Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
Thread hii ni maalum kwa mapicha na maelezo japo kwa muhtasari juu ya mali na miliki za maselebu wa bongo hasa wasanii wa muziki na filamu.
Tofauti na wenzetu wa nchi nyingine hata ndani ya Africa Mashiriki inaonekana wasanii wetu wana mafanikio finyu sana kiasi kuwa wengine wanaishia kuwa na fedha za kupiga pamba na kubadilishia mboga
Leo naanza na msanii maarufu na mwanadada gaidi ama Zay to the B...
Zay B: Nani anasema nimefulia?
Yawezekana amefulia kimuziki lakini sio kimali...
Kutoka Bongo mwana Hip Hop wa kike aliyeleta mapinduzi katika game ya muziki wa kizazi kipya kwa upande wa wasichana, Zainabu Lipangile a.k.a Zay B (PICHANI JUU) mwishoni mwa wiki iliyopita alidondoka ndani ya safu hii na kupiga stori mbili tatu ikiwemo kutangaza baadhi ya aseti anazomiliki hivi sasa kama alivyofanya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.
Ndani ya safu hii Zay B alisema kwamba wapo baadhi ya watu, wakiwemo wasanii wenzie wamekuwa wakivumisha maneno mitaani kwamba hivi sasa amefulia baada ya kupotea kwenye game kwa muda mrefu kitu ambacho amekikanusha, ndiyo sababu iliyomfanya atangaze mali zake.
Unajua watu wengine huwa wanakosa ishu za kuongea, mimi kutosikika siyo kwamba nimefulia, kuna ishu kibao nafanya zinazoniingizia kipato, kwanza muziki wa Bongo haulipi na umejaa majungu. Ningekuwa nimefulia ningeweza kujenga nyumba au kununua gari? Alihoji Zay B huku akionesha picha za nyumba yake zilizokuwa kwenye simu.
Mwanadada huyo alisema kwamba mjengo huo ameushusha pande za Buyuni, Pugu nje kidogo ya Dar es Salaam huku akimiliki gari aina ya Toyota Premio. Mbali na hayo pia nimesaini mkataba wa kufanya kazi ya muziki na Kampuni ya Butile Africa Group ya Afrika Kusini, watu wasifikiri nipo nipo tu, sijafulia kihiivyo,.
Hili ni jumba la kifahari la mwanadada ZAY B
Na huu ndio mchuma wake makini aina ya TOYOTA Premio
Tofauti na wenzetu wa nchi nyingine hata ndani ya Africa Mashiriki inaonekana wasanii wetu wana mafanikio finyu sana kiasi kuwa wengine wanaishia kuwa na fedha za kupiga pamba na kubadilishia mboga
Leo naanza na msanii maarufu na mwanadada gaidi ama Zay to the B...
Zay B: Nani anasema nimefulia?
Yawezekana amefulia kimuziki lakini sio kimali...
Kutoka Bongo mwana Hip Hop wa kike aliyeleta mapinduzi katika game ya muziki wa kizazi kipya kwa upande wa wasichana, Zainabu Lipangile a.k.a Zay B (PICHANI JUU) mwishoni mwa wiki iliyopita alidondoka ndani ya safu hii na kupiga stori mbili tatu ikiwemo kutangaza baadhi ya aseti anazomiliki hivi sasa kama alivyofanya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.
Ndani ya safu hii Zay B alisema kwamba wapo baadhi ya watu, wakiwemo wasanii wenzie wamekuwa wakivumisha maneno mitaani kwamba hivi sasa amefulia baada ya kupotea kwenye game kwa muda mrefu kitu ambacho amekikanusha, ndiyo sababu iliyomfanya atangaze mali zake.
Unajua watu wengine huwa wanakosa ishu za kuongea, mimi kutosikika siyo kwamba nimefulia, kuna ishu kibao nafanya zinazoniingizia kipato, kwanza muziki wa Bongo haulipi na umejaa majungu. Ningekuwa nimefulia ningeweza kujenga nyumba au kununua gari? Alihoji Zay B huku akionesha picha za nyumba yake zilizokuwa kwenye simu.
Mwanadada huyo alisema kwamba mjengo huo ameushusha pande za Buyuni, Pugu nje kidogo ya Dar es Salaam huku akimiliki gari aina ya Toyota Premio. Mbali na hayo pia nimesaini mkataba wa kufanya kazi ya muziki na Kampuni ya Butile Africa Group ya Afrika Kusini, watu wasifikiri nipo nipo tu, sijafulia kihiivyo,.
Hili ni jumba la kifahari la mwanadada ZAY B
Na huu ndio mchuma wake makini aina ya TOYOTA Premio