Zitto na Wabunge, Zitto na CHADEMA, Zitto na Urais...

li, kuhusu zitto kunitmia, jamen ndo mana nasema hawa watu wanaonijadili hawanijui. mim siwez ktmiwa na zitto! zitto akiwa na story yenye vigezo naweza muandika hata mara mia. ktk hlo siyumbi mim ni journalist. tatu, jamani, rejeeni maktaba muangalie story za epa. nilikuwa bega kwa bega na dk slaa tngu alipolipua bungeni n uraiani, hadi ernst n young na hadi balali anafukuzwa! cjui dk slaa aliwah kunipa sh ngap mana nimemuandika kuliko zitto! mim sinunuliki, nina msimamo na ni mwanamapinduzi wa kweli. kuh

aisee!uyu ndio uyo mwandishi wa mwananchi??gazeti linaloongozwa kwa kusomwa nchini!!!

Hii nchi ipo katika hali mbaya sana kama waandishi wenyewe ndio hawa..ebu angalieni anavyowasilisha hoja zake..inauzunisha sana...oooh Tanzania yangu!!
 
Napita nawaachia wakubwa waseme, lkn wote wanajua kuwa wanafaa, lkn wanachama bado hawajasema chochote.
 
kweli zito ni mzt ndo mana haishi kujadiliwa.
sory, napita tu
 
KITAKACHOIUA CHADEMA NI UKABILA NA UKANDA. NA HAWAMTAKI ZITO KWA SABABU HATOKI KASKAZINI. ILA NZITO ANGETOKA KASKAZINI AU ANGEKUWA MCHAGA ANGEPITA HATA KABLA YA HIYO 2015. watu wa kaskazini wanaitaka nchi hii kwa gharama yeyote ile. mimi kumbukumbu yangu tokea yameingia mageuzi tanzania . i mean mfumo wa vyama vyingi kila uchaguzi wa raisi unapofanyika basi katika wagombea uraisi wa kutoka kaskazini hawapungui asilimia 70. tokea enzi za MREMA RAISI, MVUNGIetc
 
Zitto na Jack Zoka pia, tuwe macho na uhusiano huu

Uhusiano kati ya Zitto na Jack Zoka ambao uliwekwa wazi na vyombo mbalimbali ni taarifa mbaya kwa wanasiasa na wananchi wanaoipenda taifa lao la Tanzania. Uhusiano huu wa Zitto na Jack Zoka ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa TISS (usalama wa taifa) umeripitiwa kuwa na historia ndefu tangu wakati wa uchaguzi mkuu. Wakati Zitto anajitapa kuwa anatetea maslahi ya wananchi, mshirika wake wa chanda na pete Jack Zoka anatuhumiwa na wanasiasa na wanachi kufanya kazi ya kuwadhuru badala ya kulilinda taifa. Kama mshirika wa Zitto anadhuru wananchi ni wazi kuwa naye Zitto ana masalahi binafsi na mabaya kwa wananchi. Maana ukitaka kujua tabia ya mtu, uliza tabia ya rafiki yake. Ni jambo la kusikitisha Zitto kuwa na uhusiano na huyu mfanyakazi wa usalama wa taifa anayedhuru watu na wakati huohuo anajidai kuwa ni mpambanaji. Uhusiano wa Zitto na Jack Zoka ulishawekwa wazi kuwa walikuwa wanawasiliana kwa simu mara kwa mara wakati wa kipindi cha uchaguzi. Tuwe macho na urafiki wao na ambao si mwema hata kidogo kwa wanasiana na wananchi wenye uchungu na taifa letu.
 
[h=2]Mdee naye amkana Zitto na Urais...[/h]
Kwenye barua yake kwenda kwa uongozi wa juu wa gazeti la mwananchi, hii ni sehemu ya barua yake.

Nasikitika kutumia nafasi hii kukuandikia kukutaarifu kuwa gazeti lako la Mwananchi la Julai 23, 2012, katika habari yake iliyoongoza ukurasa wa kwanza (lead story) limenilisha maneno na kunikuu isivyo sahihi.

Katika habari hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho “Wabunge wamsafishia Zitto njia ya urais 2015,” gazeti lako limeandika hivi “Mdee aliyepewa nafasi ya kuwasalimia wananchi alisema amekuwa na Zitto tangu Chuo kikuu cha Dar es Salaam na kwamba kutokana na ujasiri na umahiri wake katika kutetea masilahi ya wanyonge na taifa, anafaa kuwa mmoja wa viongozi wa juu katika Taifa.”

Gazeti lako pia katika aya iliyofuata limenukuu kuwa mimi nimesema;

“Ndugu zangu watu wa Kigoma, kwa kweli mna bahati sana, achilia mbali kuwa na vipaji katika sanaa ya muziki na michezo hasa mpira wa miguu, lakini mna wanasiasa wakali ambao ni tishio hapa nchini. Mimi namkubali sana Zitto Kabwe na ninaamini kuna siku atakuwa kiongozi wa juu katika nchi yetu," alisema Mdee”

Nasikitika kusema kuwa gazeti lako limeandika habari zisizo za kweli kwa kunilisha maneno na kudai kuwa mimi ndiye nimesema maneno hayo, kisha kuyaweka kwenye nukuu, likisema kuwa ni nukuu yangu. Sijajua nia au kusudio la gazeti lako kuamua kupotosha ukweli na kushindwa kabisa kuninukuu kwa usahihi, kama inavyotakiwa katika misingi ya taaluma ya habari.

Nasikitika pia kusema kuwa gazeti lako ambalo limeonekana kujijengea heshima miongoni mwa wasomaji wa kada mbalimbali nchini na hivyo linapaswa kuwa mfano wa kuigwa, linaweza kusigina misingi ya uandishi wa habari na hususan katika kufuata maadili ya taaluma hii muhimu, kwa kiwango cha kufanya moja ya dhambi kubwa ya kukilisha maneno chanzo cha habari.

Kwa ajili ya kutunza heshima ya gazeti lako, lakini pia kwa ajili ya maslahi mapana ya taaluma ya habari na jamii ya Watanzania, nakuandikia kulitaka gazeti lako likanushe maneno liliyoninukuu katika toleo hilo la Julai 23, 2012. Ni vyema sana hilo likafanyika kwa uzito unaostahili kama ilivyoandikwa katika toleo hilo.

Habari hiyo imeniletea usumbufu mkubwa hasa kwa wanachama wa chama changu, CHADEMA, ambao wanajua kuwa chama chao makini ni mahiri katika kufuata katiba, kanuni na taratibu katika kuendesha mambo yake kwa manufaa ya watu wote. Napenda kuwa mmoja wa Watanzania makini na viongozi wanaojua wajibu, ikiwemo kufanya nini na kusema nini, mahali gani na wakati gani.

Nakutakia utekelezaji mwema katika hilo.
 
hahaha wale wa Slaa mapovu yanawotoka kweli kweli ama kweli ZZK ni zaidi ya tishio kwao
 
I alwayz believe Zitto atakuwa mtu wa kwanza kuivuruga chadema one day, bt how and when mi nasubiri tuuuuu! binafsi though jamaa hua na upeo na points za hapa na pale kwenye masuala nyeti ila kwa kweli simuamini kabsaaaaaa hata kidogo, nadhani ana tamaa ya madaraka au ana njaaa sana. Ngoja nisubiri
 
Haya mambo yanaelekea kulekule ya Rutto na Railla Odinga, hapa mimi naona kung'aa kwa Zitto na kukubalika kwake ndio kunakuza chama jamani, 2ache mtimanyongo kama anaweza kuchukua Urais 2015 kwanini 2cmpe nia yetu ni mabadiliko sio unafiki? Kijana kigoma kaonyesha mabadiliko ya dhahiri kabisa, kutangaza kwake nia ni ushujaa wa wazi wa kujikubali!
 
Haya mambo yanaelekea kulekule ya Rutto na Railla Odinga, hapa mimi naona kung'aa kwa Zitto na kukubalika kwake ndio kunakuza chama jamani, 2ache mtimanyongo kama anaweza kuchukua Urais 2015 kwanini 2cmpe nia yetu ni mabadiliko sio unafiki? Kijana kigoma kaonyesha mabadiliko ya dhahiri kabisa, kutangaza kwake nia ni ushujaa wa wazi wa kujikubali!

Tatizo lipo moja tu na la msingi, WAKATI.
Huu sio wakati muafaka.
Nadhani unajua kuwa chama chake kipo katika harakati za kuunganisha Watanzania kujikomboa kupitia M4C.
Pia nadhani unajua kuwa naye ni mmoja kati ya viongozi wa juu kabisa wa chama hicho.
 
Zito ni muislamu, hatufai ndani ya CHAMA ni bora
aondolewe mbona kuna wachungaji wengi wazuri tu
wanaweza kuchukua nafasi yake. Hivi hamuoni kuwa
waislamu waklishika nchi inaenda vibaya?

acha ujinga wewe, siasa na dini ni sawa na ncha mbili ambazo hazikutani.Issue ya zitto cdm sio dini bali ni matendo yake na uswahiba usiotetereka na maadui wa kisiasa wa cdm mfano: Magamba kupitia kwa JK.
 
Tatizo lipo moja tu na la msingi, WAKATI.
Huu sio wakati muafaka.
Nadhani unajua kuwa chama chake kipo katika harakati za kuunganisha Watanzania kujikomboa kupitia M4C.
Pia nadhani unajua kuwa naye ni mmoja kati ya viongozi wa juu kabisa wa chama hicho.

nakubaliana na wewe. Zitto avute subira,chama kiimarishwe chn ya Dr. Baadae atafaa kuiongoza nchi la chama kitagawanywa kwa uroho wa madaraka.
 
Zitto Kabwe ni Utoto unaomsumbua nawahakikishia akikua ataacha, na ndio maana haina ubishi kuwa Zitto anatumika kuleta migogoro ndani ya CDM isiyona Tija, na niwachache ndani ya CDM wanaoweza kukubaliana nae ila ni wengi mno nje ya CDM wanaompa kiburi na jeuri hii, am sure wote wanaomshabikia hakuna anaeweza kumpa kura, na akitaka ajue Kwamba CDM ni Umma na si yeye atoke CDM akatangaze kugombea Urais ADC aone kama kuna watu watamjadili na kumwona wa maana, Zitto ni Tatizo CDM
 
Back
Top Bottom