ZEC: Sheria ya Uchaguzi Zanzibar inaruhusu mtu kujitoa, si chama

MKWEPA KODI

JF-Expert Member
Nov 28, 2015
28,707
71,003
Tume ya uchaguzi Zanzibar imekataa kuondoa jina la Maalim Seif kwenye uchaguzi wa marudio zanzibar utakaofanyika hapo march 20 mwaka huu

Chanzo: Magazeti ya leo

Siku za hivi karibuni CUF ilitoa tamko la kua CUF kujitoa uchaguzi wa marudio zanzibar.

Tamko lile ni batili kwa mujibu wa kifungu cha 28 cha sheria ya uchaguzi ya Zanzibar AMBACHO KINATAMBUA MTU KUJITOA NA SI CHAMA KUJITOA katika uchaguzi majina yakishapitishwa na tume. CUF walichokifanya ni kinyume cha sheria.

Soma hapo sheria nzima nimeweka. CUF wamefanya makosa mengine matano ya kisheria zaidi ya hili ila siweki silipwi kwa kazi hiyo.Ila hilo tu la kutoa tamko la kujitoa ni GRAVE LEGAL MISTAKE NUMBER ONE.

Matano yaliyobaki nabaki nayo

CHECK: http://zec.go.tz/en/wp-content/uploads/2015/08/Kanuni.pdf
 
Huu mziki unaendelea kubadilika midundo. .

Je, Sheria inalizungumziaje hili swala? Kwanini hawa wanang'ang'ania CUF kuwepo. ?
Hapa wataanza kuleta doubts bila sababu za msingi. ...
Busara itumike na sio mabavu. ...
Neno busara hapo sahau wao wanacho taka ni ushindi,ccm ni sheedah
 
Hiyo exercise haitobadilisha ballot papers yaani hazitoprintiwa upya! Ballot papers zilezile ndio zitahusika on 20th March! Hata kama mgombea kafariki halitofutwa jina lake
 
Hiyo exercise haitobadilisha ballot papers yaani hazitoprintiwa upya! Ballot papers zilezile ndio zitahusika on 20th March! Hata kama mgombea kafariki halitofutwa jina lake
Una maanisha karatasi za kupigia kura zilikuwa nyingi kiasi hicho? Hivi asilimia ngapi ya waliojiandikisha walijitokeza kupiga kura?
 
Daa sasa wanamlazimisha mtu kugombea wakati hataki, hii siasa bongo ni jipu
Hahaaa.. Hii nchi ni jipu ati.. Mpaka ije itumbuliwe na nchi kama Nigeria ndipo itakuwa sawa. Sasa mtu hataki kula chakula ya nini kumburuza kwenye mavumbi kumpeleka mezani ili ale..? Kuna nini mmeweka kwenye chakula..?? Nyie fanyeni uchaguzi wenu bana. Hapa naona Tanzania ya kuwekewa vikwazo inatunyemelea..!!!
 
Back
Top Bottom