JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.
usimfananishe Zito na kina Mkono, wana pesa wale hawategemei serikali wanajenga kwa pesa zao mfukoni.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.
Karibu kwa Mchango wako wa kwanza wenye ujumbe mzito kuliko michango elfu moja ya baadhi ya wana JF humu.
Zitto aliingia mkataba wa kuwatumikia watu wake na hajafanya hilo,anasema hivi sasa anamiliki magari matano ndani ya miaka mitatu ya bungeni, chanzo chake ni watu wa Mwandiga waliompa ile fursa ya yeye kuwa Mbunge na kupata marupurupu hayo. sio sisi JF tuliompa nafasi hiyo.bahati mbaya wachangiaji wengine hapa wana roho mbaya na kuwachukia watu wa Mwandiga wasipelekewe maendeleo na mbunge wao.
Basil Mramba amejenga shule 32 jimboni mwake na mbili za ghorofa kwa msaada wa Waarabu, Yona pamoja na nafasi zote hajafanya kitu kwao.Anna Kilango anapiga vita ufisadi lakini hasahau watu wake wa SAME MASHARIKI kuwapelekea maendeleo.
DR.Salim Ahmed Salim analaumiwa na watu wake kwa kutokupeleka maendeleo kwao.wema huanzia nyumbani,Lwakatare kwa nafasi ya ubunge wa bukoba mjini miaka mitano iliyopita amewafanyia mambo mengi watu wake.kwanini Zitto tumdanganye kuwa ni kamanda wa nchi?