Zitto, Mnyika wafichua upotoshaji bajeti ya Mkulo; Spika Makinda akiri, amtaka Mkulo arekebishe

HTML:
1. Wakati Waziri akitaja kuwa kipaumbele cha kwanza cha bajeti hiyo ni kumaliza tatizo la Umeme na hivyo kutamka kwamba ametenga shilingi 537 Bilioni, , upembuzi uliofanywa na Kambi yetu ya Upinzani kwenye vitabu vya bajeti (Kitabu Namba II na IV) vilivyotolewa na serikali yenyewe, umebaini kuwa Wizara ya Nishati na Madini imetengewa jumla ya kiasi cha shilingi 402,402,071,000 kwa mujibu wa fungu la 58. Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya Matumizi kawaida shilingi 76,953,934,000 na kwa upande wa bajeti ya Maendeleo zimetengwa shilingi 325,448,137,000. Shilingi Bilioni 325 zilizotengwa katika Bajeti ya Maendeleo ya Wizara ya Nishati na Madini zinatosha kwa mradi mmoja tu wa umeme wa 160MW, 100 Dar es Salaam na 60 Mwanza. Hakuna mradi wowote mpya wa umeme unaonekana katika Bajeti. Ni dhahiri kuwa kauli ya Mkulo ililenga zaidi kuwajengea wananchi matumaini hewa kuliko kuchukua hatua za kweli za kumaliza tatizo la umeme.
Ukisoma hii kwa umakini ya miradi ya umeme, wanasema kuwa walishaanza kutenga fedha kwa ajili ya kazi hizo. Hapa Mh Zitto sijui anasemaje

 
Big up Chadema Mnaonyesha ukomavu kwa kujua nafasi yenu na wajibu wenu kwa umma wa watanzania, tu nyuma yenu
 
mkuu, mbona mistari yako inasomeka kama unaomba huruma ya zitto vile, eti oh .... nakuheshimu, oh .... bwana mdogo, agrrr wewe ungeshusha nondo, mpaka sasa zitto kajenga point nzitto, unasomeka kujivua gamba!!!!!! ha ha ha.
 
hili ni tatizo la nchi kuendeshwa kwa kuangalia upepo wa siasa na inaposahau vipaumbele vyake, matokeo yake ni kujikuta inaangukia pua.
hakuna ufanisi kwenye kichwa cha serilkali isiyokuwa na viongozi walio commited.


mwanga huleta mwanga, giza huleta giza.

Kwa muono wako viongozi walio committed ni hao wenye kutoa taarifa yenye upotoshaji wa makusudi? soma juu kidogo hapo uone mapungufu ya hii taarifa ya waziri kivuli.
 
mkuu, mbona mistari yako inasomeka kama unaomba huruma ya zitto vile, eti oh .... nakuheshimu, oh .... bwana mdogo, agrrr wewe ungeshusha nondo, mpaka sasa zitto kajenga point nzitto, unasomeka kujivua gamba!!!!!! ha ha ha.

Heshima ni kitu cha bure. Jibu hoja.
 
HTML:
6. Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya Bajeti kulipa Madeni na Kulipana Posho (Asilimia 27 – 14% kulipa madeni na 13% kulipa Posho mbalimbali).
Hiv nini maana ya country credit rating. Kwahiyo hapo inamaana madeni yasilipwe au nini? Kwenye posho ni tatizo na madeni je? Kutokulipa ni kwa kudefer deni ni kuongeza interest rates na pia kupunguza burgaining power kwenye future borrowings na pia venues za kukopa. Kwenye posho ni tatizo.
 
Binafsi nakupongeza sana Mh Zitto kwa kuchochea mjadala wa budget ndani ya jamvi hili,umetusaidia sana ambao hatujaona hivyo viambatanishio(vitabu vya maelezo). Katika budget hii ya mh Mkullo nimehuzunishwa na mambo makubwa mawili

1. Kwa nini serikali inang'ang'ania kujenga nyumba wakati iliziuza kwa bei ya kutupa ilizokuwa inamiliki? serikali imeuza nyumba kwa bei za mpaka millioni 3 leo wanataka kujenga kwa mamillioni mengine!!!kwa nini kazi hiyo isifanywe na NHC na serikali iwe mpangaji tu? serikali haina watalaamu wa kujenga ndo maana nyumba ya millioni 70 tunapewa repoti kuwa imejengwa kwa millioni 200. NHC wanadesign na kujenga kwa kutumia watalamu wake wa ndani na hivyo ni rahisi kuwabana kwa report zao na kuwafanya wawajibike.

2. Kwa nini serikali inafanya ubaguzi wa wafanyakazi? kuondoa kodi kwenye posho za wafanyakazi wa serikali wakati wengine wataendelea kulipia ni ubaguzi wa wazi ambao kimsingi utaipunguzia serikali mapato na mwisho wa yote hata mfanyakazi mwenyewe anapunjika na kuwa na mafao yasiyoreflect maisha aliyokuwa anaishi wakati anafanya kazi.....tuliondokana na mambo haya na bado tunarudi kulekule, zamani ilikuwa kwamba mtu analipwa allowance nyingi sana na hakatwi kodi kama housing allowance,transport allowance,medical n.k...unakuta mtu ana income ya 2M ila mshahara wake ni laki 3 tu,mafao ya mtu huyu yatakuwa calculated from laki tatu na kujikuta anapata kitu kidogo sana kama pension...matokeo yake atakufa mapema sana kwa frustrations na badala yake mifumo hii inatengeneza mafisadi wengi zaidi. Leo hii kwa bahati mbaya sana nimesimuliwa na mtumishi wa hazina kuwa kuna vikao watumishi wa wizara ya fedha wanalipwa zaidi ya 3M kama posho ya kikao kimoja na mara nyingine mpaka 7M kwa kikao kimoja kwa mtu mmoja...na ndo hao walioandaa budget hii kuwa sasa wasilipe kodi kwa kuwa waliona zinapungua....Shame on them!!!!!

Mh Zitto, kuna mapato ambayo kwa muda mrefu naona yanapotezewa tu ila yanaweza kuwa na mantiki na kuiongezea serikali mapato makubwa....nyanja hiyo ni upangishwaji binafsi wa nyumba!, mimi na nalipa TZS 4M kwa mwaka nyumba ya kawaida sana ila mwenye nyumba halipi kodi kwa mapato hayo, kuna watu wanamiliki zaidi ya nyumba 10 Dar na wanapangisha kinyemela na kuingiza zaidi ya TZS 40M kwa mwaka na haikatwi kodi wakati mfanyakazi mwenye income ya chini ya laki 2 analipa kodi kila mwezi!!!inaweza isiwe effective sana mwanzoni lakini itatengemaa kukiwa na proper follow ups na urasimishaji wa umiliki wa nyumba hizi.

sehemu nyingine ni kuhusu wafanyakazi ambao ni foregners,wengi wanajificha kwenye kichaka cha exparts lakini ni Ulongo tu , mfano mzuri ni Airtel, imeoutsource vitengo vya operations, customer care na ITambavyo kimsingi ndo vilikuwa vinaajiri watz wengi sana.....makampuni yaliyopewa kazi ni ya India na top positions zote zimechukuliwa na wahindi...Unyapala is back! watz wanachumia juani wao wanalia kivulini.
wanalipwa vizuri sana, transport allowance ni around USD2500,housing allowance ni USD3000 and above na mishahara ni mikubwa zaidi .....kibaya zaidi hawalipi kodi.Kuna nchi ambazo exparts wanalipa kodi kwenye nchi wanazofanya kazi,kwa nini kwetu hawalipi??
serikali haijafanya wajibu wake kuongeza wigo/nyanja za kodi, wamekomaa kuongeza kodi kwenye bia na sigara and the likes wanafikiri watasaidia kumbe waaaaaaaaapi bana, kwa mnywa pombe na mvuta sigara hataacha kwa sbb ya bei ila maisha yatamuwea magumu na atapunguza matumizi ya lazima kama chakula bora na kuwekeza kwenye mapombe zaidi na masigara zaidi...tokea wameanza kupandisha bei watu wanaacha??

agriiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!! aiiiiiiiiiiihhhh! hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!....basi tu mwe!
 
Wewe use your brain rather than your effort,your future is still in your hands,if this is not my country i could leave but i should fight till the end,hivi huoni ZITTO alicho analyze,kweli wewe GAMBA na unaakili mgando huna huruma na watanzania,haya wasalimu Masaki mwambie na yule mdogo wako aliyepo MAREKANI anayesoma kwa wizi wa kodi za watanzania anarudi Tanzania kuwasalimu maskini wa Tanzania

Jibu hoja, achana na mimi na gamba langu, mdogo wangu, na kukaa masaki, unafikiri hao unaowataka wakichukuwa uongozi watakuja kukaa "uswazi"? au watakupeleka wewe huko "masaki"?
 
Hii inasaidi wanaichi wakawaida kujua kilichojiri kwenye bajeti hiyo. Napata tashwishwi hasa pale kwenye Traffic Notification maana hata ikiwa 300,000/- bado haitasaidia kupunguza makosa y barabarani maana askari wetu si wazalendo ni wala rushwa na wananchi wengi pia si wazalendo wataishia kulipia hongo na kutokulipa fine. Huu ni mtaji kwa askari barabarani.
 
3. Wakati Waziri akisema Bungeni kuwa Bajeti ya mwaka 2011/2012 itapunguza posho kama sehemu ya mkakati wa serikali wa kuthibiti matumizi, nanukuu "kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija (uk.53)", ukweli ni kuwa Bajeti ya serikali ya mwaka 2011/2012 imetenga jumla ya shilingi 0.987 trilioni ambazo ni sawa na asilimia 13 % ya bajeti yote ya serikali kwa ajili ya kulipa posho chini ya vifungu vinavyojulikana kama "Personnel allowances (non discretionary na In-kind").

6.
Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya Bajeti kulipa Madeni na Kulipana Posho (Asilimia 27 – 14% kulipa madeni na 13% kulipa Posho mbalimbali).

Masahihisho....0.987 Trilion iliyotengwa kwa posho ni sawa na 7.3% ya bajeti nzima na sio 13% kama iliyoandikwa hapo juu.
 
Cha kushangaza! wengi wa changiaji humu, wanasifia na kuponda bila mantiki. Ni matatizo tuliyonayo Tanzania. Upinzani haumaanishi hata mema tuyapinge.

Taarifa ya Zitto inaonesha kabisa kuwa ni upinzani usio na mantiki, mpaka kiasi inanishangaza, najiuliza kwa hayo aliyoyaandika, alikuwa labda ametingwa na kazi nyingi sana mpaka akakubali kuandika mambo yanayoitia aibu kambi ya upinzani?

Kutumia nembo za bunge na kuishusha hii taarifa kwenye tovuti ambayo wengi, wa ndani na wa nje, wataiona na kuona makosa ya kipuuzi kabisa kutoka kwa Waziri kivuli wa fedha? Hata namba zinampiga chenga! ni kujivunjia hadhi kwa Zitto. Hivi Zitto na umakini wake wote anaweza kufanya makosa ya kijinga kama niliyoyaainisha katika post yangu hapo juu? Au Regia? Halafu kwa nembo ya Bunge?

Inasikitisha sana, hata kukiwa na kosa moja tu la spelling kwa taarifa muhimu kama hiyo lazima ikemewe sana seuse hiyo yenye makosa mpaka ya sentensi nzima. Ni aibu kwa upinzani na inaonesha jinsi upinzani unavyokurupuka kutafuta makosa mpaka kiasi wao wanajiingiza kwenye makosa makubwa.

Au ndio yule Zitto anaesemwa kuwa yuko pale si kwa ajili ya upinzani na ana agenda zake? Nashindwa kuelewa.

Naomba Zitto au Regia aliyobandika hiyo taarifa, wawaombe radhi wa Tanzania kwa kuwawekea taarifa yenye nia ya kuupotosha umma ya ama kwa makusudi kabisa au kwa uzembe wa kukurupuka.

Na hata baada ya makosa yote hayo, wanazi wa cdm bado wanashangilia tu, inanikumbusha ile habari ya "kufungwa twafungwa lakini chenga twawala". Nawaonea huruma kwa kutoyaona makosa ya viongozi wao.

Hujaonyesha hata sehemu moja ya hii taarifa iliyokosewa na Waziri Kivuli. Wewe ndiye unataka kutupotosha eti "Kutumia nembo za bunge na kuishusha hii taarifa kwenye tovuti ambayo wengi, wa ndani na wa nje, wataiona na kuona makosa ya kipuuzi kabisa kutoka kwa Waziri kivuli wa fedha??. Nchi ni yetu siyo ya watu wa nje tumearifiwa watu wa hapa bongo. Wewe mwenzetu na wenzako wenye kipaumbele cha watu wa nje wanaowasaidia hadi kufikiri ndiyo mnataka tukubali upuuzi. Grow up
 
Mimi ningekuwa Rais wa Tanzania leo hii. Kitu cha kwanza kukifanyia kazi ni tatizo la umeme. Ningehakikisha ndani ya miaka mitano nchi inapata umeme wa kutosha na ambao hakukatiki hovyo. Hii ingesaidia nchi kuongeza uzalishaji katika viwanda na shughuli nyingine nyingi zinazotegemea umeme. Kuongeza uzalishaji kutaongeza kodi ya serikali.

Nishati ya uhakika ya umeme ina manufaa mengi sana kwa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Mimi nashangaa sana viongozi wetu bado wanapiga danadana kwenye suala la umeme hata baada ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika.

Pili ningewekeza kwenye elimu. Kuhakikisha kuwa elimu inayotewa nchini ni ya kiwango cha juu katika kila ngazi. Mkulima ambaye hakusoma hataweza vipi kufuatilia mbinu za kilimo cha kisasa? Vijana ambao hawakufundisha mbinu za kubuni biashara na kazi kujiari watafanikiwa kivipi? Taifa la watu wasiolemika ni Taifa mfu. Kuelemika sio kuwa na vyeti vya madigrii mengi bali kuwa na uwezo wa kuelewa na kutambua mazingira na jinsi kukabiliana nayo.

Sasa ukiangalia hii budget ya serikali hakuna haya mambo.
 
Hii inasaidi wanaichi wakawaida kujua kilichojiri kwenye bajeti hiyo. Napata tashwishwi hasa pale kwenye Traffic Notification maana hata ikiwa 300,000/- bado haitasaidia kupunguza makosa y barabarani maana askari wetu si wazalendo ni wala rushwa na wananchi wengi pia si wazalendo wataishia kulipia hongo na kutokulipa fine. Huu ni mtaji kwa askari barabarani.

Askari hawezi kula rushwa bila kupewa. Wewe kama raia ukiacha kutoa rushwa huyo askari atahongwa na nani?
 
Masahihisho....0.987 Trilion iliyotengwa kwa posho ni 7.3% ya bajeti na sio 13% iliyoandikwa hapo juu.
Duh! Zitto hebu safisha hii hali ya hewa hapa JF najua wanahabari pinzani wananukuu hizi hoja.
 
Mimi ningekuwa Rais wa Tanzania leo hii. Kitu cha kwanza kukifanyia kazi ni tatizo la umeme. Ningehakikisha ndani ya miaka mitano nchi inapata umeme wa kutosha na ambao hakukatiki hovyo. Hii ingesaidia nchi kuongeza uzalishaji katika viwanda na shughuli nyingine nyingi zinazotegemea umeme. Kuongeza uzalishaji kutaongeza kodi ya serikali.

Nishati ya uhakika ya umeme ina manufaa mengi sana kwa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Mimi nashangaa sana viongozi wetu bado wanapiga danadana kwenye suala la umeme hata baada ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika.

Pili ningewekeza kwenye elimu. Kuhakikisha kuwa elimu inayotewa nchini ni ya kiwango cha juu katika kila ngazi. Mkulima ambaye hakusoma hataweza vipi kufuatilia mbinu za kilimo cha kisasa? Vijana ambao hawakufundisha mbinu za kubuni biashara na kazi kujiari watafanikiwa kivipi? Taifa la watu wasiolemika ni Taifa mfu. Kuelemika sio kuwa na vyeti vya madigrii mengi bali kuwa na uwezo wa kuelewa na kutambua mazingira na jinsi kukabiliana nayo.

Sasa ukiangalia hii budget ya serikali hakuna haya mambo.

Na hicho ndicho anakifanya Rais kwa sasa.
 
Hujaonyesha hata sehemu moja ya hii taarifa iliyokosewa na Waziri Kivuli. Wewe ndiye unataka kutupotosha eti "Kutumia nembo za bunge na kuishusha hii taarifa kwenye tovuti ambayo wengi, wa ndani na wa nje, wataiona na kuona makosa ya kipuuzi kabisa kutoka kwa Waziri kivuli wa fedha??. Nchi ni yetu siyo ya watu wa nje tumearifiwa watu wa hapa bongo. Wewe mwenzetu na wenzako wenye kipaumbele cha watu wa nje wanaowasaidia hadi kufikiri ndiyo mnataka tukubali upuuzi. Grow up

Tatizo lenu ni kukurupuka, nenda kaisome post #49 halafu urudi useme ni nini kile nilichokionesha.
 
Inasikitisha sana kuona serikali inawahadaa wananchi kwa kutoa figure batili hii inaonyesha jinsi serikali hii isivyokuwa makini na maisha ya watz.
 
Masahihisho....0.987 Trilion iliyotengwa kwa posho ni sawa na 7.3% ya bajeti nzima na sio 13% kama iliyoandikwa hapo juu.

icon1.png
Re: Zitto: Taarifa kwa Vyombo vya Habari kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Serikali 2011/2012

quote_icon.png
Originally Posted by Regia Mtema
3. Wakati Waziri akisema Bungeni kuwa Bajeti ya mwaka 2011/2012 itapunguza posho kama sehemu ya mkakati wa serikali wa kuthibiti matumizi, nanukuu "kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija (uk.53)", ukweli ni kuwa Bajeti ya serikali ya mwaka 2011/2012 imetenga jumla ya shilingi 0.987 trilioni ambazo ni sawa na asilimia 13 % ya bajeti yote ya serikali kwa ajili ya kulipa posho chini ya vifungu vinavyojulikana kama "Personnel allowances (non discretionary na In-kind"). Kwa hiyo, kauli ya Waziri Mkulo kuwa serikali itapunguza posho sio kweli. Tunautaka umma wa Watanzania usikubali kurubuniwa.

6. Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya Bajeti kulipa Madeni na Kulipana Posho (Asilimia 27 – 14% kulipa madeni na 13% kulipa Posho mbalimbali).




Masahihisho....0.987 Trilion iliyotengwa kwa posho ni 7.3% ya bajeti na sio 13% iliyoandikwa hapo juu.

Mimi naona kama vile wewe ndiye hujaelewa hii taarifa. Mimi nilivyoelewa ni kuwa shilling 0.987trillion ni sawa na 13% ya bajeti yote ya serikali kwa ajili ya posho chini ya vifungu vinavyojulikana kama Personnel allowances (non discretionary na In-kind").


Yaani ni 13% ya bajeti ya vifungu vinavyojulikana kama Personnel Allowances(non discretionary na In-kind) tu. Na siyo bajeti yote ya serikali ya Shs 13trillion.


Sasa bajeti ya Personnel Allowances (non discretionary na In-kind sisi wananchi wa kawaida hatujui ni ngapi kwani hatujaona vitabu vya bajeti. Lakini kwa kuangalia hii taarifa tunaweza kufanya hesabu rahisi (Shs 0.987trilion gawanya kwa 13% = Shs7.592trillion) hii bajeti ni Shs7.592trillion
 
Masahihisho....0.987 Trilion iliyotengwa kwa posho ni sawa na 7.3% ya bajeti nzima na sio 13% kama iliyoandikwa hapo juu.

Hapo ninafikiri alikuwa akimaanisha asilimia 13 % kwa ajili ya "public expenditure" yaani kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya serikali.

Na hapo ni pabaya kwani ni wangapi huwa wanapata hizo posho?
Hawa ni wale watu ambao wanafanya kazi serikalini halafu moja ya majukumu yake ni kushiriki kupanga mipango ya idara yake lakini cha ajabu ni kuwa unakuta analipwa sitting allowance kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha kupanga mpango wa mw2aka tena kwenye ukumbi wa mikutano ndani ya jengo la ofis yake.

wanaolipwa hizi sitting allowance ndfani ya idara za serikali hawafiki hata aslimia 25 ya watendaji wote serikalini , hivyo ni bora wafanyakazi wapige kelele ili fedha hizo ziondolewe na zikishaondolewa watakaoathiorika ni maboss zaidi na hivyo watakuwa wa kwanza kuwatetea wafanyakazi wa kada ya kati na chini ili waongezewe mishahara .

Wakiongezewa mishahara ni kuwa watanufaika hata mwishoni kwani hata pensheni zao zitaweza kuongezeka na kuwa kubwa na hivyo kuwanufaisha zaidi.

Hii ni sawa na mwalimu anaingia darasani kufundisha kwanza alipwe sitting allowance, nafikiri ndio kilichokuwa kinamaanishwa hapo
 
Back
Top Bottom