Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
Ni ukweli usiopingika kuwa chadeam ni chama kikubwa kwasasa lakini hicho sio kigezo cha kukifanya kijione kiko sawa na ccm na kuweza kupambana na ccm ambacho kina mtaji wa mamilioni ya watanzania mjini na vijijini! lakini tukiwa tumebakiza siku chache kabla ya uchaguzi mdogo wa ARUMERU, zifuatazo ni sababu chache za msingi zitakazo iangusha chadema na kuicha ccm ikiibuka kidedea
1. UDHAIFU WA NASSARI
Ni ukweli ulio wazi Nassari ni mgombea ambae kiwango chake kipo chini sana katika kujenga hoja na kuzitetea,marafiki zake wa karibu wamepruv hilo, pia hana mvuto wa kisiasa kama mshindani wake wa karibu SIOI! Pia Nassari amekuwa akibebwa zaidi na umaharufu wa viongozi wake wa juu wa chama i.e MBOWE na SLAA ambao wamepiga kambi mjini ARUMERU ili kumpigia kijana wao kampeni, ili la kubebwa na kina Slaa, hata RAIA mwema wamelipruv, nanukuu"Mgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari, licha ya uwezo wake binafsi wa kujieleza lakini kwa sehemu kubwa uzito wake jukwaani unahusisha umaarufu wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbroad Slaa, ambaye bado hajapoteza mvuto wa kisiasa kwa wakazi wa Arumeru'
2.WAPIGA KURA VIJANA
ni jambo lililo wazi kwamba chadema inategemea sana vijana zaidi katika kampeni zake na ndio mtaji mkubwa sana wa chama hicho, sasa vijana wengi waliojiandikisha pale arumeru wengi wako shuleni kwasasa, wengine vyuoni hivyo uwezekano wa kukosa kura ni mkubwa
pia ukiangalia mahudhurio na aina ya ushabiki wa kampeni za CHADEMA, ni dhahiri kuwa wapiga kura wengi wa chama hicho ni vijana.
Ni katika mtazamo huo ambamo changamoto inayojitokeza ni kuwa vijana wengi wenyeji wa Arumeru Mashariki hawakujiandikisha kupiga kura katika kata za jimbo hilo.
Wengi wamejiandikisha katika maeneo wanakoendesha shughuli zao za kujikimu kimaisha, ambazo ni Mererani, kwenye mgodi wa Tanzanite, eneo lililopo Jimbo la Simanjiro, linaloongozwa na Christopher ole Sendeka. Mbali na Mererani, vijana wengi wa jimbo hilo wamejiandikisha kupiga Arusha Mjini, wanakoendesha shughuli zao za kila siku hii kwa kiasi kikubwa itamwangusha bwana NASSARI, sababu ccm imejiwekeza katika kada mbalimbali za watu kuanzia watoto,vijana na wazee ambao kikukweli ndio hazina kubwa ya ccm
3.NGUVU KUBWA YA CCM ARUMERU
siamini ni kwa jinsi gani chadema inaweza shinda katika jimbo ambalo viongozi wote kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya ni ccm, hapa ni kujidanganya! lazima chadema wakubali kuwa pale ARUMERU sio pao,kwa mtaji huu ccm inaweza kucheza both macro and micro politics ilhali kujihakikishia ushindi mkubwa
4.PROPAGANDA ZA WAZI ZA CHADEMA
Chadema katika kampeni zake nyingi imekuwa ikimwaga propaganda nyingi sana kuhusu ccm, wananchi wa arumeru wamekuwa na ccm kwa muda mrefu kwahiyo wanajua fika yanayosemwa sio sahii! ingawa hata ccm imekuwa ikitoa propaganda kali na wengie wamesikika wakitoa matusi makali kwa viongozi wa chadema ila kuna msemo wa kiswahili unaosema "zimwi likujualo....."
kwa uchache hayo ni mambo yatakayoiangusha chadema tarehe 1 april 2012
1. UDHAIFU WA NASSARI
Ni ukweli ulio wazi Nassari ni mgombea ambae kiwango chake kipo chini sana katika kujenga hoja na kuzitetea,marafiki zake wa karibu wamepruv hilo, pia hana mvuto wa kisiasa kama mshindani wake wa karibu SIOI! Pia Nassari amekuwa akibebwa zaidi na umaharufu wa viongozi wake wa juu wa chama i.e MBOWE na SLAA ambao wamepiga kambi mjini ARUMERU ili kumpigia kijana wao kampeni, ili la kubebwa na kina Slaa, hata RAIA mwema wamelipruv, nanukuu"Mgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari, licha ya uwezo wake binafsi wa kujieleza lakini kwa sehemu kubwa uzito wake jukwaani unahusisha umaarufu wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbroad Slaa, ambaye bado hajapoteza mvuto wa kisiasa kwa wakazi wa Arumeru'
2.WAPIGA KURA VIJANA
ni jambo lililo wazi kwamba chadema inategemea sana vijana zaidi katika kampeni zake na ndio mtaji mkubwa sana wa chama hicho, sasa vijana wengi waliojiandikisha pale arumeru wengi wako shuleni kwasasa, wengine vyuoni hivyo uwezekano wa kukosa kura ni mkubwa
pia ukiangalia mahudhurio na aina ya ushabiki wa kampeni za CHADEMA, ni dhahiri kuwa wapiga kura wengi wa chama hicho ni vijana.
Ni katika mtazamo huo ambamo changamoto inayojitokeza ni kuwa vijana wengi wenyeji wa Arumeru Mashariki hawakujiandikisha kupiga kura katika kata za jimbo hilo.
Wengi wamejiandikisha katika maeneo wanakoendesha shughuli zao za kujikimu kimaisha, ambazo ni Mererani, kwenye mgodi wa Tanzanite, eneo lililopo Jimbo la Simanjiro, linaloongozwa na Christopher ole Sendeka. Mbali na Mererani, vijana wengi wa jimbo hilo wamejiandikisha kupiga Arusha Mjini, wanakoendesha shughuli zao za kila siku hii kwa kiasi kikubwa itamwangusha bwana NASSARI, sababu ccm imejiwekeza katika kada mbalimbali za watu kuanzia watoto,vijana na wazee ambao kikukweli ndio hazina kubwa ya ccm
3.NGUVU KUBWA YA CCM ARUMERU
siamini ni kwa jinsi gani chadema inaweza shinda katika jimbo ambalo viongozi wote kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya ni ccm, hapa ni kujidanganya! lazima chadema wakubali kuwa pale ARUMERU sio pao,kwa mtaji huu ccm inaweza kucheza both macro and micro politics ilhali kujihakikishia ushindi mkubwa
4.PROPAGANDA ZA WAZI ZA CHADEMA
Chadema katika kampeni zake nyingi imekuwa ikimwaga propaganda nyingi sana kuhusu ccm, wananchi wa arumeru wamekuwa na ccm kwa muda mrefu kwahiyo wanajua fika yanayosemwa sio sahii! ingawa hata ccm imekuwa ikitoa propaganda kali na wengie wamesikika wakitoa matusi makali kwa viongozi wa chadema ila kuna msemo wa kiswahili unaosema "zimwi likujualo....."
kwa uchache hayo ni mambo yatakayoiangusha chadema tarehe 1 april 2012