Zitto: Sheria ya utawala wa Bunge kifungu cha 19 imevunjwa na spika

Swali ni je, Zitto amewasiliana na Spika officially kumwambia haya kimaandishi? Isije kuwa umaarufu search kwenye facebook tu...
 
Ni vituko zaidi ya vioja mi naona sheria ya m2 kuwa mbunge mi naona ingebadilishwa kbs.
Nilimsikiliza huyu bi kiroboto yaani kaongea uharisho mtupu naona kanya kwa mdomo.
Kwani hayo maisha yanapanda kwa wabunge 2???

Au wao ni kundi la wa2ambao hawatakiwi kbs kuguswa na hii hali ya mabadiliko ya life???

Hapo ndiyo nipatapo mashaka na wabunge naona sasa wameamua ku2thibitishia kuwa ubunge ni kazi nzuri sana inayolipa zaidi ya uuzaji wa madawa ya kulevya.
 
Katika hili la kupinga kwa kinywa kipana kusudio la MATUMIZI MABAYA YA KODI ZETU chini ya uangalizi wa Mhe Spika pamoja na Dr Kashilila, hakika rafiki yangu Zitto umenikuna sana!!!!!

HUU NDIO UZALENDO WA KWELI NA KULE KUSIMAMIA KIDETE MASLAHI YETU UMMA WA TANZANIA. Zitto ukiendelea hivi BILA KUYUMBAYUMBA katika mambo ya msingi kama hivi kwetu sisi walipakodi, mwezetu huenda huko baadaye tukafikiria kuzungumza lugha moja na wewe huko mbele ya safari na wala si vinginevyo.

Timu zima ya CHADEMA na Dr Slaa kwa kipekee; hasanteni sana kwa kulea mbegu mpya ya vijana wenye kuanza kuleta japo ka-nuru dogo ya UADILIFU UONGOZINI, ULINZI IMARA WA MASLAHI YA UMMA na kwa kwa sana kuzungumza lugha moja ya SIASA ZA TAIFA ZAIDI kuliko zile za uchochoroni.

Maslahi ya Umma na uzalendo wa kweli mbeeeele kama tai huku tukikemea kwa nguvu zote hili li-baba la UFISADI nchini lililopewa jina jipya la 'MASLAHI YA CHAMA KWANZA' huko kwa watani zetu kisiasa nchini.
 
Bunge linatunga sheria lenyewe kisha lenyewe linazikiuka. Makinda ana masuali ya kujibu kwa wananchi, yeye yupo juu ya sheria?
 
Pengine Bunge letu la Dodoma hivi sasa ni KIWANDA MAARUFU CHA KUTUNGA SHERIA MBALIMBALI LAKINI KWAO WAO SHERIA HIZO HUTUNGWA TU KWA AJILI YA 'AKINA WALE' mbamo wao kamwe hawamo na wala hawahusiki kabisa nazo hizo sheria zenyewe.

Na hapo ndipo kilio chetu wananchi kinpoanzia na hata kuanza kitiwa wazimu tunapoona sheria n MELEKEZO HALALI YA KATIBA YETU YA NCHI zote zinapokiukwa tu makusudi kwa kufukuzia tu hii BABA YA UFISADI nchini inayopambwa sana hivi sasa kwa jin la 'MASLAHI YA CHAMA' badala ya maslahi ya Umma.

Hakika natami kusikia siku moja kwamba vyombo vyetu vya sheria, ulinzi na usalama vinageuka mbogo kwa mtu yeyote na au taasisi yoyote nchini itakayobainikika kuvuruga MASLAHI YA UMMA (Masla ya walipakodi kwa ujumla wetu sote) kwa kuendekeza maslahi binafsi.

Hakika siku hiyo mambo yote yatakua ni shwaaari bila kelele hivi za kila leo. Lakini kwa mtindo huu wa sasa, sijanyamaza bado!!!


Bunge linatunga sheria lenyewe kisha lenyewe linazikiuka. Makinda ana masuali ya kujibu kwa wananchi, yeye yupo juu ya sheria?
 
Tatizo Zitto ni kama vile yupo peke yake kwenye suala la kupinga posho/ongezeko la posho kwa wabunge. Angekuwa ana support kubwa walao toka kwa wabunge wenzake huenda hali ingekuwa tofauti. Wabunge wanadhani kuwa wao ni malaika wako tofauti na watanzania wengine! Wanakera sana wanapodai kuwa wanatumia hizo pesa kuwasaidia wananchi! Kama hiyo ndio sababu si watugawie sisi wenyewe direct! Aghaaaaaaaa! Mtu waweza tukana bure!
 
Wewe kweli huna tofauti na gamba ! Yaani mpaka kwenye hujui Zitto ameanza lini kulipigia kelele?
Swali ni je, Zitto amewasiliana na Spika officially kumwambia haya kimaandishi? Isije kuwa umaarufu search kwenye facebook tu...
 
Wewe kweli huna tofauti na gamba ! Yaani mpaka kwenye hili hujui Zitto ameanza lini kulipigia kelele?
Swali ni je, Zitto amewasiliana na Spika officially kumwambia haya kimaandishi? Isije kuwa umaarufu search kwenye facebook tu...
 
Zitto na wenzio hakikisheni munatusimamia wananchi tusidhurumiwe,Spika amepotoka anaweza kuwa anawahonga wabunge wa chama chake kwa kupitisha muswada wa katiba mbovu lakini nyie kuweni kwa niaba yetu hata kama ukibaki peke yako ,sauti yako itasaidia tuu
 
Mkuu Zitto viongozi wa Tanzania wanajali sana matumbo yao,badala ya kujali masilahi ya wananchi ambao kupitia kura zao wamewawezesha kuwa viongozi kwa kuamini kuwa wangeweza kutetea maslai yao.Kifupi viongozi wa Tanzania hamuaminiki kabisa na wananchi kutokana na kuleta siasa katika kila jambo.
 
NAWACHUKIA SANA WABUNGE WA CCM,ina maana kupanda kwa gharama za maisha wanaumia wao tu?sisi wengine hatuumii?amenikera sana huyo bibi punguani kusema eti vyumba vimefika 100,000.mbona kuna hotel nzuri tu za 30,000 kwani wakilala hawapati usingizi?we Makinda acha kutufundisha ukatili, agriiiiiiiiiiii kum........
 
Zitto anasema from facebook

" Spika wa Bunge anajua kwamba posho zote hulipwa Baada ya Rais kuidhinisha. Posho anazotangaza hazijaidhinishwa kwani uthibitsho wa kuidhinisha ni Masharti Mapya ya Kazi kwa Wabunge ambayo hayajatolewa na Ofisi ya Rais. Hivyo kitendo cha kuanza kulipa posho mpya bila Masharti Mapya ya kazi za Wabunge ni kukiuka sheria ya utawala wa Bunge kifungu cha 19.
Tume ya Bunge inapaswa kuwajibika kwa kutumia vibaya mamlaka yake, posho mpya zifutwe na zilizolipwa zirejeshwe mara moja kwani zimelipwa kinyume na sheria.

Spika anapaswa kuheshimu sheria ambazo Bunge limepitisha na kwenda kinyume na sheria kwa makusudi ni kosa la kuvuliwa Uspika.

Wabunge wasifanye mchezo na suala la posho. Wananchi wamekasirishwa sana na kwa kweli hatuwaelewi. Wakati Bunge la Tisa lilisifika kwa kupambana na ufisadi, Bunge la kumi litabatizwa Bunge la Posho. Ni lazima tukatae kuonekana tunajijali badala ya kujali wananchi.

Namsihi Spika aachane kabisa na suala hili la posho. Tukazane kukuza uchumi wa nchi ili wananchi wapate ajira, kodi iwe nyingi na tuongeze mishahara kwa wafanyakazi wote. Hoja ya ugumu wa maisha ni kwa wananchi wote sio wabunge peke yao.

Jambo la kuzingatia kwa sasa ni kwamba, iwapo posho hizi zitalipwa kwa wabunge, nini kitazuia posho Kama hizo kulipwa kwa wabunge wa Bunge Maalumu la katiba? Huo mzigo serikali itaubeba namna gani na Hali hii ya uchumi?

Wabunge tujielekeze katika kukuza uchumi, kuongeza uzalishaji viwandani, mashambani na kwenye shughuli nyingine za huduma za kiuchumi. Tuachane na fikra za posho
."

Zito ni mzalendo wa ukweli
 
Nasikia haya yanafanyika pia:
-Waziri au naibu wake au Mkuu wa Mkoa ambaye ni Mbunge wanachukua "per diem" maofisini kwao kwenda kuhudhuria vikao vya bunge. Wakifika Bungeni wanavuta tena "per diem" inayotolewa na Bunge.
-Tume ya Utumishi ya Bunge ikishaamua juu ya posho hizi malipo yanafanyika haraka hata kabla Rais hajaridhia!
-Nyongeza hii ya posho imetokana na Wabunge kukatazwa kuchukua bahasha za khaki kutoka Taasisi za UMMA wanazotembelea.
-Bunge sasa ni Bodi ya wakurugenzi ya serikali. Wanakimbizana na posho zinazolipwa kwa wakurugenzi wa bodi mbalimbali za UMMA.
 
CCM imejaza genge la wezi na wala rushwa, what do you expect?
 
Kuna kila sababu sasa ya kuwashughulikia kibinafsi viongozi wote wanaotumia ofisi zao vibaya.
Tumeshuhudia na tunaendelea kuona na kusikia viongozi wakitumia vyeo vyao kujinufaisha wao binafsi, familia zao, ndugu jamaa, marafiki na hata washirika wao. Hii ni fedheha kubwa kwa jamii yetu na haipaswi kuachwa iendelee hata kidogo.
Uongozi wa taasisi mbali mbali za uma umekuwa wa mzunguko wa wale wale walaaniwa wa siku zote wanowatesa wananchi tangu enzi hizo, wamejenga umoja na mazoea ya kujipendelea wenyewe na hakuna wa kumuwajibisha mwingine.
Mbaya zaidi wananchi wamezoea udhalilishwaji huu na hawaoni tatizo kubwa.
Na tuanze sasa miaka mingine hamsini ya UHURU kwa kuhamasisha UKOMBOZI WA FIKRA za wananchi walio wengi ili kuwaondoa hawa viongozi wanyonyaji na walafi wa kijinga.
Maneno matupu hayavunji mfupa!
 
ifikie mahali raia tuseme basi inatosha kwa vitendo zaidi ya kulalamika tu kila siku kwenye media,vinginevyo ni kama kuwapa fursa wao (viongozi)kuendelea na huu umangimeza dhidi ya raia
 
"Wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa Rais, taarifa za Bunge zinaeleza kuwa mchakato wa nyongeza za posho ulipitia hatua karibu zote katika Bunge.

Hatua hizo ni pamoja na kujadiliwa na kupitishwa na Tume ya Bunge inayoundwa na makamishna ambao ni wabunge pia, Kamati ya Uongozi ya Bunge inayoundwa na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge na mwisho, wabunge wote kupewa muhtasari husika na kujadili na kisha, kukubali au kutokubali taarifa husika.

Kwa hiyo, Raia Mwema, kupitia vyanzo vyake vya habari, limejiridhisha kuwa Bunge lilifikia uamuzi wa kuongeza posho hizo na wabunge wa kambi ya upinzani na chama tawala kwa ujumla wao, walikubali uamuzi huo.

Inaelezwa kuwa mbunge pekee mwenye msimamo mkali dhidi ya kuchukua posho ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, ambaye hata hizi posho za zamani amegoma kuzichukua kwa muda mrefu sasa."

Source: Raia Mwema

Najiuliza kama Zitto alikuwa Bungeni, na kama hakuwa bungeni hizi habari zilimpita? Je Mnyika naye hizi habari zilimpita. CDM naona mmpeoteza uelekeo na hasira ya wananchi itawashukia 2015. Mlishindwaje kuibua hili jambo kule kule Dodoma, leo hii mnakuja na upupu kuandika kwenye FB na JF ? Hamkujua? mlifanya nini. Yale yale kama ya muswaada wa katiba, mlikuwa na nafasi ya kisheria ya kuuzia, mkalewa mkaacha, then mkasusa, kutafuta cheap popularity, stop your madness guys, Watanzania watapoteza imani na nyie.
 
Back
Top Bottom