Ziara za CDM - Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Zanzibar

Mtaji wa CCM ni ujinga wa watanzania,ndio maana wana ngome ktk mikoa hiyo ambayo wanaongoza kwa ujinga na umaskini

kama mikoa hii ndiko kwenye ujinga na umaskini kwanini mmekimbia huko kaskazini kuja coast?
Au ujinga wetu ni kuwauzia maeneo mkajenga ili muweze kujisitiri na familia zenu? Wapwani kuwa wakarimu kuwakaribisha ndio mtutusi? Hivi mlitaka na sisi tuwe wabaguzi kama mlivyo kule kwenu kwamba ukiwa mgeni huuziwi eneo?
Hivi sisi wa pwani na wale mnao ua bibi zenu wenye macho mekundu ukidai ni wachawi na albino ili mpate utajiri nani ni mjinga? Kisha mmezoea pia kuwaita wa pwani ni washirikina bila kutoa ushahidi, kama ni great thinker, jiulize hivi, ulishawahi kusikia pwani wameua albino? Wameua vikongwe kwa imani za kishirikina?
 
Heshima kwako Gamba Jipya.

kwediembele ni kijiji kilicho ndani sana toka barabara kuu Dar - Tanga 40 km zipo bendera za CHADEMA,


Mkuu heshima mbele,

Nilipokuwa Dar nilipata fursa ya kutembelea maeneo ya kigamboni mji mwema, kuna vijana wana vitu wanaviita camps/gangs kuna bendera nyingi za us kuliko hata DC.
 
Mkuu haya mambo ya daftari la wapiga kura ndiyo yalifanya msije kuchukua majibu ya urais, usiangalie majina kwenye daftari, angalia watu wanaokwenda kwenye kituo na kupiga kura, kwa utafiti uliofanyika na shilika lisilo la kiserikali la proxy data limebaidi watu wa coast waliojitokeza kupiga kura ni asilimia 87, wakati kanda ya ziwa ilikuwa asilimia 51.

Asante, ngoja tuendelee kutumia ngome zetu.


Watu wasiojua hesabu utawajua tu. Ndugu yangu Gamba Jipya ni vema ufanye conclusion based on ABSOLUTE FIGURE ya wapiga kura kuliko RELATIVE FIGURE. Ni kwa sababu inawezekana mikoa ya Coast waliopiga kura ni watu 87,000 kati ya watu 100,000 waliojiandikisha thus making 87%, wakati Mwanza waliopiga kura ni 255,000 kati ya watu 500,000 waliojiandikisha, thus making 51%.

Na kama hesabu za wapiga kura kati ya Coast na Mwanza zitakuwa na nature kama hiyo, ni wazi hoja yako ni dhaifu. So katika masuala ya kujadili idadi ya wapiga kura base your arguments based on ABSOLUTE FIGURE.

TUENDELEE KUJADILIANA.
 
Hongera sana mkuu wangu,utatukanwa sana,lakini ukweli ndio huo,wanasema (wanaojifanya wana data) kuwa wajinga ndio mtaji wa ccm na kuwa mikoa ya kusini ndio wajinga hivyo wakaipa ccm ushindi. halafu hao hao walio na data feki wanasema kuwa wajinga hao ni sehemu tu ya werevu wa huko waliko werevu wasiopiga kura. hebu fikiria hoja kama hizo zinaashiria nini kama sio kuidhalilisha JF inayoaminika kuwa na great thinkers.wengi wao wanaishia matusi na kejeli.dalili ya kuishiwa hoja.
 
Kuwa na ngome ni jambo moja na kulinda ngome ni jambo la pili, ukweli ni kwamba huko ambako cdm wameweza kuwa na ngome awali ilikuwa ngome ya chama cha magamba ila kwa uzembe wa kutokulinda ngome wamejikuta wakipoteza.

Sasa kwa taarifa yako hizo ngome zilizosalia tumejipanga kuzivunja na kuzitwaa, labda mjipange upya lakini kwa team hii iliyopo tutawashinda bila ujanja.
 
Mkuu haya mambo ya daftari la wapiga kura ndiyo yalifanya msije kuchukua majibu ya urais, usiangalie majina kwenye daftari, angalia watu wanaokwenda kwenye kituo na kupiga kura, kwa utafiti uliofanyika na shilika lisilo la kiserikali la proxy data limebaidi watu wa coast waliojitokeza kupiga kura ni asilimia 87, wakati kanda ya ziwa ilikuwa asilimia 51.

Asante, ngoja tuendelee kutumia ngome zetu.


Watu wasiojua hesabu utawajua tu. Ndugu yangu Gamba Jipya is better ufanye conclusion based on ABSOLUTE FIGURE kuliko RELATIVE FIGURE. Inawezekana waliopiga kura mikoa ya Pwani ni watu 87,000 kati 100,000 waliojiandikisha thus making 87%. Na kwa upande wa mwanza inawezekana waliopiga kura ni watu 255,000 kati ya 500,000 thus making 51%.

Kama nature ya hesaba za waliojiandikisha na kupiga kura katika maeneo hayo zina behave hivyo ni wazi umefanya wrong conclusion.
So make conclusion base on ABSOLUTE FIGURE rather than RELATIVE FIGURE

TUENDELEE KUJADILIANA.
 
Dodoma, Singida, Tanga, Lindi na Mtwara ni mikoa iliyokuwa na shule zilifofanya vibaya zaidi ktk mtihani wa kidato cha nne mwaka jana (yaliyotolewa mwaka huu). Shule kutoka mikoa hiyo zilikuwa mojawapo ya shule 10 zilizofanya vibaya zenye wanafunzi zaid ya 40 na shule 10 zilizofanya vibaya zenye wanafunzi chini ya 40. Tatizo ni ufahamu, ni elimu. Hakuna ngome ya CCM sehemu ambazo watu wana mwamko wa elimu na ufahamu mkubwa wa jinsi nchi yetu invyoendeshwa. Kwakuwa matatizo ni mwalimu mzuri, huko nako ukombozi utafika tu- just a matter of time.
 
Hapa mitaa ya daraja mbili niko na dogo Godbless yeye yuko chakali amevuta na ile kitu ya huku.

Mzee ulijitambulisha kama mjibu hoja kwa hoja sasa akitokea wa kukutukana usihangaike naye wewe endelea kujibu hoja. Kwani ukiwa vitani na vikosi ishiri vya wapambanaji vikosi kumi na tano vikaangamizwa unatarajia nini kama si aidha kukimbia uwanja wa vita au vikosi vilivyosalia kuangamizwa kama vile vya mwanzo?
 
Watu wasiojua hesabu utawajua tu. Ndugu yangu Gamba Jipya is better ufanye Conclusion based on ABSOLUTE FIGURE rather than RELATIVE FIGURE. Inawezekana waliopiga kura mikoa ya Pwani ni watu 810,000 kati ya watu 1,000,000 thus making 87%. Na kwa upande wa Mwanza inawezekana waliopiga kura ni watu 2,550,000 kati ya watu 5,000,000 thus making 51%.

Na kama hesabu za wapiga kura za maeneo hayo zina behave hivyo ni wazi umefanya wrong conclusion. So take care while making making conlusion on numbers. Base on ABSOLUTE FIGURE rather than RELATIVE FIGURE.

TUENDELEE KUJADILIANA!
 
Hii mikoa ni ngome yetu, CDM hawakubaliki kabisa na uzuri ni kuwa hata wao wanalifahamu hili na ndiyo maana huwa hawaendi kwenye ngome hizi, hata ufunguzi wa matawi katika vyuo vilivyo maeneo hayo ni ndoto, ha hii ni over 20% ya kura Tanzania, Tunaingia 2015 tukiwa na mtaji wa kura milioni 5 za wanachama pamoja na asilimia 20% ya mikoa hii, jipangeni kwa 2025.

Walienda kuwapa pole wahanga wa maandamano Arusha.
Wakaenda kuwapa pole wahanga wa North Mara

Jiulize ni kwa nini hawajaenda kuwapa pole wahanga waliobomolewa nyumba na mabanda yao Znz?

Na kwa nini wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana waliikwepa sana mikoa hii?.

Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Zanzibar ni maji marefu.
Hahahahaaaa......! Kweli wewe ni "GAMBA JIPYA"
 
Chadema kitawafikia hadi huko msijali mbona mtapata ukombozi.. najua mnajivunia mikoa hiyo kwa kuwa iko nyuma sana kwa elimu ya uraia... nadhani mngejisifia kwa maendeleo kumbe umaskini uliokithiri... Huu upepo hauzuiliki ndugu!
 
Wananchi wa pemba pia wamekiri kua mkombozi pekee wa maendeleo ni chadema!source bbc juma haji duni sijamsikia tena baada ya cuf kuolewa na ccm
 
Hii mikoa ni ngome yetu, CDM hawakubaliki kabisa na uzuri ni kuwa hata wao wanalifahamu hili na ndiyo maana huwa hawaendi kwenye ngome hizi, hata ufunguzi wa matawi katika vyuo vilivyo maeneo hayo ni ndoto, ha hii ni over 20% ya kura Tanzania, Tunaingia 2015 tukiwa na mtaji wa kura milioni 5 za wanachama pamoja na asilimia 20% ya mikoa hii, jipangeni kwa 2025.

Walienda kuwapa pole wahanga wa maandamano Arusha.
Wakaenda kuwapa pole wahanga wa North Mara

Jiulize ni kwa nini hawajaenda kuwapa pole wahanga waliobomolewa nyumba na mabanda yao Znz?

Na kwa nini wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana waliikwepa sana mikoa hii?.

Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Zanzibar ni maji marefu.

mkuu inaonesha wewe si mwelewa wa mitihani.
waulize wote waliofaulu mitihani je walianza na maswali magumu au mrahisi.
na wale waliofeli nao swali hilohilo,ndipo na wewe ujipime na ujue ni kwa nini ulifeli darasani?
chadema wanamaliza mtihani dakika zikiwa hata nusu hazijaisha.ccm wamekaa darasani dakika zimeisha hawajajibu hata swali moja kwa sbb ya kuanza na swali gumu na mpaka leo hawajalipatia jibu.
ccm walianza na kuwafurahisha mafisadi.
chadema wanaanza na wananchi.
mpaka hapo utajua muda watakapo ingia znz,tanlindi na pwani watamaliza kazi kiulaiiini.
peopless powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr.
 
Back
Top Bottom