Elections 2010 Zijue Halmashauri zitakazoongozwa na Chadema

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Halmashauri nane nchini zitaongozwa na vyama vya upinzani baada ya kupata viti vingi vya udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa wiki iliyopita.
Halmashauri hizo ni Karatu, Manispaa ya Moshi, Kigoma Mjini, Moshi Vijijini, Ukerewe, Jiji la Mwanza, Kasulu na Mbulu.
MWANZA
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitaliongoza Jiji la Mwanza linaloundwa na majimbo ya Ilemela na Nyamagana kufuatia kushinda kata 11 dhidi ya kata nane zilizochukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Uchaguzi katika kata za Mirongo na Mkuyuni uliahirishwa hadi baadaye. Hata hivyo, matokeo yake hayawezi kusababisha athari yoyote kwa kuwa hata kama CCM itashinda itakuwa na viti 10 na isitoshe kata hizo inasemekana ni ngome za Chadema.
KARATU
Katika matokeo ya udiwani Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilishinda halmashauri ya Karatu kwa kupata kata 10 na kata nne kuchukuliwa na Chama Cha mapinduzi (CCM).
UKEREWE
Katika Jimbo la Ukerewe, Chadema imefanikiwa kupata viti 13 kati ya 24 vya udiwani hali inayokiwezesha kuongoza halmashauri hiyo, CCM imepata viti 10 huku CUF ikiwa na kiti kimoja.
KiGOMA MJINI
Chadema imeshinda katika kata 10 wakati CCM imeshinda katika kata tisa.
JIMBO LA MOSHI MJINI
Chadema italiongoza jimbo la Moshi Mjini baada ya kupata kata 17 kati ya kata 21. CCM imepata kata nne.
MOSHI VIJIJINI
Halmashauri ya Moshi Vijijini inayoundwa na majimbo ya Moshi Vijijini na Vunjo, itaongozwa na Chadema kwa kushirikiana na TLP baada ya kupata viti 16 dhidi ya 15 za CCM.
Katika Jimbo la Moshi Vijijini CCM ilipata kata tisa, Chadema kata saba na TLP sifuri wakati katika Jimbo la Vunjo TLP ilipata kata saba, Chadema kata mbili na CCM kata sita.
KASULU
Halmashauri ya Kasulu pia imekwenda kwa upinzani uliopata madiwani 14 dhidi ya madiwani 11 wa CCM. Halmashauri hiyo itaongozwa kwa pamoja kati ya Chadema kilichopata viti madiwani wane na NCCR-Mageuzi kilichopata madiwani 10.
MBULU
Halmashauri ya Mbulu itaongozwa na Chadema baada ya kushinda kata 17 dhidi ya kata 15 zilizochukuliwa na CCM.
ARUSHA
Hata hivyo, katika Jimbo la Arusha Mjini huenda likaongozwa kwa mseto baada ya Chadema kupata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10. Kwa kuwa Chadema kilishinda ubunge na mbunge ni sehemu ya madiwani, hivyo chama hicho na TLP vitakuwa na madiwani 10 sawa na CCM hivyo kuongoza kwa mseto.
Hata hivyo, idadi ya madiwani wa viti maalum inaweza kuamua ni chama kipi kiongoze halmashauri hiyo. Chadema kimepata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10.
 
Ubungo na Kawe zinfanya manispaa moja ya kinondoni, sijajua Chadema wamepata madiwani wangapi.wenye data atujuze pls.
 
Halmashauri nane nchini zitaongozwa na vyama vya upinzani baada ya kupata viti vingi vya udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa wiki iliyopita.
Halmashauri hizo ni Karatu, Manispaa ya Moshi, Kigoma Mjini, Moshi Vijijini, Ukerewe, Jiji la Mwanza, Kasulu na Mbulu.
MWANZA
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitaliongoza Jiji la Mwanza linaloundwa na majimbo ya Ilemela na Nyamagana kufuatia kushinda kata 11 dhidi ya kata nane zilizochukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Uchaguzi katika kata za Mirongo na Mkuyuni uliahirishwa hadi baadaye. Hata hivyo, matokeo yake hayawezi kusababisha athari yoyote kwa kuwa hata kama CCM itashinda itakuwa na viti 10 na isitoshe kata hizo inasemekana ni ngome za Chadema.
KARATU
Katika matokeo ya udiwani Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilishinda halmashauri ya Karatu kwa kupata kata 10 na kata nne kuchukuliwa na Chama Cha mapinduzi (CCM).
UKEREWE
Katika Jimbo la Ukerewe, Chadema imefanikiwa kupata viti 13 kati ya 24 vya udiwani hali inayokiwezesha kuongoza halmashauri hiyo, CCM imepata viti 10 huku CUF ikiwa na kiti kimoja.
KiGOMA MJINI
Chadema imeshinda katika kata 10 wakati CCM imeshinda katika kata tisa.
JIMBO LA MOSHI MJINI
Chadema italiongoza jimbo la Moshi Mjini baada ya kupata kata 17 kati ya kata 21. CCM imepata kata nne.
MOSHI VIJIJINI
Halmashauri ya Moshi Vijijini inayoundwa na majimbo ya Moshi Vijijini na Vunjo, itaongozwa na Chadema kwa kushirikiana na TLP baada ya kupata viti 16 dhidi ya 15 za CCM.
Katika Jimbo la Moshi Vijijini CCM ilipata kata tisa, Chadema kata saba na TLP sifuri wakati katika Jimbo la Vunjo TLP ilipata kata saba, Chadema kata mbili na CCM kata sita.
KASULU
Halmashauri ya Kasulu pia imekwenda kwa upinzani uliopata madiwani 14 dhidi ya madiwani 11 wa CCM. Halmashauri hiyo itaongozwa kwa pamoja kati ya Chadema kilichopata viti madiwani wane na NCCR-Mageuzi kilichopata madiwani 10.
MBULU
Halmashauri ya Mbulu itaongozwa na Chadema baada ya kushinda kata 17 dhidi ya kata 15 zilizochukuliwa na CCM.
ARUSHA
Hata hivyo, katika Jimbo la Arusha Mjini huenda likaongozwa kwa mseto baada ya Chadema kupata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10. Kwa kuwa Chadema kilishinda ubunge na mbunge ni sehemu ya madiwani, hivyo chama hicho na TLP vitakuwa na madiwani 10 sawa na CCM hivyo kuongoza kwa mseto.
Hata hivyo, idadi ya madiwani wa viti maalum inaweza kuamua ni chama kipi kiongoze halmashauri hiyo. Chadema kimepata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10.

Ahsante kwa kutujuza, ila nakukumbusha kuwa umesahau manispaa ya musoma ambako nyinyiemu iliambulia kata mbili tu za udiwani.
 
Ahsante kwa kutujuza, ila nakukumbusha kuwa umesahau manispaa ya musoma ambako nyinyiemu iliambulia kata mbili tu za udiwani.
Ni kweli ongeza na Musoma. Matokeo haya ni funzo kubwa kwa majimbo yale ambayo ni masikini sana kama huko Tunduru,Kilwa,Singida nk kuwa kuikumbatia CCM ni kuukubali umasikini wa kudumu.
Muda mchache ujao halmashauri hizi zitakuwa kama ilivyokuwa Karatu kimaendeleo. Karatu ubadhilifu umepigwa vita kwa kiwango cha juu sana kiasi cha madiwani kugoma kulipia gharama za malazi na chakula kwa maafisa wa ziara ya makamu wa Rais kwa vile tayari walishalipwa na ofisi yao huko walikotoka. Ni halmashauri gani inayoongozwa na CCM inaweza kuthubutu kufanya hivyo?
 
Halmashauri nane nchini zitaongozwa na vyama vya upinzani baada ya kupata viti vingi vya udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa wiki iliyopita.
Halmashauri hizo ni Karatu, Manispaa ya Moshi, Kigoma Mjini, Moshi Vijijini, Ukerewe, Jiji la Mwanza, Kasulu na Mbulu.
MWANZA
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitaliongoza Jiji la Mwanza linaloundwa na majimbo ya Ilemela na Nyamagana kufuatia kushinda kata 11 dhidi ya kata nane zilizochukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Uchaguzi katika kata za Mirongo na Mkuyuni uliahirishwa hadi baadaye. Hata hivyo, matokeo yake hayawezi kusababisha athari yoyote kwa kuwa hata kama CCM itashinda itakuwa na viti 10 na isitoshe kata hizo inasemekana ni ngome za Chadema.
KARATU
Katika matokeo ya udiwani Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilishinda halmashauri ya Karatu kwa kupata kata 10 na kata nne kuchukuliwa na Chama Cha mapinduzi (CCM).
UKEREWE
Katika Jimbo la Ukerewe, Chadema imefanikiwa kupata viti 13 kati ya 24 vya udiwani hali inayokiwezesha kuongoza halmashauri hiyo, CCM imepata viti 10 huku CUF ikiwa na kiti kimoja.
KiGOMA MJINI
Chadema imeshinda katika kata 10 wakati CCM imeshinda katika kata tisa.
JIMBO LA MOSHI MJINI
Chadema italiongoza jimbo la Moshi Mjini baada ya kupata kata 17 kati ya kata 21. CCM imepata kata nne.
MOSHI VIJIJINI
Halmashauri ya Moshi Vijijini inayoundwa na majimbo ya Moshi Vijijini na Vunjo, itaongozwa na Chadema kwa kushirikiana na TLP baada ya kupata viti 16 dhidi ya 15 za CCM.
Katika Jimbo la Moshi Vijijini CCM ilipata kata tisa, Chadema kata saba na TLP sifuri wakati katika Jimbo la Vunjo TLP ilipata kata saba, Chadema kata mbili na CCM kata sita.
KASULU
Halmashauri ya Kasulu pia imekwenda kwa upinzani uliopata madiwani 14 dhidi ya madiwani 11 wa CCM. Halmashauri hiyo itaongozwa kwa pamoja kati ya Chadema kilichopata viti madiwani wane na NCCR-Mageuzi kilichopata madiwani 10.
MBULU
Halmashauri ya Mbulu itaongozwa na Chadema baada ya kushinda kata 17 dhidi ya kata 15 zilizochukuliwa na CCM.
ARUSHA
Hata hivyo, katika Jimbo la Arusha Mjini huenda likaongozwa kwa mseto baada ya Chadema kupata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10. Kwa kuwa Chadema kilishinda ubunge na mbunge ni sehemu ya madiwani, hivyo chama hicho na TLP vitakuwa na madiwani 10 sawa na CCM hivyo kuongoza kwa mseto.
Hata hivyo, idadi ya madiwani wa viti maalum inaweza kuamua ni chama kipi kiongoze halmashauri hiyo. Chadema kimepata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10.

Ongezea na Hanang' kule alikoshinda mary nagu halmashauri inaundwa na chadema:yield:
 
Nina wasiwasi na Moshi Vijijini. Mzee wa kiraracha anaweza kulalia ccm
 
Kwa Halmashauri ya Arusha Mjini, uwezekano ni mkubwa wa kuongozwa na CHADEMA, sababu madiwani wa viti maalum wanapatikana kutegemeana na idadi ya kura za mgombea ubunge. kwa vile Arusha Mjini mgombea ubunge wa CHADEMA alipata kura 56,196 (58.3%) dhidi ya kura 39,362 (38.8%) alizopata mgombea wa CCM, yaani tofauti ya kura 18,736 hivyo CHADEMA itatoa madiwani wengi wa viti maalum na hivyo kupelekea kuwa na madiwani wengi na hivyo Halmashauri ya Arusha mjini itakuwa chini ya CHADEMA.

Hali hii inaweza kutokea hata katika majimbo mengine ambayo mgombea wa ubunge wa CHADEMA ameshinda kwa tofauti ya kura nyingi na kuna tofauti ndogo ya madiwani kati ya CCM na CHADEMA kama Hai na mbozi
 
Nadhani hilo ni jambo jema kwa halmashauri kadhaa kuchukuliwa na wapinzani ili tuone uongozi wao unakuwaje na kama wanaweza kuondoa uozo uliopo kwenye halmashauri zetu.
ila ninavyofahamu mimi chama kinachoongoza kupata madiwani wengi katika halmashauri ndio humtoa meya na haihesabiwi kama upinzani au chama tawala.vyama vyote vinauwanja sawa hivyo basi halmashauri ya moshi vijijini itaongozwa na ccm sababu ndio imepata viti vingi
 
Halmashauri nane nchini zitaongozwa na vyama vya upinzani baada ya kupata viti vingi vya udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa wiki iliyopita.
Halmashauri hizo ni Karatu, Manispaa ya Moshi, Kigoma Mjini, Moshi Vijijini, Ukerewe, Jiji la Mwanza, Kasulu na Mbulu.
MWANZA
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitaliongoza Jiji la Mwanza linaloundwa na majimbo ya Ilemela na Nyamagana kufuatia kushinda kata 11 dhidi ya kata nane zilizochukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Uchaguzi katika kata za Mirongo na Mkuyuni uliahirishwa hadi baadaye. Hata hivyo, matokeo yake hayawezi kusababisha athari yoyote kwa kuwa hata kama CCM itashinda itakuwa na viti 10 na isitoshe kata hizo inasemekana ni ngome za Chadema.
KARATU
Katika matokeo ya udiwani Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilishinda halmashauri ya Karatu kwa kupata kata 10 na kata nne kuchukuliwa na Chama Cha mapinduzi (CCM).
UKEREWE
Katika Jimbo la Ukerewe, Chadema imefanikiwa kupata viti 13 kati ya 24 vya udiwani hali inayokiwezesha kuongoza halmashauri hiyo, CCM imepata viti 10 huku CUF ikiwa na kiti kimoja.
KiGOMA MJINI
Chadema imeshinda katika kata 10 wakati CCM imeshinda katika kata tisa.
JIMBO LA MOSHI MJINI
Chadema italiongoza jimbo la Moshi Mjini baada ya kupata kata 17 kati ya kata 21. CCM imepata kata nne.
MOSHI VIJIJINI
Halmashauri ya Moshi Vijijini inayoundwa na majimbo ya Moshi Vijijini na Vunjo, itaongozwa na Chadema kwa kushirikiana na TLP baada ya kupata viti 16 dhidi ya 15 za CCM.
Katika Jimbo la Moshi Vijijini CCM ilipata kata tisa, Chadema kata saba na TLP sifuri wakati katika Jimbo la Vunjo TLP ilipata kata saba, Chadema kata mbili na CCM kata sita.
KASULU
Halmashauri ya Kasulu pia imekwenda kwa upinzani uliopata madiwani 14 dhidi ya madiwani 11 wa CCM. Halmashauri hiyo itaongozwa kwa pamoja kati ya Chadema kilichopata viti madiwani wane na NCCR-Mageuzi kilichopata madiwani 10.
MBULU
Halmashauri ya Mbulu itaongozwa na Chadema baada ya kushinda kata 17 dhidi ya kata 15 zilizochukuliwa na CCM.
ARUSHA
Hata hivyo, katika Jimbo la Arusha Mjini huenda likaongozwa kwa mseto baada ya Chadema kupata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10. Kwa kuwa Chadema kilishinda ubunge na mbunge ni sehemu ya madiwani, hivyo chama hicho na TLP vitakuwa na madiwani 10 sawa na CCM hivyo kuongoza kwa mseto.
Hata hivyo, idadi ya madiwani wa viti maalum inaweza kuamua ni chama kipi kiongoze halmashauri hiyo. Chadema kimepata madiwani 8, TLP 1 na CCM 10.

na hizi ndio halamashauri ambazo zitakua kwa kasi katika miaka hii mitano
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom