This is the peak of hypocritical-deception.
People are scheming for mass sympathy. They are playing a game of ''give a baby some candy so as to collect the knife in his hand''.
Halafu hili la urais si alisema mwaka huu hatalizungumzia tena?
Kweli kasuku ni kasuku tu.
"Nitalipia ada wanafunzi wote waliofaulu kwenda kidato cha kwanza katika kata ya Kagera". Hili nalo alihitaji kujitangaza hadharani? Mbona hasemi hao wanafunzi wako wangapi?
Ada yenyewe sh. 20,000/-. tu.Mbona hata mimi nalipia wanafunzi 20 kila mwaka kule kijijini kwe
Halafu hayo mambo kama walishayamaliza ndani ya chama, kwa nini anayafufua tena?
Nimeamini huyu jamaa anapenda sifa za kijinga. Au ana lake jambo.
Naibu Katibu mkuu wa Chadema Zitto Kabwe aliyeweka kambi jimboni kwake amesema Ccm ianutumia kakikundi kadogo ndani ya chama kuwachonganisha.
Amesema pia kuwa anaweza asigombee nafasi yoyote ndani ya chama lakini atabaki kuwa mwanifu sana kwa chama chake.
Amesema ameweka kambi jimbo kuwadhibiti Ccm wasiwapotoshe wapiga kura wake.
Pia ameawataka viongozi wa chama jimboni mwake kutomtegemea yeye peke yake kujenga chama.
SOURCE: Tanzania Daima ingawa RFA walmelichakachua katika kulisoma.
Humjui ZITTO wewe?huyu dogo ameshanunuliwa muda mrefu sana,ni ndumila kuwili,kuna watu wanamtumia huyu.Yawezekana ikawa kweli...ila ZITTO ana matatizo binafsi ambayo CCM wana take advantage...japo siamini kama ni msaliti ndani ya chama........
This is the peak of hypocritical-deception.
People are scheming for mass sympathy. They are playing a game of ''give a baby some candy so as to collect the knife in his hand''.
Ben Saanane,
Ulikuja jukwaani ukamshutumu ZZK kuwa alikuwa kiongozi wa kundi la wasaliti wa CDM ambalo wewe mwenyewe ulikuwa mshiriki. Ukaliambia jukwaa la JF kuwa una ushahidi wa mambo yote uliyokuwa umeyasema juu shutuma ulizotoa.
Mwenyekiti wa BAVICHA katika taarifa yake kwa ya vyombo vya habari baada ya kikao kilicho fukuza "masalia" alise wewe Ben Saanane umesamehewa kwa sababu umekiri makosa na umeomba msamaha kwa kumchafua kiongozi mwandamizi wa CDM (hakutajwa jina ila kila anaefuatilia JF anamjua ni nani, walisoma post zako). Siku ya pili ukaja ukapinga hapa JF kwa kutaja jina kuwa hujawahi wala hutawahi kumuomba msamaha ZZK kwa sabab huna kosa lolote ulimfanyia ZZK, jambo linaloonesha kimisingia ni kweli ulikuwa na ushahidia wa kutosha katika shutuma zako kwa ZZK.
Yaliyojiri juzi yamejiri na wana JF wameyasikia, kila mmoja moyoni anajiuliza hivi hili suala la ZZK na ushahidi wa Ben Saanane ulipolekwa CDM limeishia vipi? Inawezeka kukawa na ushahidi wa uhakika(kiasi cha kupingana na mwenyekiti wako wa BAVICHA juu ya wewe kuomba msamaha) wa sauti na video wa ndugu ZZK akisaliti chama halafu CDM wakamuacha hivi hivi tu?
Hebu tufanunulie au nifafanulie hili jambo limekuaje ndugu Saanane!
Je, hivi ni kweli ulipeleka ushahidi wako wa uhakika ndani ya chama?
Je, CDM kimetupilia mbali au kudharau ushahidi wako?
Je, kuna mchakato wowote unaendelea ndani ya chama kuhusu shutuma zako hizi kubwa kubwa kwa ndugu ZZK?
Je, bado uko katika msimamo ule ule kuwa ZZK ni msaliti na alikuwa kiongozi wako katika usaliti?
Je, kwa nini usiuweke ushahidi hapa JF kama ulivyo weka shutuma hasa ukizingatia kuwa chama hakija chukua hata hatua ya kumjadili mtuhumiwa ZZK?
Je, wewe kama mwana CDM unaemini katika mabadiliko ya kweli unalionaje hili suala ya ndugu ZZK kubaki ndani ya CDM ilihali wewe una ushahidi usio na mashaka kuwa anakisaliti chama?
Ben,
Ulikuja hapa JF ukayaanzisha na ukatueleza haya mambo, hebu yamalize basi. La sivyo picha inageuka, tena inageuka sana. Wewe unakuwa ndio msaliti(tena usaliti wa aina mbaya kabisa) na ZZK anachukua ushujaa na pongezi zote wana JF walizokupa hapa jukwaani.
Zitto,
Ndugu naomba nikuulize swali. Kama yote aliyosema Ben Saanane juu yako si ya kweli na amekusingizia shutuma zote, na msingi wa kusamehewa kwake BAVICHA ni kuomba msamaha kwa makosa yake yote ikiwemo kukushutumu wewe, na ndugu Saanane amepinga hapa JF kuwa hajawahi kuomba wala hatawahi kukuomba msamaha juu ya suala la kukushutumu kuwa kiongozi wa masalia, mbona huyu kijana hajachukuliwa hatua yoyote na chama? mbona vijana wenzake walio toa shutuma dhidi ya viongozi wengine wamechukuliwa hatua na chama?
Hebu tufafanulieni hili jambo, mmoja kati yenu hatakiwi aendelee kuwepo CMD, ila nyote bado mpo CDM!! Kuna jambo haliko sawa hapo.
Huu ufa tuuzibe leo, kabla hujamuangukia mtu halafu ukatulazimu tujenge ukuta.
Mkuu naona kama alisingiziwa kwa kuwa kama hakusingiziwa na alikuwa kinara wa masalia kwa nini wasimjadili na kumfuta? Iweje wafuasi wafutwe wakati kinara na mfadhili wao bado anaendelea kuwepo chamani? Naona kama Zitto alikuwa anasingiziwa tu na hao akina Mr 8 O'clock kwani waliothibitishwa na Chama kuwa wasaliti wamepata haki yao.
Hii nadhani ungemtumia PM tu au ungemfuata kule facebook.Ni faraja kuwa umeona ukweli na kuwatambua wabaya wa CDM. Mpende adui, na ukimjua dui wako huwa hakusumbui. Ni vema umeuambia umma kuwa hakuna mgogoro CDM bali ni hali ya demokrasia, maana watu walikuwa wanakuelewa vibaya. Kweli umekomaa! Bravo!!!!!!!!!!!!!
Hii nadhani ungemtumia PM tu au ungemfuata kule facebook.
Unaharaka ya wapi ndugu?
Unadhani Chadema huwa kinakurupuka tu kufanya maamuzi ya siasa zake makini zenye mafaa kwa taifa?
CCM hawana jipya tena! Tumewakamata juu na chini!