Ziara ya Hillary Clinton kuja: Picha na Matukio

bora aje aone mitambo yao bwana ni wapi ulisikia mwenye mali hapiti kukagua mali zake karibu mama na pia usisahau kumuamuru JK abinafsishe shirika la tanesco ili nalo limilikiwe na watu wa marekani tupate maisha mazuri kama new york ambako umeme kukatika ni kama jua kuanguka vile,pia usisahau kumtembelea na mama yake ghailan yule mliyemfunga umpe pole ya kuondokewa na mwanaye kipenzi ambaye hadi leo anaaamini mmemsingizia yeye alikuwa tu mpishi wa osama na si vinginevyo kwenye kupika mabomu ya nai!!
 
Kwa hiyo mkuu unataka kutueleza kuwa sisi TZ tayari tupo ktk mikono ya USA

Na si hivyo tu yaani tunabadilishana URANIUM kwa VYANDALUA hii kweli ni biashara kichaa,

Uko sahihi! Wasiwasi wangu hawa wakubwa wanaweza kutuvuruga vibaya sana maana wanatabia ya kung'ata na kupuliza. Na kwa nchi ambayo ina weak leadership na almost no-visionary kama ya kwetu we could well end up in a mess!
 
Hivi unafikiri kuna kinachoendelea hapa ambacho hakiwahusu hawa wanaomuabudu Lucifer!Hata thamani ya hela,uchumi wetu mpaka hali yako ya maisha wao ndo wanaamua,mgao uliopo ni wao wanasababisha halafu wanaleta mipango wapate hela
 
Mh..mitambo imetakasika baada ya wamarekani
kuichukua.sasa mbona bado twakatiwa umeme? Halafu hao wamerikan lini wameshinda tenda?
Na ilitangazwa lini?
Tuliyoyakataa dowans si ndo hayahaya ama?
 
Uko sahihi! Wasiwasi wangu hawa wakubwa wanaweza kutuvuruga vibaya sana maana wanatabia ya kung'ata na kupuliza. Na kwa nchi ambayo ina weak leadership na almost no-visionary kama ya kwetu we could well end up in a mess!
ishu sio weak leadership hata slaa angekua rais wa nchi hamna anaeweza kupinga america wakishataka lao lazima liwe. angalia nchi zinazoipinga nini kinawapata
 
Ndiyo maana wahuni wanajisemeaga! "Heri kuwa Mb.......Ulaya kuliko kuzaliwa......." Hawakukosea. Lakini mimi, Namshukuru Mungu kuniweka hai, tena ktk nch nzuri ya Tz. Ila BWANA awakemee mafisadi wote, akiwamo JK wao.
 
Ndiyo maana wahuni wanajisemeaga! "Heri kuwa Mb.......Ulaya kuliko kuzaliwa......." Hawakukosea. Lakini mimi, Namshukuru Mungu kuniweka hai, tena ktk nch nzuri ya Tz. Ila BWANA awakemee mafisadi wote, akiwamo JK wao.
 
Uko sahihi! Wasiwasi wangu hawa wakubwa wanaweza kutuvuruga vibaya sana maana wanatabia ya kung'ata na kupuliza. Na kwa nchi ambayo ina weak leadership na almost no-visionary kama ya kwetu we could well end up in a mess!

Mkuu kuna movie moja niliambiwa inazungumuzia hawa jamaaa ingawaje sijaiona. The confess of Economic. Mbinu yao ya kwanza ni kuingia kwa kiongozi wa kitaifa na kama akikubali (akiwa dhaifu) basi mambo yanaisha vizuri lakini akiwa ngangari wanarudi kwa wananchi kwa kuichonganisha serikali na wananchi ambapo huishi umwagaji wa damu na matakwa yao hukamilika. e.g DRC,Libya. Wakishindwa kabisa basi wanatafuta sababu na kukuvamia kama Iraq. Kwa hiyo hawa watu siyo wazuri kabisa na Tanzania kuna category tunayoangukia hapo juu. Kazi ipo dungu zangu.
 
Hapo umenena kweli, tutegemee kupata umeme lakini Uranium, Copper, Dhahabu, Diamond, Nickel na bila kusahau kitu ghali Tanzanite kubebwa kama njugu au maharage ya mbeya tena bila Taxes wala kupitia DIA au KIA ni juu kwa juu hadi akili itakapotuingia vizuri.
...Mi nadhani mama anakuja kukagua ka-mradi kao na mzee Bill sioni mantiki ya huyo mama eti kufanya ziara ya kukagua hiyo mitambo. Lazima watakuwa wanakuja ku-confirm kama deal iko poa. Nadhani hata G.W Bush alipokuja na mambo yake ya vyandarua vya mbu alitembela pia kale kamradi kake ka kuchimba nikel kule kabanga ngara. Nadhani hawa watu wanatumia vizuri kulala kwetu usingizi wa pono..
 
nawakubali wote mliochangia, kama tujuavo mzungu hawezi kukupa kitu cha bure.
kwa ufupi kuna gesi CH4 ambayo ni ghali na haihitaji kusafishwa tena makampuni mengi
tayari yapo tanzania kwa ajili hiyo,,kama viongozi watakuwa makini itasaidia kuongeza uchumi wa nchi,
kodi itakuwa kubwa itawezesha pato la taifa kuongezeka, maisha yataboreka.
kama kweli wanataka kuboresha umeme na kuongeza vyanzo vingine sio mbaya kuliko kuwaachia mafisadi kufaidi 10%.
kwa mnaoukumbuka wamarekani walitaka kuujenga uwanja wa ndege wa kigoma uwe wa kisasa kabisa,ili kusaidia madege yao kutua kwa ajili ya masuala ya kulinda amani Congo(tunajua wanaiba madini mle).tatizo serikali yetu ikasema wapewe hizo hela za kujenga wajenge wao marekani ikajitoa,.wangekubali tungefaidi uwanja. haya yetu macho kwa hawa wamarekani na nchini mwao vyuo vingi wanafundisha kiswahili kwa kasi ili waje wakae nchini mwetu,mda sii mrefu tutatawaliwa sio kiuchumi tu hata kisiasa.
 
inaonyesha syimbio company ni ya halali,hapo naona hatujapigwa changa la macho
Kweli wewe ni Mtorii sijui umetumia kigezo gani kujua kama hiyo kampuni ni ya ukweli. Wewe una utumwa wa kiakili, wewe ukiona mzungu tu unamuona mkweli
 
Mh..mitambo imetakasika baada ya wamarekani
kuichukua.sasa mbona bado twakatiwa umeme? Halafu hao wamerikan lini wameshinda tenda?
Na ilitangazwa lini?
Tuliyoyakataa dowans si ndo hayahaya ama?
swala la tenda usiliongelee kabisaa
mmarekani anapotaka kitu haitaji mambo ya tenda kama unataka kumpa tenda basi urudishe vyandaluwa vyake alivyokupa bure,urudishe dawa zake za kutuliza ukimwi na mengine yasiyokuwa na tija sana kwa uchumi wa taifa letu
 
...Mi nadhani mama anakuja kukagua ka-mradi kao na mzee Bill sioni mantiki ya huyo mama eti kufanya ziara ya kukagua hiyo mitambo. Lazima watakuwa wanakuja ku-confirm kama deal iko poa. Nadhani hata G.W Bush alipokuja na mambo yake ya vyandarua vya mbu alitembela pia kale kamradi kake ka kuchimba nikel kule kabanga ngara. Nadhani hawa watu wanatumia vizuri kulala kwetu usingizi wa pono..

Bush alikuja kubadilishana KIGAMBONI na VYANDALUWA
Hii nchi bana
 
mama anaingia na JK huyooooooooooooooooo mkutano wa Sadeki kusini??!! mama kukagua mitambo LE na AR saaaaaaaafi!!

Kuna kitu kimoja watu hawajagundua kuhusu Kikwete - kila anapokuja mgeni 'mahsusi' yeye huondoka ili hapo mbeleni kama kutatokea utata na yeye atalalamika na kusema 'hajui'. Mfano, alipokuja Al-adawi Kikwete aliondoka na tunaambiwa bwana huyo alienda Ikulu kwa mazungumzo na Makamu wa Rais! Sasa anakuja Hillary Clinton kukagua mitambo (imagine Hillary anatoka State dept USA kukagua mitambo ya bei ndogo kabisa Ubungo!!!) Rais wetu huyoooo South.

Ndio, najua Ikulu watasema anahudhuria mkutano wa SADC, je ni kweli Rais wetu anaependa kupiga picha na mastaa hakujuwa kama Hillary anakuja wakati wa mkutano wa SADC na hivyo kuagiza Foreign Affairs wampe tarehe nyingine huyu mama? Maana Kikwete anakosa 'great opportunity' ya kupiga picha na one of the 'original celebraties wa kisiasa'!
 
Wajuaa wanatoa pesa nyingi sana kwenye bajeti na miradi mingine!!hilo ni onyo kwa JK na serikali yake kuacha ufisadi kwa faida maendeleo ya wananchi!!wameamua kutusaidia kuinunua iuze umeme bei ndg sana....ili Tanesco imudu kusambaza umeme pia mpango upo kununua iptl kumaliza ufisadi sekta ya nishati na madini!!! wameamua kutusaidia......tuna shida lakini wizi na tamaa umetujaa!!!RA na EL watalipwa chao waachane na mitambo ile!!!kumbuka walikopa kwa el adawi!!
Yetu macho mwaka huu tunalo Watanzania, tutakimbilia wapi????????????
 
Cha msingi mi navyoona inabidi tuadopt kwa kasi hii hali, tutumie vizuri chance zozote zitakazo jitokeza ili tuweze kuendelea. Ukiangalia kwa makini bado tuko vizuri kwani sisi bado ni sawa na kinyonga, utatukuta tupo na Rusia (na Miradi ya Uranium), China( Wezi wa kimya kimya) na hawa jamaa zetu USA (wezi wa kujitangaza) na South Africa. Hawa wote wanafukuzia dili hapa kwetu, kwa hiyo ni mhimu tuzichange karata vizuri ili likija kulipuka walau tubaki na utaalamu wa kujitegemea.
 
Back
Top Bottom