mbogo31
JF-Expert Member
- Nov 28, 2008
- 711
- 173
Kama Bunge limepokea ipo haja ya kufanya mjadala mpana kuhusu Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya Mwaka 2002 badala ya judali tu matamko ya Mhe. Waziri Mkuu na Mawaziri. Sheria hiyo pamoja na Kanuni za Utumishi wa Umma, 2003, Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma 2009, Nyaraka mbali mbali za utumishi na maagizo yanayotolewa yana kasoro kubwa ambazo leo ndiyo zinachochea migomo ya moja kwa moja watumishi kama huu wa madaktari au ya chini chini ambayo ni ya hatari zaidi inayofanywa na watumishi wengine wa umma. Ni kawaida siku hizi katika ngazi zote kukuta watumishi wanapiga tu soga badala ya kufanya kazi na mahali pengine viongozi wao; Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wamejikuta wakifanya kazi ya kusaini barua za maagizo, ajira, kualika watu kwenye tafrija na maonyo badala ya kuketi na kufikiri ni kwa kiasi gani wanaweza kutumia dhamana zao kutafuta njia za kukuza uchumi (Kama huamini uliza Wizara ya Afya, TAMISEMI na Utumishi utajua). Pamoja na maboresho ya Serikali yanayoendelea bado changamoto ni nyingi mno kiasi kwamba ni vigumu kujua ni wapi hasa tunaelekea. Kimsingi Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeshindwa kujipambanua kama taasisi inayopaswa kuwa na dira ya kuongoza utumishi Tanzania. Kila mtu ana fanya lake ili mradi siku zinakwenda. Wazee wazoefu kama Mhe. William Shelukindo na Mhe. Ntukamazina wanaweza kuona na kusema ni kwa kiwango gani Utumishi imepoteza dira.
Kaka umenena Vyema, nchi kwa hivi sasa haina Dira.