TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Mkuu Ritz heshima sana,
Mkuu wangu Zitto hana sifa za kugombea urais wa JMT kwa katiba ya sasa ambayo imebainisha wazi umri wa kugombea ni miaka 40.Katiba mpya inaweza kufanyiwa marekebisho ya kupunguza umri ili kukidhi matakwa ya Zitto kugombea nafasi hiyo kubwa na nyeti hapa nchini Tanzania.
Iwapo katiba mpya itafanyiwa marekebisho ya kupunguza umri Zitto atakuwa na sifa ya kugombea urais wa JMT.Chama chake hakitakuwa na kipingamizi cha kumzuia atashindanishwa na wanachama wengine atakayepata kura nyingi kuliko wenzake atapewa nafasi ya kugombea.
Zitto Kabwe atatakiwa kujiweka karibu na wanachama wa chama chake kwa kushiriki kukijenga na kuhakikisha kinaenea kila pembe ya nchi.Operesheni zinazoendelea kama Sangara na M4C ni jukwaa atakalotakiwa kulitumia vyema ili kujiweka karibu na wanachama na wapenzi wa CDM wakati huo huo akiomba katibu mpya ya mwaka 2014 ipunguze umri wa mgombea urais.
Maoni yangu mpaka sasa sijaona Zitto akishiriki kukijenga chama chake kupitia M4C badala yake ameanzisha kikundi chake nje ya programs za chama chake kwa minajili ya kutengeneza mazingira yatakayomhakikishia anapewa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama.Nadhani bado unakumbuka mbunge wa Kigoma Kusini Mheshimiwa David Kafulila alivyokuwa akibwabwaja bungeni kwamba sasa ni zamu ya Kigoma !.
kafulila alikosea sana kwamba sasa ni zamu ya kigoma wakati wenye chama chetu bado hatujatoa rais hata mara moja(kaskazini)
Last edited by a moderator: