Zitto, Mnyika wafichua upotoshaji bajeti ya Mkulo; Spika Makinda akiri, amtaka Mkulo arekebishe

Zitto,

Nakuheshimu sana mdogo wangu.

Nasikitika sana ninapoona, kwa umakini wako wote ulionao, unaaandika kwa kubabaisha na kupotosha. Mimi sijaipitia bajeti yote, lakini hayo ulyoainisha hapo ya ama umefanya makusudi kupotosha katika maandishi yako ya ama hujui namna ya kuandika, hususan ikija kwenye namba.

1. Mstari wa kwanza umeandika "shilingi 537 Bilioni", mstari wa tatu na wa nne ukaandika "shilingi 402,402,071,000 milioni" na "shilingi 76,953,934,000 milioni" na "shilingi 325,448,137,000." halafu mstari wa nne ukarudia tena "Shilingi Bilioni 325".

Swali: Kwanini "shilingi 537 Bilioni" ziwe ni billioni? na kwanini "shilingi 402,402,071,000 milioni" na "shilingi 76,953,934,000 milioni" ziwe millioni? na kwa nini "shilingi 325,448,137,000." ziwe si millioni wala billioni? na halafu "Shilingi Bilioni 325" ziwe tena billioni?

shilingi 402,402,071,000 Equiv to 402.4bilioni kwamba kwenye hotuba ametamka Umeme umetengewa Bil 537 lakini kwenye vitabu, wizara ya nishati na madini imetengewa only bil 402.4
Matumizi ya wizara yatakuwa bil 76.9 matumizi ya kawaida na bil 325.5 maendeleo. [76.9 + 325.5 = 402.4] swali hapo bil 135 za ziada zimeingiaje kwenye hotuba ya Mkullo?
2) Unaeleza kuwa: kiasi cha shilingi 11.6 trilioni wakati mwaka huu wa 2011/2012 serikali ina bajeti ya jumla ya shilingi 13.525 trilioni. Kati ya ya fedha hizo za mwaka 2011/2012, kiasi cha shilingi 1.901 trilioni ambazo ni sawa na asilimia 14.06% ya bajeti yote, kitatumika kulipia deni la Taifa.

Halafu unasema: Kwa mantiki hiyo, mtaona kuwa fedha kwa ajili ya kuendesha serikali pamoja na kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zitabaki kuwa ni kiasi cha shilingi trilioni 11.624 ambazo ni sawa na fedha za bajeti ya mwaka uliomalizika wa 2010/2011

Swali : Mbona hizo "shilingi trilioni 11.624" "za bajeti ya mwaka uliomalizika wa 2010/2011 huoneshi ngapi kati ya hizo zililipa madeni?

3) Swali: Jee, bajeti ya mwaka uliomalizika wa 2010/2011 zilikuwa ngapi? mbona huoneshi?

4) Kauli ilikuwa baadhi ya posho zitafutwa na baadhi ya posho zitapunguzwa.

Jee, ni nini kilichozugwa hapo?
.
Na kauli uliyowekea "bold" haihusiani na kufutwa au kupunguzwa kwa posho, kauli hiyo inaongelea "kusamehe" kodi, sasa mdogo wangu Zitto huelewi maana ya kusamehe kodi? Kama huelewi, hiyo kauli inamaanisha zile posho ambazo hazijafutwa na ambazo zimepunguzwa na ambazo hazijapunguzwa, zitasamehewa kodi. Sasa nini unachoona hakiko sawa hapo?

5) Labda ili ueleweke vizuri, ungeweka hizo faini ambazo zitafikia 50,000/= na ambazo zitazidi zaidi ya 50,000 na kufikia 300,000/= Usitupotoshe na usiupoteshe umma kwa kuwaambia kuwa huku hivi huku hivi.

Kwa kukukumbusha tuu, ingawa faini za barabarani tunazijuwa kikawaida ni 20,000/= tuliona hata Chenge alichapwa faini ya 700,000/= kwa makosa hayo hayo ya barabarani. Nimekutajia ya Chenge kwa kuwa ndio kesi maarufu na ni wengi wanayoifahamu. Kwa mantiki hiyo, inabidi ufafanue kwa kina hiyo faini ya 300,000 na ya 50,000. Tafadhali usipotoshe watu.

Hapo hapo, sentensi yako hii haieleweki "kwa sababu serikali katika bajeti vyake rasmi vya bajeti imeamua kufanya marekebisho". sijui inamaanisha nini?

6) Jee, ulitaka serikali isilipe madeni? na Jee, ulitaka serikali isilipe posho?, kama hutaki serikali ilipe posho, kwanza onyesha mfano kwa kuzikataa posho zako kama mbunge, kwani mojawapo ya wenye posho kubwa katika watumishi wa serikali ni wabunge. Halafu onesha na takwimu za bajeti iliyopita, asilimia ngapi ililipa madeni na asilimia ngapi ililipa posho. Usiandikie mate na wino upo.

7) Tunaisubiri kwa hamu na kama ni nzuri tutaiomba serikali iifate, kwani upinzani ndio kazi yake kuu, kukosoa ili serikali ijirekebishe.

Kwa kusherehesha tu, ningeomba ajibu Zitto mwenyewe kama anavyonukuliwa kuwa ndio muandishi wa taarifa hii, nikimuomba mleta mada Regia Mtema ajibu ntakuwa sikutenda haki kwani yeye inaonesha kuwa ni kipaza sauti tu cha Zitto.

Nadhani hii taarifa ndio ina kusudio la kupotosha wananchi kwa kuandikwa ndivyo sivyo.

on red
 
Nashangaa sana nnapoona hata Zitto ambae ni Waziri kivuli wa Fedha haelewi "strategy" za kuainisha kulipa madeni kwenye bajeti. Kasoma uchumi kweli huyu?

Unakumbuka Zitto aliwahi kusema kuwa serikali imekopa kulipa mishahara? unakumbuka Mkullo alisema nini?

Naamini anataka kuwakamata hawa jamaa ili waseme kuwa hayo madeni walikopa kwa ajili ya nini? na hatimaye amkamate mkullo kwa uwongo wake , na sio suala jepesi kama unavyotaka kulifanya lionekane hapa.
 
Inasikitisha kama kweli ndio wamechakachua hadi kusoma figures ni hatari sana kuwa na serikali ya aina hii tuliyonayo Tanzania. nimei download hiyo budget iliniisome week end nikiwa nimetulia
 
Tatizo lenu ni kukurupuka, nenda kaisome post #49 halafu urudi useme ni nini kile nilichokionesha.

Post niliyoinukuu haikuwa na maelezo ya #49 sasa sijui nani kakurupuka kama siyo wewe kuweka post isyokamilika. Issue iko pale pale toa figures sahihi zinazochallenge za Zito na implications zake. Kinachozungumziwa ni implications za bajeti kulingana na matumaini ya uongo ya kisiasa kwenye bajeti yanayotplewa naq serikali chovu.
 
Kwa muono wako viongozi walio committed ni hao wenye kutoa taarifa yenye upotoshaji wa makusudi? soma juu kidogo hapo uone mapungufu ya hii taarifa ya waziri kivuli.

Ni kweli viongozi kama Mkullo hawafai kwani haiwezekani mtu tena kiongozi analidanganya taifa kwenye hotuba ya bajeti hii ni hatari.

Jana alisema hii ni bajeti ya nishati ila hakuna pesa huko kwenye nishati sasa hapo si nio kulipotosha taifa ?

Jana alisema kuwa faini itakuwa elfu hamsini kumbe kwenye vitabu imeandikwa ni laki tatu huyu hafai.

Jana alisema watapunguza kodi na tozo mbalimbali kwenye mafuta ila ukisoma bajeti yake yote iliyoko kwenye tovuti ya wizara ya fedha hakuna kipengele hata kimoja kinachozungumzia jambo hilo hii ni hatari kuwa na waziri kama huyu.

Anapaswa aondoke kwani haiwezekani kuwa na waziri kama hyu ni mzigo kwa taifa.
 
Jibu hoja, achana na mimi na gamba langu, mdogo wangu, na kukaa masaki, unafikiri hao unaowataka wakichukuwa uongozi watakuja kukaa "uswazi"? au watakupeleka wewe huko "masaki"?

Think critically and be smart,your not reasonable man,kuwa mzalendo usitetee ujinga,kipi hujaelewa ambacho kimesemwa na ZITTO ili usaidiwe?haya nenda ofisi za CCM ukachukue posho kwa kazi uliyotumwa ya kupinga kila kitu.KIJANA WA NAPE
 
Ni kweli viongozi kama Mkullo hawafai kwani haiwezekani mtu tena kiongozi analidanganya taifa kwenye hotuba ya bajeti hii ni hatari.

Jana alisema hii ni bajeti ya nishati ila hakuna pesa huko kwenye nishati sasa hapo si nio kulipotosha taifa ?

Jana alisema kuwa faini itakuwa elfu hamsini kumbe kwenye vitabu imeandikwa ni laki tatu huyu hafai.

Jana alisema watapunguza kodi na tozo mbalimbali kwenye mafuta ila ukisoma bajeti yake yote iliyoko kwenye tovuti ya wizara ya fedha hakuna kipengele hata kimoja kinachozungumzia jambo hilo hii ni hatari kuwa na waziri kama huyu.

Anapaswa aondoke kwani haiwezekani kuwa na waziri kama hyu ni mzigo kwa taifa.

8. Mheshimiwa Spika, Bajeti ya mwaka 2011/12 itazingatia
vipaumbele vifuatavyo:
i) Umeme;
ii) Maji;
iii) Miundombinu ya usafiri na usafirishaji (reli, bandari,
barabara, viwanja vya ndege, Mkongo wa Taifa);
iv) Kilimo na umwagiliaji; na
v) Kupanua ajira kwa sekta binafsi na ya umma.

Wakati wa faini za 20,000 mbona chenge alipigwa 700,000? Jee si kosa la barabarani?
 
jamani ama kweli ccm ni soo ni hatari hawa watu wanatuumiza hivi hivi tunaona ama kweli chadema mnafaa kuichukua hii nchi hivi mnajua mkiitisha maandamano nchi nzima lazima tutoke na kuelekea ikulu pale yule mzee atoke pale, mimi sina cha kuongezea ila nawshukuru sana chadema kwa kutufumbua macho mzidi kulindwa na Mungu mpaka kieleweke
 
hivi mkuu unajua hata ukiongeza trillion 2 baada ya miezi nane takuwa dola ngapi?
Nani kasifia hiyo miradi mbuzi?
Hili ni tatizo linalotukumba wote, UELEWA. Zitto hazungumzii kuongeza kiwango cha budget anaeleza vipaumbele, posho zitolewe huko ziwekwe kwenye maendeleo.
Hivi unauliza swali au unauliza jibu? Nani kasifia hiyo miradi mbuzi? Ni wewe uliesema miradi ya kusambaza umeme(kama sitakosea ni kusambaza nguzo za umeme , kwani umeme wenyewe hakuna) kutoka Iringa hadi Shinyanga na mengineyo, sio kusifu huko?
 
Chadema yaichana Bajeti ya Serikali Thursday, 09 June 2011 23:37

Neville Meena, Dodoma
KAMBI ya Upinzani Bungeni imedai kwamba kuna upotoshaji mkubwa katika Bajeti ya Serikali iliyowasilishwa bungeni juzi na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, huku ikidai kwamba bajeti hiyo ni ya kulipa posho na madeni.Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kambi hiyo mjini Dodoma na kusainiwa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe inabainisha kuwa upembuzi uliofanywa umebaini kuwapo kwa upotoshaji mkubwa wa kitakwimu na kimaudhui uliofanywa kwalengo la kuwajengea matumaini wananchi.

"Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya bajeti kulipa madeni na kulipana posho (asilimia 27), asilimia 14 kulipa madeni na asilimia 13 kulipa posho mbalimbali," ilisema taarifa hiyo.

Miongoni mwa maeneo ambayo yanadaiwa kuwa na upotoshaji ni kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la umeme, ongezeko la jumla la Bajeti ya Serikali ikilinganishwa na ile ya mwaka 2010/11, posho mbalimbali, faini kwa madereva wazembe na ulipaji wa madeni ya Serikali.

Hakuna mradi mpya wa umeme
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tamko la Serikali kwamba imetenga kiasi cha Sh537 bilioni kwa ajili ya kutatua tatizo la umeme, si kweli kwani kwa jumla Wizara ya Nishati na Madini, imetengewa Sh402.071 bilioni na kwamba hakuna mradi mpya wa umeme hata mmoja utakaoanzishwa.

"Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya matumizi ya kawaida Sh76,953,934,000 na kwa upande wa bajeti ya maendeleo zimetengwa Sh325,448,137,000. Sh325 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ya Wizara ya Nishati na Madini zinatosha kwa mradi mmoja tu wa umeme wa 160 MW, 100 Dar es Salaam na 60 Mwanza,"inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema katika taarifa hiyo kuwa, kutokana na hali hiyo hakuna mradi mpya wa umeme unaoonekana katika bajeti hiyo na kwamba kauli ya Mkulo ililenga zaidi kuwajengea wananchi matumaini hewa na si hatua za kweli kumaliza matatizo ya umeme nchini.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hakuna ongezeko lolote halisia la fedha katika bajeti ya mwaka huu, kwani kati ya Sh13.525 trilioni zilizotengwa, Sh1.901 trilioni, sawa na asilimia 14.06 ya bajeti yote ni kwa ajili ya kulipa madeni ya Taifa.

"Kwa mantiki hiyo, mtaona kuwa fedha kwa ajili ya kuendesha Serikali pamoja na kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zitabaki Sh11.624 trilioni ambazoni ni sawa na fedha za bajeti ya mwaka unaomalizika wa 2010/2011," alisema Zitto katika taarifa yake hiyo na kuongeza: "Kwa kuzingatia kwamba thamani ya shilingi imekuwa ikishuka, bajeti iliyotangazwa ni ya kulipa madeni".

Bajeti ya posho sasa Sh987 bilioni
Kuhusu hatua za kupunguza posho, kiongozi huyo alisema hakuna ukweli wa kauli hiyo kwani Serikali imetenga kiasi cha Sh987 bilioni kwa ajili ya kulipa posho mbalimbali, fedha ambazo ni sawa na asilimia 13 ya bajeti nzima.

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa kutokuwapo kwa nia ya dhati ya kupunguza posho, inaonekana katika hatua za kufanya marekebisho katika sheria ya kodi sura ya 332 ili kusamehe kodi ya mapato katika posho wanazolipwa wafanyakazi wa Serikali na wanaofanya kazi katika taasisi zinazopata ruzuku kutoka kwenye Bajeti ya Serikali.

"Hii inaonyesha kuwa kauli ya kufuta au kupunguza posho ilitolewa na Serikali ili kupumbaza wananchi, lakini haina udhati,"alisema.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa bajeti imeongeza mzigo mkubwa kwa wananchi kutokana na hatua yake ya kuongeza kiwango cha faini kwa madereva wazembe kutoka Sh20,000 hadi Sh300,000, na kwamba kiasi cha Sh50,000 kilichotangazwa na Waziri Mkulo juzi kinatofautia na maelezo kwenye vitabu vya bajeti.

Alisema hatua hiyo itawaathiri wananchi hasa vijana walioajiriwa ama kujiajiri katika huduma za usafiri na usafirishaji na kwamba kipengele hicho pia kinalenga kuuhadaa umma.

Serikali juzi ilitangaza hatua kadhaa za kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima katika mwaka wa fedha wa 2011/2012, lakini fedha za matumizi mengineyo, maarufu kama Other Charges (OC), zimeongezwa kwa asilimia 8.62 ikilinganishwa na Bajeti ya Serikali inayofikia ukomo tarehe 30 mwezi huu.

Fedha za OC katika bajeti mwaka ujao wa fedha ni Sh3.089 trilioni ikilinganishwa na kiasi cha Sh2.823 kilichotengwa katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, likiwa ni ongezeko la Sh266.599 bilioni.

Fungu la fedha za OC ndilo hutumika kugharimia posho mbalimbali kwa watumishi wa umma na uendeshaji wa semina, warsha na makongamano pamoja na kugharimia safari za viongozi ndani na nje ya nchi.

Kafulila adai bajeti haijazingatia vigezo vya uchumi
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila aliliambia Mwananchi katika viwanja vya Bunge kuwa, hali hiyo inadhihirisha kwamba bajeti iliyowasilishwa na Mkulo ililenga zaidi kutafuta kuungwa mkono kuliko kuzingatia vigezo vya kiuchumi.

"Kama mwaka wa fedha unaoishia mwishoni mwa mwezi huu fedha za OC ni kidogo kuliko zile ambazo zimetengwa mwaka ujao wa fedha, basi ni dhahiri kwamba hatuwezi kusema posho zitapunguzwa, hapa nadhani kuna tatizo,"alisema Kafulila.

Alisema fungu la fedha za OC lazima lipitiwe upya kwani fedha zilizotengwa ni zaidi ya kiasi cha fedha ambazo Serikali imeomba kutoka kwa nchi wahisani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

"Iwapo fedha za OC ni Sh3 trilioni na fedha za miradi ya maendeleo tunazoomba kutoka kwa wafadhili ni kiasi hicho hicho, utaona kwamba ni jambo la kushangaza, hapa kuna mambo mengi ya kuweka sawa,"alisema Kafulila, huku akibainisha kuwa bajeti hiyo ya Serikali si mbaya sana kwani imekumbuka umuhimu wa miundombinu ya usafirishaji.

Akiwasilisha bungeni juzi Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/12, Waziri Mkulo alibainisha hatua kadhaa za Serikali kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima akiahidi kupunguza posho zisizo na tija, safari za ndani na nje za viongozi na ukubwa wa misafara ya viongozi hao ili fedha husika ziweze kutumika kugharimia shughuli nyingine za maendeleo.

"...........Serikali itasitisha ununuzi wa samani za ofisi, hususan zile zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija, kupunguza matumizi ya mafuta kwa magari ya Serikali, kupunguza safari za ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na ukubwa wa misafara na kuendelea kupunguza semina na warsha, isipokuwa pale inapobidi na kwa kibali cha Ofisi ya Waziri Mkuu..," alisema Mkulo.

Sh3 trilioni kutoka nchi wahisani
Kadhalika majedwali ya ufupisho wa hesabu za bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12 yanabainisha kuwa fedha za maendeleo zinazotarajiwa kutoka kwa nchi wahisani ni kiasi cha Sh3.054 trilioni. Kiasi hicho kinazidiwa kwa asilimia 18.9 sawa na Sh5.853 bilioni kikilinganishwa na fedha za OC ambazo ni Sh3.089 trilioni.

Katika bajeti hiyo, fedha zote zilizotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Sh4.925 trilioni, ambapo fedha za ndani ni Sh1.871 trilioni.
Mchanganuo mzima wa bajeti hiyo unaonyesha kuwa fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa ni sawa na asilimia 31 ya bajeti nzima, wakati fedha za matumizi mengineyo (OC) ni sawa na asilimia 32, mishahara asilimia 23, malipo ya madeni asilimia 8, madeni mengine asilimia 3 na riba ya madeni ya ndani na nje asilimia 3.
 
Mwalimu,
Zitto kasema serikali haijawekeza fedha nyingi kwenye nishati,
Nikasema...hata mimi siisifii miradi mbuzi ila kihistoria,serikali hutegemea wahisani kwenye miradi ya nishati,kwani wewe umeona hapo kwenye bajeti wamezungumzia hata huo mradi wa NSSF kuwekeza kiwira ili kuzalisha 400mw?..kwa mfano tu!
Kama hujaona,haimaanishi huo mradi hautafanywa,may be still NSSF itawekeza..naomba uelewe hii kwa sababu nasikia headache kwa kukuelewesha.
 
1. Nadhani Zitto anajua kuwa nishati hapa Tanzania hujengwa kutokana na misaada na mikopo kutoka nje.Hata TANESCO hutafuta funds na mikopo kutoka nje ya serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali,mfano ule wa kusambaza umeme kilomita 667 toka Iringa mpaka shinyanga ambao umekuwa funded na European Investment Bank,shs bilioni 150...je ulikuwa kwenye bajeti yoyote?

2.Kulipa deni la taifa ni moja kati ya matumizi ya maendeleo,ina facilitate uwezo wa kupata mikopo.

3. Kuhusu posho, ni wajibu wetu watanzania, hasa wafanyakazi wa serikali kuamua au kujitolea kutokuzipokea au kuomba kupunguziwa kwa asilimia hamsini..... hapatakalika!

4. Jumatano nakuchallenge Zitto, usome bajeti itakayoonyesha vyanzo mbadala vya kodi na makato ya matumizi, ili elimu iwe bure!...cos you promised this in your campaigns na ilani ya CDM, kama haita-include free education huo utakuwa ni uhuni tu! Ninayo video ya Mnyika akielezea what you will do in your first year kwenye utawala kama mngepata ridhaa.

Hapo mkuu umechemsha! Na hata waliokugongea likes nadhani hawajakuelewa vizuri.
 
brilliance and seriousness ya zitto ndipo ninapoipendea hapa

no doubt ... good job

pull up your socks
 
Chadema yaichana Bajeti ya Serikali Thursday, 09 June 2011 23:37 Neville Meena, DodomaKAMBI ya Upinzani Bungeni imedai kwamba kuna upotoshaji mkubwa katika Bajeti ya Serikali iliyowasilishwa bungeni juzi na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, huku ikidai kwamba bajeti hiyo ni ya kulipa posho na madeni.Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kambi hiyo mjini Dodoma na kusainiwa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe inabainisha kuwa upembuzi uliofanywa umebaini kuwapo kwa upotoshaji mkubwa wa kitakwimu na kimaudhui uliofanywa kwalengo la kuwajengea matumaini wananchi. "Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya bajeti kulipa madeni na kulipana posho (asilimia 27), asilimia 14 kulipa madeni na asilimia 13 kulipa posho mbalimbali," ilisema taarifa hiyo. Miongoni mwa maeneo ambayo yanadaiwa kuwa na upotoshaji ni kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la umeme, ongezeko la jumla la Bajeti ya Serikali ikilinganishwa na ile ya mwaka 2010/11, posho mbalimbali, faini kwa madereva wazembe na ulipaji wa madeni ya Serikali. Hakuna mradi mpya wa umemeKwa mujibu wa taarifa hiyo, tamko la Serikali kwamba imetenga kiasi cha Sh537 bilioni kwa ajili ya kutatua tatizo la umeme, si kweli kwani kwa jumla Wizara ya Nishati na Madini, imetengewa Sh402.071 bilioni na kwamba hakuna mradi mpya wa umeme hata mmoja utakaoanzishwa. "Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya matumizi ya kawaida Sh76,953,934,000 na kwa upande wa bajeti ya maendeleo zimetengwa Sh325,448,137,000. Sh325 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ya Wizara ya Nishati na Madini zinatosha kwa mradi mmoja tu wa umeme wa 160 MW, 100 Dar es Salaam na 60 Mwanza,"inaeleza sehemu ya taarifa hiyo. Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema katika taarifa hiyo kuwa, kutokana na hali hiyo hakuna mradi mpya wa umeme unaoonekana katika bajeti hiyo na kwamba kauli ya Mkulo ililenga zaidi kuwajengea wananchi matumaini hewa na si hatua za kweli kumaliza matatizo ya umeme nchini. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hakuna ongezeko lolote halisia la fedha katika bajeti ya mwaka huu, kwani kati ya Sh13.525 trilioni zilizotengwa, Sh1.901 trilioni, sawa na asilimia 14.06 ya bajeti yote ni kwa ajili ya kulipa madeni ya Taifa. "Kwa mantiki hiyo, mtaona kuwa fedha kwa ajili ya kuendesha Serikali pamoja na kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zitabaki Sh11.624 trilioni ambazoni ni sawa na fedha za bajeti ya mwaka unaomalizika wa 2010/2011," alisema Zitto katika taarifa yake hiyo na kuongeza: "Kwa kuzingatia kwamba thamani ya shilingi imekuwa ikishuka, bajeti iliyotangazwa ni ya kulipa madeni". Bajeti ya posho sasa Sh987 bilioniKuhusu hatua za kupunguza posho, kiongozi huyo alisema hakuna ukweli wa kauli hiyo kwani Serikali imetenga kiasi cha Sh987 bilioni kwa ajili ya kulipa posho mbalimbali, fedha ambazo ni sawa na asilimia 13 ya bajeti nzima. Taarifa hiyo ilibainisha kuwa kutokuwapo kwa nia ya dhati ya kupunguza posho, inaonekana katika hatua za kufanya marekebisho katika sheria ya kodi sura ya 332 ili kusamehe kodi ya mapato katika posho wanazolipwa wafanyakazi wa Serikali na wanaofanya kazi katika taasisi zinazopata ruzuku kutoka kwenye Bajeti ya Serikali. "Hii inaonyesha kuwa kauli ya kufuta au kupunguza posho ilitolewa na Serikali ili kupumbaza wananchi, lakini haina udhati,"alisema. Taarifa hiyo ilieleza kuwa bajeti imeongeza mzigo mkubwa kwa wananchi kutokana na hatua yake ya kuongeza kiwango cha faini kwa madereva wazembe kutoka Sh20,000 hadi Sh300,000, na kwamba kiasi cha Sh50,000 kilichotangazwa na Waziri Mkulo juzi kinatofautia na maelezo kwenye vitabu vya bajeti. Alisema hatua hiyo itawaathiri wananchi hasa vijana walioajiriwa ama kujiajiri katika huduma za usafiri na usafirishaji na kwamba kipengele hicho pia kinalenga kuuhadaa umma. Serikali juzi ilitangaza hatua kadhaa za kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima katika mwaka wa fedha wa 2011/2012, lakini fedha za matumizi mengineyo, maarufu kama Other Charges (OC), zimeongezwa kwa asilimia 8.62 ikilinganishwa na Bajeti ya Serikali inayofikia ukomo tarehe 30 mwezi huu. Fedha za OC katika bajeti mwaka ujao wa fedha ni Sh3.089 trilioni ikilinganishwa na kiasi cha Sh2.823 kilichotengwa katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, likiwa ni ongezeko la Sh266.599 bilioni. Fungu la fedha za OC ndilo hutumika kugharimia posho mbalimbali kwa watumishi wa umma na uendeshaji wa semina, warsha na makongamano pamoja na kugharimia safari za viongozi ndani na nje ya nchi. Kafulila adai bajeti haijazingatia vigezo vya uchumiMbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila aliliambia Mwananchi katika viwanja vya Bunge kuwa, hali hiyo inadhihirisha kwamba bajeti iliyowasilishwa na Mkulo ililenga zaidi kutafuta kuungwa mkono kuliko kuzingatia vigezo vya kiuchumi. "Kama mwaka wa fedha unaoishia mwishoni mwa mwezi huu fedha za OC ni kidogo kuliko zile ambazo zimetengwa mwaka ujao wa fedha, basi ni dhahiri kwamba hatuwezi kusema posho zitapunguzwa, hapa nadhani kuna tatizo,"alisema Kafulila. Alisema fungu la fedha za OC lazima lipitiwe upya kwani fedha zilizotengwa ni zaidi ya kiasi cha fedha ambazo Serikali imeomba kutoka kwa nchi wahisani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo. "Iwapo fedha za OC ni Sh3 trilioni na fedha za miradi ya maendeleo tunazoomba kutoka kwa wafadhili ni kiasi hicho hicho, utaona kwamba ni jambo la kushangaza, hapa kuna mambo mengi ya kuweka sawa,"alisema Kafulila, huku akibainisha kuwa bajeti hiyo ya Serikali si mbaya sana kwani imekumbuka umuhimu wa miundombinu ya usafirishaji. Akiwasilisha bungeni juzi Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/12, Waziri Mkulo alibainisha hatua kadhaa za Serikali kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima akiahidi kupunguza posho zisizo na tija, safari za ndani na nje za viongozi na ukubwa wa misafara ya viongozi hao ili fedha husika ziweze kutumika kugharimia shughuli nyingine za maendeleo. "...........Serikali itasitisha ununuzi wa samani za ofisi, hususan zile zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija, kupunguza matumizi ya mafuta kwa magari ya Serikali, kupunguza safari za ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na ukubwa wa misafara na kuendelea kupunguza semina na warsha, isipokuwa pale inapobidi na kwa kibali cha Ofisi ya Waziri Mkuu..," alisema Mkulo. Sh3 trilioni kutoka nchi wahisaniKadhalika majedwali ya ufupisho wa hesabu za bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12 yanabainisha kuwa fedha za maendeleo zinazotarajiwa kutoka kwa nchi wahisani ni kiasi cha Sh3.054 trilioni. Kiasi hicho kinazidiwa kwa asilimia 18.9 sawa na Sh5.853 bilioni kikilinganishwa na fedha za OC ambazo ni Sh3.089 trilioni. Katika bajeti hiyo, fedha zote zilizotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Sh4.925 trilioni, ambapo fedha za ndani ni Sh1.871 trilioni.Mchanganuo mzima wa bajeti hiyo unaonyesha kuwa fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa ni sawa na asilimia 31 ya bajeti nzima, wakati fedha za matumizi mengineyo (OC) ni sawa na asilimia 32, mishahara asilimia 23, malipo ya madeni asilimia 8, madeni mengine asilimia 3 na riba ya madeni ya ndani na nje asilimia 3.
Asante mkuu nafikiri Zomba amejibiwa kwa ufasaha.yale makosa ya milioni na bilioni yamerekebishwa.hoja ya ulinganifu wa bajeti iliyopita na hii pia imejibiwa otherwise Zomba adhibitishe kuwa kunaongezeko.najua mlikuwa mnachokonoa ili Zitto ateme madini humu alafu kesho mpate hoja za waandishi wenu uchwara kuandika.
 
Hongereni sana wapiganaji wetu, matunda ya kuwaweka mstari wa mbele yanadhihirika. Endeleeni kutufungua macho wananchi na moto huu wa CDM kutetea wana wa nchi ya Tanzania hakuna wa kuuzima, unasimamiwa na Mungu mwenyewe kwa vile ni matendo meme kwa nchi aliyotupa Mungu. Tunamwomba Mungu sana nchi yetu ipate ukombozi wa kweli kupitia watetezi wa kweli CDM.
Aluta continue, Mungu awabariki sana.
 
Hivi kweli serikali ya Jk imeamua kuwa ya kisanii pasee! Hana aibu! Upuuzi gani huu!
Kuwahadaa wa tz ni kosa linalowapasa kujiuzulu woote...!
 
Nadhani hiyo budget ikataliwe warudi kwenye drawing board waandae budget nyingine halafu baada ya hapo wawajibishwe.

Hizi sio zama za usanii, ni zama za innovation na entreprenuership. Sasa kama haupo innovative na kuwa na mawazo ya entreprenuership huna nafasi katika dunia ya leo zaidi ya kuwa mtumwa wa wengine

Tubadilike jamani.


Haswaa mkuu, hicho ndicho kingetakiwa kifanyike. Kwa bahati mbaya katiba tuliyonayo kwa sasa hairuhusu wabunge kukataa budget ya serikali. Wakifanya hivyo, Rais aweza kulivunja Bunge kwa kutumia Kifungu cha 90 (b) sehemu ya tatu ya katiba yetu (mbovu). Kifungu chenyewe kinasema: "Rais hatakuwa na uwezo wa kulivunja Bunge wakati wowote, isipokua tu:..... (b) Kama Bunge limekataa kupitisha Budget iliyopendekezwa na serikali''.
 
icon1.png
Re: Zitto: Taarifa kwa Vyombo vya Habari kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Serikali 2011/2012
quote_icon.png
Originally Posted by Regia Mtema

Mimi naona kama vile wewe ndiye hujaelewa hii taarifa. Mimi nilivyoelewa ni kuwa shilling 0.987trillion ni sawa na 13% ya bajeti yote ya serikali kwa ajili ya posho chini ya vifungu vinavyojulikana kama Personnel allowances (non discretionary na In-kind”).


Yaani ni 13% ya bajeti ya vifungu vinavyojulikana kama Personnel Allowances(non discretionary na In-kind) tu. Na siyo bajeti yote ya serikali ya Shs 13trillion.


Sasa bajeti ya Personnel Allowances (non discretionary na In-kind sisi wananchi wa kawaida hatujui ni ngapi kwani hatujaona vitabu vya bajeti. Lakini kwa kuangalia hii taarifa tunaweza kufanya hesabu rahisi (Shs 0.987trilion gawanya kwa 13% = Shs7.592trillion) hii bajeti ni Shs7.592trillion

Hapo ninafikiri alikuwa akimaanisha asilimia 13 % kwa ajili ya "public expenditure" yaani kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya serikali.

Someni tena, mtaelewa alichokiongelea ni 13% ya bajeti nzima...

Bajeti ya serikali ya mwaka 2011/2012 imetenga jumla ya shilingi 0.987 trilioni ambazo ni sawa na asilimia 13 % ya bajeti yote ya serikali kwa ajili ya kulipa posho

6.
Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya Bajeti kulipa Madeni na Kulipana Posho (Asilimia 27 – 14% kulipa madeni na 13% kulipa Posho mbalimbali).

Imetolewa leo, Mjini Dodoma, na

Zitto Zuberi Kabwe

Waziri Kivuli wa Fedha
Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni


Bajeti ya posho sasa Sh987 bilioni
Kuhusu hatua za kupunguza posho, kiongozi huyo alisema hakuna ukweli wa kauli hiyo kwaniSerikali imetenga kiasi cha Sh987 bilioni kwa ajili ya kulipa posho mbalimbali, fedha ambazo ni sawa na asilimia 13 ya bajeti nzima.
.
 
Back
Top Bottom