Zitto aibua mazito bungeni: Ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti, ufisadi wa hati fungani ya Sh1.2 Trilioni

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
Zitto%20aomba%20kura.jpg


WAKATI kasi ya 'tumbuaji' majipu inayofanywa na Rais John Magufuli, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameibuka na kusema bado Rais hajagusa kansa ya ufisadi na badala yake anachokifanya ni kupapasa tu.

Amesema pamoja na jitihada ambazo Rais ameanza kuchukua kuhusiana na suala hilo, lakini bado hajagusa maeneo nyeti ambayo yamekuwa kilio kikubwa cha Watanzania ikiwamo suala la Tegeta Escrow, ambalo mpaka sasa mtambo wa IPTL upo chini ya matapeli na kila mwezi serikali inalipa zaidi ya Sh. bilioni nane.

Ufisadi mwingine ambao alisema haujaguswa ni wa hati fungani wa dola za Marekani milioni sita, ambao watu waliohusika wakiwamo benki ya Standard ya Uingereza ambao walitoa rushwa hiyo na waliopokea rushwa maafisa wa Wizara ya Fedha bado hawajafikishwa mahakamani na badala yake waliofikishwa mahakamani ni madalali tu.

Zito alisema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati kifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho. Alisema suala la hati fungani serikali inalazimika kulipa riba, hivyo imeongeza deni la taifa Sh. trilioni 1.2 bila riba na kwamba hadi mwaka 2020 serikali itakuwa imelipa zaidi ya
Sh. trilioni 1.8 ambazo ni zaidi ya Sh. bilioni 600.

Alisema badala ya Rais Magufuli kushughulikia ufisadi huo ambao Watanzania wanaupigia kelele pamoja na kuweka mfumo madhubuti ambao utazuia rushwa, mpaka sasa hajafanya hivyo.

Kadhalika, Zitto alisema mpaka sasa Magufuli anafanya kazi kidikteta kwa kupoka madaraka ya watendaji wake wa chini na kwamba hadi sasa Baraza la Mawaziri lililopo ni kama hewa kwa kuwa mawaziri hawajapewa nyenzo za kazi isipokuwa Rais wao ndiyo anafanya kazi zote.

Source: Nipsahe
 
Ni kweli na asipogutuka miaka mitano itaisha pasipo kutekeleza ahadi nyingine kwa kuzingatia majipu zaidi mwisho wa siku Tanzania ya Viwanda ikabaki kwenye simulizi tu
 
Mwacheni Rais afanye kazi! Atafanya mangapi kwa wakati mmoja?! Ukimuangalia vzr Zitto ana hulka ya kutafuta na kupenda sifa.
 
.. lakini Zitto amesahau kutaja ushirikiano wa pembe tatu - ZZK - RD - JK. tunasubiri kuona JPM akiushughulikia pia.
 
Zitto%20aomba%20kura.jpg


WAKATI kasi ya 'tumbuaji' majipu inayofanywa na Rais John Magufuli, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameibuka na kusema bado Rais hajagusa kansa ya ufisadi na badala yake anachokifanya ni kupapasa tu.

Amesema pamoja na jitihada ambazo Rais ameanza kuchukua kuhusiana na suala hilo, lakini bado hajagusa maeneo nyeti ambayo yamekuwa kilio kikubwa cha Watanzania ikiwamo suala la Tegeta Escrow, ambalo mpaka sasa mtambo wa IPTL upo chini ya matapeli na kila mwezi serikali inalipa zaidi ya Sh. bilioni nane.

Ufisadi mwingine ambao alisema haujaguswa ni wa hati fungani wa dola za Marekani milioni sita, ambao watu waliohusika wakiwamo benki ya Standard ya Uingereza ambao walitoa rushwa hiyo na waliopokea rushwa maafisa wa Wizara ya Fedha bado hawajafikishwa mahakamani na badala yake waliofikishwa mahakamani ni madalali tu.

Zito alisema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati kifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho. Alisema suala la hati fungani serikali inalazimika kulipa riba, hivyo imeongeza deni la taifa Sh. trilioni 1.2 bila riba na kwamba hadi mwaka 2020 serikali itakuwa imelipa zaidi ya
Sh. trilioni 1.8 ambazo ni zaidi ya Sh. bilioni 600.

Alisema badala ya Rais Magufuli kushughulikia ufisadi huo ambao Watanzania wanaupigia kelele pamoja na kuweka mfumo madhubuti ambao utazuia rushwa, mpaka sasa hajafanya hivyo.

Kadhalika, Zitto alisema mpaka sasa Magufuli anafanya kazi kidikteta kwa kupoka madaraka ya watendaji wake wa chini na kwamba hadi sasa Baraza la Mawaziri lililopo ni kama hewa kwa kuwa mawaziri hawajapewa nyenzo za kazi isipokuwa Rais wao ndiyo anafanya kazi zote.

Source: Nipsahe
Nafikiri Zito yeye awarudishie fedha zao hao waliomnunua awambie kazi imenishinda. Hata hao waliomnunua wameona juhudi zake.Rais hawezi kufanya kazi kwa shinikizo bali kwa kadri atakavyojiridhisha kuwa hatua hizi zinafaa.
Ubadhilifu upo sehemu nyingi iweje mtu mmoja pekee ndio unaiona IPTL tu. Jamani Tanzania inao wanasiasa wengi eti hawaoni tatizo la IPTL ila ni Zito pekee. Hapa kuna kitu. Iliwahi kusemwa aliwahi kudaiwa kuwa Zito ameshitakiana na hao IPTL. Huenda hii ikawa ni sababu ya yeye kuiandama IPTL na sasa anataka Mh Rais amsadie kulipa kisasi kwa nguvu.
 
safi sana Zito kwa kumkumbusha Raisi nadhani atayatendea kazi mawazo yako akishindwa wananchi tutakupeleka. ikulu 2020 ili uenndeleze alipoishia.
 
Wakati mwingine in vigumu kuelewa Mh.Zitto anacho simamia/msimamo wake!!! Alisena atatupatia list ya mafisadi walioficha fedha haramu kwenye Mabenki ya Uswiss - mpaka Leo yupo kimya i.e hana ubavu wa kuwataja - leo hii anamsema sema Dk.Magufuli kwamba hajafanya lolote la maana linapokuja suala kushughulikia mafisadi!!! Huu kama sio unafiki tuiteje?
 
Kinachonikera ni ile tabia ya baadhi ya mijitu kutaka kumfanya magu kama ndiye mungu wao yani hawataki akosolewe hata akifanya jambo la hovyo wao ni kusapoti tuu. Na yeyote anayekosoa wanamwona kama anakufuru
 
Wakati mwingine in vigumu kuelewa Mh.Zitto anacho simamia/msimamo wake!!! Alisena atatupatia list ya mafisadi walioficha fedha haramu kwenye Mabenki ya Uswiss - mpaka Leo yupo kimya i.e hana ubavu wa kuwataja - leo hii anamsema sema Dk.Magufuli kwamba hajafanya lolote la maana linapokuja suala kushughulikia mafisadi!!! Huu kama sio unafiki tuiteje?
mbona alishaleta majina ya wahindi kibao
 
Nguvu zilizotumika kule Zanzibar zitumike pia kwa haya Mafisadi anayosema Zito yuko sahihi ,hili suala la IPTL kwa nini halishughulikiwi hili ni JIPU la kitambo sana lishaiva muda ndio huu litumbuliwe.
 
Angalau Zitto katoa ya moyoni yale ambayo chama chake kinayafikiri ni muhimu yafanyiwe kazi yasiachwe kiporo ni maoni ya chama si yake binafsi haifai kuyachukulia kama maoni binfsi bali ni mtizamo wa chama chake
 
Haka katoto kana Kimbelembele na ujuaji ujuaji ndio Sababu wachaga walikafukuza Chadema!
 


Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe jana aliibua mambo mazito bungeni wakati akichangia mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Rais –Tamisemi na Utawala Bora, likiwamo la ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti kutokana Bunge kupitisha bajeti Sh23.7 trilioni huku Serikali ikija na bajeti ya Sh29 trilioni.

ZITTO.jpg


Mambo mengine yaliyobainishwa na mbunge huyo ni sakata la ufisadi wa hati fungani ya Sh1.2 trilioni katika Benki ya Standard ya Uingereza na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kushindwa kutoa majibu ya uchunguzi wa miamala kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow kwenda Benki ya Stanbic.

Kuhusu bajeti, Zitto alisema kuna ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015 katika mchakato wa bajeti ya mwaka 2016/17 kwamba kifungu cha 8 cha sheria hiyo kinaeleza namna ambavyo mfumo wa bajeti ya Serikali unapaswa kuwa.

“Vifungu cha 8(1)(b) na 9(1)(a) na 19(1) vinataka ‘mpango na miongozo ya bajeti’ ipitishwe na Bunge katika mkutano wake wa Februari kila mwaka. Bunge lilikaa kama Kamati ya Mipango na kupitisha Mpango wa Bajeti uliokuwa na Bajeti ya Sh23.7 trilioni,” alisema.

Alisema kiasi hicho ni tofauti na bajeti inayojadiliwa sasa ya Sh29.5 trilioni na kubainisha kuwa jambo hilo si utawala bora kwa maelezo kuwa utungaji wa bajeti umeainishwa kisheria na kama sheria hazifuatwi, ni vigumu hata Bajeti yenyewe kutekelezwa.

“Ili kurekebisha hali hii ni lazima Bunge likae tena kama kamati ya mipango na kupitisha upya viwango vya juu vya bajeti kabla ya mjadala wa bajeti kuendelea au angalau kabla ya kupitisha bajeti kuu, Juni 2016,” alisema na kwamba bajeti za taasisi hazimo kwenye vitabu vya bajeti ya Serikali kinyume na sheria ya bajeti.

Kuhusu ufisadi wa Sh1.2 trilioni, mbunge huyo alisema mwaka 2013, Serikali ilikopa fedha hizo kutoka nje kwa msaada wa Benki ya Standard ya Uingereza ambayo sasa inaitwa Standard Bank, kwamba mkopo huo wenye riba inayoweza kupanda umeanza kulipwa Machi mwaka huu.

Alisema mkopo huo utalipwa mpaka mwaka 2020 kwa mikupuo tisa inayolingana na kuongeza kuwa mkopo huo umegubikwa na ufisadi huku baadhi ya Watanzania wakiwa tayari wamefikishwa mahakamani wakihusishwa na sehemu ya mkopo huo.

“Jambo la kushangaza ni kwamba wanaosemekana kula rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Vilevile, waliotoa rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Waliopo mahakamani ni wanaosemekana kutumika kupeleka rushwa. “Mjumbe kashtakiwa, lakini aliyemtuma hajashtakiwa na aliyepelekewa kilichotumwa hajashtakiwa. Hapa kuna tatizo la msingi ambalo tukilitatua Serikali yetu itaepuka masuala kama haya siku za usoni.”

Alisema ana barua ya kundi la Watanzania zaidi ya 2,000 wakitaka benki hiyo ya Uingereza ichunguzwe katika suala hilo la hati fungani huku Takukuru ikitumia taarifa ya Taasisi ya Uingereza ya (SFO) katika kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya Watanzania wanaotajwa katika sakata hilo.

Alisema SFO haikufanya uchunguzi dhidi ya benki hiyo ya Uingereza na kushangazwa na Tanzania kusaidiwa kesi hiyo na wataalamu kutoka nchi hiyo.

“Iwapo tutafanikiwa kuonyesha kuwa Benki ya Standard ilihonga kupata biashara nchini kwetu, Tanzania itakuwa fundisho kwa kampuni ya kimataifa kwamba Afrika siyo mahala pa kuhonga na Tanzania haitalipa mkopo huu na riba zake na tutaokoa zaidi ya Sh2 trilioni katika deni la Taifa,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
 

Attachments

  • Mchango wa Ndg. Zitto Kabwe Bungeni 28 Aprili 2016 .pdf
    13.1 KB · Views: 102
Back
Top Bottom