Zitto, Kafulila, Kitila Mkumbo, Hussein Bashe na akina Ben Saanane waweza Kuanzisha chama kingine?

Wacheni waanzishe hicho chama.. kiitwe Chama Cha Wanafiki- CCW ama Chama Cha Virus (Vimeo) CCV.
waroho wa madaraka wanajifanya maaruku zaidi ya Vyama... Wanafiki
 
The Boss,

Tanzania kila kitu kinawezekana.


sasa hapo wafuasi wake si watu wa kuonewa huruma kwa kweli???
yaani kuna watu wanafikia mpaka kushauri Lema agombee urais mwaka 2015..
hii nchi ina vituko vipya kila siku
 
Uongozi una asili mbili: WATU & HAKI. Na Walinzi wa HAKI za WATU ni watu wenyewe, si mtu mmoja mmoja kwani hakuna mtu aliyejuu au aliyekuwa muhimu kuliko CHAMA;

mkuu umemaliza, wanasiasa wengi wa tanzania na hasa vijana wanaoibukia kwenye siasa wakishalewa sifa tu wanajiona wao wko juu ya chama, na hili tatizo linasababishwa na media zetu.
 
Kings maker wa Tanzania atakuwa yuko kazini, sidhani kama ataweza kudhofisha CDM. Labda aliyekitabiria CDM kuwa chama imara nchini mchakato wa kuwa Mwenye Heri unaosimamiwa na Uganda usimame NA aliyelaza moto wa Mwenge kwenye nembo ya BOT badala ya kusimama moto ule ajitoe CDM na kuazisha chama kingine.
Waanzishe tu,watanzania tutawahukumu kwa unafiki wao.Tena napendekeza Bashe ndio awe mgombea wa urais,ili Rost tamu
asikasirike!
 
Kings maker wa Tanzania atakuwa yuko kazini, sidhani kama ataweza kudhofisha CDM. Labda aliyekitabiria CDM kuwa chama imara nchini mchakato wa kuwa Mwenye Heri unaosimamiwa na Uganda usimame NA aliyelaza moto wa Mwenge kwenye nembo ya BOT badala ya kusimama moto ule ajitoe CDM na kuazisha chama kingine.
Waanzishe tu,watanzania tutawahukumu kwa unafiki wao.Tena napendekeza Bashe ndio awe mgombea wa urais,ili Rost tamu
asikasirike!
 
mkuu utajivunjia heshima ukija na jazba hapa
sikusema sio haki wala sikusema wamevunja sheria

wewe ukija hapa ukisema Mzee Majuto anafaa kugombea urais mwaka 2015
hatutasema huna haki
lakini tutakuwa na haki ya kuhoji busara zako....

Kila nikionaga Avatar ya huyu jamaa naanza kuogopa kwamba kuna mtu either anatukanwa, karipiwa au anafokewa. Anahitaji wanasaikolojia wa kumsaidia kucontrol jazba zake, maana duh! Umemjibu vizuri leo.
 
Kingarama hayo maneno yenye rangi nyekundu wengi hawayafahamu bahati mbaya hata uongozi wa CDM unaamini kila anachosema Lema.Jiulize kwenye mgogoro wa meya ulishawahi kusikia maoni ya katibu/mwenyekiti wa wilaya au mkoa ?Lema ni katibu wa wilaya,Lema ni mwenyekiti wa wilaya,Lema ni mwenyekiti wa mkoa,Lema ni Katibu wa mkoa,Lema ni mbunge wa Arusha mjini,Lema ni Alfa na Omega.



Vituko haviishi kwa kweli. Mimi Lema kwa kweli huwa sielewi nini hasa anakisimamia. Kuna wakati Jenerali Ulimwengu alitushauri kabla hatujachagua Rais angalau tujiridhishe Huyo anayetaka kuwa Rais wetu aliwahi kuandika wapi mawazo yake ili tuyatambue. Lema ni mtu wa kulaumu bila ya kutoa suluhisho.

Kwa mfano watu wengi hawajui kwamba na Lema naye ni sehemu ya mgogoro wa umeya Arusha. Lema aliingilia mamlaka ya uongozi wa CHADEMA Mkoa na Wilaya kwa kutoa maamuzi ya kuonesha kwamba yeye ni "makini" na kwa bahati mbaya CHADEMA inaamini kwamba Lema ni nembo ya CHADEMA Arusha kwa hiyo kati ya kuchagua uongozi wa chama na mbunge CHADEMA kikachagua Mbunge.
 
Kuna kundi la vijana ndani ya ccm nalo lina harakati za kichinichini likijumuisha wabunge vijana.Uchaguzi wa 2015 kama mambo ndiyo haya basi utakuwa mgumu sana
 
ndiyo wewe ni mbaguzi kwa kigezo cha umri dhidi ya wazee

Siyo kweli, kwani mfano nikisema wewe hujui hisabati na kweli ukawa hujui hisabati nakuwa nakuwa nimekubagua ki msingi wa masomo?
 
Kibs achana na washabiki,

..... ukijiita makini huo umakini unatoweka? hata kama ni majivuno wewe mwenyewe kujiita makini.
Uwezi kujiita makini ilhali ufuati misingi yoyote ya kukufanya uwe makini, misingi hiyo inaanzia kwenye tabia binafsi na jinsi jamii inavyokuona, matendo yako na ushauri wako juu ya mambo mbalimbali ya kimsingi katika kujenga jamii nzima. Ndio maana umakini hauwezi kutokana na mashabiki wako pekee, zaidi ni jamii nzima inayokuzunguka ambayo ina weza kuona chanya na hasi juu yako.
 
Tatizo liko hapa...wanaotoa maoni na kusema kwa uhuru wanalalamika kwamba demokrasia na uhuru wa mawazo unaminywa kwa maslahi binafsi ya wachache

Wanaoshindwa kuvumilia uhuru wa mawazo na kuona maslahi yao yako hatarini basi husingizia siri za chama,vikao au uhuru bila nidhamu.So uhuru wa mawazo,demokrasia na wigo wa mamlaka ndani ya vyama vya siasa uende sambamaba na dhana ya uwajibikaji na kuzingatia maslahi mapana ya chama.Hii ni kwa viongozi wa vyama vya siasa na wanachama wa chama husika

Wakati mwingine tunaipinga CCM kwamba inaminya uhuru wa mawazo na demokrasia.Pia tunapinga na kulaani matumizi ya maneno kama siri za jeshi au nyaraka za siri.hii imekuwa silaha kubwa kwa madikteta wote kwenye vyama vya siasa na viongozi wa serikali (hasa viongozi dhaifu).Ndiyo maana leo hii unaona south Africa bado Zuma amekaliwa kooni na Archbishop Desmund Tutu(Mshindi wa Tuzo ya amani ya Nobel) pamoja na wanaharakati wengine juu ya mswada kandamizi na utakaofifisha dhana ya uwazi na uwajibikaji (mswada wa kulinda nyaraka za siri)

Niseme tu kwamba kiongozi dhaifu au adui wa Demokrasia hana chama,kabila wala dini.Mathalani watetezi wa haki na uhuru wa maoni au demokrasia hawana kabila,dini,wala chama cha siasa.Madikteta ni madikteta tu

kitendo cha Kafulila kupiga magoti mbele ya Mbatia uku anamwaga machozi,ni ishara tosha kwamba alikuwa kwenye majuto makubwa...kama vijana wenyewe ndio hawa wasiojua hata wanasimamia nini, wanaojutia ata maamuzi yao ambayo leo wanatuambia ya msingi,ni bora tuendelee kungoja...labda kama zile kelele mwanzoni hazikuwa akili zake,kuja kustukia..duh ameponzwa!
 
Chama kingine? hawawezi. Ninachokiona ni jitiohada za kutaka kupanua demokrasia ndani ya vyama vya siasa.

Wanatoa ujumbe mahsusi wa kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kujenga tabia ya kuvumiliana na watu wanaopishana nao mitazamo ya masuala mbalimbali hata kama wako ndani ya chama kimoja. Kwamba watu wote lazima wawe na mtazamo mmoja juu ya kila jambo ni kitu hakiwezekani na kwahiyo, haki ya mtu kuwa na mawazo tofauti na kiongozi wake ni lazima ilindwe na iheshimiwe.

Katika hili,niko pamoja na Zitto, Dr. Kitila, Ben Saanane, Kafulila na wengine wote wanaopigania demokrasia halisi ndani ya vyama vya siasa. Lazima tutoke kwenye maigizo ya demokrasia ndani ya vyama na tuwe na demokrasia ya kweli. Hakuna kushabikia nidhamu ya uoga kwa sasa.


Kwakiasi kikubwa na kubaliana na wewe zaidi kuliko mtoa hoja kwamba kufanana katika ukweli wa jambo hakuna maana yakuwa kila mara hilo likitokea basi watu wanakuwa suspecious kwamba watu wanaanzasha chama. Ni wakati wa watanzania na hasa vijana na watu wenye umri wa utu uzima kuacha siasa za kuviziana na badala yake kusimamia misingi ya ukweli huku tofauti zetu za kiitikadi zikibakia kama chache ya kuendeleza democracy na kusukuma maendeleo kwa haraka na kwa nguvu ndogo.

Ukiangalia sana utaona hapa Kafulila is victimised kwa pretense ya nidhamu na kila mwenye matamanio ya Tanzania njema angepaswa kabisa kumuunga mkono bila kujali hapo zamani alikosea wapi (if at all alikosea ama alitafsiriwa kukosea baada ya kukataa kuburuzwa kama alivyofanya sasa). Kunatofauti kati ya nidhamu na uoga/unafiki. Nidhamu ni kuheshimu mamlaka pale yanaposimama katika haki na uogoa/unafiki nikukubali kubariki kosa kwasabau tu kosa hilo limetendwa na mheshimiwa. democracy ina mipaka yake na pia inamapungufu yake kama haitachukuliwa katika context yake. Katika democracy kuna wakati wengi wanaweza kuwa katika makosa na mmoja tu akawa yuko right kwasababu tu pengine yeye ameona mbali zaidi ya wengine; mfano ni wakati Tanzania ilipoingia katika muundo wa vyama vingi. Wengi walikataa huo mfumo lakini wachache kwakuwa walijua tunakoelekea ili kutuepusha na majanga makubwa zaidi hapo baadaye wakaona kuwa hata pamoja na kuwa wengi wamesema hapana hiyo 'hapana' ni ya muda mfupi tu kwakua hawawezi kuona mbele na watakapofika hapo mbele kuweza kuona ndiyo yao itasababisha maafa kwetu sote kama wachache wenye nguvu watakataa kubadilika.

Nirahisi sana kumhukumu Kafulila ukiwa kijana anayeaminiwa na baadhi ya viongozi ndani ya chama chako lakini bila kujua kuwa Kafulila anawakilisha matamanio ya wengi pamoja na wewe ambayo kwa uoga tu na unafiki umeamua kuukataa huu ukweli ambao Kafulila anauwakilisha. Lakini ukumbuke kwamba maisha hayako static ni very dynamic je yumkini hao leo unaoogopa kuwaambia ukweli wakija learn thru mistake na kumkubali Kafulila na kukuona wewe kuwa mzigo na kikwazo kwao kwasababu tu Kafulila ameweza kuvuta hisia ya vijana wote wakitanzania utaficha wapi uso wako? Tuchukulie mfano wa Zitto alipofukuzwa ndani ya Bunge na Samwel Sitta wakati huo alionekana pengine ni mtu asiyenaheshima na pengine tukifungua kurasa za JF wapo leo ambao wanamwona alikosa nidhamu. Lakini ni ukweli ambao hata tusipopenda kuusema kile kilikuwa kitendo cha kishujaa na kilileta mapinduzi ya fikra kwa wengi hata wengine leo hii akiwepo huyo Sitta mwenyewe kupenda kujipambanua upande wa Zitto katika baadhi ya mambo anayosimamia. Kupitia ujasiri huo vijana wengi wamekubalika na hatimaye kupigiwa kura na raia watanzania kuingia bungeni leo hii. Huo ulikuwa mchango mkubwa sana kwa siasa na vijana Tanzania bila kujali itikadi ya chama; lakini wengi wa vijana hawanahabari kuwa bila hilo wala vijana wengi wasingeweza kuipenda CHADEMA hata kusababisha CCM kubadili siasa zake; na pengine hata wabunge na viongozi kama kina Nape; Mwigulu; Deo Filikunjombe; yule mbunge wa Mtera etc wasingeweza pewa fursa ama kuwakilisha au hata kuongoza chama chao.

Natoa wito kwa vijana kuwa na sauti moja pale mmoja wao anapoonewa nakupelekea uonevu huo kusaidia ku-set precendence kwenye siasa na uongozi wa nchi yetu. Ni vyema basi kila mmoja akachukua jukumu la kumsaidia mwenzake kila inapowezekana katika yale mazuri huku tukikubali kutofautina ki-itikadi lakini tukiungana katika yale ya msingi ili sauti zetu ziwe kubwa kiasi cha kutoweza kuburuzwa na wachache ambao wameamua kutumia siasa kama njia ya kushibisha matumbo yao na familia zao huku jamii yote ya watanzania wakiangamia kwa uduni wa maisha.

Lakini hili pia lazima kulizingatia si wakati wote wazee wanakuwa na matatizo na wala si wazee wote wenye maono sawa na hao wachache walioamua kujibinafsishia nchi na kuifanya kuwa kama shamba lao. Wazee wanabusara na wameona mengi na kwakupitia wao tutaweza kuzitumia nguvu zetu za ujana kwa namna inayofaa zaidi. Ndipo sasa inabidi tuwaheshimu na kuwaenzi bila kuwageuza kuwa miungu ama sanamu za kuabudu.
 
..hawa vijana wapiganie kuwa na INDEPENDENT CANDIDATES.

..siasa za vyama ni "udikteta," yaani udikteta wa walio wengi dhidi ya wachache.

..ukiwa ktk chama chochote kile uamuzi wa mwisho hufanyika kwa njia ya kura.

..kama hoja yako imeshindwa kwa kura, basi huna budi kuheshimu uamuzi wa kura.

..tatizo ninaloliona mimi ni hawa vijana mara kwa mara kutokukubaliana na maamuzi yaliyopigiwa KURA katika VIKAO rasmi vya chama.
 
Godbless Lema ni jembe ulaya ni zaidi ya makini na ameongea fact,,uyo kafulila mnayemtetea kama kweli alikuwa anasimamia ukweli kwann alipiga magoti na kulia ??!
 
Kutoa hoja kuwa kuna ubaguzi kati ya wazee na vijani sio sahihi,kwa hilo tunapotoka. Leo hii wengi wetu humu JF tunaweza kuchambua na kuchangia hoja kwa umakini kutokana na uzoefu na mazingira tunayoishi.Huwezi ukazungumzia uzoefu na mazingira ya mwanadamu katika kumjenga kifikra bila kuzungumzia umri,sitaki kujikita katika kuelezea ama kutetea hoja za wazee kuwa wao wapo makini zaidi ya vijana sababu ya umri ila ni muhimu kwetu sisi vijana kujifunza kwa sababu kesho sisi ndio hao wazee ambao tunawaona wanatutenga.Suala la Zitto na kundi lake la kina Kafulila kuanzisha chama ama kujiona wao ni vijana wenye maono na upeo mkubwa halitafanikiwa kama kweli lipo.Wale tunofuatilia siasa za Tz mtakubaliana nami kuwa CDM kufikia hapo walipo leo wametoka mbali sana.Ni chama makini kinachozingatia Itikadi na kusoma alama za nyakati.Hakuna mtu mwenye nguvu binafsi anayeweza akajisifia kuwa yeye akiondoka CDM chama kitakufa unless chama kiache misingi yake na kishindwe kusoma za nyakati.Kuhusu lema huo ni mtazamo wake.
 
Hivi unajua kwamba Makamu wa Rais wa Marekani Bwana. Joe Biden aliwahi kusema hadharani kwamba Bwana. Baraka Obama hafai kuwa Rais wa Marekani kutokana na kutokuwa na uzowefu wa sera za mambo ya nje? Sasa Biden alivunja nidhamu ya chama chake?

Hiyo ilikuwa ni wakati kumtafuta mgombea wa raisi ndan ya chama, so campaing na challenges kama hizo huwa zipo. Hata hapa kwetu vyama vinapotafuta mgombea kuna kuwa na makundi ndan ya vyama. Na hizo argument alizotoa joe biden ni challenges za maana sio kama hapa kwetu, watu wanaanza kuhoji dini au ukanda anaotokea mgombea as if kipimo cha uongozi bora

Think big
 
Mambo Mengine nimecheka sana.sasa ni kwa nini mtu asifikirie kuwa Rais kama JK ameweza kuwa Rais? Lakini hatutaki kuelekea huko ati just because JK ameweza

Viongozi ni Reflection ya sisi wananchi.Tanzania sasa naona tunaelekea kubaya,siku hizi watu wanaweza kuongea hoja yoyote tu ya kijinga jinga (no offense) na ikaitwa Falsafa,Loh !

Anyways,About opposition camp:

One had wondered what they are waiting for and for how long they think they can afford to wait with the unfolding political reality in Tanzania, knowing too well that they both would attract an avalanche of many more political parties and groups than they bave recorded separately.

We all should wonder why it is often so hard for political parties to come together to form a formidable force in Tanzania. Why would they rather stay apart like the proverbial scattered twigs of a broom that would never sweep a grain?

Don't the legion of opposition parties in Tanzania know that a government has no obligation to perform optimally unless there is a formidable opposition, an alternative government, waiting to replace it, and that they, the opposition parties, have been slowing down Tanzania's progress by being disunited, fragmented, even when a one-party system is staring them in the face? Hata ndani ya vyama vyetu tunashindwa kuonyesha dhamira ya kuwa kitu kimoja (kwa maslahi ya watanzania) pamoja na kuvumiliana kwenye mambo ambayo ni fundamental?

Perhaps political immaturity or crass nativity is it that has been disuniting the opposition in Tanzania; the mentality of an over joyous decolonized people who would rather ceaselessly scramble for vacated political offices merely for the joy of it.

This spirit of greed for power and positions which led to formation of mushroom political parties had led to proliferation of Regions and local governments, has led to falsification of census figures and voters registers, corrupted electoral system and the endemic economic crimes that have slow Tanzania's progress for fifty years.

Not even military interregnums would (if the prevailing System keep on existing) tame the crude love of power which now shamefully suggests that our leaders were all along imitating the colonialists whose mission was to acquire the wealth of our nation for their home government. And, ironically, the dubious leaders have been looting our treachery to the banks of the former colonial masters for safe-keeping!

So,kwa case ya kuanzisha chama cha siasa pia watu wanastahili kuwa makini.Watanzania hawahitaji utitiri wa vyama.Wanahitaji mawazo mbadala ya kuipeleka nchi mbele,kulinda uhuru wao na raslimali za taifa hili kwa manufaa ya watanzania wote.i believe that,Tanzania inaweza kuwa giant of Africa tukizingatia haya pamoja na kubadili mindset za watanzania.Tujiulize sasa sisi kama taifa

Where does our democracy stand?
American democracy stands on "taxation without representation is discrimination and deprivation" It is this that led to the American dream and declaration of independence. That stand has kept that nation till date. All the parties clearly agree with that only they take different methods or approaches to solving its problems.

We need to get a bearing. Our democracy really has no ground on which it stands. We have people in power or contesting power for power sake.
My people, why do we want democracy? Why not monarchy or something else?Let us redefine our social political destiny ......It's our turn .
 
Back
Top Bottom