Zitto na ndoto za kusadikika

Jasho la Damu

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
956
120
Najaribu kutazama mienendo ya Mhe Zito Zuberi Kabwe na kukuta ndoto nyingi za kusadikika alizokuwa nazo.
Ukweli ni kwamba ni dhamira ya wazi ya ndg Zito kabwe kutaka kujenga historia katika nchi hii ya kuwa Kiongozi wa juu ambaye kijana zaidi ndani ya chama na serikali kama alivyopata wahi kuwa Mwl.Nyerere. Ndani ya chama kwa maana ya kuwa M/kiti na ndani ya Serikali kwa maana ya kuwa Rais. Ni ndoto nzuri kwake lkn bila shaka anaona kuna vizuizi vingi vitakavyozuia ndoto zake kutimia.
 
Ni ukweli usiopingika miongoni mwa wanaCDM na watz walio wengi wanaamini ya kwamba kuna watu ambao wana uwezo mkubwa kuliko Zito wa kushika madaraka anayoyaota Zito pengine hii inatokana na uzoefu waliokuwa nao katika siasa ama uwezo wa kufumbua na kutafuta suluhisho la matatizo ya watz.
Hakuna siri tena, Matatizo ya Zito yameanza kuonekana baada kushauriwa kuacha kugombea nafasi ya Uenyekiti ndani ya CDM.
Nyerere aliwai kumkataa Kikwete kwa kisingizio cha umri mdogo leo kikwete ni over 55 yrs old.
 
Pamoja na Kikwete kuwa umri mkubwa lkn leo hii tunaona nchi inavyoyumba kwenye nyanja zote za kiuchumi na kisiasa. Simaanishi kwamba nyerere alikosea kumkataa kikwete kwa kigezo cha umri bali umri ulikuwa ni fumbo la kumaanisha hana uwezo wa kuongoza, leo imethibitika na tunajionea. Siamin kama leo hii nyerere angekuwepo CDM angekubali Zito awe m/kiti ama awe Rais. Wana Cdm tuwe makini tusirudie makosa tuliyoyafanya kwa JK 2.

viva CDM, viva Tanzania.
 
duh, nahisi maada ina kile kiarufu ambacho hakizoeleki. subiri michango ya great thinkes na wanaharakati.
ainisha hayo matatizo ya zitto ili tuende sambamba na pia vigezo ulivyotumia kupima uwezo wake ukilinganisha na wanaCDM wengine.
 
duh, nahisi maada ina kile kiarufu ambacho hakizoeleki. subiri michango ya great thinkes na wanaharakati.
ainisha hayo matatizo ya zitto ili tuende sambamba na pia vigezo ulivyotumia kupima uwezo wake ukilinganisha na wanaCDM wengine.

Huhitaji kuumiza kichwa khs uwezo wa Zito na Dr.Slaa na wengineo wafananao slaa.Kuhitaj umaarufu binafsi kuliko chama ni tatizo pia.Angalia hoja za Zito ndani ya chama na jamii kisha compare to Dr. Slaa n etc
 
Pamoja na Kikwete kuwa umri mkubwa lkn leo hii tunaona nchi inavyoyumba kwenye nyanja zote za kiuchumi na kisiasa. Simaanishi kwamba nyerere alikosea kumkataa kikwete kwa kigezo cha umri bali umri ulikuwa ni fumbo la kumaanisha hana uwezo wa kuongoza, leo imethibitika na tunajionea. Siamin kama leo hii nyerere angekuwepo CDM angekubali Zito awe m/kiti ama awe Rais. Wana Cdm tuwe makini tusirudie makosa tuliyoyafanya kwa JK 2.

viva CDM, viva Tanzania.
Hivi kweli wewe ni mwanachama wa CDM? Au wewe ni wa magamba? maana haiingii akilini mfuasi wa CDM kuja hapa jamvini na kumwaga sumu za uchonganishi kwa viongozi!....mara ya kwanza mlisema oooh Zitto hashiriki maandamano na amejitenga na wapiganaji....sasa leo Zitto kaamua kurudi kundini alafu mtu kama wewe unakuja kumwaga upupu mwingine. Haipendezi mkuu!
 
Umesimamia wapi we mwanaharakati mbona kama hueleweki vile? Huwa unashirikisha ubongo au hisia tu? Hii nchi ina kazi kweli kweli we ndo tukutegemee kwenye mustakabali wa nchi? JIPANGE TU MKUU!
 
Hii gharama ya kuwa muha ndani ya kampuni ya wachaga, utatukanwa kila kukicha hadi ukome. Lakini na wewe kiboko unawamiliki wote kuanzia mwenye kampuni,CEO hadi vinuka mkojo wote.
 
Mwandishi anaonesha dhahir kua anachuki binafsi na Mh Zito,Kwani yale maneno anayo yasema dr slaa si anapashwa na watu wake wa chini au aningia mitaani kutafuta hoja?i

Sioni hiyo tofauti ya Dr Slaa na Zito na huenda ikawa zito ni bora zaidi kwakua ni kijana na siasa amezianza mapema zaidi.

Zito nikiongozi mzuri na simbaguzi na hashabikii siasa za chuki.
 
Hivi kweli wewe ni mwanachama wa CDM? Au wewe ni wa magamba? maana haiingii akilini mfuasi wa CDM kuja hapa jamvini na kumwaga sumu za uchonganishi kwa viongozi!....mara ya kwanza mlisema oooh Zitto hashiriki maandamano na amejitenga na wapiganaji..

Wana-CDM hatuwez kufumbia macho mabaya anayofanya zito ndani ya chama kwa kuhofia atachukiana na viongozi wenzake. Hatutasubiri mpaka CDM ijivue ndo tuanze kutafuta mchawi il hali tulimfahamu na tukamficha kwa woga. wake up
 
tatizo la cdm
wengi wao ni wanaharakati but sio leaders
unaweza kuwa mwanamapinduzi au mwanaharakati mzuri sana

but to be a government leader ni shughuli nyingine
 
Tusiwe wavivu wa kufikiri ama kupenda hata kinachokuumiza. Simchukii Zito, tena alikuwa role model wangu wakati alipokuwa na dhamira ya kweli ya kumtetea mtz mnyonge lkn sasa hiyo dhamira inatoweka kwa kasi ya ajabu. Ni lazima tumkosoe ili afahamu mapungufu yake.
 
Hapa wanajamakii mnatudanganya nilicho waelewa ni kuwa zito co wenu.nandomana leo mnamuita kaswahili,mara mdogo,unazani unaweza kumfananisha na mbowe? Misijaona tofauti ya dr.slaa na Zito. Au ni hio Phd ya Theology ya Rome? Kama hamumtaki mnyanganyeni hyo nafac .kwani kigoma wanamchagua kwa kuwa ye ni CDM?WANAMCHAGUA KWAKUA MPIGANAJ Ndomana kigoma almost imechukuliwa NCCR.Chukua mwanangu hyo. Naamin zito ndo kichwa chadema na anaweza hamuoni marais vijana duniani na misimamo yao?zito anaweza zito anaweza. Kinyume na hapo chadema inaagenda nyingne nyuma ya pazia.mnatutisha wenzangu wapiganaji.
 
tatizo la cdm
wengi wao ni wanaharakati but sio leaders
unaweza kuwa mwanamapinduzi au mwanaharakati mzuri sana

but to be a government leader ni shughuli nyingine

Sijui kama unafahamu ulichoandika! kwani kuwa govt leader ni lazima uwe fisadi, muongo au mwizi? usituaminishe ujinga.
 
Huhitaji kuumiza kichwa khs uwezo wa Zito na Dr.Slaa na wengineo wafananao slaa.Kuhitaj umaarufu binafsi kuliko chama ni tatizo pia.Angalia hoja za Zito ndani ya chama na jamii kisha compare to Dr. Slaa n etc

Mmmh mie napita, lakini hako katatizo kweli kapo ila tu muangalie tu hi sredi inavyotekwa taratibu na wa magamba, otherwise ni busara kutokuizungumzia kwa sasa kwani tuna mengi mengine!
 
Mmmh mie napita, lakini hako katatizo kweli kapo ila tu muangalie tu hi sredi inavyotekwa taratibu na wa magamba, otherwise ni busara kutokuizungumzia kwa sasa kwani tuna mengi mengine!

Kuwa mwanachama wa CDM haimanish hauna uhuru wa kukosoa viongozi wako, siku zote mficha maradhi kifo kinamuumbua.Tusipojifunza kupitia Mrema na nccr, CCM na kujivua gamba, basi CDM itakufa haraka kwa kuendekeza hofu ya kutukuzana.
 
Mbona kuna mambo mengi ya kuzungumza au kushauri chama kuliko hili lako la kumsakama mtu mmoja,hebu shauri kuliko kubomoa au kumlenga mtu,humkubali zito uchaguzi wa chama ukifika chukua fomu gombea nafasi zake labda utakuwa na mchango mkubwa kichama kuliko zito,Zito bado anabaki kuwa ni kiigizo(role mode) wa vijana ktk siasa za vyama vingi(wapinzani) nchini.acha mipasho mzee yusufu bado anahitaji watu wakiimba nae
 
Mimi nahisi kuwa kny hii chadema kuna siri nyingine,mbona wadau wanamsakama zito sanaaa!ok chamaana kwani ha2wez kumchagua naibu katibu wa chama m2 mwengine kama mnaona hafai,kaswahili! nanikwel mswahili kwa tafsir niijuayo? Tuache fikira za kijinga juu yake mnaanza kikiarabu kakikundi ke2 cha Kiroma kwani yeye haucki nini?.Ok chadema bila zito haiwezekani? ndo mana mlisababisha mandamano kigoma yalishndikana.2jipange wanangu wenyewe majungu juu ya zito co pouwa.
 
Pamoja na Kikwete kuwa umri mkubwa lkn leo hii tunaona nchi inavyoyumba kwenye nyanja zote za kiuchumi na kisiasa. Simaanishi kwamba nyerere alikosea kumkataa kikwete kwa kigezo cha umri bali umri ulikuwa ni fumbo la kumaanisha hana uwezo wa kuongoza, leo imethibitika na tunajionea. Siamin kama leo hii nyerere angekuwepo CDM angekubali Zito awe m/kiti ama awe Rais. Wana Cdm tuwe makini tusirudie makosa tuliyoyafanya kwa JK 2.

viva CDM, viva Tanzania.

Inayumba? huu si ukweli. nyerere ndio aliiyumbisha sana hii nchi, labda hamuelewi wala hamsomeshwi yaliyojiri wakati wake. Sijui kama umewahi kusikia tarehe 20, sijui kama umewahi kusikia, kesi za majaribio ya kupinduliwa kwa nyerere? sijui kama umewahi kusikia kesi za uhaini wa Zanzibar, sijui kama umewahi kusikia namna alivyodhulumu watu mali zao? sijui kama umewahi kusikia alivyohamisha watu kwa nguvu kwenda vijivji vya ujamaa na wengi wao kufa kwa njaa, maradhi, kuliwa na wanyama wakali, kugongwa na nyoka? sijui kama umeshawahi kusikia ya Mwamwindi? sijui kama umewahi kusikia ya Kambona? sijui kama umewahi kusikia ya Mtemvu? sijui kwama umewahikusikia ya Chipaka? sijui kwama umewahi kusikia Y Suleima Takadiri? sijui kama umewahi kusikia Hashim Haji Abdallah? na mengi sana mengineyo.

Nyerere was never a saint as depicted.
 
Kwa kanisa nyerere alikua mtakatifu kwakua alikua mstari wa mbele kuipigania katolik na kulilinda kanisa ukitaka kujua haya soma vitabu hv.KANISA KATOLIKI NA SIASA ZA TANZANIA BY padre mkatoliki John Shivalon,pia soma The guardian angel by Anord Besase wa uganda.wacha hii nchi mnasema hamna dini ni uongo ukitaka kujua tena umeshawah kusoma barua knda kwa Papa JP.kuwa kanisa ki2 cha kujivunia ni kuwa na Tume ya kijesh ya kivita ya katoliki!je ni yanini? Kwahyo cshangai kupigwa kwa vijembe kwa Jk,cunajua tena nchi inayo dini!dini yenyewe nihyo yenye Chama cha dini Mndelevu na Maandamano na hii ya China Chama Mwalimu. Kwani hujaona hata Kabwe anaitwa mswahil bado hujaelewa 2.!
 
Back
Top Bottom