ZEC: Sheria ya Uchaguzi Zanzibar inaruhusu mtu kujitoa, si chama

Inawezekana imeenda shule, lakini suala la msingi linabakia palepale. Je Tamko la Jecha kufuta uchaguzi ni halali kikatiba na kisheria?
Kama si halali, hii yote inayofuata, kutangaza marudio ya uchaguzi ni kuzidi kuongeza tatizo.
Tatizo zaidi lipo hapa.
Je ZEC (au Jecha) ina mamlaka kisheria ya kufuta au kutengua matokeo ya uchaguzi? Matokeo ambayo ZEC na wasimamizi wa uchaguzi majimboni walishayatangaza, kuyabandika kutani na kuwakabidhi washindi(wateule) vyeti vya ushindi?

Link ZEC: Sheria ya Uchaguzi Zanzibar inaruhusu mtu kujitoa, si chama
Tume haina mamlaka hayo, hayo ni mamlaka ya Mahakama baada ya kupelekewa malalamiko na kuyasikiliza na kuyatolea maamuzi kwa haki
 
Apo katiba inavyunjwA hadharani na watu wanetea kana kwamba wapo sahihi iko wapi Tanzania huru yenye kueshimu katiba huu uchama ni mbaya sana ndo umetufikisha apa Leo tunaitaji tume huru
 
Ni kweli Zanzibar bila CUF haiwezikani na ndiyo maana ccm wanalazimisha USHIRIKI wa CUF kwenye uchaguzi wao japo kuwa wenyewe CUF hawako tayari
 
Kwa nini CUF na maalim Seif wasiende mahakamani kupinga karatasi za kupigia kura kuwekwa picha ya mtu ambaye hashiriki uchaguzi.
Mtu anapojitoa kutoshiriki hawezi kulazimishwa.
Uchaguzi utakua ni batili kwa kuweka majina na picha za watu ambao hawakushiriki uchaguzi.

Leo nimeshangaa kumbe tume ya uchaguzi ni huru.
Mbona misingi ya kuundwa kwake sio huru.
Tume imeundwa na Rais wa chama Tawala halafu inaitwa huru na haiingiliwi.

Wazanzibar mtapanga wenyewe kwa kuwa mahakama zipo.
 
Wajumbe wa ZEC wako nane.Hao wawili ndio wameleta longolongo.Sita hawana tatizo.Na sheria za maamuzi kwenye vikao ni wengi ndio wanashinda.Hao wawili ni asilimia 25 tu ya wajumbe wa ZEC.Asilimia 75 WAKO VIZURI WAKO PAMOJA NA JECHA.Hao wawili hawajitambui wa ZEC wanajitambua zaidi kama wana CUF.
Acha maneno mengi wajumbe sita in wa ccm
 
hii dhulma hii ni bora wakatangaza tu kuwa wanataka CCM ishinde baasi, hakuna haja ya kuharibu mabilioni kwa uchaguzi hewa
 
uchaguzi.jpg


TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR IMEKATAA KUONDOA MAJINA NA PICHA ZA WAGOMBEA WA VYAMA VILIVYOKATAA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA MARUDIO - SASA WANAIJUA SHERIA ILA MAMLAKA YA JECHA KUFUTA UCHAGUZI HAWAFUATI SHERIA!

"Habari zinaarifu kuwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar( ZEC) imegoma kuondoa picha za wagombea Urais, Udiwani na Uwakilishi kutoka vyama vilivyotangaza kutoshiriki uchaguziwa marudio, ikiwemo jina na picha Maalim Seif Sharif Hamad. Hilo lilifahamika jana mjini Unguja baada ya kigogo mmoja wa ZEC ambaye hakuwa tayari kutaja jina kusema kuwa sheria hazimruhusu mgombea yeyote kujitoa mwenyewe kwa utashi wake binafsi.

Kiongozi huyo alisema kwa mujibu wa kifungu cha 36 cha sheria ya uchaguzi namba 11 ya mwaka 1984, mgombea hawezi kujiondoa kwa utashi wake baada ya Tume kukamilisha kazi ya uteuzi ambayo ilifanyika kabla ya Oktoba 25 mwaka jana. "Ieleweke kwamba mgombea urais anaweza kujiondoa katika kinyang'anyiro kwa kuwasilisha taarifa za maandishi yeye mwenyewe ofisi za ZEC kabla ya saa 10 jioni ya siku ya uteuzi." Alisema ofisa huyo akinukuu kifungu cha katiba."

Chanzo : Mwandishi Wetu

Zanzibar Post
 
Back
Top Bottom