Zitto Kabwe: Nusu ya walimu wanalipwa mishahara ya bure, hawafundishi

Bila kuboresha maslahi yao, tusitarajie muujiza toka kwa walimu. Wataendelea kutofundisha kwani wengi wao wanatumia muda wa kazi kujiongezea kipato. Wengi wa walimu vijana ni bodaboda huku walimu ambao ni akina mama wa makamo kazi yao kubwa ni kuzungusha vitumbua na visheti mitaani. Suluhisho ja utoro wa walimu shuleni si kuwasema bungeni, bali ni kuwapatia mishahara inayokidhi angalau theluthi ya mahitaji yao pamoja na kuwapatia posho ya kufundisha na hata kuwapandisha vyeo kwa wakati. Hapo watakuwa wanabaki vituoni huku wakijituma kwa 100%
 
Zaidi ya nusu ya wabunge wanalipwa mishahara ya bure. wangi husinziasinzia na kugonga meza kuunga mkono hoja.hufanya ziara majimboni uchaguzi ukikaribi.ofisi ya mbunge muda mwingi umefungwa
 
Tufanye mjadala wa kitaifa na mapendekezo yote yapelekwe Serikalini kwa kufanyiwa kazi hata kwa awamu! Kuna mambo mengi sana kwenye sekta ya elimu, motisha uwezo wao madaraja kozi fupi na ndefu mitaala pia!
brother ni muda wa action na sio mijadala tena tangu enzi za mwalimu julius Nyerere mpaka enzi za mwalimi sijui nani vile bado tujadili tu? wafanye maamuzi tu waifanye sekta ya ualimu ionekane yenye umuhimu kisha tuone matokeo yake sio mtu anaishi kwa laki tano kwa mwezi hapo katikati hakuna chochote wakati mwenzake mwenye elimu sawa analipwa zaidi ya milioni na marupurupu kibao unategemea nani afanye kazi kwa moyo hapo
 
kabla yakumtupia lawama mwalimu hebu rudini nyuma kidogo angalieni hali ya huyu mwalimu; mshahara kiduchu.mazingira ya kazi bado ni shida.darasani unapewa watoto nyomi.acheni jamani.
Hata akipewa mshahara wa 10m bado uwajibikaji utakuwa ni wahofu tuuu
 
Hili hata halina ubishi, walimu tubadilike. Hasira zetu juu ya serikali tusizihamishie kwa wanafunzi wasio na uwezo wa kujitetea. Tunawadhurumu watoto haki zao na baadae tunazalisha vijana wasiojielewa, wavuta bangi, wazurulaji n.k
Mmh!
 
kabla yakumtupia lawama mwalimu hebu rudini nyuma kidogo angalieni hali ya huyu mwalimu; mshahara kiduchu.mazingira ya kazi bado ni shida.darasani unapewa watoto nyomi.acheni jamani.
Basi angeacha kazi, mbona kuna watu kibao wanafanya kazi ngumu kwa malipo kiduchu na bado wanafanya kwa ufanisi? Mfano walinzi. Wamekuwa watu wa kulalamika kila siku wakati hawatimizi wajibu wao!!! Wafanye kazi kwa bidii then wailaumu serikali kwa kutowajali, hapo hata sisi wananchi tutawatetea....siyo kwa mtindo huu wa kuzurula ovyo na kusubiri huo mshahara wanaouita mdogo! Wanaboa.
 
kiukweli wabunge wameamua kuwashupalia walimu. mbona hawazungumzii changamoto kubwa zilizopo shule za umma ? hususani ukosefu wa walimu wa sayansi na hisabati? je kina zitto hawalioni hili? any way kwa hiyo wabunge wanalipwa mishahara ya halali?
Tatizo letu tunapenda kuharalisha uovu kwa uovu!!! Kwanini tusianze kulishughurikia hili la walimu kutotimiza wajibu wao then hayo mengine yafate? Inamaana unaona sawa tu walimu wanavyozurula ovyo mitaani wakati wanetu wako madarasani wakiwasubiri!!!? Huoni kama hili ni hatari zaidi!? Tunajenga kizazi kipi cha kesho!!? Comment za aina yako zinanipa picha kwanini miaka50+ ya uhuru bado tuko palepale.
 
Chanzo cha walimu kutoingia darasani kwa asilimia kubwa ni selikari. Hii ni kwa sababu madhingira ya kufundishia na kujifunzia Kwa mwanafunzi siyo rafiki pamoja na maslahi duni Kwa walimu vilevile malimbikizo mbalimbali Kwa baadhi ya walimu.
 
Basi angeacha kazi, mbona kuna watu kibao wanafanya kazi ngumu kwa malipo kiduchu na bado wanafanya kwa ufanisi? Mfano walinzi. Wamekuwa watu wa kulalamika kila siku wakati hawatimizi wajibu wao!!! Wafanye kazi kwa bidii then wailaumu serikali kwa kutowajali, hapo hata sisi wananchi tutawatetea....siyo kwa mtindo huu wa kuzurula ovyo na kusubiri huo mshahara wanaouita mdogo! Wanaboa.
Kwani wewe unadhani ni walimu wote wanaula huo mshahara wa bure!? Mbona kuna shule znafaulisha vema tu kwa muda mrefu tu? Nini cha maana wamepewa hao watumishi wa hzo shule ili kukazia uwajibikaji wao, sanasana na wao c wanaonekana wala mshahara wa bure na kudharaulika na baadhi ya wanajamii wenzao kutokana na uduni wa maisha yao? Think big!
 
Waalimu wa serikalini wana mishahara midogo sana pia mazingira magumu. Serikali isikimbie majukumu itimize wajibu. Huyo Zitto ni wa kumdharau tu.
 
Back
Top Bottom