Zitto ajieleza mbele ya Sekretariat ya CHADEMA kwa masaa 3, kukutana na vyombo vya habari

Zitto anatisha moja wa vijana mwenye kusimamia anachokiamini na kinachomtesa Sasa ni hiyo misimamo Yake believe me
 
Kwa tabia yake ya undumila kuwili Zitto hawezi kuponyoka. Kama kweli anamilki Hummer na magari mengine kama ilivowahi kuripotiwa kuwa alimsadia magari Kafulila kwenye kampeni, Zitto ni fisadi hakuna shaka. Kinachofurahisha kwenye mchezo huu wa kuvuana nguo, hakuna fisi atayenusurika kutokana na ukweli kuwa hata hao wanaowashutumu wenzao hawafanyi hivyo kwa uzalendo bali visasi vya kuzuiwa kuliibia shirika la Umeme. Mhando si wa kwanza. Dr Idris Rashid aliiba sana ukiachia mbali familia na shemeji za Mkapa waliotumia Net Group Problems kulimaliza kabisa shirika letu.Bado serikali ambayo huwa halipii umeme inaotumia. Msururu ni mrefu kama uchunguzi wa kina utafanyika.

mkuu kwa hiyo mafisi yanagombea mzoga?
 
dr slaa ni mmoja wa wanaosemekana kuusaka urais 2015
je zitto ana imani dr slaa kuongoza sekretarieti? Ukizingatia wanaomchafua zitto ni wabunge wapenda posho na wasaka urais kutoka vyama vyote

kwani yeye zitto atake posho za nini wkt mafisadi wamemuwezesha?....tuulize sisi tunaomjua zitto in and out sio nyie mnaomuona mbele ya vyombo vya habari...zitto is a dangerous person bora hata kikwete
 
Aeleze na Ndege ya TANAPA yeye huwa anaitumia kama nani na kwa mamlaka yapi? Kama mwenyekiti Wa kamati ya Bunge ya Mahesabu ya mashirika ya umma ataweza kukagua TANAPA kwa haki? Zitto ni fisadi, aeleze Gari aliyopewa na Nimrod Mkono na huo mshahara anaolopwa na Rostam Azizi ni kwa kazi ipi.

Tukubali tukatae zitto anatumika ku distabilise Chadema kumbuka wakati wa kampeini kule Arumeru watu wako kwenye battle field dakika za lalasalama nakumbuka zilikua zimebaki siku mbili tuu anaibuka na hoja ya kugombea uraisi ili ahamishe ajenda kuu ya kampeini thank God kwa busara ya Dr. Slaa alivo uliza juu ya kauli ile ya Zitto alisema hawezi kuzungumzia upuzi maana ajenda iliyopo ni Nasari kuingia bungeni. Ila kwa hili kapatikana na mengine yatafumuka hata mama yake mzazi aliwahi kukiri hadharani kwamba mwanae anatumiwa
 
zito ni mbunge makini,the issue is anajichanganya sana na mambo mengi ya kipuuzi mara mafisadi,mara bongo movie,mara urais.i stated onde before,zito turudishie zitto wetu yule mzalendo mwenyekuweka maslai ya taifa mbele anayebeba sura ya tanzania yenye haki.please zitto what is happening,mbona kila siku wewe kwa mabaya tu??usiniambie ni wanakusingizia maana hata kipofu atakushangaa,actually ni lazima tusemwe ili tujue udhaifu wetu,lakini si kila linalisemwa ni kweli,but ni wajibu wetu kujichunguza na kubadilika.
jitathimini brother!mchango wako unahitajika kuijenga nchi hii.

Duh, unamahaba ya that na mpiganaji Zito Z. Kabwe
 
Kauli hii iko kwenye ukurasa wake wa twitter.

"Kwa masaa 3 nimejieleza mbele ya sekretariat ya chama kuhusu tuhuma za rushwa dhidi yangu. Niliomba kutaka kutoa maelezo kwa katibu Mkuu".

Amekiomba chama kifanye uchunguzi juu yake na kuchukua hatua akibainika.

Nadhani huu ni uamuzi wa busara sana badala ya kusubiri maneno yazidi kukua ni vizuri kumaliza udhia mapema.
Nadhani sasa sekretariati imepata mengi kutoka kwake na hivyo kuinufaisha sana kamati kuu itakapokutana kwa ajili ya kutafakari tuhuma hizo dhidi yake.

Narudia tena kumshauri kamanda Zitto ajiepushe na tabia ya kupenda kuwa msemaji wa kila kitu kinachojitokeza mbele yake, afanye hivyo pale anapolazimika tu. Kama anajitambua kwamba yeye ni "presidential hopeful" lazima ajilinde kwa kauli na matendo yake. Hii vita baridi ccm wanayopigana nae yeye hajaijua kwakuwa wamekuwa wakimpamba na yeye akaanza kujisahau kumbe walikuwa wanamlia timing wammalize.
 
Last edited by a moderator:
Kilaza wa jimbo la Tabora, Rage mzee wa bastora ameomba muongozo wa spika kuwa kwa nini Mh. Tundu Lissu kataja majina ya wabunge wala rushwa wa CCM pekee na ameacha wa CHADEMA. Sasa anataka muongozo ili na Zitto atajwe.

Nae si ataje kama anakithibitisho kama Lisu?
 
zito ni mbunge makini,the issue is anajichanganya sana na mambo mengi ya kipuuzi mara mafisadi,mara bongo movie,mara urais.i stated onde before,zito turudishie zitto wetu yule mzalendo mwenyekuweka maslai ya taifa mbele anayebeba sura ya tanzania yenye haki.please zitto what is happening,mbona kila siku wewe kwa mabaya tu??usiniambie ni wanakusingizia maana hata kipofu atakushangaa,actually ni lazima tusemwe ili tujue udhaifu wetu,lakini si kila linalisemwa ni kweli,but ni wajibu wetu kujichunguza na kubadilika.
jitathimini brother!mchango wako unahitajika kuijenga nchi hii.
Kama kukusikia amekusikia abakize utekelezaji tu, namuomba zitto baada ya hii inshu kupita ajirekebishe kuna kitu atakuwa amejifunza kwani bado tunamuhitaji sana kwa ukombozi wa taifa letu. Rudi kundini kaka anza kusambaza M4C kama zamani.
 
Kupitia akaunti yake ya Twitter, naibu kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni ameweka wazi nia yake ya kuelezea kila kitu kuhusiana na tuhuma za rushwa dhidi yake, atakapofanya mkutano na waandishi wa habari kesho saa tano asubuhi kwenye ofisi za Bunge za jijini Dar.

Zitto Kabwe: Kesho Nitazungumza na waandishi wa Habari ofisi za Bunge Dar Es Salaam kuanzia saa tano asubuhi. Kuendelea kukaa kimya ni silaha kwa adui.
 
i shocked!! siamin...ila acha wafanye uchunguz kwanza bado sija muhukum!!!! ana nafas bado....
 
Labda anataka kujiuzulu Ubunge na Nyazifa zake zote ndani ya Chama. I like Zitto lkn kama hii ya Rushwa ni kweli basi siasa ni mchezo mbaya sana.
 
dr slaa ni mmoja wa wanaosemekana kuusaka urais 2015
je zitto ana imani dr slaa kuongoza sekretarieti? ukizingatia wanaomchafua zitto ni wabunge wapenda posho na wasaka urais kutoka vyama vyote

Nadhani si kumchafua kwani najua lisemwalo lipo na kama halipo laja, kwa uande wangu sina imani na zito kwani ukiangalia dhahiri zito wa miaka iliyopita bungeni siyo huyu wa leo yaani sijaona uzalendo wake wa awali
 
Hawezi kukwepa mtego huu alioandaliwa na mafisadi....lazima ang'oke tu hana jipya zaidi ya kutaka misifa
 
dr slaa ni mmoja wa wanaosemekana kuusaka urais 2015
je zitto ana imani dr slaa kuongoza sekretarieti? ukizingatia wanaomchafua zitto ni wabunge wapenda posho na wasaka urais kutoka vyama vyote

Mkuu, hivi unajua kwamba Dr Slaa aliombwa kukubali kugombea urais kupitia chama chake CDM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010?
Hakuwahi kusema hata mara moja hadharani, kwamba anataka kugombea urais.

Kwa sababu hiyo hana sababu ya kumfitini Mhe. Zito, kwa sababu hakuna anayejua nani ataombwa tena kugombea Urais kupitia CDM japo intuitively watu wanahisi kwamba atakuwa ni Dr. tena.
 
Zottophobiasis, that is what you can easily say! kuna mambo mengi sana juu ya Zitto. Nigekuwa mshauri wake wa karibu ningemshauri akanushe kuwatetea TANESCO na kwamba hakujua kama wako hivyo, siyo mungu yeye akajua kila kitu lakini Zitto hakuchukua rushwa hata kidogo, mi naamini kabisa.
Zitto zitto!! What more can I say???
 
pole bro Zitto! mi ni mmoja ambaye na admire misimamo yako juu ya unayoyaamini! But be careful na hao magamba, they are very tricky?
 
Back
Top Bottom