Watu kila mara wanajiuliza kwa nini kila siku, kila mara, kila mahala ni Zitto, Zitto, Zitto hadi inatia kichefuchefu
Ukweli ni kwamba ni yeye anapenda iwe hivyo kwa kuwa hajakamilisha kazi aliyotumwa. Mpaka pale itakapokamilika, tutaendelea kusikia vitimbwi na show mbalimbali za huyu kijana.
Akihitimisha mchango wako Bungeni, Zitto kasema, nilipewa mchango na Tundu Rissu lakini mwandiko wake ni mbaya sana kwa hiyo nimeshindwa kuusoma. Tujiulize:
1. Je, kweli kulikuwa na ulazima wa yeye kutamka au kutoa taarifa hiyo Bungeni? Faida yake ni nini maana haiongezi chochote (katika mchango wake) wala hawezi kuwahi nafasi kwamba pengine Rissu akirudi basi akute nafasi aliyo bukiwa na mwenzake.
2. Hata kama ilikuwa lazima aseme, Je, ilikuwa lazima atamke sababu na kuchagua maneno mwandiko mbaya sana?' angalia kuna kivumishi sana kama vile mbaya haingetosha!
Si kwamba Zitto ni mzito wa kuelewa, la hasha, anafanya makusudi akijua kuwa mambo kama haya ya kuwadhalilisha wenzake yanaweza kuleta vurugu ndani ya chama na hivyo kukisambaratisha.
Amenihudhi sana, kama si kweli yanayosemwa juu yake, kwa nini asingekaa tu na kutulia kisha aje amweleze Rissu sababu iliyofanya asiwasilishe ujumbe wake. Au kama kwa hekima yake ambayo inashangaza bado aliona ni lazima kutoa taarifa hiyo ya makabidhiano ambayo Wabunge wengine hawahusiki na wala haiongezi chochote cha maana kwenye hansad ,kwa nini asingesema tu kuwa nilipewa mchango na Mbunge mwenzetu lakini kwa bahati mbaya nimeshindwa kuusoma .
Kweli sasa tunaaamini, kazi ya double agency ni ya kipuuzi sana maana ni ya kutekeleza kile usichoamini na kuamini kile usichotekeleza! Zitto hawezi kuaminika tena katika jamii ya wasema kweli.
Ukweli ni kwamba ni yeye anapenda iwe hivyo kwa kuwa hajakamilisha kazi aliyotumwa. Mpaka pale itakapokamilika, tutaendelea kusikia vitimbwi na show mbalimbali za huyu kijana.
Akihitimisha mchango wako Bungeni, Zitto kasema, nilipewa mchango na Tundu Rissu lakini mwandiko wake ni mbaya sana kwa hiyo nimeshindwa kuusoma. Tujiulize:
1. Je, kweli kulikuwa na ulazima wa yeye kutamka au kutoa taarifa hiyo Bungeni? Faida yake ni nini maana haiongezi chochote (katika mchango wake) wala hawezi kuwahi nafasi kwamba pengine Rissu akirudi basi akute nafasi aliyo bukiwa na mwenzake.
2. Hata kama ilikuwa lazima aseme, Je, ilikuwa lazima atamke sababu na kuchagua maneno mwandiko mbaya sana?' angalia kuna kivumishi sana kama vile mbaya haingetosha!
Si kwamba Zitto ni mzito wa kuelewa, la hasha, anafanya makusudi akijua kuwa mambo kama haya ya kuwadhalilisha wenzake yanaweza kuleta vurugu ndani ya chama na hivyo kukisambaratisha.
Amenihudhi sana, kama si kweli yanayosemwa juu yake, kwa nini asingekaa tu na kutulia kisha aje amweleze Rissu sababu iliyofanya asiwasilishe ujumbe wake. Au kama kwa hekima yake ambayo inashangaza bado aliona ni lazima kutoa taarifa hiyo ya makabidhiano ambayo Wabunge wengine hawahusiki na wala haiongezi chochote cha maana kwenye hansad ,kwa nini asingesema tu kuwa nilipewa mchango na Mbunge mwenzetu lakini kwa bahati mbaya nimeshindwa kuusoma .
Kweli sasa tunaaamini, kazi ya double agency ni ya kipuuzi sana maana ni ya kutekeleza kile usichoamini na kuamini kile usichotekeleza! Zitto hawezi kuaminika tena katika jamii ya wasema kweli.