Zitto ajieleza mbele ya Sekretariat ya CHADEMA kwa masaa 3, kukutana na vyombo vya habari

Aeleze na Ndege ya TANAPA yeye huwa anaitumia kama nani na kwa mamlaka yapi? Kama mwenyekiti Wa kamati ya Bunge ya Mahesabu ya mashirika ya umma ataweza kukagua TANAPA kwa haki? Zitto ni fisadi, aeleze Gari aliyopewa na Nimrod Mkono na huo mshahara anaolopwa na Rostam Azizi ni kwa kazi ipi.

Ila Zito bwana unajiachia kirahisi mno. Nilikuona pale Saadani unakula bata na magari ya Tanapa, unaingia kichwakichwa mno. Kama una vacation unashindwaje kutafuta usafiri wako? ndege utumie za tanapa na magari pia? we bado kijana sana na chanel ushaikamata unataka uvimbiwe leo kesho ushindwe kula? Taratibu mzee utapotea na masiasa yenu ya kuviziana ndo balaa.
 
zito ni mbunge makini,the issue is anajichanganya sana na mambo mengi ya kipuuzi mara mafisadi,mara bongo movie,mara urais.i stated onde before,zito turudishie zitto wetu yule mzalendo mwenyekuweka maslai ya taifa mbele anayebeba sura ya tanzania yenye haki.please zitto what is happening,mbona kila siku wewe kwa mabaya tu??usiniambie ni wanakusingizia maana hata kipofu atakushangaa,actually ni lazima tusemwe ili tujue udhaifu wetu,lakini si kila linalisemwa ni kweli,but ni wajibu wetu kujichunguza na kubadilika.
jitathimini brother!mchango wako unahitajika kuijenga nchi hii.
:spy: Ngoma kivuma sana hupasuka.
 
yameaanza kutimia maana Zitto ni ndumilakuwili. What goes around comes around

Akichomoka kwenye hili tunamtaka Zitto mwenye msimamo, one straight forward!

Tumechoka na Zitto mwenye roho kibao! Mara CHADEMA, NCCR, CHAUMA, CCM!
anatuchosha sana!
Zitto akitulia ana future kubwa CHADEMA!
 
Unajua kama Nilivyowahi kusema ya Kwamba imeshaonekana Kuiangusha Chadema ni kupitia a weak link na ikaonekana ni Zitto baada ya Marehemu Chacha...Kwanza wakajaribu sana kumkosanisha na Mbowe, Ikashindikana ila kuharibu mahusiano yao wenyewe lakini haikukigawa chama. Ya pili wakamtumia tena Zitto ktk Ukaskazini na Udini ikafanya kazi kubwa sana na lawama zikaanza kuingia vichwani mwa watu lakini ajabu chama ndio kikapata umaarufu zaidi ujio 2010..Baada ya kushindwa kote njia nyingine imejitokeza ambayo ni Zitto mwenyewe kuwa sababu achukiwe ndani na pengine kujitenga na chama hivyo kuwagawa ktk makundi mawili. Na hakika hii imeonekana inafanya kazi maana kweli Zitto anachukiwa na wanaChadema. Naye anaanza kuamini kama hana nafasi ndani ya Chadema na wanaChadema nao wanafunga uwezekano wa Zitto kufikia ambition yake.. In fact it's working japo very slow lakini inafanya kazi..

Halafu, Zitto hana makosa kujibu tuhuma hizi mbona Dr.Slaa alikuwa akizijibu nyingi tu hadi wakaenda personal na watu walikuwa nyuma yake hata kaa wanajua kweli tuhuma ni nzito...Kwa nini Zitto asijibu, isipokuwa kosa la Zitto ni kutojipanga nyuma ya chama ktk majibu yake. Kila kitu anachukulia personal kama wanavyotaka, badala ya kutumia kofia ya chama kujikinga. Niliwashtua both Zitto, Mbowe na Wanachamema hapa toka mwaka 2009 lakini watu hawaniamini.. Ninaujua mji wa Dar kama kiganja cha mkono na najua mengi yanayofanyika nyuma ya pazia japo niko nje ya nchi.

Hii tabia ya Zitto kujifanya independent (kwa sababu haamini mtu) wakati akitumia jukwaa la CDM ndio inayomweka bayana zaidi kisiasa. Anatakiwa kujifunza zaidi siasa, maana ndipo imani na uzalendo huanzia ili mawazo binafsi kuongoka. Let them say maadam mnaelewa malengo yao, nia zao haitawaumiza vichwa..

Kwa haya uliyoandika Mkandara wewe ni mwamba.Umemaliza kila nilichotaka kusema.Niseme tu Zitto anapaswa kujifunza kwa tukio hili.Wanachadema hawamchukii Zitto kama Zitto bali wanachukia tabia yake ambayo wanaona ni ya usaliti.Wanachadema hawako tayari kumvumilia mtu yeyote wanayeona anataka kukwamisha juhudi za kuipeleka CDM Ikulu.Kitendo cha Zitto kuropoka kila mara mambo ya Urais huku wenzake wakiwa wamejichimbia vijijini kuimarisha chama hakika kinakera sana.Yampasa kuiga busara za Mbowe,Dr Slaa,Mnyika,Dr Kitila na wengine.Asipobadilika tena sasa naamini hatakaa abadilike milele.
 
zito ni mjanja sana amewaingiza jamaa choo cha kike ili wajiingize kumlaumu kwa ushabiki wa kichama ,sasa kwa sababu wamemfanya kuwa mtuhumiwa kwa kumrushia makombora naye atahitaji sasa kumalizia kwa kuwaangamiza wote wahusika,subiri kesho saa 5 ataongea na vyombo vya habari muone sakata hilo hapo ndipo mtakapochuja.
 
Zitto amehongwa. Sitahudhuria mkutano wake kesho. Hafai hata kidogo. Mtaka yote,hukosa yote. Ptuuu!
 
Nimesikia uchunguzi unafanyika. Kwa nini tusisubiri huo uchunguzi utoe taarifa yake? Iwapo Zito ana hoja za kupinga tuhuma hizo kwa nini asisubiri kamati ya haki na maadili ya Bunge inayofanya uchungu ili akatoe maelezo yake huko. Kutaka kutoa maelezo yake kwa waandishi wa habari kesho ni kama ameshikwa na kiwewe (ame panic). Watu wenye akili watahoji kama hahusiki na tuhuma hizi, kwa nini ashikwe na kiwewe? Wanaotuhumiwa ni wengi, kwa nini yeye tu ashikwe na kiwewe na atake kuongea na waandishi wa habari? Bila shaka kuna jambo. Jambo gani hilo analotaka kulizuia lisichunguzwe. Nadhani kijana wangu Zito atulie, uchunguzi utamtetea kama anasthili kutetewa na hastahili kutetewa aombe radhi jamii itamwelewa itamsamehe kwa kuwa ni kijana mdogo anakuwa kwa hali zote, itamlea. Bado ana nafasi ya kujirekebisha akatufaa kesho. Jamii ya kitanzania haitupi mtoto anayekuwa kisiasa kama yeye. Bora kijana nayethubutu kutenda japo kwa makosa anatupa mwanya wa kumjua ni malezi gani tumpatie. Tutampa na tumonya mambo ambayo anapaswa kuyaogopa kama ukoma.
Kwa nadharia ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Zito anapaswa kuogopwa kama UKOMA kwa sababu anakimbilia Ikulu mahali patakatifu kabisa. Kikwete alipatafuta Ikulu kwa muda wa miaka 15, Watanzania wenyew tayari tujionea jinsi asivyofaa. Tukirudia makosa kwa Zito tena, tutakuwa hatufundishiki
 
kwani yeye zitto atake posho za nini wkt mafisadi wamemuwezesha?....tuulize sisi tunaomjua zitto in and out sio nyie mnaomuona mbele ya vyombo vya habari...zitto is a dangerous person bora hata kikwete

come again, so interesting!
 
Zitto is clean and smart, no discussion. Alafu kamanda tunakuomba husijiweke karibu na ma ccm kwa kigezo siasa sio huasama, we love you Zitto, sio marafiki wema hawo, then uwe makini na kauli unazotoa, wewe ni kiongozi mkubwa kamanda. Si unawaona Lissu, Dr Slaa, Mbowe na Mnyika wapo makini na kauli zao wanapozungumza mahala popote.

This guy called Zito is neither clear nor smart!! Ana madudu mengi ya rushwa na undumilakuwili. Mla rushwa namba mpja na data zake ziko wazi tokea issue ya Richmond and Dowans ilipotokea. Nilimpenda Zitto tangu akiwa TGNP lakini mara alipoingia bungeni na kuanza kujihusidha na rushwa badala ya kuweka maslahi ya taifa mbele, nememwondoa kwenye wakombozi wa nchi hii. He could make a good leader but he should not be trusted anymore!!
 
This is a very serious statement mkuu unaweza kusema zaidi maana u,emoshutua sama mkuu

Yes! The boy is very dangerous! Hafai hafai hafai, period! If you don't trust me, mpeni uongozi wa juu wa nchi muone! Heri atawale Kingunge Ngumbale Mwiru!
 
Ishu ya Tanesco haijaanza leo kuna wakuregenzi wengi sana wamepitia hilo shilika lakini mambo yalikua yanafichwa na hawasemi.kuna maswali mengi ya kujiuliza;
1.Je kuchuma Tanesco kumeanza ss hivi au kitambo?
2.Wakurugenzi waliopita hawakuliona hili?
3.Waliopokea rushwa Zito yupo au wenzake ndo walipokea na yy hakujua ?
4.Je kuna watu walipandikizwa kupokea rushwa makusudi ili kuwachafua wengine ambao wako safi?
5.Hatua gani walichukuliwa mawaziri na makatibu waliopitia hii wizara na kukumbwa na kashfa?
 
kaka Mtoi nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja. So far haijawa proved kama Zitto amekula rushwa. He will remain innocent unless proved guilty. Tuache siasa za hisia watanzania
 
nimesema humu kuwa jina la zitto halimo kwenye list bali kikao cha jana usiku ndicho kinataka kuhakikisha kuwa zitto anawekwa kwenye list na anatajwa na ilikuwa moja ya maazimio yaliyokwenda kw spika jana usiku...nilidokeza juu ya kikao hicho katika thread hii hapa chini.....na subirini hiyo kesho zitto akiongea na waandishi wa habari ndio mtaujua ukweli wa hili ninalosema

mkuu funguka zaidi.
 
zito ni mbunge makini,the issue is anajichanganya sana na mambo mengi ya kipuuzi mara mafisadi,mara bongo movie,mara urais.i stated onde before,zito turudishie zitto wetu yule mzalend..........
Mamajack mbona unajichanganya. Hayo uliyoyataja yanaonyesha kuwa Zitto siyo makini. The guy is too CHILDISH.
 
Zitto hiyo ndio turning point yako kisiasa. Unatoka kwenye mafanikio ya siasa za nadharia (uwezo mkubwa wa kujenga hoja nzito na kusimamia sheria) na sasa unaingia hatua ya pili ya mafanikio ya siasa za vitendo (kuthibitishwa kwamba rushwa kwako ni mwiko na hukula hela ya mtu). Baada ya hatua hii ya pili, wimbi kubwa la watanzania waliojenga hofu na hisia potofu juu yako, ghafla watabadilika na kujenga imani kubwa kwako. Zawadi yetu kwako itakuwa ni
kukukabidhi kijiti hapo 2015 uongoze taifa.
 
dr slaa ni mmoja wa wanaosemekana kuusaka urais 2015
je zitto ana imani dr slaa anaweza kuongoza sekretarieti? ukizingatia wanaomchafua zitto ni wabunge wapenda posho na wasaka urais kutoka vyama vyote, (hii ni kutokana na maelezo ya zitto mwenyewe)

Kwani hiyo Sekretarieti anakaa Dr. Slaa peke yake? Pamoja na kwamba Dr. Slaa ndiye mtendaji mkuu wa chama haimaanishi kwamba atakachosema au kukitolea maoni ndani ya kikao ndicho kitakuwa maamuzi ya sekretarieti au chama. Maamuzi katika vikao si suala la kichwa kimoja bali ni maamuzi ya wajumbe wote inclusively.
 
Back
Top Bottom