia kwanini Zitto ametoa comment hyo? Maneno ya Marytina yalistahili kusemwa? Hayakuwa 7bu ya zito kureact hivyo? Alimaanisha nini kusema Zitto hawezi kuwa Rais akiwa CDM, labda CCM au NCCR? Kwa mtazamo wangu alimaanisha Zitto despite mchango wake kuikuza CDM hawamuhitaji. Lets b fair to both of them kwa kuwaeleza wote walipokosea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom