Bwana zito kabwe amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa anamwomba katibu mkuu wa chadema Dr. Slaa kuitisha kikao cha dharura kulizugumzia swala hilo la posho kupandishwa kinyamela kwa kuwa sera ya CDM ya mwaka 2010 inakataa posho kubwa za watumishi wa serikali. Zitto amesema watajadili hizo posho na kutoa tamko kwani posho za wabunge zimepanda kimya kimya.