Zitto Naibu katibu Mkuu hata vikao vya chama anaadimika?

Niliwahi ona video sehemu katika simu ya mtu..Gesture yake jukwaani wakati Mr II a kiperfom pale Arumeru katika kampeni za Nassari haikuwa nzuri.Hasa pale watu walipokuwa wamshangilia sana mh II wakija jukwaani kuwashika mikono makamanda.Zitto alionyesha dharau n akutokubaliana na hali ile ya kukubalika kwa Mr. II.Zitto alikuwa dettached sana na watu emotionally,hata yeye mwenyewe akiangalia video yake kama CDM wanazo ataona hili.

Ilikuwa hali ya kuhofia kuwa siyo pekee tena katika CDM+ ilikuwa hali kama vile wale watu si waelewa sana na zile shamrashamra na hisia ni za kipuuzi na si worth it.

Mheshimiwa usihofu kwani mimi ndivyo nilivyo nisione kitu.Kwani mara nyingi attention yangu kwa vitu vidogo ipo karibu sana.Ni mheshimiwa tuu akaangalie vizuri video za mikutano ya pale user river.Niliona hofu kama ya mtoto anayokuwa nayo anapozaliwa mdogo wake.Hii nilikuja thibitisha bunge lilipoanza Zitto alikuwa naive sana kuuliza maswali ya nyongeza kabla ya kuja stabilize baadaye.

Hilo nalo Nicholas ni jambo la kuangalia sana katika safu ya uongozi. Kuna udhaifu ambao viongozi wengi Tanzania katika siasa na hata sekta binafsi mmoja wapo au baadhi wanapofanya mambo mazuri au kuwa na dalili ya kuvutia hadhara hugeukwa kuwa adui kwa wale wanaotafuta kuonekana pekee ndio wajulikane. Kasoro hii inatokana na ubinafsi (selfishness, self-esteem, etc). Tunapokuwa na mmoja tu wa kumpitisha bila kupingwa kwa sababu ya kukosa mshindani au washindani wa kuwashindanisha katika nafasi hiyo, matokeo tunayajua, mambo haya siyapendi. Bora tuwe na wengi, anayepenya awe kweli amechujwa kwa kiwango cha mategemea kuwa atakuwa na kiwango cha uongozi.

Matokeo ya viongozi wa aina hii ni kutafuta zaidi popularity kwa wananchi badala ya uwajibikaji wa kweli. Tunaposhabikia popularity kwa viongozi badala ya kuangaliwa uwajibikaji ndipo jipu linapokuja kupasuka wakati wamepenya kwa popularity na kisha kuishia kuwa watalii muda wote wa uongozi wao.

Tusisubiri kipindi cha uchaguzi, tuwachambue sasa hivi, na wale wanaoona tunaonyesha kasoro nyingi ambazo zinaweza kuwakosesha sifa za uongozi watazifanyia kazi ili waingie kwenye ushindani wa kweli na wakiibuka ni kutokana na ukweli wa utendaji wao.

Tukumbuke daima usemaji mwingi mjengo si kiwango halisi cha uwajibikaji. Kikwete ninavyomkumbuka alivyookunjua kucha zake na kuvalia njua suala la hayati Kighoma Malima na kusababisha kujiuzuru uwaziri wa fedha, si Kikwete huyu wa leo, kwa nini? Hatukuangalia mambo mengi katika uwajibikaji, ila tuliangalia jambo moja moja tu kama ndio kigezo cha kuongoza nchi.
 
Nakumbuka miaka ya nyuma,kwenye ile issue ya Zimbabwe alipokuwa akissugest tusaidie kumwondoa Mugabe,nilimwambia awaonee huruma wananchi masikini wa Kigoma kaskazini.Sidhani kama walimchaguwa afanye hayo anayoyafanya.Ni kama anawatumia kama ngazi.Ndo maana alitaka sijui kugombea jimbo gani vile?Najuwa wabunge wengi wana agenda nyingine binafsi nk.However si haki kabisa kuwasahau wapiga kura wako na majukumu yako kwa jimbo lako kwasababu ya personal interests zako.Ubinafsi haufai kwenye kuwatumikia wananchi.Its not about the people no more.

jmushi1 asante kwa kuoanisha hilo na tukio la Zimbabwe.
Nikupe mfano mmoja ambao unaweza kutoa picha ya uwajibikaji kwa chama na umma.
Lema anajituma, anafanya jitihada za kuhuisha chama vijijini na po pote na haogopi lo lote. Anachohitaji ni kukomaa zaidi kupata busara na hekima, kwani kwa sasa anatumia saidi hisia na moto moto wa ujana na nafasi fulani fulani amekosa kutumia busara, mambo mengi si lazima kujiingiza kichwa kichwa, inabidi kutumia busara na hekima kuyakwepa yasikupate yasikupotezee muda.
Lema anafaa kuwa kiongozi ila anahitaji muda kukomaa, nafasi ya uongozi kwa sasa anatakiwa awe na mtu juu yake wa kumsaidia.

Zitto anajitahidi sana kutumia muda mwingi Bungeni na katika Kamati ya bunge kuibua madhaifu ya serikali, lakini hayuko tayari kuonyesha madhaifu hayo ya serikali awapo nje ya bunge. Tafsiri ni nyepesi anatumia bunge kama kinga ya kujitangaza kupata popularity badala ya nafasi nyingi kutokana na nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama. Mpaka sasa binafsi sijaona wazi wazi uwajibikaji waka kama Naibu katibu Mkuu Chadema, ila anasikika tu Bungeni kwa sababu bungeni ukiwa mbunge una kinga ya kutochukuliwa hatua za kisheria au kushtakiwa kwa unayotamka bungeni.

Naweza kutoa dondoo moja katika hilo kuhusu Zitto, hivi karibuni alisema ataweza kuanika majina ya walioficha pesa huko Uswiss. Serikali isipofanya hivyo, atafanya hivyo bungeni si sehemu nyingine na kwamba anajua nafsi nzuri kwa yeye ni bungeni na wala si sehemu nyingine. Je, kwa nini asitumie nafasi ya mikutano ya chadema ambayo viongozi wa kitaifa huandamana pamoja kwenda kulipua hayo? Anaogopa nini kusema hayo kwenye mikutano hiyo na kuishia kuyasema bungeni kwa vile litamlinda?
 
Jamani Mh Zitto kajimaliza mwenyewe nahawezi tena kushindana na kasi ya makamanda wapya wa M4C
 

Kama ukiwa mwalimu shuleni unaweza kushangaa kijana mdogo tu anaweza kukuendesha kwa ujanja wa kutoroka kwa visingizio mbalimbali, utakapokuja kugundua ni too late.

Kitu kimoja unaweza kugundua jeuri ya mtu anapokuwa na udhuru wa mahudhurio katika mazingira ya aina fulani tu, na mazingira ambayo si hatarishi ni mwepesi kutotoa udhuru. Hakuna tukio hata mmoja ambalo Mheshimiwa Zitto amehusika matukio ambayo viongozi wenzake wanajituma katika mazingira hatarishi kutetea mabadiliko nchini.

Hata watu maarufu duniani waliojitolea kuleta mabadiliko katika nchi walipambana na mengi kama mzee Madiba kukaa miaka 26 gereani na leo matunda yake wanayafurahia wengi nchini Afrika Kusini. Mwono huo ndio tunaoutazamia kwa viongozi na makamanda wanaoendesha vuguvugu la mageuzi nchini.

:A S 465:ZUBERI ZITTO SI SHUPAVU KUPAMBANA NA MAGUMU:A S 465:​

Ninachoshangaa ni kuwa hata yale mazuri pia huwa hamu acknowledge hata siku moja. Tukio la kuuwawa kwa Mwangosi Zitto hakuwepo, unless kama mlifanya teleconference napo akakataa kujihusisha hapo sawa, ila kama ni physical meeting then you don't have to make a big fuss out of it.
Zitto kuelekea Uchaguzi wa mwaka 2010, alifanya kampeni majimbo sio chini ya 15 kwa gharama zake na si gharama za chama, hilo huwa hamlisemi. Jimboni kwake(Kigoma) Dr. Slaa alipata kura 45%, wakati ambapo Kilimanjaro alipata kura 36%. Ameongelea Bungeni suala la accountability, hiyo ni kujitoa mhanga, ku motion kumuondoa Prime Minister on his face, nani anaweza kufanya hivyo? Let us be realistic and face it. Had it been viongozi wengine wangesifiwa, ila since ni Zitto mko silent, stop hating. Suala la posho, chama kilikubaliana kutokuchukua posho, kabaki amekomaa mwenyewe mpaka leo hii hachukui posho, malipo yake ni kumchukia na majungu na uzandiki, acheni hayo mambo nyie. Msipende kujazana ujinga, jaribuni ku reason.
 
attachment.php


Katika operation ya vuvuvuvu la mabadiliko, Zitto Kabwe haonekani kuandamana na makamanda wenzake, wakati akiwa Kaimu Katibu Mkuu ambaye ndiye kijana wa kuwa mstari wa mbele katika mapambano.

Isitoshe hata kikao hiki kilichofanyika Jijini Dar alitazamiwa kuwa katika picha, labda imekatwa alikaa pembeni, tukumbuke yeye ni kiongozi mwandamizi, lakini naona yuko makini kutokea katika picha za misafara ya kumsindikiza Kikwete kutalii. Hii imekaaje?

Tunahitaji Zitto aje kujibu haya, ndio uwajibikaji tunaohitaji sasa hivi. Tunahitaji viongozi wa chama wanaowajibika kwa chama na wananchi chama tunachotegemea kuchukua dola, na hivi kujihakikishia viongozi watakaowajibika kwa wananchi na wananchi wawe na haki ya kuwajibisha wasipowajibika kiutendaji.

Kiongozi anayefanya kazi kwa ujanjaujanja na kukwepakwepa magumu ni hatari kwamba siku yakitokea magumu anaweza kuwatelekeza wenzake na hata kukitelekeza chama chake.

Sio tatizo...hata Arfi hayupo hapo.Hicho cheo kinafuata mfumo wa ki ccm,kuna manaibu wawili,mmoja bara mwingine visiwani,lakini yoyote anaweza kufanya kazi upande wowote akiidhinishwa na Slaa.(mwangalie naibu katibu mkuu-visiwani wa tatu kutoka kulia mstari wa mbele).CDM ni chama kikuu cha upinzani,na ZZK naibu kiongozi bungeni,si ajabu kukumbwa na shughuli nyingi za kibunge.Katika viongozi wa juu wa sasa ni ZZK na mbowe wenye masaa mengi katika kuifikisha CDM hapo ilipo.Acha majungu unaua chama ndugu.
 
zitto, halima mdee, j mnyika..wakiwa bungeni kelele nyingi but when it really matters KIMYA.....
 
attachment.php


Katika operation ya vuvuvuvu la mabadiliko, Zitto Kabwe haonekani kuandamana na makamanda wenzake, wakati akiwa Kaimu Katibu Mkuu ambaye ndiye kijana wa kuwa mstari wa mbele katika mapambano.

Isitoshe hata kikao hiki kilichofanyika Jijini Dar alitazamiwa kuwa katika picha, labda imekatwa alikaa pembeni, tukumbuke yeye ni kiongozi mwandamizi, lakini naona yuko makini kutokea katika picha za misafara ya kumsindikiza Kikwete kutalii. Hii imekaaje?

Tunahitaji Zitto aje kujibu haya, ndio uwajibikaji tunaohitaji sasa hivi. Tunahitaji viongozi wa chama wanaowajibika kwa chama na wananchi chama tunachotegemea kuchukua dola, na hivi kujihakikishia viongozi watakaowajibika kwa wananchi na wananchi wawe na haki ya kuwajibisha wasipowajibika kiutendaji.

Kiongozi anayefanya kazi kwa ujanjaujanja na kukwepakwepa magumu ni hatari kwamba siku yakitokea magumu anaweza kuwatelekeza wenzake na hata kukitelekeza chama chake.

Mleta huu uzi umetumwa?hahahaaa!the next prezidaa zzk hafanyi siasa za dharura kama ufinyu wa akili zako unavyodhani?peleka taarifa kwamba kwa bahati mbaya hujamkuta kaenda malaysia.hahahahaaaaa!
 
Ukitaka kujua kwamba chadema tatizo ni urais zitto anaoenda kuupata 2015 ndio unaowasumbua kwenye hiyo safu ukiangalia vizuri utaona makamu mwenyekiti wa cdm mh arfi hayupo pichani,na hata ziara nyingi huwa haonekani,swali ni je kati ya naibu katibu na makamu mwenyekiti nani ana cheo cha juu?kwanini iwe zitto zitto kila siku?hahahaa urais?mbona huo ataupata tu(katiba mpya)makamu mwenyekiti nae akitangaza nia tu utaona atakavyoanza andamwa!usishibe upepo.
 
Usipokuwa mchungaji au padre tegemea "Madongo" chadema.

Unless uwe kama darasa la saba au usiwe na ambition yeyote kama Arfi
 
Ninachoshangaa ni kuwa hata yale mazuri pia huwa hamu acknowledge hata siku moja. Tukio la kuuwawa kwa Mwangosi Zitto hakuwepo, unless kama mlifanya teleconference napo akakataa kujihusisha hapo sawa, ila kama ni physical meeting then you don't have to make a big fuss out of it.
Zitto kuelekea Uchaguzi wa mwaka 2010, alifanya kampeni majimbo sio chini ya 15 kwa gharama zake na si gharama za chama, hilo huwa hamlisemi. Jimboni kwake(Kigoma) Dr. Slaa alipata kura 45%, wakati ambapo Kilimanjaro alipata kura 36%. Ameongelea Bungeni suala la accountability, hiyo ni kujitoa mhanga, ku motion kumuondoa Prime Minister on his face, nani anaweza kufanya hivyo? Let us be realistic and face it. Had it been viongozi wengine wangesifiwa, ila since ni Zitto mko silent, stop hating. Suala la posho, chama kilikubaliana kutokuchukua posho, kabaki amekomaa mwenyewe mpaka leo hii hachukui posho, malipo yake ni kumchukia na majungu na uzandiki, acheni hayo mambo nyie. Msipende kujazana ujinga, jaribuni ku reason.

Sijawa na chuki, wala majungu au uzandiki na mambo mengine unayosema mdau mwenzetu. Upembuzi wangu si kwa tukio moja kwani picha ni taswira yanye kusaidia kujenga hoja yangu. NImeeleza kwamba matukio mengi ama nilivyoainisha Zitto hajatokea isipokuwa yale ambayo hayana misukosuko.

Zitto mwenyewe amejibu mada hii kwenye mtandao mwingine kuwa waliopata misukosuko ni kwa kujitakia. Hayo ndiyo majibu yanayoweza kutupatia picha ya nini anafikiria wenzake matatizo yanayowapata katika shughuli za kujenga Chama.

Kuwa kiongozi bora si katika usemaji mzuri bungeni, la hasha, kuna mengi zaidi ya usemaji, kwani kama ni usemaji bungeni wapo wengi tu wanafanya hivyo lakini si kigizo cha kwamba wote wale wanafaa kuwa viongozi wa juu.

Tunachojadili hapa ni kuonyesha mapungufu ambayo Zitto kama binadamu ye yote anayo mapungufu ambayo tunayaona, na hivyo ayafanyie kazi ili kuweza kujiandaa kuwa kiongozo bora.

Wengine tulio na upeo zaidi katika kuainisha ubora wa viongozi twaweka kando ushabiki wa kile moyo ukipenda, bali hali halisi kama mambo ambayo kiongozi wa juu anatakiwa awe na ushujaa na uwazi bila woga ambao unaweza kumfanya afanye kazi kiujanjaujanja kumbe kuwa kiongozi wa juu kitu kama hicho hakipo, na kama atafanya ujanja ujanja mambo yataharibika, he must face all.
 
Sio tatizo...hata Arfi hayupo hapo.Hicho cheo kinafuata mfumo wa ki ccm,kuna manaibu wawili,mmoja bara mwingine visiwani,lakini yoyote anaweza kufanya kazi upande wowote akiidhinishwa na Slaa.(mwangalie naibu katibu mkuu-visiwani wa tatu kutoka kulia mstari wa mbele).CDM ni chama kikuu cha upinzani,na ZZK naibu kiongozi bungeni,si ajabu kukumbwa na shughuli nyingi za kibunge.Katika viongozi wa juu wa sasa ni ZZK na mbowe wenye masaa mengi katika kuifikisha CDM hapo ilipo.Acha majungu unaua chama ndugu.

Arfi ni mzee ambaye hatumtegemei kwa majukumu zaidi ya uongozi kitaifa, tunachofanya ni kuandaa damu changa kwa uongozi wa baadaye ili tuwaivishe vizuri. Hatutaki marais wa nchi yetu kuwa kama ma-be show.
 
Mleta huu uzi umetumwa?hahahaaa!the next prezidaa zzk hafanyi siasa za dharura kama ufinyu wa akili zako unavyodhani?peleka taarifa kwamba kwa bahati mbaya hujamkuta kaenda malaysia.hahahahaaaaa!

Mdau mwezetu, matarajio yangu ni kuwa ungeenda mbali zaidi katika kuandaa safu nzuri ya uongozi ambayo haitaleta kashkash na kuanza kutimuana kwa sababu ya kutowajibika au kukwepa majukumu magumu.

Yaliyotokea juzi kufukuzwa uanachama Madiwani wa Mwanza ambapo mara baada ya uchaguzi Mkuu uliopita Dr. Slaa alisema wanataka Halmashauri ya jiji la Mwanza liwe mfano wa halmashauri nyingine nchini, lakini kabla ya kufikia katikati ya muhula kuna kutimuliwa meya na baadhi ya madiwani wake kuvuliwa uanachama, hapa kuna kasoro ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi.

Ninaloliongelea ni kwa ajili ya kuwajenga hawa viongozi yasitokee hayo, kwani madhaifu hayo tunayajua na yametajwa na kujadiliwa mara kadhaa hapa, cha msingi ni kuwa wazi na kuyaanika ili kuwasaidia kujisahihisha kuwa na kiwango tunachotarajia na tufurahie matunda yake.

Huku kushabikia viongozi kwa mtindo wa kushangilia timu ya mpira itatufanye tuwe kama tumezipumzisha kwanza akili zetu na kitu kingine tulichokizoea kukiita "kile moyo ukipenda" kukiendekeza hatu wote tunatumbukia nacho shimoni.
 
Sijawa na chuki, wala majungu au uzandiki na mambo mengine unayosema mdau mwenzetu. Upembuzi wangu si kwa tukio moja kwani picha ni taswira yanye kusaidia kujenga hoja yangu. NImeeleza kwamba matukio mengi ama nilivyoainisha Zitto hajatokea isipokuwa yale ambayo hayana misukosuko.

Zitto mwenyewe amejibu mada hii kwenye mtandao mwingine kuwa waliopata misukosuko ni kwa kujitakia. Hayo ndiyo majibu yanayoweza kutupatia picha ya nini anafikiria wenzake matatizo yanayowapata katika shughuli za kujenga Chama.

Kuwa kiongozi bora si katika usemaji mzuri bungeni, la hasha, kuna mengi zaidi ya usemaji, kwani kama ni usemaji bungeni wapo wengi tu wanafanya hivyo lakini si kigizo cha kwamba wote wale wanafaa kuwa viongozi wa juu.

Tunachojadili hapa ni kuonyesha mapungufu ambayo Zitto kama binadamu ye yote anayo mapungufu ambayo tunayaona, na hivyo ayafanyie kazi ili kuweza kujiandaa kuwa kiongozo bora.

Wengine tulio na upeo zaidi katika kuainisha ubora wa viongozi twaweka kando ushabiki wa kile moyo ukipenda, bali hali halisi kama mambo ambayo kiongozi wa juu anatakiwa awe na ushujaa na uwazi bila woga ambao unaweza kumfanya afanye kazi kiujanjaujanja kumbe kuwa kiongozi wa juu kitu kama hicho hakipo, na kama atafanya ujanja ujanja mambo yataharibika, he must face all.

Unapozungumzia mtandao ambao Zitto ameliongelea hilo ni upi na lini?????Tunaomba uthibitishe hilo.
 
hakiamungu huyu jamaaa MAMLUKI IPO SIKU MTAKUJA KUBARIANA NA MIMI,,,VIJANA WENZAKE OWTE WAKOBIZE NA MABADILIKO YAANI YAANI YEYE HAELEWEKI HATA ANAHAMASISHA NINI?????
 
nachopenda na nafurahi,chama kinajua zitto ni nani na anafanyanya nn,so km chama kimeshachukua precaution...aangalie anajimaliza mwenyewe kisiasa
 
Back
Top Bottom