Zitto: Sijengwi na Kikwete, najijenga mwenyewe

Status
Not open for further replies.
Zitto yasije ya kukupata ya Rep Anthony Weiner....hizi social networking zina athari zake
 
"Tanzania Daima Leo habari yao kuu ni 'Kikwete amjenga Zitto'. Nisingeshangaa Kama habari hii ya kizushi ingetoka Jamboleo. Nashangaa habari hii kuandikwa na gazeti linalomilikiwa na Kiongozi Mkuu wa Chama changu. Sijengwi na mtu, NINAJIJENGA!"
Nimeyapitia tena maoni ya Zitto kwenye Facebook kama nilivyoyanukuu hapo juu. Labda upeo wangu wa kuona mambo ni mdogo, lakini sijaona ni namna gani maoni haya ni tatizo kwa chama kama wengine wanavyodai. I think some colleagues here are just too sensitive with what Zitto says and does! Ni mara ngapi Tanzania Daima wameandika habari ambazo ukisoma huamini kwamba ni Gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa Chama Kikuu cha Upinzani? Sasa kulishangaa Gazeti linalomilikuwa na Kiongozi wa chama upinzani kwa kuandika habari za kiaina haina maana moja kwa moja kwamba unamshangaa kiongozi huyo, unalishangaa gazeti!!
Mkuu Kitila, nakubaliana na wewe kuwa watu ni too sensitive, lakini natofautiana nawe kuwa maoni ya Zitto hayakuwa na tatizo. Lau kama angekomea kweny neno Jambo leo isingekuwa na shida, kuendelea na kumtaja kiongozi wa chama chake ilikuwa ni direct implication ya maudhui ya gazeti na mmiliki vikiunganishwa na Chama.

Mfano, nikisema maoni yametolewa na Kitila Mkumbo, hapo hakuna tatizo. Nitakaposema maoni yaetolewa na Kitila Mkumbo ambaye ni mhadhiri wa Chuo kikuu nitakuwa na maana zaidi ya niliyokusudia, na sijui wewe ungehisi vipi. Hapa ndipo neno 'connotation' linapoingia.

Habari ya uongozi kwa vijana iliwekwa na Zitto mwenyewe na imejadiliwa hata hapa JF. Hiyo haiondoi ukweli kuwa gazeti la Tanzania daima halikupaswa kutafuta ufafanuzi zaidi ili kumpa Zitto haki ya kujieleza na kueleweka.

Kwa upande mwingine Zitto angeliweza kuwasiliana na mhariri wa gazeti au mwenyekiti wa Chama chake kabla hajaweka katika FB.
Ieleweke kuwa habari si 'mbwa kumg'ata mtu bali mtu kung'ata mbwa' na viongozi wote wanatakiwa walielewe hili vema.

Zitto kama kiongozi na mwanasiasa mahiri alitakiwa apime uzito wa kauli yake kabla ya kwenda kutoa malalamiko katika jamii anayoijua ipo too sensitive juu yake. Kwanini jamii ipo sensitive kwake!! ni kutokana na mlolongo wa matukio mfululizo yanayojenga shaka zaidi.
Kitendo cha kutoa malalamiko FB hakikuwa cha busara, uanglaifu ulihitaji zaidi. Hebu ona kauli ndogo inavyoweza kuleta mtafaruku ndani ya base ya Chama na sijui hicho ndicho kilikusudiwa au la. Nashangaa amewasiliana na mhariri baada ya tafrani kupamba moto, ndio, ni ukomavu na pia ushahidi kuwa alipaswa afanye hivyo mapema.

Ushauri wangu kwa Zitto ni kuwa kama Public figure anatakiwa awe na mawasiliano yasiyotia shaka au kuzusha hoja. Kama mwanasiasa anatakiwa awe vibrant lakini aangalie thin line between make or break. Afahamu kuwa kazi yake nzuri ndiyo inamjenga kisiasa, kauli ya kuwa anajijenga kisiasa inamtia matatani zaidi kuliko kumjenga. Mathalani ,watu watahoji kama anayoyasimamia yanatoka moyoni au ni kwa dhima ya kujijenga kisiasa. Ikifika hapo anapoteza Public trust ambayo ni muhimu sana unapojijenga kisiasa.

Wanasiasa wakomavu hutumia wingi (we do abcd, tumefanikiwa kwa abcd, tunatarajia abcd, tuta abcd), kutumia kauli ya nita au nina au nime inamtenga kiongozi na wenzake na political base as whole. Kiongozi ataonekana selfish, aggrandize, pompous, boisterous etc mambo yanayoondoa sifa ya uongozi.

Vyombo vya habari vina wamiliki na watendaji ambao ni wanataaluma (editors) na hili la Zitto nadhani angeulizwa mhariri zaidi ya mmiliki.
Sijui kama Mbowe anapitia habari zote kila siku, na mbona gazeti hilo limekuwa likiandika habari nyingi za Chadema na Zitto pia bila kumpa credit Mbowe? Hapa ni suala la ku-balance information zaidi. Kulaumu gazeti bila mawasiliano kuna ongeza wigo wa jamii ya too sensitive kwa kushirikisha vyombo vya habari, je hili ni jema kujijenga kisiasa?

Mara nyingi imeandikwa kuwa kuna tatizo ndani ya structure ya Chadema. Ingawa inakanushwa lakini dalili zinaanza kujitokeza hata kama watu hawakubali. Viongozi wa kitaifa wanapokosa uvumilivu na busara si dalili njema. Yapo mambo yanayoweza kumalizwa ndani ya vikao na si kwenye magazeti au mbao za matangazo. Labda hili likumbushe zaidi kauli ya kila mara, Chama ni Imara lakini structure ina matatizo.
 
Kila ninapoinua kichwa na kusoma habari na kusikia zitto anazungumzia maswala ya chama cdm na uchaguzi moja kwa moja namwona kweli zitto sijui kazaliwa na tatizo gani. Kwa kifupi ni hivi, sipendi na sitaki keleza maneno mengi kuhusu huyu jamaa yetu zitto. Zitto umeshaonekana kwa kifupi kuwa ni unanjama mbili kubwa za katika chama cha wananchi cdm (1) kuhakikisha unapanda kisiasa na kuwa raisi kwa ndoto zako (2) kuhakikisha influence yako katika chama kuuwa cdm na tumeona ushirikiano wako na serikali ya kikwete.

Ni bahati sana kwamba zitto bado upo ndani ya cdm, tunajua zitto ni kama kidonda kinachopona na wakati ukipita kinarudi tena (dunda ndugu). Wanachama wa cdm tusiwe na wasi wasi sana kuhusu zitto, mikakati ipo na imeshaandaliwa jinsi ya kudeal na wanachama wa aina tofauti ndani ya cdm.

'chadema is movement and not political party'


Katika facebook wall yake, Zito Kabwe amelilaumu gazeti la Tanzania daima kwa kuandika habari inayohusu Zitto kujengwa na Kikwete. Binafsi sina shida na lawama alizolitupia gazeti, kwa kuwa kiuhalisia kwa kuandika hivyo kunawapotezea imani wapinzani dhidi ya Zitto. Hilo naungana naye kwa asilimia nyingi, kwamba Tanzania Daima haikupaswa kuandika hivyo.

Lakini kilichonisikitisha ni kitenda cha Zitto kuweka hoja zake kwa kulihusisha gazeti la Tanzania Daima na Mbowe (mwenyekiti wa CHADEMA). Sidhani kama mhariri wa gazeti anapoihariri habari huwa anampelekea Mbowe aangalie kama habari hiyo inakubalika au haikubaliki. Kwahiyo sioni mantiki ya kuihusisha habari ile moja kwa moja na Mbowe. Na kwa namna nyingine naona kama kauli ya Zitto imelenga kuibua mgogoro mwingine na viongozi wenzake ndani ya chama.
Nawasilisha.
 
Hivi kwa ukaribu alionao Zito na Rais Kikwete atashindwa kweli kuwa anampatia mikakati ya Chadema kuiondoa CCM madarakani?, am so afraid with this guy.
 
Bwana mdogo mbona alishaisha huyu
mimi nilipomuona tu amaeanza kuendesha yale magari ya zamani ya wanajeshi wa wakimarekani nikajua oooh tayari kisha zimishwa na wajanja!
 
Ukaribu siyo hoja kwa sababu upinzani siyo uadui.Tatizo ni huyu jamaa zto kutokuwa mtulivu kimsimamo. Huyu jamaa ni kama bendera anafuata mwelekeo wa upepo au kama ugonjwa wa bp. Huwezi ukamlinganisha na watu kama JOHN MYKA na dr wa ukwel
 
Hivi kwa ukaribu alionao Zito na Rais Kikwete atashindwa kweli kuwa anampatia mikakati ya Chadema kuiondoa CCM madarakani?, am so afraid with this guy.

mjumbe usidhani kuwa rais wa nchi anashindwa kupata mikakati ya chama cha upinzani mpaka awatumie wanachama wa chama hicho. ila mara nyingi marais wanafuatilia mikakati ya vyama vya upinzani kwenye awamu ya kwanza . kwasasa kikwete hana cha kupoteza kuwaachia wapinzani ili mradi wamuhakikishie ya kuwa hakuna mambo yeyote ya kufikishana mahakamani. kwa jk ni bora chadema wachukue kuliko lowassa
 
Bwana mdogo mbona alishaisha huyu
mimi nilipomuona tu amaeanza kuendesha yale magari ya zamani ya wanajeshi wa wakimarekani nikajua oooh tayari kisha zimishwa na wajanja!


nilihuzunishwa sana na hili,tuna safari ndefu kupata watu wanaofaa kututoa hapa tulipo
 
Ila nina swali. Kuwa mwanasiasa wa upinzani ina maanisha usiwe urafiki na wale wa chama tawala? Kuwa wapinzani kikazi (kwenye majukwaa ya siasa) ina maanisha kuwa wapinzani hata personally?
 
Bwana mdogo mbona alishaisha huyu
mimi nilipomuona tu amaeanza kuendesha yale magari ya zamani ya wanajeshi wa wakimarekani nikajua oooh tayari kisha zimishwa na wajanja!

Hapa hapana, anauwezo wa kununua ile gari sio ghali kwa kipato halali anachopata, hii sio point. Huu ni wivu. leta hoja.
 
Zitto nikikumbuka ile story ya gazeti la mwanahalisi alilotowa mawasiliano yake na mkurugenzi wa usalama wa taifa na Rostam Aziz nilimtoa akilini kabisaaa. Maana kwanza hakukanusha maana alijua ni kweli hakuwa na jinsi. Pia nilisikia fununu huko nyuma kuwa Rostam Azizi ndiye aliyemnunulia gari la kimarekani na kumjengea nyumba hivyo baada ya mwanahalisi kuandika nika-comfirm. Zitto si mwenzetu katika kupigania wanyonge kwa sababu yeye sasa hivi si mnyomnge tena.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom