Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,900
- 21,988
Zitto msifu Ngeleja amshauri ahame CCM
Na Said Mwishehe
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Bw. Kabwe Zitto 'amemfagilia' Waziri wa Nishati na Madini, Bw. William Ngeleja, na kusema anafurahishwa na uchapakazi wake ambapo amewapongeza wananchi wa Sengerma kwa kuchagua kuwa mbunge wao.
Akizungumza na wananachi juzi katika mkutano wa hadhara 'Operesheni sangara' uliofanyika katika Wilaya ya Sengerema ikiwa ni sehemu ya mikutano Kanda ya Ziwa, Bw Kabwe alisema wananchi walifanya uamuzi mzuri kumchagua Bw. Ngeleja ambaye amekuwa akifanya vizuri katika shughuli zake za uongozi.
Bw. Kabwe alisema tangu Bw. Ngeleja alipoteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini, amefanya kazi zake vizuri na kwa umakini mkubwa jambo ambalo linaleta matumaini makubwa kwa kuwa na viongozi wa aina hiyo.
Ndugu zangu wa Sengerema naomba niwashukuru kwa kumchagua Ngeleja kuwa mbunge wenu, yuko makini na anajua anachokifanya katika shughuli zake na tunaweza kusema ni moja kati ya viongozi makini wa CCM. Unapoona kiongozi anafanya vizuri lazima usifie ndiyo maana nimeona ni vema nikaawaeleza, alisema Bw. Kabwe.
Alisema amepunguza baadhi ya matatizo ambayo yalikuwa yakitokea katika wizara hiyo kwa mawaziri waliopita ya kuingiza nchi katika mikata mibovu lakini yeye amekuwa makini na kuhakikisha serikali haingii katika matatizo kama ya Richmond.
Bw. Zitto alisema kitu ambacho kinaweza kumkwamisha Bw. Ngeleja kufanya kazi zake vizuri, ni chama alichokuwepo ambacho kitamfanya asiweze kuendelea na kuchapa kazi kama ilivyokuwa sasa na kumshauri aondoke huko na kutafuta chama ambacho kitamfanya aendelee kuwajibika vizuri.
Ngeleja ni mchapa kazi mzuri lakini kwa kuwepo kwake CCM kutamharibia na kumuweka katika wakati mgumu hivyo anapaswa kuondoka na kwenda chama ambacho kitamfanya aendelee, kiongozi kijana anawajibu wa kupima chama gani akienda ataweza kuendelea na majukumu ya kuwatumikia wananchi, alisema.
Na Said Mwishehe
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Bw. Kabwe Zitto 'amemfagilia' Waziri wa Nishati na Madini, Bw. William Ngeleja, na kusema anafurahishwa na uchapakazi wake ambapo amewapongeza wananchi wa Sengerma kwa kuchagua kuwa mbunge wao.
Akizungumza na wananachi juzi katika mkutano wa hadhara 'Operesheni sangara' uliofanyika katika Wilaya ya Sengerema ikiwa ni sehemu ya mikutano Kanda ya Ziwa, Bw Kabwe alisema wananchi walifanya uamuzi mzuri kumchagua Bw. Ngeleja ambaye amekuwa akifanya vizuri katika shughuli zake za uongozi.
Bw. Kabwe alisema tangu Bw. Ngeleja alipoteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini, amefanya kazi zake vizuri na kwa umakini mkubwa jambo ambalo linaleta matumaini makubwa kwa kuwa na viongozi wa aina hiyo.
Ndugu zangu wa Sengerema naomba niwashukuru kwa kumchagua Ngeleja kuwa mbunge wenu, yuko makini na anajua anachokifanya katika shughuli zake na tunaweza kusema ni moja kati ya viongozi makini wa CCM. Unapoona kiongozi anafanya vizuri lazima usifie ndiyo maana nimeona ni vema nikaawaeleza, alisema Bw. Kabwe.
Alisema amepunguza baadhi ya matatizo ambayo yalikuwa yakitokea katika wizara hiyo kwa mawaziri waliopita ya kuingiza nchi katika mikata mibovu lakini yeye amekuwa makini na kuhakikisha serikali haingii katika matatizo kama ya Richmond.
Bw. Zitto alisema kitu ambacho kinaweza kumkwamisha Bw. Ngeleja kufanya kazi zake vizuri, ni chama alichokuwepo ambacho kitamfanya asiweze kuendelea na kuchapa kazi kama ilivyokuwa sasa na kumshauri aondoke huko na kutafuta chama ambacho kitamfanya aendelee kuwajibika vizuri.
Ngeleja ni mchapa kazi mzuri lakini kwa kuwepo kwake CCM kutamharibia na kumuweka katika wakati mgumu hivyo anapaswa kuondoka na kwenda chama ambacho kitamfanya aendelee, kiongozi kijana anawajibu wa kupima chama gani akienda ataweza kuendelea na majukumu ya kuwatumikia wananchi, alisema.