Wadau Zitto Kabwe na Julius Mtatiro wana nafasi zinazofanana ndani ya vyama vyao wote ni manaibu katibu wakuu Tanzania bara.Lakini kwa siku za karibuni Julius Mtatiro anaonekana kuwa msaada mkubwa kwa chama chake na kukijengea mtazamo chanya kwa wananchi.Chadema inaonekana kama haina naibu katibu mkuu kwani kila mara ni lazima tamko lolote rasmi la kichama atoe Katibu mkuu au mkurugenzi wa mambo ya nje John Mnyika.Je ina maana hakuna umuhimu wowote wa chadema kuwa na Naibu katibu mkuu bara?? Au kikatiba hii nafasi haimpi madaraka makubwa ya kitaifa kama kwa chama cha CUF??. Inasemekana Naibu katibu mkuu wa Chadema bara anaonekana ofisi za makao makuu ya chama wakati wa vikao vya kamati kuu tu...Je tupendekeze hii nafasi Chadema ifutwe?? Chadema isipokuwa na mtu mahiri wa kutoa matamko ya kichama kila siku hakika itafunikwa na CUF siku si nyingi.Haiwezekani kumtegema Katibu Mkuu kila siku azungumze...yeye anapaswa kutoa matamko maalum tu kwani hakika kwa sasa hivi DR Slaa ndiye kiongozi mkuu wa upinzani Tanzania angalau kwa sasa,hawezi kuwa msemaji wa chama kila siku wananchi watamchoka haraka...Nawasilisha...