Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Wadau naomba mnisaidie kuchanga mawazo.
Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.
Anasema mume wake amemtelekeza yeye na mtoto wake tangu alipokuwa na ujauzito wa miezi minne.Huyu shostito anafanya kazi kampuni moja ya simu na mumewe anafanya kazi serikalini.
Kisa cha mume kumkimbia ni kuwa mwanamke amekaidi kutekeleza matakwa yake. Mume anataka mkewe auze gari aliyonunua kabla hawajaoana na wahame toka kwenye nyumba wanayoishi mwenge iliyolipiwa na mke.Mume alihamia nyumbani kwa mkewe kabla hawajaoana, na mwanamke alinunua gari kabla hawajaoana, na jamaa hakuchangia hata senti moja.
Mwanamke kakataa kuuza gari ila amekubali kuhama nyumba kwa masharti kwamba iwe ni maeneo ya mwenge, sinza, kinondoni, ubungo ama mabibo. Mumewe anataka wahamie mbagala, kwamba ndipo anaweza kumudu kulipa kodi ya nyumba, hataki mkewe aongeze hata senti.Mume kuona mwanamke hatekelezi matakwa yake akaona isiwe tabu, kafunga virago amehamia mbagala.
Wadau mnisaidie, nimshaurije huyu shostito?
Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.
Anasema mume wake amemtelekeza yeye na mtoto wake tangu alipokuwa na ujauzito wa miezi minne.Huyu shostito anafanya kazi kampuni moja ya simu na mumewe anafanya kazi serikalini.
Kisa cha mume kumkimbia ni kuwa mwanamke amekaidi kutekeleza matakwa yake. Mume anataka mkewe auze gari aliyonunua kabla hawajaoana na wahame toka kwenye nyumba wanayoishi mwenge iliyolipiwa na mke.Mume alihamia nyumbani kwa mkewe kabla hawajaoana, na mwanamke alinunua gari kabla hawajaoana, na jamaa hakuchangia hata senti moja.
Mwanamke kakataa kuuza gari ila amekubali kuhama nyumba kwa masharti kwamba iwe ni maeneo ya mwenge, sinza, kinondoni, ubungo ama mabibo. Mumewe anataka wahamie mbagala, kwamba ndipo anaweza kumudu kulipa kodi ya nyumba, hataki mkewe aongeze hata senti.Mume kuona mwanamke hatekelezi matakwa yake akaona isiwe tabu, kafunga virago amehamia mbagala.
Wadau mnisaidie, nimshaurije huyu shostito?