Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,040
Leonard Mubale na Richard Katunka, Kigoma
MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongela kutowashinikiza wananchi wachague viongozi wa kisiasa wanaowataka.
Badala yake, Zitto ametaka viongozi hao wa serikali kuacha wananchi wenyewe wafanye maamuzi wenyewe ya kumpata kiongozi bora.
Akizungumza katika kampeni za ubunge Jimbo la Kigoma Kusini juzi, Zitto alisema wakuu hao wa serikali kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitumia madaraka yao kuwashawishi wananchi wawachague viongozi wanaowataka wao.
Katika mkutano huo, uliofanyika kwenye viwanja vya Communte Mwanga mjini, Zitto alisema tabia hiyo ni mbovu kwa kuwa inadumaza demokrasia nchini.
"Kila siku mkuu wa mkoa akiwa na gari la serikali yuko ofisi za CCM..., mbona haji na gari lake ofisi za Chadema?.
Watuachie wilaya na mkoa wetu wala wasitugawe kwa misingi ya udini, waje wafanye kazi zao na wasituingilie, alisema Zitto.
Huku akiwa anashangaliwa na umati uliokusanyika uwanjani hapo, Zitto alisisitiza; "hapa ni kwetu na sisi ndio wenye uchungu wa mji wetu watatuchaguliaje nani awe mbunge na nani awe diwani. Nina uwezo wa kufuata na kuwaeleza ana kwa ana ila nataka waelezwe na wapambe wao," alisema.
Katika mkutano huo, Zitto alimnadi mgombea ubunge wa Chadema Ally Khalfani Mleh na kuwaomba wakazi wa jimbo hilo, kumchagua ili awe mbunge wao.
Alisema endapo mgombea huyo wa Chadema atachaguliwa, ataongeza nguvu kwa wabunge wa upinzani bungeni.
Katika hatua nyingine, mgombea ubunge huyo, alisema endapo atachaguliwa atahakikisha anashirikiana na uongozi wa manispaa kurejesha hadhi ya manispaa hiyo.
Mleh ambaye ni mchumi kitaaluma, alisema kwa kipindi chote ambacho CCM imekuwa ikiongoza jimbo hilo, maisha ya wakazi wake hususani vijana na kina mama yamezidi kuwa magumu kila kukicha.
"Mkinichagua mikakati yangu ya awali kabisa ni kukutana na makundi ya vijana na kinamama na kujadili matatizo hayo kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi," alisema.
Chanzo: Zitto amlipua RC, DC Kigoma
MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongela kutowashinikiza wananchi wachague viongozi wa kisiasa wanaowataka.
Badala yake, Zitto ametaka viongozi hao wa serikali kuacha wananchi wenyewe wafanye maamuzi wenyewe ya kumpata kiongozi bora.
Akizungumza katika kampeni za ubunge Jimbo la Kigoma Kusini juzi, Zitto alisema wakuu hao wa serikali kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitumia madaraka yao kuwashawishi wananchi wawachague viongozi wanaowataka wao.
Katika mkutano huo, uliofanyika kwenye viwanja vya Communte Mwanga mjini, Zitto alisema tabia hiyo ni mbovu kwa kuwa inadumaza demokrasia nchini.
"Kila siku mkuu wa mkoa akiwa na gari la serikali yuko ofisi za CCM..., mbona haji na gari lake ofisi za Chadema?.
Watuachie wilaya na mkoa wetu wala wasitugawe kwa misingi ya udini, waje wafanye kazi zao na wasituingilie, alisema Zitto.
Huku akiwa anashangaliwa na umati uliokusanyika uwanjani hapo, Zitto alisisitiza; "hapa ni kwetu na sisi ndio wenye uchungu wa mji wetu watatuchaguliaje nani awe mbunge na nani awe diwani. Nina uwezo wa kufuata na kuwaeleza ana kwa ana ila nataka waelezwe na wapambe wao," alisema.
Katika mkutano huo, Zitto alimnadi mgombea ubunge wa Chadema Ally Khalfani Mleh na kuwaomba wakazi wa jimbo hilo, kumchagua ili awe mbunge wao.
Alisema endapo mgombea huyo wa Chadema atachaguliwa, ataongeza nguvu kwa wabunge wa upinzani bungeni.
Katika hatua nyingine, mgombea ubunge huyo, alisema endapo atachaguliwa atahakikisha anashirikiana na uongozi wa manispaa kurejesha hadhi ya manispaa hiyo.
Mleh ambaye ni mchumi kitaaluma, alisema kwa kipindi chote ambacho CCM imekuwa ikiongoza jimbo hilo, maisha ya wakazi wake hususani vijana na kina mama yamezidi kuwa magumu kila kukicha.
"Mkinichagua mikakati yangu ya awali kabisa ni kukutana na makundi ya vijana na kinamama na kujadili matatizo hayo kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi," alisema.
Chanzo: Zitto amlipua RC, DC Kigoma