Zitto hayuko tayari kuwa kiongozi!

Utabiri umetimia ubishi wa kutokusiliza tangu niandike 2010!. Ukitaka mawazo zitto ni bip kwenye email hapa nitakupa mawazo ni jinsi gani ya kufanya kwani wengine tunaona mbali ushauri wa bure tu!
 
Kamundu

Yaani umekichana chadema live kabisa bila wewe kujua, umefikiri unajenga kumbe unamaliza kabisa

Chama chenye sera nzuri kinaongozwa na watu na michango ya watu, ni sawa na harusi hata kama una fedha nyingi bila watu kuchanga haifurahishi, maana haishirikikiki!! umenena live chadema ni cha wachache wafanyabiashara!!! wafanya bishara hawako tayari kwenda jela kwa ajili ya manufaa ya wananchi wako tayari kulinda fedha na status zao!

Hivi umefikiria ulichoandika maan naona umeeleza ukweli wa moyoni kitu ambacho chadema wengi huwa wanabisha na wewe live umeeleza ni wafanyabiashara, believe me, Ndesamburo na hao wengine lazima wanapata faida!!!how?? au wanajitolea tu lwa sababu wanakupenda sana!!!

Huyo slaa ni mroho wa hela na alihaidiwa mshahara fulani akikosa urais, unalijua hilo

Kuhusu Zito well, kuna mawali mengi BEING PROFESSOR AU ACADEMICIAN AS NOTHING TO DO WITH POLITICS!!! POLITICS IS NOT PROFESSIONAL FOR PARTICIPANTS; IS OPTION ONLY FOR POLITICAL SCIENTIST!!
Ndiyo maana kuna mainjinia akina Mwandosya, chemist Dr.Magufuli, n.k you can be politician still you can excell to your professional , hapa inahitaji akili kidogo tu, na siamini kabisa kuwa una umri huo. Dr.Magufuli amepata masters na PhD akiwa kiongozi/mwanasiasa (record this)

Umeweka vijembe eti hakuna mfanyabiashara mkubwa Mha!!! yaani umeleta ukabila live ule tunaopigana nao humu!!! ar you sure

FYI Zito ameingia chadema akiwa na miaka 16!!! na amepokelewa na hao unaowasema na leo hii wamempa unabibu katibu mkuu!! japo unafikiri unawasemea akina Slaa ila wengi wanakushangaa lengo la hii post ni nini?? wapi umemkamata amefanya kosa gani (with evidence) na maoni yako ya kutokuwa na imani naye yanapingana na maoni ya kamati kuu ya chadema akiwamo meti na ndesamburo!!

By the way unasoma chuo gani huko marekani? maan paragraph hamna I mean post yako haivutii kabisa

Mleta hoja haoni hata aibu kujinasibisha na watu kama Zitto.
Hoja zake kazijenga kipuuzi na wanaomuunga mkono ni kwa sababu ya chuki zao za kipuuzi dhidi ya Zitto.
Zitto si failure wa kisiasa ni hakupatana ba viongozi wenzake ndani ya cdm huku kila upande ukijustify misimamo yao kwa njua mbalimbali.
Mimi naiunfa mkono cdm lakini moyoni mwangu huzuni kukosa mtu jana Zitto.
Watu wa juu mna namna yenu ya kufanya siasa ila sio siri Zitto anajua kufanya siasa na mtu chini kabisa wala haihitaji kupigiwa debe ili apendwe tofauti na viongozi wengi si cdm tu hata vyama vingine sifa na uhodari wao unapigiwa kampeni mpaka mtu unajiuliza kunani?
Zitto ametoka cdm na baadhi yetu tutamkumbuka sana kwa mazuri mengi kuliko "mabaya"yaonwayo na wachache tu !
 
Last edited by a moderator:
Mimi ninachokiona ni kushindwa Kusimama kutetea pale watu waliofukuzwa kwa Ajili ya Siasa zake waliofukuzwa kwa usaliti ...Sasa mwisho amekutwa yeye...yaani hili sakata unaweza kuandika andiko la kisomi Pamoja na like la NCCR Mrema ...utagundua namna gani kuna tofauti ya strategy ..

Wakati Kafulila anafukuzwa wote tunaujuwa alikua anatetea nini ...ACHA Yule ma'am wa NCCR ,Kina MTELA ,Juliana ,Dandu,na hawa wa ACT ...Mwigamba na Mkumbo ....yaani vyote Hivyo ni vichwa ambavyo mwaka huu lazima wangeshinda Ubunge sehemu wanapotoka .....lakini Sasa wengi future Yao imeharibika ....
 
Mimi ninachokiona ni kushindwa Kusimama kutetea pale watu waliofukuzwa kwa Ajili ya Siasa zake waliofukuzwa kwa usaliti ...Sasa mwisho amekutwa yeye...yaani hili sakata unaweza kuandika andiko la kisomi Pamoja na like la NCCR Mrema ...utagundua namna gani kuna tofauti ya strategy ..

Wakati Kafulila anafukuzwa wote tunaujuwa alikua anatetea nini ...ACHA Yule ma'am wa NCCR ,Kina MTELA ,Juliana ,Dandu,na hawa wa ACT ...Mwigamba na Mkumbo ....yaani vyote Hivyo ni vichwa ambavyo mwaka huu lazima wangeshinda Ubunge sehemu wanapotoka .....lakini Sasa wengi future Yao imeharibika ....

Tena kibaya ni kuwa wapo ambao ALIOFANYA nao mambo yalipogunduliwa akawakana
 
Nilitokea kumjua zitto kutokana na marafiki zangu waliosoma naye kule Galanos. Vilevile mimi nilisoma Galonos form five mwaka 1994-1995 miaka miwili kabla ya zitto. Vilevile zitto nimempita mwaka moja kwani yeye kazaliwa 1976 na mimi 1975. Kwa ujumla mimi nilijiona nafanana sana na huyu kijana mpya ambaye ameingia kwenye siasa na hivyo alivyotembelea USA nilihakikisha ninaongea naye kwani niliona ni watu wa rika moja na tutaelewana zaidi kuliko wazee wengi wanakuja huku.

Zitto alivyokuja aliniambia mimi na vijana wengine anataka kupumzika siasa na kwenda kusoma PHD. Vilevile tulimuuliza kama anataka msaada wowote atwambie akasema kapata shule nyingi ikiwa pamoja na Preston University amboyo ni chuo kizuri sana kiko State ya New Jersey. Alisema alitaka kusoma mambo ya economics contracts ili aweze kufundisha kwenye chuo kimoja nafikiri Dodoma kuhusu mikataba kama ya madini na n.k kwani alisema nchi yetu inahitaji wataalamu wa mikataba. Vilevile tuliongea mambo mengi na kibinafsi ambayo sitataka kuyasema. Kwa ujumla Zitto alituambia na kuonekani waziwazi hapendi siasa na hana furaha na kitu anachofanya.

Vilevile alionyesha waziwazi anapenda kuwa Professor wa chuo kikuu chochote. Zitto alitoa ahadi nyingi ikiwa ni pamoja ya kujibu email zetu na kutusaidia kuelezea mambo fulani muhimu ambayo watu wengi wa diaspora tulikuwa tunaona kama yanahitaji mwangeaji.

Zitto alishangaza wengi kwani hajafanya hata kitu kimoja alishokuwa anasema ikiwa ni pamoja na kwenda chuo, kujibu email na kuwasiliana na kuongea mambo muhimu ya diaspora ambayo tulikubaliana naye kutusaidia ku lobby. Vilevile Zitto alionekana hana experience ya maisha kama kufanya kazi ya kawaida au kufanya biashara!.

Kwa mawazo yangu Zitto ni mapepe ni kijana mwenye akini lakini anatakiwa kutulia na kujua anataka kufanya nini hasa kwenye maisha. Vilevile Zitto haelewi kwa undani ni kwanini Chadema iko imara kuliko nyama vingine.

Chadema iko imara kwasababu
(1)Viongozi na waanzilishi wa Chadema wamejitosheleza kiuchumi na hawana tamaa. Uhodari wa kuongea na ushabiki hautoshi kukuza chama kikubwa kama Chadema. Mrema alikuwa ni hodari na mwenye kipaji cha mvuto kwa wananchi lakini kwasababu ya umasikini wake alikuwa nategemea sana serikali kuanzia ruzuku hadi nyumba aliyokuwa anakaa. Hii ilimfanya Mrema kutangatanga bila mafanikia na kuhama vyama bila mafanikio makubwa kwasababu Mrema alikuwa hajajitosheleza na maisha aliyokuwa nayo na alitegemea sana serikali. Zitto ni kama Mrema ingawa Tatizo lake hajui anachotaka bado!

(2)Mboe, Slaa, Ndesamburo na Mtei. Dr Slaa alikuwa padre ambaye alishazoea kuishi maisha marahisi na ya wito hivyo hawezi kutapatapa. Mboe, Ndesamburo na Mtei ni wafanya biashara wakubwa wenye akili ya biashara na wanafanya biashara ambazo hazitegemei serikali hivyo serikali haiwezi kuwatisha. Mtei ana biashara ya kupeleka maua nje, Ndesamburo ana viwanda na hoteli na Mboe ana hoteli hivyo hawa watu hawawezi kudanganya na watu wa serikalini. Ndesamburo kununua Helikopta mbili kwa chama ni mfano kwani ameonyesha anafanya vitu kwa wito na sio shida.

(3)Viongozi wa Chadema wana ongoza chama kibiashara hii inawezekana isionekane waziwazi lakini Mboe ni mtu muhimu kuliko Zitto kwasababu anajua kuongoza. Zitto anafikiri kidemokrasia lakini kwenye kampuni hakuna demokrasia bali productivity. Mboe ana results na Zitto hana, Mboe ana experience za utawala Zitto hana, Mboe anajua anachokitaka na Zitto hajui. Hivyo Zitto anaweza akawa ni mtu mwenye kipaji cha akili zaidi ya Zitto na Mvuto zaidi ya Mboe lakini hana uwezo wa kuongoza kwasasa zaidi ya Mboe!.

Mboe vilevile anavitu kama magazeti n.k ambavyo ni muhimu kutoa habari na Zitto hata email hajibu!. Chadema ingekuwa haina watu matajiri kwenye chama na wenye wito chama kingeshakufa sikunyingi sana. Huwezi kupambana na CCM kwa sera pekee! Zitto.

Zitto ni lazima uelewe kwamba mafanikio ya Chadema ni ya wito na utajiri wa waanzilishi na viongozi na si uhodari wa kuongea pekee. Kuna watu watakudanganya uhame chama kwa kuweka udini na kukupa kichwa kwamba wewe una kipaji utafanikiwa popote lakini kuwa mwanasiasa hodari si sawa na kuwa kiongozi hodari!. Mboe ni muhimu kwa Chadema kuliko wewe. Je ni mfanya biashara gani mkubwa ni muha wa kigoma!!.

Ni lazima uwaheshimu watu waliokutoa kigoma mpaka hapo ulipo kwani hawa wanaokushauri uhame ndiyo wa kwanza watakao kuita Muha wa kigoma anayetangatanga na hutakuwa na watu wenye nia nzuri kwako bali kukutumia tu. Hivyo Zitto tulia na jenga imani na jifunze kutoka kwa kina ndesamburo, Slaa na Mboe jinsi ya kufanikiwa kimaisha bila siasa!.Muda wako utakuja hapo utakapojua ni kitu gani unataka kufanya, vilevile acha uongo!.

Zitto kwasasa hauko tajari kuwa mwenyekiti wa Chadema.
mleta hoja ana mtazamo wa kibaguzi na hoja dhaif sana CDM haijafika ilipo sasa sababu ya utajiri wa viongoz wala sababu inaongozwa na kabila fulan, imefika hapa sababu ya seraa hasa kuwasrmea wanyonge na kuwatetea. mleta mada kwanza ameikimbia nchi ameamua kuwa mtumwa ktk nchi nyingine na hafaham siasa za ktz zinavyoendeshwa
 
Kwaheri former Mh. Zitto Kabwe
Kamundu, you are a wise man, mungu atakulipa nashukuru kuwa huu ujumbe umetoka diaspora manake sisi local huyu bwana mdogo alishaacha kutusikia maana tayari alishajiona hatuna sera, walau wewe unayekaa marekani labda hicho kinaweza kuwa kigezo walau. Ila asante kwa kuwa mkweli na kusema kisomi. Tatizo ni kwamba huyu dodo alishaimbiwa kwa miaka lakini alishakula najisi, allishasema Chadema bila yeye hapana, atafanya kila mbinu kife. mtu huyu anamzigo mzito, maana kuwa selfish kiasi hiki ni laana. Kwamba uko radhi chama kinachotetea watoto, albino, yatima wanaweke wajawazito kifutike kama hakitakuvumilia wewe? Kwanza nani angebaki kwenye chama cha Zitto na yeye anajua ndio maana haendi ACT.

Mahakama imemsaidia kufikia maamuzi ili aende kwenye chama anachokiamini

Anachotaka ni kutumia nguvu, hekima na fedha za wengine kujijenga yeye. Hapo ndipo alipochina. Sasa ndio amejua kuwa hana kitu chochote aje mtaani atatukuta. Huyu dogo ananunuliwa kwa pesa yoyote. Kwa mfano wakati serikali imewagomea Mwananchi Communication kuendelea kuongozwa na mkenya Sam Shorlei, Zitto alipewa hela na National Media Group, specifically mkurugenzi wao waweru kwenda bungeni kupinga mkenya kunyimwa extension ya kibali cha kazi, nili happen kuwa Nairobi wakati huo kikazi na kuambiwa moja kwa moja kwamba swala la kibali cha Sam Shorley halina tabu kwa kuwa kuna mwanasiasa wamem contract ku challenge huo uamuzi wa serikali. Na ndip maana sikushangaa kumsikia Zitto bungeni akipinga hatua ya Tanzania kutaka nafasi hiyo iende kwa Mtanzania. He is that cheap. Huyu ndio bwana aliyesema akihisi kukosa anachotaka ataua hao anaowatuhumu, familia nzima mpaka panya na mende.

Hivi ana uwezo wa kulazimisha kuwa member wa umoja usiokutaka?
hana kwa sababu chama ni makubaliano hata kama cha siasa, wenzake wako busy na ukombozi wa nchi na watanzania 45m hawana muda mchafu na yeye. Nchi nzima imeshamjua kuwa ni mamluko rahisi (cheap), si kweli kuwa hakujua habari ya mahakama kukaa, ndio maana alitangaza kuwa ataamua hatima akiamini mahakama za CCM ziko upande wake. Asichokijua ni kwamba hata huko mahakamani wameichoka CCM na hawana sababu ya kupindisha maamuzi. Ukiwa na mungu hakuna nguvu itakayokuwa juu yako. Watanzania wako na Mungu naye atawavusha hapa kama alivyovusha wa Israel bahari ya shamu. Hakuna kitakachozuia ukombozi wetu tumechoshwa na serikali inayotutesa kiasi hiki
 
Utabiri umetimia ubishi wa kutokusiliza tangu niandike 2010!. Ukitaka mawazo zitto ni bip kwenye email hapa nitakupa mawazo ni jinsi gani ya kufanya kwani wengine tunaona mbali ushauri wa bure tu!

Mawazo yako ni ya Kimbumbu sana kwamba huwezi kuwa kiongozi kama siyo tajiri? hapo una maana gani kwambamba uongozi waachiwe tu kina Manji, Bhakresa na kina Mbowe kwa sababu ni Matajiri?
Unasema CDM inaendeshwa kibiashara hii maana yake? au unamaanisha CDM ni Kampuni au SACCOS?
 
Ninaona nichukuwe muda huu kufafanua vizuri vitu vichache. (1) Kwanza kibinafsi nampenda Zitto kuliko viongozi wengine wa Chadema. Hii sio unafiki bali ni ukweli na labda inasababishwa na ukweli kwamba mimi na Zitto ni watu wa rika moja na ninaona kama anaweka kuelewa vitu zaidi kuliko wazee.(2) Kuhusu Kigoma: Sina maana mbaya kwa watu waliotokea Kigoma na kama kuna mtu ameona nimebagua naomba msamaha kwani nilikuwa sina nia mbaya. Kuna watu wengi wengi wanafahamu kwamba mtoto wa Kikwete alikuwa rafiki wa Zitto walipokuwa Chuo kikuu hivyo basi ingekuwa rahisi kwa Kikwete kumuamini Zitto wakati anaonyesha nia yake ya kugombea. Ukweli ni kwamba CCM na Kikwete hawakuamini kama kijana mdogo kama Zitto alivyokuwa angeweza kuwa mbunge!. Chadema walimuamini Zitto kuliko CCM ingawa Zitto hakusoma na mtoto wa kiongozi yeyote wa Chadema wala hakukuwa na urafiki wa aina yeyote bali waliona kipaji na walimuamini Zitto. Ukweli ni kwamba hata sasa hivi CCM haiwezi kumpa Kijana wa Kigoma ambae hana pesa nafasi ya kuwa mgombea wao. Serikali ya CCM imesahau Kigoma kwa miaka mingi na ilikuwa inacheka wabunge wa CCM zamani walipokuwa wanaomba barabara na miradi mingine ya maendeleo. Serikali imeanza kuamini Kigoma baada ya Chadema kushinda. Kuwaita waha wa Kigoma ndivyo CCM ilivyokuwa inasema kichinichini na mimi nimejaribu kuisema hadharani.(3) Kuhusu wafanyabiashara wa kutokea Kigoma: Ni kweli kwamba hakuna wafanyabiashara na kama wapo ni wa chache. Mimi nilikuwa nataka kumuelewesha Zitto kwamba alisokuwa mwangalifu atabaki mwenyewe kwani hao CCM kwa miaka mingi hawakusaidia watu wa Kigoma na hakutakuwa na watu wengi mtaani wa kumsaidia pale atakapo anguka. Kigoma sio stable kwasasa na Zitto anatakiwa asaidie maendeleo badala ya kutangatanga. Movement ya maendeleo ya Kigoma haitapata mvuto kama utahama kwasababu hakuna watu wengi wenye nguvu za kiuchumi na kisiasa waliotokea huko. Kikitokea kitu Arusha, Kilimanaro, Mwanza au Mbeya utaona kinatangazwa kwasababu kuna wanasiasa na wafanyabiashara wengi wametokea huko! Mengi atatangaza kwenye TV, Mboe ataandika kwenye gazeti n.k. Zitto huna hiyo nguvu kwasasa na nina wasiwasi ukianza kutangatanga hao CCM ndiyo wa kwanza kukucheka. Zitto nyumbani Kigoma bado hakujatulia. Mboe mwenzako analami mpaka kijijini kwasababu lami ya mboe na mengi ni hiyohiyo.Huu ni ukweli nilazima ujue uko nafasi gani ili uweze kuleta maendeleo kwa jamii yako.Usipigane hata simu moja kama unajua utashidwa na hauko tayari. Zitto ukiwa mvumilivu utashinda lakini kwasasa hauko tayari unahitaji muda kujua ni kitu gani unataka kufanya.
Mkuu umeongea mambo mengi sana lakini umenigusa tu umevyotutukana sisi waha ASANTE KWA HILO.Jambo la msingi la kuzingatia na kuelewa ni kwamba CDM ni chama cha baadhi ya watu MATAJILI km ulivyosema na sio cha watu MASIKINI WAKIGOMA.Na kupitia zitto mmetuonyesha hilo hatutakiwi ndani ya CDM.Kuipa kura CCM siwezi lakini kura sintopiga tena ndani ya maisha yangu maana inaonekana siasa ni yawatu WENYE PESA ZAO TU.ZITTO KABWE elewa wewe hutakiwi kuwa kiongozi wa CDM kisa sisi WAHA ni MASIKINI na CDM ili uwe kiongozi mkubwa lazima uwe TAJILI.
 
Mawazo yako ni ya Kimbumbu sana kwamba huwezi kuwa kiongozi kama siyo tajiri? hapo una maana gani kwambamba uongozi waachiwe tu kina Manji, Bhakresa na kina Mbowe kwa sababu ni Matajiri?
Unasema CDM inaendeshwa kibiashara hii maana yake? au unamaanisha CDM ni Kampuni au SACCOS?

Mkuu huyu mtoa mada amejaribu kuonyesha ubaguzi wa wazi kabisa.
 
Mtoa mada ni mwehu tu hizi porojo kaandika kwenye MTANZANIA DAIMA linunuliweama njugu pale UFIPA
 
Mleta mada unaujumbe wenye mantiki sana kwa Zitto, uimara wa Chadema ni kutokana na viongozi wake wakuu kujiweza kiuchumi.

Bila hivyo chadema ingeendelea kuwa chama cha kawaida kama cuf na NCCR mageuzi.
 
Uongozi ni zaidi ya zaidi ya theories ni jinsi unavyoishi na watu kama unakaa na watu kwa kuaminiana, mna kula pamoja, kunywa pamoja, familia zinajuana hayawezi kutokea ya Zitto. Zitto angeweza akawa mwenyekiti kama angesubiri na kujijenga kwanza kuaminiana na wanachama na viongozi wenzake. Marafiki hawasemani kwenye vyombo vya habari Zitto alibaki na nia ya binafsi zaidi na ndiyo maana imekuwa tatizo. Chadema bado ni chama kidogo kwa idadi ya viongozi hivyo huwezi kuwa Naibu katibu ukawa kama mfanyakazi kwenye kampuni ni lazima uweze kuishi na wenzako vizuri na kwa kuheshimiana.
 
Ajabu ni pale wanaosikitika zaidi ni CCM kuliko Chadema. Mtoa mada salute, ZZK kalewa sifa za watoto wa fb na twiter ukichanganya na sifa za kina Mwigulu, anahisi na kujona yupo juuu sana. Anasahau hao hao ndio walikuwa wanamshauri na kumsapoti afungue kesi wakati anajua vifungu vya katiba vitamnyonga. Tana uamuzi umetolewa na mahakama ajabu lawama wabebe Chadema. Come on guys! Katiba lazima iheshimiwe hata kama hamtaki. Kama mbaya badilisheni vifungu vibaya ila hatutaki kuendesha nchi kishkaji kama wanavyofanya CCM now. Zito hujiulizi unapambana na CCM eti hao ndio wanaokusifu kuwa mpambanaji hodari lol! Swallow your pigish pride brother!
 
Nilitokea kumjua zitto kutokana na marafiki zangu waliosoma naye kule Galanos. Vilevile mimi nilisoma Galonos form five mwaka 1994-1995 miaka miwili kabla ya zitto. Vilevile zitto nimempita mwaka moja kwani yeye kazaliwa 1976 na mimi 1975. Kwa ujumla mimi nilijiona nafanana sana na huyu kijana mpya ambaye ameingia kwenye siasa na hivyo alivyotembelea USA nilihakikisha ninaongea naye kwani niliona ni watu wa rika moja na tutaelewana zaidi kuliko wazee wengi wanakuja huku.

Zitto alivyokuja aliniambia mimi na vijana wengine anataka kupumzika siasa na kwenda kusoma PHD. Vilevile tulimuuliza kama anataka msaada wowote atwambie akasema kapata shule nyingi ikiwa pamoja na Preston University amboyo ni chuo kizuri sana kiko State ya New Jersey. Alisema alitaka kusoma mambo ya economics contracts ili aweze kufundisha kwenye chuo kimoja nafikiri Dodoma kuhusu mikataba kama ya madini na n.k kwani alisema nchi yetu inahitaji wataalamu wa mikataba. Vilevile tuliongea mambo mengi na kibinafsi ambayo sitataka kuyasema. Kwa ujumla Zitto alituambia na kuonekani waziwazi hapendi siasa na hana furaha na kitu anachofanya.

Vilevile alionyesha waziwazi anapenda kuwa Professor wa chuo kikuu chochote. Zitto alitoa ahadi nyingi ikiwa ni pamoja ya kujibu email zetu na kutusaidia kuelezea mambo fulani muhimu ambayo watu wengi wa diaspora tulikuwa tunaona kama yanahitaji mwangeaji.

Zitto alishangaza wengi kwani hajafanya hata kitu kimoja alishokuwa anasema ikiwa ni pamoja na kwenda chuo, kujibu email na kuwasiliana na kuongea mambo muhimu ya diaspora ambayo tulikubaliana naye kutusaidia ku lobby. Vilevile Zitto alionekana hana experience ya maisha kama kufanya kazi ya kawaida au kufanya biashara!.

Kwa mawazo yangu Zitto ni mapepe ni kijana mwenye akini lakini anatakiwa kutulia na kujua anataka kufanya nini hasa kwenye maisha. Vilevile Zitto haelewi kwa undani ni kwanini Chadema iko imara kuliko nyama vingine.

Chadema iko imara kwasababu
(1)Viongozi na waanzilishi wa Chadema wamejitosheleza kiuchumi na hawana tamaa. Uhodari wa kuongea na ushabiki hautoshi kukuza chama kikubwa kama Chadema. Mrema alikuwa ni hodari na mwenye kipaji cha mvuto kwa wananchi lakini kwasababu ya umasikini wake alikuwa nategemea sana serikali kuanzia ruzuku hadi nyumba aliyokuwa anakaa. Hii ilimfanya Mrema kutangatanga bila mafanikia na kuhama vyama bila mafanikio makubwa kwasababu Mrema alikuwa hajajitosheleza na maisha aliyokuwa nayo na alitegemea sana serikali. Zitto ni kama Mrema ingawa Tatizo lake hajui anachotaka bado!

(2)Mboe, Slaa, Ndesamburo na Mtei. Dr Slaa alikuwa padre ambaye alishazoea kuishi maisha marahisi na ya wito hivyo hawezi kutapatapa. Mboe, Ndesamburo na Mtei ni wafanya biashara wakubwa wenye akili ya biashara na wanafanya biashara ambazo hazitegemei serikali hivyo serikali haiwezi kuwatisha. Mtei ana biashara ya kupeleka maua nje, Ndesamburo ana viwanda na hoteli na Mboe ana hoteli hivyo hawa watu hawawezi kudanganya na watu wa serikalini. Ndesamburo kununua Helikopta mbili kwa chama ni mfano kwani ameonyesha anafanya vitu kwa wito na sio shida.

(3)Viongozi wa Chadema wana ongoza chama kibiashara hii inawezekana isionekane waziwazi lakini Mboe ni mtu muhimu kuliko Zitto kwasababu anajua kuongoza. Zitto anafikiri kidemokrasia lakini kwenye kampuni hakuna demokrasia bali productivity. Mboe ana results na Zitto hana, Mboe ana experience za utawala Zitto hana, Mboe anajua anachokitaka na Zitto hajui. Hivyo Zitto anaweza akawa ni mtu mwenye kipaji cha akili zaidi ya Zitto na Mvuto zaidi ya Mboe lakini hana uwezo wa kuongoza kwasasa zaidi ya Mboe!.

Mboe vilevile anavitu kama magazeti n.k ambavyo ni muhimu kutoa habari na Zitto hata email hajibu!. Chadema ingekuwa haina watu matajiri kwenye chama na wenye wito chama kingeshakufa sikunyingi sana. Huwezi kupambana na CCM kwa sera pekee! Zitto.

Zitto ni lazima uelewe kwamba mafanikio ya Chadema ni ya wito na utajiri wa waanzilishi na viongozi na si uhodari wa kuongea pekee. Kuna watu watakudanganya uhame chama kwa kuweka udini na kukupa kichwa kwamba wewe una kipaji utafanikiwa popote lakini kuwa mwanasiasa hodari si sawa na kuwa kiongozi hodari!. Mboe ni muhimu kwa Chadema kuliko wewe. Je ni mfanya biashara gani mkubwa ni muha wa kigoma!!.

Ni lazima uwaheshimu watu waliokutoa kigoma mpaka hapo ulipo kwani hawa wanaokushauri uhame ndiyo wa kwanza watakao kuita Muha wa kigoma anayetangatanga na hutakuwa na watu wenye nia nzuri kwako bali kukutumia tu. Hivyo Zitto tulia na jenga imani na jifunze kutoka kwa kina ndesamburo, Slaa na Mboe jinsi ya kufanikiwa kimaisha bila siasa!.Muda wako utakuja hapo utakapojua ni kitu gani unataka kufanya, vilevile acha uongo!.

Zitto kwasasa hauko tajari kuwa mwenyekiti wa Chadema.

Hahahahaha mkuu kajipange umpya umetumwa na mbowe chadema wacheni udini na ukabila
 
Back
Top Bottom