Zitto alipuka posho za wabunge kuongezeka kimya kimya

Ihselegn

Member
Nov 3, 2011
20
1
Bwana zito kabwe amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa anamwomba katibu mkuu wa chadema Dr. Slaa kuitisha kikao cha dharura kulizugumzia swala hilo la posho kupandishwa kinyamela kwa kuwa sera ya CDM ya mwaka 2010 inakataa posho kubwa za watumishi wa serikali. Zitto amesema watajadili hizo posho na kutoa tamko kwani posho za wabunge zimepanda kimya kimya.
 
si kwa CDM tu.wananchi wote wana haki kujulishwa na hizo mamlaka. Isije kuwa ni mchezo umefanyika kuwa instead of receiving double allowances which leads complains lets double it so as we get the same without complains
 
Kweli hii serikali ni kama sikio la kufa, nasikia baadhi ya watumishi bado hawajapata mishahara wao wanakimbilia kupandisha maposho.
Watoto wetu hawana vitabu, madawati, madawa hakuna lakini wao wanajali matumbo yao tu.
Zitto walipue hao.
 
Bwana zito kabwe amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa anamwomba katibu mkuu wa chadema Dr. Slaa kuitisha kikao cha dharura kulizugumzia swala hilo la posho kupandishwa kinyamela kwa kuwa sera ya CDM ya mwaka 2010 inakataa posho kubwa za watumishi wa serikali. Zitto amesema watajadili hizo posho na kutoa tamko kwani posho za wabunge zimepanda kimya kimya.

Hapa CDM hatuwezi kuongea tukaeleweka na kumbuka hoja ya kuongezeka kwa posho ilianzishwa na mbunge wa CUF jina si mkumbuki
mbunge wangu Joseph Roman Selasini akaichangia na kuiundia hoja kua kweli posho iongezwe wakamshangilia kweli
ila makamanda wa ukweli walikua Arusha kwenye kesi na Mpiganaji Zitto alikua India ndo maana wao watashangaa
ila kama ulifuatilia bunge utakumbuka hiyo siku mbunge wangu alipotoa boko
 
Zitto anatafuta sifa tena.

Sifa zipi?Kwa lipi?Asifiwe na nani?Hivi unajua hizo posho ni kodi zetu ambazo tunazilipa kwa jasho?Hivi mtu kuhoji mgawanyo usio sawa wa keki yetu anakuwa anatafuta sifa?Sasa nimeamini kumbe nchi ikilaaniwa na sehemu ya wananchi wake nao wanalaaniwa!
 
Bado kuna watu wanayapenda hayo yanayofanywa chini ya Uvungu, kiasi watu wanapouliza wanasema inatafutwa sifa!!!!! Kweli safari ni ndefu sijui nao wamo?
 
ishakula kwetu tena....uroho umewazidi huku wananchi wakitopea katika lindi la umasikini.....hawa wabunge wanawawakilisha wananchi wa nchi ipi ?
 
Zitto anatafuta sifa tena.
Ndio maana mmetandikwa na Anti Virus with no apology na wale Vinega kutokana na huu upuuzi wenu. Muulize Masoud Kipanya atakwambia kuwa nanii yako Ruge sio mtu mzuri. Kwanza we hulipi kodi Tanzania unafagia barabara US huwezi kuwa na uchungu na hizi hela zetu tunazokatwa kila kukicha kama kodi
 
Bwana zito kabwe amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa anamwomba katibu mkuu wa chadema Dr. Slaa kuitisha kikao cha dharura kulizugumzia swala hilo la posho kupandishwa kinyamela kwa kuwa sera ya CDM ya mwaka 2010 inakataa posho kubwa za watumishi wa serikali. Zitto amesema watajadili hizo posho na kutoa tamko kwani posho za wabunge zimepanda kimya kimya.

Hivi issues za posho anayezungumzia ndani ya CDM ni zito tu?

huyu jamaa alikuwa india wakati wenzake CDM wanavuta mshiko wa nguvu bungeni...leo hii analalamika na kutaka slaa awaite wote wajadili???

Zito CDM wenzako siyo wasafi kivile..sema lingine
 
Zitto alikua akifanya mahojiano na cloud radio, na taarifa hiyo kurushwa katika kipindi cha amplifier cha clouds jion ya leo.
 
Bwana zito kabwe amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa anamwomba katibu mkuu wa chadema Dr. Slaa kuitisha kikao cha dharura kulizugumzia swala hilo la posho kupandishwa kinyamela kwa kuwa sera ya CDM ya mwaka 2010 inakataa posho kubwa za watumishi wa serikali. Zitto amesema watajadili hizo posho na kutoa tamko kwani posho za wabunge zimepanda kimya kimya.

Kwani wabunge ni watumishi wa serikali?
 
Hivi issues za posho anayezungumzia ndani ya CDM ni zito tu?

huyu jamaa alikuwa india wakati wenzake CDM wanavuta mshiko wa nguvu bungeni...leo hii analalamika na kutaka slaa awaite wote wajadili???

Zito CDM wenzako siyo wasafi kivile..sema lingine
Zitto mwenyewe India alienda kwa kodi zetu!
Kwa hiyo ngoma ni droo tu
 
Kwani wabunge ni watumishi wa serikali?
vyovyote itakavyokuwa either watumishi wa serikali au wa umma,la msingi ni kuwa posho na mishahara yao vinatoka hazina kuu! Na ni kodi za watanzani! Wasijigawie watakavyo huku watanzania wengine tunakufa njaa!
 
Back
Top Bottom