MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Muhibu Said
Kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya kumtahadharisha Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kwamba kama anataka kurejea bungeni baada ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani afanye kazi ya ziada, imemchefua mbunge huyo.
Pinda alitoa kauli hiyo wakati akifanya majumuisho ya mjadala wa hoja ya hotuba ya bajeti ya ofisi yake katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2009/10, bungeni mjini Dodoma juzi.
Zitto, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema alisema kupitia ujumbe wake mfupi wa maandishi alioutuma kwa Nipashe kutoka Nakuru, nchini Kenya jana kuwa, kitendo kilichofanywa na Pinda, ni cha kumshambulia.
Hata hivyo, alisema anamheshimu sana Pinda hivyo, hataki kulumbana naye.
Lakini akamtaka kupima kauli anazozitoa kwa vile zinaweza kuwafanya watu makini wahoji uelewa wake wa demokrasia.
Kuhusu Pinda kunishambulia bungeni jana kauli yangu ni hii. Ninamheshimu sana Pinda na sitaki malumbano nae. Namshauri atazame kauli zake maana zinapelekea watu makini waanze kuhoji uelewa wake wa demokrasia, alisema Zitto.
Akijibu hoja mbalimbali za wabunge 206 waliochangia moja kwa moja na kwa maandishi, Pinda alisema Zitto alitaka kutumia ujenzi wa barabara za lami alizokwenda kuzizindua hivi karibuni kujipatia umaarufu kuwa kazi hiyo imefanyika kutokana na msukumo wake na wa chama chake cha Chadema.
Pinda alisema Zitto alitaka kutumia ujenzi wa barabara za lami zilizojengwa mkoani Kigoma kuwa zimetokana na ushawishi wa chama chake wakati si kweli, bali ni mpango wa serikali.
Wakati wa uzinduzi, nilikwenda Kigoma, kwa bahati mbaya Zitto hakuwapo, nilipouliza wapiga kura wake kuwa mbunge wenu yuko wapi, wengine walisema amehama, wengine walisema sijui yuko Busanda, ila mimi nasema, kwa hali niliyoiona kule jimboni mwake, 2010 Zitto itabidi ajipange sawa sawa, vinginevyo , alisema Pinda na kuibua kicheko kutoka kwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
NIPASHE JUMAPILI
Kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya kumtahadharisha Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kwamba kama anataka kurejea bungeni baada ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani afanye kazi ya ziada, imemchefua mbunge huyo.
Pinda alitoa kauli hiyo wakati akifanya majumuisho ya mjadala wa hoja ya hotuba ya bajeti ya ofisi yake katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2009/10, bungeni mjini Dodoma juzi.
Zitto, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema alisema kupitia ujumbe wake mfupi wa maandishi alioutuma kwa Nipashe kutoka Nakuru, nchini Kenya jana kuwa, kitendo kilichofanywa na Pinda, ni cha kumshambulia.
Hata hivyo, alisema anamheshimu sana Pinda hivyo, hataki kulumbana naye.
Lakini akamtaka kupima kauli anazozitoa kwa vile zinaweza kuwafanya watu makini wahoji uelewa wake wa demokrasia.
Kuhusu Pinda kunishambulia bungeni jana kauli yangu ni hii. Ninamheshimu sana Pinda na sitaki malumbano nae. Namshauri atazame kauli zake maana zinapelekea watu makini waanze kuhoji uelewa wake wa demokrasia, alisema Zitto.
Akijibu hoja mbalimbali za wabunge 206 waliochangia moja kwa moja na kwa maandishi, Pinda alisema Zitto alitaka kutumia ujenzi wa barabara za lami alizokwenda kuzizindua hivi karibuni kujipatia umaarufu kuwa kazi hiyo imefanyika kutokana na msukumo wake na wa chama chake cha Chadema.
Pinda alisema Zitto alitaka kutumia ujenzi wa barabara za lami zilizojengwa mkoani Kigoma kuwa zimetokana na ushawishi wa chama chake wakati si kweli, bali ni mpango wa serikali.
Wakati wa uzinduzi, nilikwenda Kigoma, kwa bahati mbaya Zitto hakuwapo, nilipouliza wapiga kura wake kuwa mbunge wenu yuko wapi, wengine walisema amehama, wengine walisema sijui yuko Busanda, ila mimi nasema, kwa hali niliyoiona kule jimboni mwake, 2010 Zitto itabidi ajipange sawa sawa, vinginevyo , alisema Pinda na kuibua kicheko kutoka kwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
NIPASHE JUMAPILI