Kufuatia hatua ya IKULU kumsafisha David Jairo, leo Bungeni kwa mujibu wa Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kunategemewa kuwaka moto kwa sababu Bunge limedharauliwa kwa kumsafisha Jairo ambaye aliwatukana wabunge kuwa ni kama komedy.
Aidha wabunge wamepania kuamua either Jairo abaki ila Pinda ajiuzuru au Jairo aondoke Pinda abaki. Uamuzi wa IKULU kumsafisha Jairo ni dharau kubwa kwa Pinda ambaye alisema angekuwa yeye angemfukuza kazi mara moja, inategemewa kuwa Pinda na wabunge wataungana kumshughulikia Luhanjo na Jairo.
Zitto kishatoa hoja bungeni ya kutaka taarifa ya CAG ipelekwe bungeni mara moja... Wabunge wengi wameunga mkono hoja hiyo, Ndugai kaenda faragha, Simbachawene kavaa joho kwa muda.
Tusubiri tuone.
Aidha wabunge wamepania kuamua either Jairo abaki ila Pinda ajiuzuru au Jairo aondoke Pinda abaki. Uamuzi wa IKULU kumsafisha Jairo ni dharau kubwa kwa Pinda ambaye alisema angekuwa yeye angemfukuza kazi mara moja, inategemewa kuwa Pinda na wabunge wataungana kumshughulikia Luhanjo na Jairo.
Zitto kishatoa hoja bungeni ya kutaka taarifa ya CAG ipelekwe bungeni mara moja... Wabunge wengi wameunga mkono hoja hiyo, Ndugai kaenda faragha, Simbachawene kavaa joho kwa muda.
Tusubiri tuone.
Here we Go
Zitto Kabwe ametoa Hoja binafsi kwa kuzingatia kanuni 51.3 kifungu F ambacho kinampa mbunge nafasi ya kutoa hoja bila kufuata utaratibu wa Taarifa.
Amenukuu Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi ambaye anasema kwa mujibu wa Taarifa ya makaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Ludovick Uttoh amethibitisha kuwa Katibu Mkuu Nishati Madini David Jairo hana tuhuma ya kujibu na arudi ofisini kuanza kazi leo huku akiwa huru kuwachukulia hatua waliomchafua kwa kashfa hizo.Zito anasema kufanya hivyo ni kuingilia shughuli za mhimili mwingine wa Dola huku mtendaji Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni Mh. Pinda alishatamka kuwa kama angekuwa ni uamuzi wake angemchukulia hatua JairoZito anasisitiza kuwa Bunge si mahakama ila kwa taarifa hiyo ya Katibu Mkuu Kiongozi ni kudhihaki shughuli za Bunge.
Kwa mantiki hiyo, namnkuu '' Napenda nitoe hoja kwa Bunge kusitisha kujadili shughuli zote za serikali mpaka hapo Tarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali itakapoletwa hapa Bungeni na kujadiliwa''Wabunge wote wanasimama kuonyesha kuunga Mkono hoja hiyo.Jambo ambalo linampa wakati mgumu Ndugai ambaye analazimika kumruhusu Lukuvi kuzungumza kama ana ufafanuzi wowote juu ya hilo.
Ngoma ni Nzito na baadhi ya watendaji wakuu wanaitana chemba kujadili suala hili huku kiti sasa kikikabidhiwa kwa Simbachawene ili kuendesha kipindi cha maswali na majibu wakati huo majadiliano yakiendelea chembe.