Zitto na harakati za kumwondoa waziri mkuu

mmeku

Member
Aug 7, 2011
43
11

Zitto aendelea kutafuta saini


Katika hatua nyingine,Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema hoja ya kumpigia Waziri Mkuu kura ya kutokuwa na imani ipo pale pale kama mawaziri wanaotajwa kwa ufisadi hawatajiuzulu kufikia kesho.
“Sisi tunasema bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa mawaziri waliotajwa hawatatoka na wasipotoka madudu haya yatarudia…kwa hiyo ni wao mawaziri kupima na kuwajibika au wamweke reheni Waziri Mkuu,”alisema.
Mbunge huyo alirejea wito wake wa kuwaomba wabunge wenye uchungu na ubadhirifu na ufisadi waunge mkono utiaji wa saini hizo na kwamba kama mawaziri watajiuzulu ifikapo Jumatatu, wataondoa hoja hiyo.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Kambi rasmi ya upizania Bungeni, Freeman Mbowe alirejea msimamo wake wa kuomba kufanyiwa mabadiliko ya katiba ya nchi na kanuni za Bunge ili Spika asiwe anatokana na chama chochote cha siasa.
Mbowe alitoa kauli hiyo kutokana na kile alichodai, hatua ya Spika Anne Makinda kutafsiri vibaya kanuni za Bunge na Katiba ya nchi ili tu kuilinda Serikali na Waziri Mkuu wake ili asipigiwe kura ya kutokuwa na imani.
“Mambo ya ajabu sana eti Spika anasema hili zoezi letu ni batili…sisi tunamshangaa, wanasheria wanamshangaa na hata wananchi wanamshangaa… anatoleaje mwongozo kwa kitu ambacho hakipo mezani kwake?”alihoji.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, alisema kanuni inataka ili hoja ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Waziri mkuu iweze kufikishwa ofisi ya Spika, ni lazima ipate sahihi za wabunge 70 na ndicho wanachokifanya.
 
Back
Top Bottom