Ziara za Lowassa na coverage anazopewa, ni utetezi?

fige

JF-Expert Member
Jul 4, 2010
376
61
Wiki hii nzima magazetini na hapa kwetu jf pametawaliwa na minyukano mikubwa kati ya aidha wafuasi wa LW na wasio,au wana magamba na wengineo.

Kikubwa kilichoibua mjadala ni jinsi inavyosemekana mh. (ingawa hili neno silipendi) LW alivyowagalagaza magamba wakashindwa kumvua gamba mwenzao.Utetezi wenyewe ni jinsi yeye anavyodai kujaribu kushawishi kuwafukuza Richmond na kwamba Mkulu ndiye aliyemkwaza.

Nimetumia neno kujaribu kwa sababu kwa mtizamo wangu ushauri ule naweza kuuita geresha *****.Nasema hivyo kwa sababu kama alishauri mara moja hajatuonyesha kama aliendelea kusisitiza ushauri wake.
Pili ,inawezekana alikuwa anashauri jambo ambalo yeye mwenyewe haliamini na ndio maana lilikosa msisitizo.

Tatu, ni je baada ya kupuuzwa alichukua hatua gani ?Kama unaweza kupuuzwa katika jambo unaloamini kwa asilimia mia uko sahihi na usichukue hatua yeyote,je sisi wananchi tuendelee kukuamini ulikuwa na nia ya dhati ya kulisimamisha ?

Kwa mawazo yangu LW angejiuzulu kabla ya kuthumiwa kwa kutetea msimamo wake,nina hakika leo hii nchi nzima ingekuwa inampigia chapuo la uraisi hata kama ana mapungufu mengine makubwa.

Mnaomtetea LW pengine hamjaona alipodondokea mnataka kupatambua anapojaribu kusimamia.
Nawasilisha
 
Unapotosha! Richmond ni ya JK basiii! Ushahidi ni mdogo sana! Kama si ya JK kwa nini mpaka leo inawauzia Tanesco umeme kwa jina la Symbiono? EL halikuwa hana nguvu ya kumpinga boss wake kwa vyovyote vile alitekeleza kila boss wake aliliridhia over n out.
 
Kuna unapana wa jambo hilo tofauti na unavyofikiri wewe ki juu juu. Hilo lilikuwa jambo zito ambalo lilibeba kashfa iliyokuwa inamuhusu rais pia. Kukurupuka kama unayotaka wewe kungesababisha mtafaruku mkubwa na mgongano wa kuiutawala. Alichofanya EL ni kutumia busara ya hali ya juu kunusuru hali. Kumbuka alitaka kuvunja mkataba wa RICHMOND, Akampigia simu raisi kutaka ushauri. Akaambiwa asubiri rais anashauriana na makatibu wa wizara. Ungekuwa wewe ungefanya nini. Aliwajibika katika hali ya kuepusha pepo mchafu katika serikali yake.
 
Binafsi naona alichofanikiwa ni kumuumbua rafiki yake na si kujiokoa
 
Kuna unapana wa jambo hilo tofauti na unavyofikiri wewe ki juu juu. Hilo lilikuwa jambo zito ambalo lilibeba kashfa iliyokuwa inamuhusu rais pia. Kukurupuka kama unayotaka wewe kungesababisha mtafaruku mkubwa na mgongano wa kuiutawala. Alichofanya EL ni kutumia busara ya hali ya juu kunusuru hali. Kumbuka alitaka kuvunja mkataba wa RICHMOND, Akampigia simu raisi kutaka ushauri. Akaambiwa asubiri rais anashauriana na makatibu wa wizara. Ungekuwa wewe ungefanya nini. Aliwajibika katika hali ya kuepusha pepo mchafu katika serikali yake.
Mkuu aliyoyakwepa wakati ule kwa kutochukua hatua ndilo anguko lake
 
Mnajaza bure server ya JF, sasa wewe kama uliziona hizo thread za Lowasa humu JF ni kwa nini usingewajibu kwenye hizo thread? huu ni utoto.
Huo nao ni mtizamo na ndio demokarasia ya jf
 
Unapotosha! Richmond ni ya JK basiii! Ushahidi ni mdogo sana! Kama si ya JK kwa nini mpaka leo inawauzia Tanesco umeme kwa jina la Symbiono? EL halikuwa hana nguvu ya kumpinga boss wake kwa vyovyote vile alitekeleza kila boss wake aliliridhia over n out.
Kama anaweza kutekeleza kila kitu bila judgement hiyo ni hatari na akubaliane na masahibu yanayotokana na kukubali kila jambo.
 
Sielewi cheo cha sasa cha Edward Lowasa.

Kila taarifa ya habari TBC, lazima aonekane. Je yeye ni mbunge tu wa Monduli au ana cheo kingine kinachompa nguvu ya hizo ziara. Je yeye ndiye remote controller ya mtawala wa juu wa nchi?

Sielewi inakuwaje mtu ambaye si mwenyekiti wa chama wala kiongozi wa serikari apewe kipaumbele katika habari za kila siku?
 
ucjari makene,ni mambo ya kawaida tu kwa viongozi wa wananchi kupata nafasi kama zile ktk vyombo vya habari hususani TBC
 
Lowassa ni:

...Mbunge
...Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
...Waziri Mkuu Mstaafu.
...Mjumbe wa CC na NEC CCM.
...Mtanzania mwenye kuitakia mema nchi yake.

Hivyo, anastahili kupewa coverage ya kutosha na TBC.
 
Sielewi cheo cha sasa cha Edward Lowasa.
Kila taarifa ya habari TBC, lazima aonekane. Je yeye ni mbunge tu wa Monduli au ana cheo kingine kinachompa nguvu ya hizo ziara.
Je yeye ndiye remote controller ya mtawala wa juu wa nchi?
Sielewi inakuwaje mtu ambaye si mwenyekiti wa chama wala kiongozi wa serikari apewe kipaumbele katika habari za kila siku?

Your a great thinker mkuu..hizi ndizo threads zinazotakiwa kuletwa hapa JF watu wafikirie na kuweka kwenye wazi nini maana ya haya yote.Nimekuwa natazama sana siku za karibuni,jamaa anafanya ziara za kufa mtu,jana alikuwa Monduli tena ndani kabisa,nikashangaa leo namuona Dar pale sabasaba...halafu kitu kinachonisumbua sijui kama nipo ok!! HIVI LOWASA NI WAZIRI MSTAAFU au WAZIRI MKUU ALIYEJIUZULU..Maana kwasasa vituo vingi vya habari vinamtamka kama waziri mkuu mstaafu kitu ambacho sidhani kama ni sawa.Tukirudi kwenye mada,huyu jamaa anajua anachofanya,hili si jambo la kawaida na hebu tujiulize..

  1. Kwanini kipindi hiki?
  2. Kwanini bungeni hasemi na anakuwa msemaji sana akiwa uraiani kwasasa kuliko kipindi chochote?
  3. Kwanini kila sehemu ambapo anahisi kutakuwa na mkusanyiko wa watu au coverage ya vyombo vya habari lazima atie timu?
Kwahili tutambue moja ni maandalizi ya uchaguzi wa NEC 2012 na maandalizi ya kuutaka uraisi 2015 ambao hataupata hata kwa dawa..hata kama atashinda kwa T.B Joshua miaka yote iliyobaki kabla ya uchaguzi wa 2015...
 
Lowassa ni:

...Mbunge
...Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
...Waziri Mkuu Mstaafu.
...Mjumbe wa CC na NEC CCM.
...Mtanzania mwenye kuitakia mema nchi yake.

Hivyo, anastahili kupewa coverage ya kutosha na TBC.

Mkuu hapo kwenye red naomba ufafanuzi..hivi ni WAZIRI MKUU MSTAAFU au ALIYEJIUZULU....maana navyojua kustaafu ni kuacha kazi kwa mujibu wa sheria kwasababu ya umri au afya au kuchoka kazi...Huyu jamaa hayupo kwenye hizo sifa,yeye alitimuliwa kwa nguvu ya umma chini ya kamati teule....Naomba maelezo plz!!
 
Sielewi cheo cha sasa cha Edward Lowasa.
Kila taarifa ya habari TBC, lazima aonekane. Je yeye ni mbunge tu wa Monduli au ana cheo kingine kinachompa nguvu ya hizo ziara.
Je yeye ndiye remote controller ya mtawala wa juu wa nchi?
Sielewi inakuwaje mtu ambaye si mwenyekiti wa chama wala kiongozi wa serikari apewe kipaumbele katika habari za kila siku?

huyu ndiye rais ajae hivyo hakuna cha ajabu hapo!
 

Your a great thinker mkuu..hizi ndizo threads zinazotakiwa kuletwa hapa JF watu wafikirie na kuweka kwenye wazi nini maana ya haya yote.Nimekuwa natazama sana siku za karibuni,jamaa anafanya ziara za kufa mtu,jana alikuwa Monduli tena ndani kabisa,nikashangaa leo namuona Dar pale sabasaba...halafu kitu kinachonisumbua sijui kama nipo ok!! HIVI LOWASA NI WAZIRI MSTAAFU au WAZIRI MKUU ALIYEJIUZULU..Maana kwasasa vituo vingi vya habari vinamtamka kama waziri mkuu mstaafu kitu ambacho sidhani kama ni sawa.Tukirudi kwenye mada,huyu jamaa anajua anachofanya,hili si jambo la kawaida na hebu tujiulize..

  1. Kwanini kipindi hiki?
  2. Kwanini bungeni hasemi na anakuwa msemaji sana akiwa uraiani kwasasa kuliko kipindi chochote?
  3. Kwanini kila sehemu ambapo anahisi kutakuwa na mkusanyiko wa watu au coverage ya vyombo vya habari lazima atie timu?
Kwahili tutambue moja ni maandalizi ya uchaguzi wa NEC 2012 na maandalizi ya kuutaka uraisi 2015 ambao hataupata hata kwa dawa..hata kama atashinda kwa T.B Joshua miaka yote iliyobaki kabla ya uchaguzi wa 2015...

bcoz EL z the next president!
 
Back
Top Bottom