Elections 2010 Zitto atoa siku saba kwa Waziri

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Monday, 27 December 2010
Anthony Kayanda, Kigoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), George Mkuchika, amepewa siku saba kuhakikisha anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Halmashauri ya Manispaa Kigoma-Ujiji aliouahirisha, licha ya Mahakama kuamua ufanyike siku uliopangwa rasmi.


Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alipokuwa akihutubia Wananchi wa Kigoma mjini kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na mustakabali wa kisiasa, ambapo alimshutumu Waziri huyo kwa kutumia Mamlaka yake vibaya.

‘Chadema tuna idadi kubwa ya madiwani zaidi ya CCM, hivyo juhudi zozote zinazofanywa na Waziri kusaidia Chama chake hazitasaidia kitu, badala yake zitaongeza hasira na chuki kwa Wakazi wa Kigoma mjini na kujikuta wakiichukia zaidi CCM na viongozi wake kwa vile anachangia kukwamisha maendeleo ya mji wetu’ alieleza Zitto.

‘Kutokana na hali hiyo, nampa Waziri wa Tamisemi siku saba ahakikishe anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ili tumpate Mwenyekiti wa baraza la madiwani na kamati zake za kudumu waanze kutuhudumia na kusimamia miradi ya maendeleo, kwa sababu kadri Waziri anavyochelewesha uchaguzi ndivyo Watendaji wanavyoweza kutumia vibaya nafasi hiyo kuharibu Halmashauri yetu” aliongeza.

Alisema baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, Chadema walishinda nafasi za madiwani katika Kata 10 dhidi ya tisa walizopata CCM, jambo lililofanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa nafasi nne za madiwani wa Viti Maalumu wakati CCM walipewa nafasi tatu za Madiwani wa Viti maalumu.

Zitto alisema chanzo cha mgogoro huo ni idadi hiyo ya madiwani wa Viti maalumu ambapo alidai kuwa CCM walikwenda Mahakama ya Wilaya Kigoma kulalamikia mgawo huo, lakini Mahakama ilitupilia mbali shauri hilo.

‘Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu” alifafanua Zitto.

‘Na hata kama Mahakama ingesema okay, CCM waongeongezewa diwani mmoja ili tulingane nao bado wasingekuwa na uwezo wa kushinda halmashauri, labda ile ndoa ya Mseto tuliyofunga nao mwaka 2005 inaonekana wameridhika nayo ndiyo maana wanataka turudiane nao, sisi tunasema kwa hilo hatupo tayari na kamwe mwaka huu hatuipotezi Manispaa ya Kigoma Ujiji’ alisisitiza.
 
Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu" alifafanua Zito.

Hivi Mkuchika anaishi dunia ipi ambayo inapingana na nguvu ya raia waliomweka yeye hapo alipo?
 
These manouvres are a recipe for unnecessary chaos. We should be more sensible and let the will of the people prevail lest we plunge this contrary into chaos or violence.
 
Zitto, hapo imekaa sawa maana ni suala la kudaihaki ya wananchi / Umma wa Tanzania kupata uwakilishi wao stahiki.

Kwa nafasi yako hiyo hiyo ya Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, sogeza mkono wako kidogo ukajumuishe na halmashauri zile nyinginezo tata nchini tupate matokeo mapema.

Nasikitika kwamba mwaka huu nilikua nalazimika kutofautiana na wewe katika maswala mengi sana sana, ila bila chuki. Na hata kesho mienendo isipokua ni ya kupigania umma na kujenga teamwork katika chama nako bado utarajie kwamba mimi na wewe bado tutakwaruzana tu licha ya urafiki wetu wa siku nyingi.

Hata hivyo, mwakani jitahidi sana ku-Reclaim the Ziitto that we had always known to be standing out steadfast in you full stop.

Vile vile anza kuiwekea mikakati murua ule mswada wa Mhe Mnyika kuhusu KATIBA MPYA kule bungeni Dodoma.
 
Zitto, hapo imekaa sawa maana ni suala la kudaihaki ya wananchi / Umma wa Tanzania kupata uwakilishi wao stahiki.

Kwa nafasi yako hiyo hiyo ya Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, sogeza mkono wako kidogo ukajumuishe na halmashauri zile nyinginezo tata nchini tupate matokeo mapema.

Nasikitika kwamba mwaka huu nilikua nalazimika kutofautiana na wewe katika maswala mengi sana sana, ila bila chuki. Na hata kesho mienendo isipokua ni ya kupigania umma na kujenga teamwork katika chama nako bado utarajie kwamba mimi na wewe bado tutakwaruzana tu licha ya urafiki wetu wa siku nyingi.

Hata hivyo, mwakani jitahidi sana ku-Reclaim the Ziitto that we had always known to be standing out steadfast in you full stop.

Vile vile anza kuiwekea mikakati murua ule mswada wa Mhe Mnyika kuhusu KATIBA MPYA kule bungeni Dodoma.
Hapo umeongea sasa ...achana na migogoro ya chama badilika na anza kujenga chama upya usisikilize waandishi wa habari sana watakupoteza
 
These manouvres are a recipe for unnecessary chaos. We should be more sensible and let the will of the people prevail lest we plunge this contrary into chaos or violence.
yeye ametumwa tu, ni kama andengenye na chitanda arusha, kila sehemu wapo.... wanatekeleza amri ya mkuu wao na wao kama wanajeshi nadhani unaelewa huwa wanatekeleza then kuhoji badae
 
Zitto Amerudi Sehemu Yake au ni Vipi?

Zitto unaona aina ya maswali ambayo vijana wenzako huwa tunajiuliza huku vijiweni. Mimi binafsi sihitaji ukaninunulie hata chupa ya fanta lakini uwe tu mtu wa kuaminika mbele ya jamii yako basi!!!!
 
mbona wabunge wengine wana zuiwa kuongea na wananchi lakini zito kila mara anaruhusiwa bila tatizo?
 
Huyu huyu Mkuchika ndie aliyekuwa waziri wa habari na michezo serikali ilopita. Huyu jamaa ni mtata saana, siku zote yupo katika kulinda maslahi ya CCM. Kumbuka aliwahi kususiwa na waandishi wa habari hasa baada ya kuzua bifu nao, na waandishi wakaamua kumweka kolokoloni (kwa kutandika habari zake ) Sijui kama adhabu ile iliisha, mimi naamini huyu jamaa BADO anastahiri ile adhabu
 
Hongera sana Zitto kawa sasa unanifurahisha sana,ni lazima uwe mwanasiasa mwenye msimamo.Naona CCM wanataka vurugu zisizokuwa za lazima!!!
 
viongozi wetu hawa (product ya CCM) kama alivyowahi kunukuliwa chenge kipindi cha Uspika.. inatakiwa kulinda maslahi ya chama na siyo ya wananchi..na ndio maana si shangai kuona mkuchikaakisindwa kutatua ssuala la Umeya kigoma...na kingine selikeli ilishaona ya kuwa raia wake hawana akilindio maana inafanya maamuzi tata..tukisema tz ni nchi ya kiimla nani atapinga? ... ni kigezo gani kilichotumika kuwapa madiwani wa3 ccm wa viti maalum kati ya nafasi hizo nne..yote kwa yote hali hii itaisha, tunachotaka ni katiba mpya
 
Zitto atoa siku saba kwa Waziri Monday, 27 December 2010 19:59

Anthony Kayanda, Kigoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), George Mkuchika, amepewa siku saba kuhakikisha anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Halmashauri ya Manispaa Kigoma-Ujiji aliouahirisha, licha ya Mahakama kuamua ufanyike siku uliopangwa rasmi.
Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema,Zitto Kabwe alipokuwa akihutubia Wananchi wa Kigoma mjini kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na mustakabali wa kisiasa, ambapo alimshutumu Waziri huyo kwa kutumia Mamlaka yake vibaya.

‘Chadema tuna idadi kubwa ya madiwani zaidi ya CCM, hivyo juhudi zozote zinazofanywa na Waziri kusaidia Chama chake hazitasaidia kitu, badala yake zitaongeza hasira na chuki kwa Wakazi wa Kigoma mjini na kujikuta wakiichukia zaidi CCM na viongozi wake kwa vile anachangia kukwamisha maendeleo ya mji wetu’ alieleza Zitto.

‘Kutokana na hali hiyo, nampa Waziri wa Tamisemi siku saba ahakikishe anaitisha uchaguzi wa kumchagua Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ili tumpate Mwenyekiti wa baraza la madiwani na kamati zake za kudumu waanze kutuhudumia na kusimamia miradi ya maendeleo, kwa sababu kadri Waziri anavyochelewesha uchaguzi ndivyo Watendaji wanavyoweza kutumia vibaya nafasi hiyo kuharibu Halmashauri yetu” aliongeza.


Alisema baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, Chadema walishinda nafasi za madiwani katika Kata 10 dhidi ya tisa walizopata CCM, jambo lililofanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa nafasi nne za madiwani wa Viti Maalumu wakati CCM walipewa nafasi tatu za Madiwani wa Viti maalumu.


Zitto alisema chanzo cha mgogoro huo ni idadi hiyo ya madiwani wa Viti maalumu ambapo alidai kuwa CCM walikwenda Mahakama ya Wilaya Kigoma kulalamikia mgawo huo, lakini Mahakama ilitupilia mbali shauri hilo.

‘Waziri Mkuchika anapaswa kujua kwamba siku ile alipoandika barua ya kusimamisha uchaguzi wa Meya (Desemba 17, 2010), Mahakama ya Wilaya Kigoma ilikuwa imetoa maamuzi ya shauri la CCM waliotaka Mahakama isimamishe uchaguzi, lakini Hakimu alilitupilia mbali shauri hilo kwa maelezo kwamba Tume ya Uchaguzi ipo sahihi katika mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu” alifafanua Zito.

‘Na hata kama Mahakama ingesema okay, CCM waongeongezewa diwani mmoja ili tulingane nao bado wasingekuwa na uwezo wa kushinda halmashauri, labda ile ndoa ya Mseto tuliyofunga nao mwaka 2005 inaonekana wameridhika nayo ndiyo maana wanataka turudiane nao, sisi tunasema kwa hilo hatupo tayari na kamwe mwaka huu hatuipotezi Manispaa ya Kigoma Ujiji’ alisisitiza.

Crap!!
Asipoitisha atafanya nini? asitishie watu nyau!!!
 
lakini nawewe mkuchikaaaaaaa soma alama za nyakati waziri,huu wakati tulionao ni tofauti sana na enzi zenu,watu wamebadilika na wana hasila kweli,wape haki yao,kwa hilo hatuko nawe juu ya hilo kwani tunahitaji maendeleo na wala sio longolongo


mapinduziiiii daimaaaaaaa
 
Mkuchika unataka KUKUCHIKA kila kitu eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee katika siasa?
 
Back
Top Bottom