Zitto ataka wabunge wa zamani waombe radhi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
• Zitto ataka wabunge wa zamani waombe radhi

Na Said Mwishehe, Mwanza
Majira

NAIBU Katibu Mkuu wa CHADEMA, Bw. Zitto Kabwe, amewataka wabunge wa mwaka 1995 hadi 2000 kuwaomba radhi Watanzania, kwa madai kuwawalipitisha sheria mbovu ya madini na kulisababisha Taifa hasara ya dola milioni 883 za Marekani ambazo ni sawa na sh. trilioni moja za Tanzania kwa sasa.

Bw. Zitto alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wananchi wa mkoa wa Mwanza eneo la Ilemela, ikiwa ni sehemu ya mfululizo wa ziara ya Operesheni Sangara inayoendeshwa na chama hicho ambayo imeandaliwa kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Alidai kuwa wabunge waliokuwa bungeni katika kipindi hicho, ndio wanaopaswa kulaumiwa kwa kupitisha muswada wa sheria ya madini, ambayo inatoa mwanya kwa kampuni za madini nchini, kukwepa kulipa kodi kwa visingizio mbalimbali na kulikosesha Taifa mabilioni ya fedha Kwa kipindi kirefu sasa na bila sababu za msingi.

Aliwaambia wananchi waliokuwa kwenye mkutano huo, kuwa mwaka 1997, Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Sheria mbalimbali za Fedha, ambayo ndiyo iliyoweka msingi wa sheria za kodi za madini bila kujali maslahi ya nchi na matokeo yake kutokea kwa hasara kubwa.

Bw. Zitto alisema katika sheria hiyo, kuna kipengele cha asilimia 15
kinachosema kuwa baada ya kampuni ya uchimbaji madini kutoa gharama zake za uzalishaji, inaruhusiwa kuongeza asilimia nyingine 15 ya gharama hizo.

Alisisitiza kuwa kutokana na sheria hiyo, tangu mwaka 1997 hadi mwaka jana, kipindi cha miaka 10, Serikali imeingia hasara ya dola milioni 883.

"Endapo fedha hizo zingekusanya zingesaidia mambo mbalimbali ya
maendeleo" alisisitiza Bw. Zitto na kuongeza: "Wabunge ndio wanapaswa kulaumiwa, lakini pia wawaombe radhi Watanzania kwa kusababisha hasara na kuzipa faida kampuni za madini," alisema.

Kutokana na hali hiyo, aliyewahi kuwa mbunge wa Kisesa kuanzia mwaka 1995 hadi 2000 kupitia UDP, Bw. Erasto Tumbo, ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA aliwaomba radhi Watanzania hadharani kwa kuwa miongoni mwa wabunge waliopitisha sheria hiyo.
 
Hata wakiomba radhi itasaidia nini? Muhimu ni bunge la sasa kurekebisha hayo mapungufu mliyoyaona.
 
Hata wakiomba radhi itasaidia nini? Muhimu ni bunge la sasa kurekebisha hayo mapungufu mliyoyaona.

Kuomba radhi ni kukiri kosa. Hivyo kujiweka wazi na kuwa tayari kuadhibiwa na kurekebesha makosa yako. Ki ujumla ni tabia nzuri, haswa kwa watu waliostaarabika.
 
Wakina Malecela, Makwetta, Mungai, Majiyatanga Mzindakaya, Makinda,Anna Abdalla, Kimiti etc; watawaomba msamaha wananchi mara ngapi kwa madudu waliopitisha muda wote huu waliokaa bungeni?? Pitisheni sheria kuwa minimum qualification ya kuwa mbunge iwe shahada ya kwanza from a recognized university; hapo ndipo hamtapata vihiyo bungeni wanaopitisha sheria bila kujua athari zake kwa nchi!! Kuomba radhi hakutoshi wananchi wamekwisha umia.
 
Wakina Malecela, Makwetta, Mungai, Majiyatanga Mzindakaya, Makinda,Anna Abdalla, Kimiti etc; watawaomba msamaha wananchi mara ngapi kwa madudu waliopitisha muda wote huu waliokaa bungeni?? Pitisheni sheria kuwa minimum qualification ya kuwa mbunge iwe shahada ya kwanza from a recognized university; hapo ndipo hamtapata vihiyo bungeni wanaopitisha sheria bila kujua athari zake kwa nchi!! Kuomba radhi hakutoshi wananchi wamekwisha umia.

Sidhani kama utashi wa mtu unatokana na usomi wa kuwa na shahada au stashahada. Mifano ni mingi tu ya mawaziri na wabunge wenye hizo shahada, lakini bado uwezo wao wa kuchanganua mambo ni finyu au umekaa kimaslahi yao binafsi. Nafikiri Prof Maghembe, Prof Kapuya na wengine wengi ni mifano mizuri tu ya wasomi waliobobea lakini wasio na utashi wa kufanya mambo kwa maslahi ya taifa. Migomo ya hivi karibuni ya walimu na wanafunzi ni mfano mzuri wa kujua viongozi wa wizara husika wana usomi kiasi gani na wanatumia vipi usomi wao kutatua matatizo.

Hoja ya msingi hapa ni kutokurudiwa makosa yaliyokwishafanyika. Kama kuna upungufu kwenye sheria za madini na sheria za kodi ambazo zinayapa makampuni ya madini unafuu kwenye kodi, basi bunge la sasa lirekebishe makosa hayo. Kuwaomba wananchi msamaha hakurudishi chochote wala kupunguza makali ya maisha. Ili msamaha uwe na maana, basi sheria husika zifanyiwe marekebisho mara moja.
 
Bunge la sasa kwa hesabbu isiyo rasmi ni zaidi ya 60% ya bunge la 1995 - 2000 hivyo kwa niaba ya wasio kuwepo Mzee Six aombe radhi Lo!
 
This is what I have to say on this issue:

1. Kuomba msamaha ni hatua ya kwanza ya bunge kujisafisha.
2. Qualification za wabunge ziwe za juu zaidi kielimu na kiutendaji, sio kuchagua watu wenye majina au waliofanya madudu hapo nyuma.
3. Mikataba yote ya NCHI IANDALIWE kupitia KAMATI ZA BUNGE na sio kupitia USIRI WA ADAM MALIMA na MAFISADI wenzake.

Kumbuka wabunge wanawawakilisha wananchi na wanajukumu la kuhakiki RASILIMALI YA NCHI inatumika kama ilivyokusudiwa.
 
Hatuna utamaduni wa 'samahani', 'pole' wala 'asante'. Kiongozi aliyewahi kukubali makosa ni baba wa Taifa aliposema huko nyuma tumefanya makosa, na binadamu sio malaika ila pia akatoa presedence ya 'Kufanya kosa si kosa, kosa kurudia kosa'.

Sheria ya madini ni mja tuu ya sheria za ajab zilizopitishwa na bunge letu. Naomba tuwasamehe maana enzi hizo muswada unaukuta siku ile ile unapoletwa. Kulikuwa hakuna
Cha-kusomwa kwa mara ya kwanza, maara ya pili na mara ya tatu. Wabunge walikuwa wausikia mara ya mwisho na ndio unagawiwa kwao siku unaposomwa, unategemea nini.

Mhe. Zito, yaliyopta si ndwele, kazi ni moja tuu, kusonga mbele, safari mbona bado ni ndefu kwa jicho hilo hilo uliloonea sheria ya madini, chungulia sheria ya TIC na vivutio kwa wanaitwa wawekezaji! Chungulia sheria ya EPZ, etc, tutabadili sheria ngapi?. Kwa taarifa tuu mpaka hii leo, ukipata mtoto nje ya ndoa, ama ukiachana na mkeo yeye akabaki na watoto, wewe baba unawajibika kutoa matunzo ya shilingi mia (100) kwa kila mtoto kwa mwezi!. Hizo gharama za matunzo kwa mujibu wa Sheria ya ndoa ya Mwaka 1971 na mpaka leo haijabadilishwa, hii ya madini ni ya juzi tuu. 1998.
 
1.
Wakina Malecela, Makwetta, Mungai, Majiyatanga Mzindakaya, Makinda,Anna Abdalla, Kimiti etc; watawaomba msamaha wananchi mara ngapi kwa madudu waliopitisha muda wote huu waliokaa bungeni??

- Kama una tatizo na hawa viongozi na waliyoyafanya huko nyuma, basi una tatizo na Mwalimu, aliyewafikisha kwenye uongozi, are you sure you want that?

2.
Pitisheni sheria kuwa minimum qualification ya kuwa mbunge iwe shahada ya kwanza from a recognized university; hapo ndipo hamtapata vihiyo bungeni wanaopitisha sheria bila kujua athari zake kwa nchi!! Kuomba radhi hakutoshi wananchi wamekwisha umia.

- Kwa kweli hoja zingine bwana, hivi Chenge na Mkapa wamesoma wapi?

- Kuhusu hoja ya Zitto, kama inasimama basi hizo radhi zinahitajika kuombwa frorm way back before 1995 to 2000, na ili hizo radhi zitusaidie nini wananchi, tunachotaka ni sheria kuchukua mkondo wake, kwenye kupitisha hiyo mikataba kuna viongozi waliofanya uhuni kisheria, sasa ungetegemea Zitto, azungumzie hizo lines ingawa ninaheshimu sana kazi yake kwa taifa, I am sorry not kwenye this ya kuombana radhi, exactly maana yake ni nini?

- Badala ya kudai sheria tuanze kudai kuombana radhi, Zitto are you kidding me!
 
Wakina Malecela, Makwetta, Mungai, Majiyatanga Mzindakaya, Makinda,Anna Abdalla, Kimiti etc; watawaomba msamaha wananchi mara ngapi kwa madudu waliopitisha muda wote huu waliokaa bungeni?? Pitisheni sheria kuwa minimum qualification ya kuwa mbunge iwe shahada ya kwanza from a recognized university; hapo ndipo hamtapata vihiyo bungeni wanaopitisha sheria bila kujua athari zake kwa nchi!! Kuomba radhi hakutoshi wananchi wamekwisha umia.

Hao kwani si wameamka hivi punde baada ya waheshimiwa Slaa na Kabwe kuwaonyesha trela ya picha yenye tttle "ufisadi" otherwise walikuwa kwenye session wanalala tu eee Mungu. Ushahidi ni baada ya TVs kuja eee Mola sikui kabla ya kuwepo TVs hali ya kusinzia ilikuwaje? Nagfikiri spika tu na mwenye la kuongea ndo alikuwa macho. I can not imagine. Wakishtuka ni kugonga meza tu na ikiwa kura inahitajika basi hata watu wawili wakisema NDIOOOOO kwa nguvu na spika akasikia kisha wanaosema hapana ikawa kimya tehn PASSED. Huo ndio ulikuwa mchezo; kwanza hata ukiongea sana ilikuwa unakaripiwa na hawakuwa na hata muda wa kupitia kanuni za bunge hivyo hata pale anapokaripiwa na spika hasomi vifungu vinavyomlinda, then hakuna kukuna vichwa, allowance then the lagers na totoz hata Mama Terry alishuhudia, anyway. But now Slaa na Kabwe kimbiza bovu!

It is very funny ukiangalia status ya siasa hivi sasa kwanza ufisadi waliukana kimanga na baada ya Slaa na Kabwe kukimbiza mbaya wakakubali. Ilikuwa enzi hizo ni thibitisha au futa kauli na kwao hili lilionekana kama capital mistake! For walikuwa si wajuzi bali maslahi yao tu mbele kwa saaaana.

Sasa ni kimbiza bovu watu wanatafuta data na wana data na wanajua wapi pa kuzisema na kivipi. Usingizi umewaisha. Kila mtu ukimtafuta kosa duniani hutakosa kosa mfano mzuri ni case za traffic barabarani, hata kama gari ni mpya kosa lipo tu, anaweza akakubast kwanini hujaosha kioo, hii inaweza kusababisha ajali kwa kuwa huoni vyema mbele. Hata kama ndo ulikuwa unaelekea kukiosha lakini kosa kimsingi liko pale pale. So that is the way but makosa ya hawa jamaa its alarming!
 
Kuomba radhi ni kukiri kosa. Hivyo kujiweka wazi na kuwa tayari kuadhibiwa na kurekebesha makosa yako. Ki ujumla ni tabia nzuri, haswa kwa watu waliostaarabika.

Tangu lini SISIEMU ikakiri kosa. Yenyewe huwa inajiaona always right. Na hata kama kosa limetendeka SISIEMU haiwezi kuomba radhi. Nafikiri ni wakati mzuri SISIEMU ikaanza kuwa na ustaarabu wa kuomba radhi.
 
Something wrong with Kabwe's comments. Didn't bunge request that mikataba yoye sasa iwe inapitia bungeni kwanza ili ijadiliwe? Sasa wabunge wa wakati ule iweje waombe msamaha for shit they didn't do?

Mikataba mibovu ya madini ya wakati ule ilifanywa behind closed doors. Do you know who was supposed to act as mshauri mkuu wa serikali in all matters madini? Mr Vijisenti himself! He sat there while Tanzania got shafted with the puny 3% taxation on royalty instead of paying taxes on profits - Moelex hebu naomba ubreak it down, man!!

Wabunge don't have to apologize shit as these deals were not tabled through them at that time. Zitto Kabwe should get his facts correct before he lays any accusations.

My two cents.......
 
watayarishaji wa hiyo miswada walikuwa wanaelewa wanacho fanya sema kuna wabunge wengine walipitisha chitalilo stlye, bila kujua wanawapitishia wenzao kula. na wengine walifuata msimamo wa chama bila kuelewa wanajitafunya wenyewe.
 
Hatuna utamaduni wa 'samahani', 'pole' wala 'asante'. Kiongozi aliyewahi kukubali makosa ni baba wa Taifa aliposema huko nyuma tumefanya makosa, na binadamu sio malaika ila pia akatoa presedence ya 'Kufanya kosa si kosa, kosa kurudia kosa'.

Sheria ya madini ni mja tuu ya sheria za ajab zilizopitishwa na bunge letu. Naomba tuwasamehe maana enzi hizo muswada unaukuta siku ile ile unapoletwa. Kulikuwa hakuna
Cha-kusomwa kwa mara ya kwanza, maara ya pili na mara ya tatu. Wabunge walikuwa wausikia mara ya mwisho na ndio unagawiwa kwao siku unaposomwa, unategemea nini.

Mhe. Zito, yaliyopta si ndwele, kazi ni moja tuu, kusonga mbele, safari mbona bado ni ndefu kwa jicho hilo hilo uliloonea sheria ya madini, chungulia sheria ya TIC na vivutio kwa wanaitwa wawekezaji! Chungulia sheria ya EPZ, etc, tutabadili sheria ngapi?. Kwa taarifa tuu mpaka hii leo, ukipata mtoto nje ya ndoa, ama ukiachana na mkeo yeye akabaki na watoto, wewe baba unawajibika kutoa matunzo ya shilingi mia (100) kwa kila mtoto kwa mwezi!. Hizo gharama za matunzo kwa mujibu wa Sheria ya ndoa ya Mwaka 1971 na mpaka leo haijabadilishwa, hii ya madini ni ya juzi tuu. 1998.

Kama hali ndiyo ilikuwa kama unavyosema, kwamba mswada unaletwa siku hiyo hiyo na kupitishwa na wabunge hata bila kuusoma, mimi naitafsiri hiyo kama dalili ya uzembe na ulimbukeni uliotukuka.

Tabia ya kufanya mambo kwa mazoea, na bila kushirikisha akili angalu kidogo, si ya wabunge wetu tu. Wengi wetu tuna kasoro hii. Tunaweza kuwa tunawanyooshea vidole hao jamaa, lakini tukitembelewa "maofisini" kwetu tutakutwa na sisi ni mule mule. Ila kwa sababu matendo yetu hayaliingizii taifa zima hasara kubwa, tunachukulia kawaida tu.

Kwani wangapi wetu tuna-sign mikataba ya kazi halafu baadaye kabisa ndio unalalamika mwajiri wako anakubana na mkataba mbovu ambao ume-sign mwenyewe? Je, wangapi hapa wakiwa katika hali mbaya na kutafuta kazi, wako tayari kumwambia HR huu mkataba haujakaa sawa? Na wangapi kati yao wako tayari kumwambi HR "thanks but no thanks" na kuiachia hiyo kazi kwa sababu kuna vipengele ambavyo hajaridhika navyo, hata kama amepigika? Kwanza wangapi hata huwa wanasoma mikataba yao ya kazi kabla ya kui-sign?

Sasa kama mmoja wetu wa aina hii amekuwa mbunge, unategemea abadilike vipi kwa kuwa mbunge tu? Je, kama kutetea maslahi yake inamuiya vigumu, vipi kutetea maslahi ya wengine ambao hata awajui? Tena akiambiwa anatengenezewa kibanda cha matofali chenye juu na chini si ndio kabisa?

Pengine hawa jamaa kuomba radhi utakuwa mwanzo mzuri wa kushtuana kwamba tupende kushirikisha akili na kujaribu kuelewa unachoamua kukifanya au kutokukifanya.

Lakini kwa mtu wa haina hiyo, sina hamu ya hata kusikia ombi lake la radhi; maana kuna uwezekano mkubwa hata aoni ni wapi amefanya kosa; ataomba radhi kwa sababu ametakiwa kufanya hivyo. Upeo wao mara nyingi unakuwa mdogo sana.

Ila kama hata baadhi yao wanaweza kuwajibishwa kwa uzembe, na kushiriki katika kuhujumu uchumi na kulipoteze mapato taifa, nadhani utakuwa mwanzo mzuri zaidi. Na hii ni muhimu mno kwa wale ambao walikuwa wanajua makusudi yaliyokuwa yanafanyika, na wale ambao walifaidika kwa njia moja ama nyingine na kupitishwa kwa sheria hizo.

Kwa upande mwingine, hivi kwa mama aliyepata mtoto nje ya ndoa inakuwaje? Halafu ukiachana na mkeo wewe ukabaki na watoto mama anatoa hiyo hiyo mia (100) kwa mwezi pia? :) Pengine hili linatakiwa lipate thread yake, lakini ni mfano mzuri wa jinsi ambavyo ni rahisi kujisahau na kufanya maamuzi kwa mazoea.
 
Kwani kuna uhakika gani kuwa sheria zinazopitishwa sasa hivi hazina kasoro?

Sadakta.

Nakumbuka mwaka 2002/2003 (nadhani) katibu mkuu wa wizara ya nishati aliletwa mlimani kuiwakilisha serikali katika mjadala uliohusu Tanesco na IPTL disgrace. Aliulizwa maswali mengi tu kama kawa aliitetea sana serikali. Na ( Zitto being katibu wa daruso wakati ule, anaweza kukumbuka alikuwepo. :) )

Nakumbuka sentensi moja ambayo aliisema kwa msisitizo ni kwamba serikali imetengeneza uataratibu mzuri wa kuhakikisha swala kama hilo halitokei.

Nilinyoosha mno mkono wangu kumuuliza swali, lakini sikupata nafasi, na nikaondoka nalo kichwani. Nilikuwa nataka kumuuliza kama anaweza akatuhakikishia kwamba hatorudi tena pale mlimani baada ya miaka kadhaa ku-defend kitu kama hicho na kusema tena, kwa mara nyingine kwamba serikali imeweka mipango mizuri ya kuhakikisha jambo kama hilo haliwezi tokea?

Kama ningefanikiwa kumuuliza ningepata sababu nzuri ya kumtembelea leo nyumbani kwake kwa kikombe cha chai angalau na kumkumbusha jibu lake.

Umeuliza swali zuri sana Mpita Njia.

Mzee wangu mmoja aliniambiaga kwamba kuona mbele sio kazi. Hata mbuzi anaona mbele. Kuona mbali ni shughuli kidogo.
 
1. Cha msingi Bunge letu liwe la Standards and Speed kama anavyodai mkuu mwenyewe Sitta.Hapo mambo yasiyo na msingi hayawezi kupitishwa kwa vigezo vya uchama na umtandao!Isipokuiwa hivi itakuwa kila siku tunawataka waombe msamaha!

2.Kama tunavyodai Tanzania inafuata utawa wa sheria basi sheria ifuate mkondo wake.Anaekosa awajibishwe kisheria.Sijaona kwenye katiba yetu ( kama ipo naweza kusahihishwa) inayosema kiongozi akikosa aombe msamaha.Huu ni utaratibu uliotumika kwenye Gentile Constitution in Greece society.

3. Mawazo yakipuuzi kama vile viongozi wakiwajibishwa wataipasua nchi yafutiliwe mbali.
Nadhani wanaoharibu amani ya nchi ni wale wanaozuia sheria kufuata mkondo wake kwa vigezo vya umatndao na chama kupasuka! Bunge na watawala wawe Imara.Wasemapo YES waaanishe hivyo na si kusema YES wakimaanisa NO
 
1. Cha msingi Bunge letu liwe la Standards and Speed kama anavyodai mkuu mwenyewe Sitta.Hapo mambo yasiyo na msingi hayawezi kupitishwa kwa vigezo vya uchama na umtandao!Isipokuiwa hivi itakuwa kila siku tunawataka waombe msamaha!

2.Kama tunavyodai Tanzania inafuata utawa wa sheria basi sheria ifuate mkondo wake.Anaekosa awajibishwe kisheria.Sijaona kwenye katiba yetu ( kama ipo naweza kusahihishwa) inayosema kiongozi akikosa aombe msamaha.Huu ni utaratibu uliotumika kwenye Gentile Constitution in Greece society.

3. Mawazo yakipuuzi kama vile viongozi wakiwajibishwa wataipasua nchi yafutiliwe mbali.
Nadhani wanaoharibu amani ya nchi ni wale wanaozuia sheria kufuata mkondo wake kwa vigezo vya umatndao na chama kupasuka! Bunge na watawala wawe Imara.Wasemapo YES waaanishe hivyo na si kusema YES wakimaanisa NO

Umeieka vizuri sana mkuu :)
 
Operesheni Sangara Chadema yageuka homa kali kwa CCM

*Makamba aagiza makada wa CCM kujibu mapigo

Na Mussa Juma, Longido


OPERESHENI Sangara inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inaonekana kukipa homa kali chama tawala, CCM ambacho sasa kimeamua kuweka mkakati wa kujibu tuhuma zinazotolewa kwenye operesheni hiyo.

Chadema ilianzisha kampeni hiyo katika maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kutangazwa kwa orodha ya mafisadi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mwembeyanga Temeke. Katika mikutano ya operesheni hiyo, Chadema imekuwa ikitoa tuhuma nyingi dhidi ya CCM na viongozi wake.

Tuhuma hizo zimemfanya katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kuamua kuwataka watendaji wake kutokaa kimya na badala yake kujibu tuhuma hizo zinazotolewa na viongozi wa Chadema.

"Napenda kutoa wito kwa viongozi, acheni kukaa maofisini, nendeni kwa wananchi bila woga. Waelezeni mafanikio ya serikali ya awamu ya nne na kujibu hoja za wapinzani," alisema Makamba.

"Viongozi wa Chadema wamekuwa wakizunguka mikoa mbalimbali nchini na kuisema vibaya CCM na serikali yake hivyo, kama wana CCM mtakaa kimya, wananchi wataamini yote yanayosemwa na Chadema."

Makamba, aliyekuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM kwenye vijiji vya Kimokouwa na Engarenaibo wilayani Longido, aliwataka wana-CCM kutoihofia Operesheni Sangara kwa sababu CCM ndio ina dhamana na serikali.


Katika ziara hiyo katibu mkuu huyo wa CCM alitumia muda mwingi kuzungumzia Operation Sangara na akakanusha kauli ya naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kuwa magari yote aina ya Mahindra, yanayotumiwa na makatibu wa wilaya na mikoa wa CCM, hayana kadi na kudai kuwa kadi hizo anazo mfanyabiashara anayetuhumiwa kuiba fedha kwenye Akaunti ya Malimbikizo ya Madeni ya Nje (EPA), Jeetu Patel.

"Huu ni uongo. Yale magari ni mali ya CCM na tulinunua kwa Sh1.6 bilioni, sasa nashangaa kusikia%2
 
Back
Top Bottom