Mbwiga_Plus
Senior Member
- Jan 5, 2011
- 163
- 42
Wanajamvi,
Nimepigiwa simu na Ndugu yangu anayeishi Dodoma mjini akinihabarisha kuwa Mheshimiwa Zitto Kabwe anajenga Hoteli kubwa sana ya Nyota 5 Mjini Dodoma, eneo liitwalo KISASA.
Hili ni jambo jema na la maendeleo sana, lakini Je Zitto, hili jambo ni kweli?
Umekuwa unapinga hata kuwa na magari ya kifahari, huku ukisema kuwa hushabikii UTAJIRI, je fedha za kupandisha jengo kubwa na la kifahari kama hilo ni hizihizi za posho zenu, au umekopa benki, au umepewa na mfadhili, au una vyanzo vingine vilivyofichama?
Tafadhali sana Zitto, njoo ujibu kwa kauli yako mwenyewe!
Nawasilisha!
Nimepigiwa simu na Ndugu yangu anayeishi Dodoma mjini akinihabarisha kuwa Mheshimiwa Zitto Kabwe anajenga Hoteli kubwa sana ya Nyota 5 Mjini Dodoma, eneo liitwalo KISASA.
Hili ni jambo jema na la maendeleo sana, lakini Je Zitto, hili jambo ni kweli?
Umekuwa unapinga hata kuwa na magari ya kifahari, huku ukisema kuwa hushabikii UTAJIRI, je fedha za kupandisha jengo kubwa na la kifahari kama hilo ni hizihizi za posho zenu, au umekopa benki, au umepewa na mfadhili, au una vyanzo vingine vilivyofichama?
Tafadhali sana Zitto, njoo ujibu kwa kauli yako mwenyewe!
Nawasilisha!
Wakati mwingine uongo na uzushi wa kipuuzi Kama huu ukiachwa kuna watakaoamini. Sio tu kujenga Hotel, sina hata kiwanja Dodoma. Sitegemei kuwa na kiwanja Dodoma wala kujenga Dodoma.
Nimezushiwa mengi sana
1. Nina nyumba Masaki
2. Nina 900m StanBic
3. Nina kiwanda cha kokotoNa mengine mengi sana.
Yote hayo sio ya kweli na kuna watu wanayaamini.
1. Sina biashara yeyote hapa Tanzania
2. Sina nyumba yeyote Dar. Nina shamba la Ekari tatu tu Mbutu na halijaendelezwa toka mwaka 2004.
3. Ninaishi flats za kupanga Tabata
4. Sina na wala sijwahi kuwa na tamaa ya utajiri katika maisha yangu. Property isn't my thing kabisa.
JF Mtu akileta accusations dhidi ya mtu mwingine tafadhali aje na ushahidi wa mfano picha ya nyumba, ushahidi wa umiliki ambao ni rahisi sana kupata CDA kwa DODOMA au Wizara ya Ardhi.
Tuache umbeya tuseme kweli. Sikatai Kusemwa kwa ya kweli. Ninajifunza sana kwa critics za ukweli. Lakini uzushi Kama huu unaumiza
Kila la kheri