Orijino Komedi walilia nauli
Tukio hilo lilitokea Novemba 11 mwaka huu ,Oysterbay jijini Dar es Salaam, katika viunga vya Club hiyo ambayo iliteketea kwa moto hivi karibuni.
Komedi walifika katika eneo hilo kwa ajili ya kurekodi picha za kipindi chao lakini waliacha jukumu hilo na kujichanganya kwenye mkutano wa waandishi wa habari na uongozi wa Club Maisha uliokuwa ukiendelea.
Wasanii wa kundi hilo waliotinga kiaina kwenye mkutano huo ni Emanuel Mugaya Masanja, Isaya Mwakilasa Wakuvwanga, Joseph Shamba Vengu, Alex Challamilah McRaegan na Lucas Mhuvile Joti.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wasanii hao walivamia mkutano huo ambapo Masanja ndiye aliyekuwa wa kwanza kupenya na kwenda kukaa kwenye safu ya mapaparazi hali iliyozua mshangao.
Baada ya mkutano kwisha Masanja alimzukia mmiliki huyo Hellen Sweya na kuomba nauli ili yeye na wenzake watimue kutoka kwenye mkutano huo.
Hata hivyo, mwanamama huyo alimjibu kuwa, hawezi kumpa nauli kwa vile hali ni mbaya na hakuwa amemwita kwenye mkutano huo.
Ndipo Masanja alipoamua kukomaa: Nimejiandikisha bwana, sijaalikwa kivipi, sasa mimi sina nauli, nipe niondoke zangu.
Akajibiwa: We Masanja usilete utani hapa. Kama ulialikwa hapa wewe ni wandishi wa chombo gani?
Hata hivyo, mchekeshaji huyo anayetumia nguvu kuchekesha, alizidi kukomaa kutaka apewe nauli ambapo safari hii alikwenda kuongea na bosi mwingine ambaye naye alimchukulia kama alikuwa akiigiza tu.
Wakati Masanja akikomaa kutaka apewe fea msanii mwenzake, Vengu alifika na kuongeza nguvu ya kudai masurufu hayo.
Mpaka mapaparazi wetu wanaondoka ukumbini hapo, haikujulikana kama wasanii hao walipewa nauli au la!
Mmefulia haooooooooooo!!!!!!!!!!!
Source: http://www.globalpublisherstz.com/2009/11/13/orijino_komedi_walilia_nauli.html
Tukio hilo lilitokea Novemba 11 mwaka huu ,Oysterbay jijini Dar es Salaam, katika viunga vya Club hiyo ambayo iliteketea kwa moto hivi karibuni.
Komedi walifika katika eneo hilo kwa ajili ya kurekodi picha za kipindi chao lakini waliacha jukumu hilo na kujichanganya kwenye mkutano wa waandishi wa habari na uongozi wa Club Maisha uliokuwa ukiendelea.
Wasanii wa kundi hilo waliotinga kiaina kwenye mkutano huo ni Emanuel Mugaya Masanja, Isaya Mwakilasa Wakuvwanga, Joseph Shamba Vengu, Alex Challamilah McRaegan na Lucas Mhuvile Joti.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wasanii hao walivamia mkutano huo ambapo Masanja ndiye aliyekuwa wa kwanza kupenya na kwenda kukaa kwenye safu ya mapaparazi hali iliyozua mshangao.
Baada ya mkutano kwisha Masanja alimzukia mmiliki huyo Hellen Sweya na kuomba nauli ili yeye na wenzake watimue kutoka kwenye mkutano huo.
Hata hivyo, mwanamama huyo alimjibu kuwa, hawezi kumpa nauli kwa vile hali ni mbaya na hakuwa amemwita kwenye mkutano huo.
Ndipo Masanja alipoamua kukomaa: Nimejiandikisha bwana, sijaalikwa kivipi, sasa mimi sina nauli, nipe niondoke zangu.
Akajibiwa: We Masanja usilete utani hapa. Kama ulialikwa hapa wewe ni wandishi wa chombo gani?
Hata hivyo, mchekeshaji huyo anayetumia nguvu kuchekesha, alizidi kukomaa kutaka apewe nauli ambapo safari hii alikwenda kuongea na bosi mwingine ambaye naye alimchukulia kama alikuwa akiigiza tu.
Wakati Masanja akikomaa kutaka apewe fea msanii mwenzake, Vengu alifika na kuongeza nguvu ya kudai masurufu hayo.
Mpaka mapaparazi wetu wanaondoka ukumbini hapo, haikujulikana kama wasanii hao walipewa nauli au la!
Mmefulia haooooooooooo!!!!!!!!!!!
Source: http://www.globalpublisherstz.com/2009/11/13/orijino_komedi_walilia_nauli.html