Zitto Naibu katibu Mkuu hata vikao vya chama anaadimika?

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
attachment.php


Katika operation ya vuvuvuvu la mabadiliko, Zitto Kabwe haonekani kuandamana na makamanda wenzake, wakati akiwa Kaimu Katibu Mkuu ambaye ndiye kijana wa kuwa mstari wa mbele katika mapambano.

Isitoshe hata kikao hiki kilichofanyika Jijini Dar alitazamiwa kuwa katika picha, labda imekatwa alikaa pembeni, tukumbuke yeye ni kiongozi mwandamizi, lakini naona yuko makini kutokea katika picha za misafara ya kumsindikiza Kikwete kutalii. Hii imekaaje?

Tunahitaji Zitto aje kujibu haya, ndio uwajibikaji tunaohitaji sasa hivi. Tunahitaji viongozi wa chama wanaowajibika kwa chama na wananchi chama tunachotegemea kuchukua dola, na hivi kujihakikishia viongozi watakaowajibika kwa wananchi na wananchi wawe na haki ya kuwajibisha wasipowajibika kiutendaji.

Kiongozi anayefanya kazi kwa ujanjaujanja na kukwepakwepa magumu ni hatari kwamba siku yakitokea magumu anaweza kuwatelekeza wenzake na hata kukitelekeza chama chake.
 
Zitto unafiki wake haufikichiki na kila kiongozi chamani anamjua. yuko tofauti na viongozi wote hapo pichani. Ni kama chagulani wa mwanza, kiama chake kinakaribia
 
Hivi Zitto kawafanya nini? FJM anatuhabarisha kwamba Zitto yupo Ughaibuni akiwakilisha Bunge la Tanzania lakini sisi tunamtafuta kwenye mikutano ya CC ya CDM.

Hivi kumbe CDM ina warangi rangi hadi kwenye CC? Au ni mwakilishi wa Chama Rafiki?
 
Last edited by a moderator:
Naona Mh. Freeman Aikael Mbowe ameketi kwa mamlaka ati kisha aishie Uenyekiti tu asipate Mamlaka ya juu? Hilo alilikubali Nyerere na kumachia Kawawa sijui wanasiasa wetu wa sasa wanaweza kufanya hivyo.
 
Hivi Zitto kawafanya nini? FJM anatuhabarisha kwamba Zitto yupo Ughaibuni akiwakilisha Bunge la Tanzania lakini sisi tunamtafuta kwenye mikutano ya CC ya CDM.
Hivi kumbe CDM ina warangi rangi hadi kwenye CC? Au ni mwakilishi wa Chama Rafiki?

images


Kimbunga, Tunashukuru kuhabarishwa kwamba yuko safarini nchi za nje, lakini ukweli haupingiki kwamba Zitto huwa na udhuru katika mikutano na majukumu ya Chadema, lakini hata siku moja sijasikia akitoa udhuru kwa shughuli za bunge au kumsindikiza Kikwete kwenye misafara yake.

Mabadiliko tunayotaka si ya kushika dola tu, ila wananchi tuwe na haki za kuhoji uwajibikaji wa viongozi wetu katika masuala muhimu ya uwajibika, ndicho tunachokifanya. Hilo linaloongelewa mara kwa mara kuhusu Zitto ni uthiitisho kwamba kuna kitu ambacho wengi hawaridhika na mwenyendo wake katika uwajibikaji wa pamoja kama viongozi chamani, yeye akiwa kiongozi mwandamizi.

Ikitokea uchaguzi ujao akiachwa nje ya CC kuna wanatakaolalamikia uamuzi huo, lakini kwa sasa wanajenga utetezi wa kumtetea. Tuwe wazi jamani, na kama anasikia malalamiko haya anatakiwa kuyafanyia kazi zi kuyadharau na kufanya mambo kiujanjaujanja.

Jukumu la uongozi si la ujanja ujanja, ndio maana tunaona yanayoendelea nchini mwetu sababu ya huu mtindo wa kuongoza nchi kiujanjaujanja.
 
Naona Mh. Freeman Aikael Mbowe ameketi kwa mamlaka ati kisha aishie Uenyekiti tu asipate Mamlaka ya juu? Hilo alilikubali Nyerere na kumachia Kawawa sijui wanasiasa wetu wa sasa wanaweza kufanya hivyo.

Tuna mengi ya kujifunza toka kwa Mzee Madiba, kwani wachache sana wenye kuwa na moyo huo wa kuona nafasi zao kwa sasa zinawatupa mkono na kinachotakiwa ni kushika kipindi kimoja kuonyesha njia ya kupita ili wanaomfuata wasipotee njia.

Naamini kizazi cha leo inawezekana tu kama mfumo wa uongozi unabadilika kwa kutanguliza zaidi uwajibikaji na kujitolea badala ya kuzidi kuongeza mianya ya ulaji kivutio kinachokuwa urimbo kwa wengi hata kuwa tayari kuua ili mradi kulinda nafasi katika kiti chake.
 
Na hawa wakoloni mgongoni mwa slaaaa wanasubiri nini kama si kutupiga mnada?? Wao wana kwao watuachie nchi yetu
 
Anasubiri apewe deaal ya kulipua ili liwe azimio serikali itekeleze na kumpatia umaarufu yeye...sasa akishiriki kwenye CC ya leo na maamuzi yake yasitekelezwe unadhani atakuwa maarufu....!
 
Jamani Zitto yuko nje ya nchi kama mwakilishi wa bunge la Tanzania CPA.

images


FJM, Umenikumbusha kwamba kamati hii ipo kikazi sehemu fulani nje ya nchi, pamoja na ukweli huo, ukiangalia picha hii utagundua kuwa pamoja na kuwa marafiki, Filikunjombe ni wa kujituma kwa sana tu bila kujibakisha hata yuko makini kuelezea uozo kwa uwazi wa chama chake yeye akiwa mfano wa wazi katika utendaji jimboni mwake, hii ni tofauti na Zitto ambaye anapima kutoka kifua mble mahali ambapo hakuna matatizo yanayoweza kumpata.

Huu si ujasiri tunaotegemea vijana wa leo, ni ujanja ujanja kama alivyowahi kumwambia Speaker Anne Makinda kwamba hatamweza kwani atatumia ujanja wa chuoni hata ashindwe kumwajibisha kuhusu kutotia kitabu cha mahudhurio bungeni.
 
Swali la kuuliza ni je, katika mkutano wa kamati kuu Godbless Lema anakaa meza kuu kama nani?

Kama mmoja wa wahusika katika meza kuu hayupo, kiti hakiwezi kubaki kitupu, kuna mmoja ataitwa kuja kiti kutokana na heshima yake aliyojijengea katika chama.

Wakumbuka maneno haya katika misahafu kwa lugha ya kilatini: "amice ascente superio" tafsiri yake (unapoalikwa usikae kiti cha mbele arusini hadi mwenye kukaribisha wageni atakapokuambia, rafiki yangu njo huku mbele zaidi, ndipo utakapokuwa na heshima mbele ya watu).
 
Hivi Zitto kawafanya nini? FJM anatuhabarisha kwamba Zitto yupo Ughaibuni akiwakilisha Bunge la Tanzania lakini sisi tunamtafuta kwenye mikutano ya CC ya CDM.

Hivi kumbe CDM ina warangi rangi hadi kwenye CC? Au ni mwakilishi wa Chama Rafiki?

kuna mtu aliwaulizia humu ndani.CDM haiishi wasurprice watu pessimistics.who knows next time ataumbuliwa, mukama alishaonja adha ya umbea.
 
Zitto Kabwe msubirini 2015 atakapokuja kuchukua form ya kugombea urais nyie pigen kazi kwanza.
 
images


FJM, Umenikumbusha kwamba kamati hii ipo kikazi sehemu fulani nje ya nchi, pamoja na ukweli huo, ukiangalia picha hii utagundua kuwa pamoja na kuwa marafiki, Filikunjombe ni wa kujituma kwa sana tu bila kujibakisha hata yuko makini kuelezea uozo kwa uwazi wa chama chake yeye akiwa mfano wa wazi katika utendaji jimboni mwake, hii ni tofauti na Zitto ambaye anapima kutoka kifua mble mahali ambapo hakuna matatizo yanayoweza kumpata.

Huu si ujasiri tunaotegemea vijana wa leo, ni ujanja ujanja kama alivyowahi kumwambia Speaker Anne Makinda kwamba hatamweza kwani atatumia ujanja wa chuoni hata ashindwe kumwajibisha kuhusu kutotia kitabu cha mahudhurio bungeni.

Unajua chuki, majungu na unafiki vimekujaa hadi hueleweki unachokisema. Tulia wewe.
 
Acheni kuchonganisha watu! Waacheni CDM wenyewe waseme kuhusu Zitto! Kuna vikao halali vya kusema hivyo. Kamati kuu wenyewe hawajasema kukosekana kwa Zitto, na inawezekana kabisa aliwapa baraka akisema I agree and Support whatever you decide!
 
zito ni msomi mwenye akili timamu. Hawezi kuhudhuria vikao vya kinafiki. Chama makini hakiwezi kutafuta picha za kwenye mitandao na kupoteza muda kuziangalia halafu na kutoa machozi kwa glaa uilty consiousness maana wao ndo wanawatuma watu, wakidhurika na polisi wanabaki kupiga usanii. Sasa wanalia nini?? Kama wangetii amri ya kusubiri sensa huyu mwandishi angekufa?? Ni kipi walichokiona ambacho walikuwa hawajakiona?? Mungu ataihukumu CHADEMA kwa unafiki na uzandiki. Huwezi kupoteza muda wa watu unawadanganya eti unataka kuwakomboa wakati unatafuta kula na njaa zako tu. Mshahara wa Slaa ni Mamilioni. Kwa nini asijilipe angalau hata milioni mbili tu?. Tusubiri uchunguzi wa Polisi habari itapatikana. Zitto wa watu mnamuonea bure mnamchinganisha, na hata kwenye hii jamii forum eti mnampambanisha na Slaa. Jamani acheni kuwagawa wa Tanzania. Ukwelo utawambua tu siku si nyingi. Mkamia maji hayanywi

Lijitu hata kuandika halijui, si upite tu kama huna hoja?? Ptuuu.
 
Back
Top Bottom