Zanzibar wapeleka barua UN kuvunja Muungano

kikubwa ni muungano kuvunjwa kipindi tukielekea mchakato wa kuunda EAST AFRICAN FEDELETION

Maswala ya shirikisho la EA hayana nguvu tena, baada ya EU kuanza kushindwa,Mjerumani anawaambia nchi za ulaya lazima zibadilike ziache uvivu, Ni ujeruman pekee iliyobaki na uchumi imara wengine wako hoi soon mtasikia mengi kwani nchi nyingi ni wavivu.Sembuse na EA ukiangalia Ni Rwanda pekee ndiyo inajenga uchumi wengine ni kupambana na wanasiasa.Uganda Museveni yuko bussy na Besigye, Tanzania wako bussy na CDM na urais 2015, Kenya wako bussy na akina uhuru kenyata na William Ruto na wanaangalia nani rais 2012.Acha wazanzibar wajitenge na wataanza kuwa bussy na yao mapya
 
ukivunjika kwa sisi tulioajiriwa tarehe 26 Aprlil tutakuwa hatupumziki tena maana hiyo ndiyo raha iliyobaki ya muungano
 
Hebu waambieni waache tamaa na upuuzi. Mnaowabeza wazanzibari kuwa wakijitenga watahamia bara mnajua kuwa ukanda wa pwani wa Tanzania na Kenya hadi Msumbiji ni eneo la zanzibar? Kenya wana mgogoro na wakenya waliopo ukanda wa pwana wanataka kujitenga na kurudi Zanzibar. Tanzania hakuna evidence kuwa eneo waliloazimwa wajerumani na sultani wamelinunua kihalali (10 Kilometer wide coastal strip from Tanga - Mozambique). Je wazanzibar wakiamua kudai eneo lao mtalitoa? Kuweni Great Thinker ni kuwaomba waache mpango wao kwani sasa hakuna mzanzibari tumechanganyika mno baina ya sisi watanganyika na wazanzibari .
 
Hakuna kitu ambacho sikipendi hapa JF kama kuona Wazanzibar wakitaka kujitenga! Maneno haya yamenichosha, nilishawahi kushauri wawatumie wabunge wa Muungano kupeleka hoja binafsi bungeni, bunge likiridhia bila shaka kutakuwa na kura ya maoni kwa Watanzania wote nao wakiridhia muungano huu ujunjike tufikirie mengine. kupeleka barua UN hakusaidii kwa vile UN hawakuhusihwa katika kuundwa kwa muungano huu, issue hii ni ya hapa hapa wala hakuna tatizo lolote, ni dhahiri Watanzania watafanya maamuzi magumu kwa maslahi yetu sote.

Tahadhari: Mwalimu alisema 'endapo Wazanzibar wataamua kuwaacha Watanganyika, Watanganyika watabaki salama lakini Wazanzibar hawatabaki salama, tutasikia Wapemba na Waunguja na baada ya hapo wataendelea kubaguana kwa vigezo vingine kwa vile dhambi waliyoifanya ni kubwa na mbaya mno'.
 
kwa sisi wabara tulioa wapemba itakuwaje??...................... Nitakuwa na mke foreigner

kwani ulianza wewe kuoa pemba??? Mbona kuna wapemba wengi walioa na kuolewa tanganyika kabla 26 april 1964 na haikuwa noma ??? Nyerere kawatia kizalazala cha muungano wake mnapata taabu sana .

Mbona nyerere mwenyewe amekufa na life goes on
 
Zanzibar hawataki Muungano.
Tanganyika hawataki Muungano.
Nani basi anaung'ang'ania?
 
hakuna kitu ambacho sikipendi hapa jf kama kuona wazanzibar wakitaka kujitenga! Maneno haya yamenichosha, nilishawahi kushauri wawatumie wabunge wa muungano kupeleka hoja binafsi bungeni, bunge likiridhia bila shaka kutakuwa na kura ya maoni kwa watanzania wote nao wakiridhia muungano huu ujunjike tufikirie mengine. Kupeleka barua un hakusaidii kwa vile un hawakuhusihwa katika kuundwa kwa muungano huu, issue hii ni ya hapa hapa wala hakuna tatizo lolote, ni dhahiri watanzania watafanya maamuzi magumu kwa maslahi yetu sote.



tahadhari: mwalimu alisema 'endapo wazanzibar wataamua kuwaacha watanganyika, watanganyika watabaki salama lakini wazanzibar hawatabaki salama, tutasikia wapemba na waunguja na baada ya hapo wataendelea kubaguana kwa vigezo vingine kwa vile dhambi waliyoifanya ni kubwa na mbaya mno'.


wewe mbona unampenda sana huyu nyerere kiumbe mfitinishaji aliyetutia umasikini wa kuendelea kwa siasa zake za kubahatisha ????
 
MBONA MNAKASIRIKA SANA UNAOVUNJIKA NI MUUNGANO WA SERIKALI NA SIO MUUNGANO WA WATU ????
MBONA WATANGANYIKA WAPO ZANZIBARI na wazanzibari wapo Tanganyika hata kabla KABLA MUUNGANO ????

Hakuna anayekasirika gavana nyie wazanzibar ndo mtaumia muungano ukivunjwa,waznz wanadanganywa na magaidi kwamba wakijitenga watapata misaada ni ulevi tu wa madaraka na mali hakuna lolote,nyie jitengeni tu tutawafukuza wote huku bara na mali na nyumba zote tunachukua
 
Me nadhani wapewe nchi yao kwani hakuna tunachofaidika nacho kutoka kwao.

Nchi yao wanayo hata sasa, hakuna aliyewanyang'anya kijisehemu kidogo hapa duniani na siku bahari ikipanda kizame sijui watakimbilia wapi, waache wajitenge waende zao kama mwanampotevu ambaye mwisho alirudi na kutaka aitwe mtumishi badala ya mtoto halali kwa baba yake. Sisi Watanganyika tutaanza kuwapokea wakimbizi wa Kizanzibar si zaidi ya miezi 6 tangu kujitenga kwao. Lakini kamwe hatutakubali kurudisha muungano ambao umetutesa tangu kuzaliwa kwetu. Itakuwa faraja kwangu binafsi kurejea katika nchi yangu Tanganyika iliyopotea katika ramani ya dunia huku Zanzibar ikiendelea kuwepo ikiwa na Rais na ikijiamulia mambo yake yenyewe.

Muungano huu ni utata mtupu, eti siku ya ajali ya MV Spice Islanders Rais wa Muungano alikuwa mgeni kama wageni wengine huku Rais wa Zanzibar akiwa ndiye mwenye msiba, sasa powers za Rais wa Muungano huko Zanzibar ziko wapi?

Let them go, go, go ... Zanzibaris! we have carried you a long distance we need to rest!
 
wewe mbona unampenda sana huyu nyerere kiumbe mfitinishaji aliyetutia umasikini wa kuendelea kwa siasa zake za kubahatisha ????
Kweli nendeni hata mkiungana na Muscat kwa babu zenu hakuna shida. Tuachie Nyerere wetu!! Hatuwahitaji stupid!!
 
hakuna anayekasirika gavana nyie wazanzibar ndo mtaumia muungano ukivunjwa,waznz wanadanganywa na magaidi kwamba wakijitenga watapata misaada ni ulevi tu wa madaraka na mali hakuna lolote,nyie jitengeni tu tutawafukuza wote huku bara na mali na nyumba zote tunachukua

hizo ndio propanganda mnazopewa kanisani??? Tizama akili yako ilivyojazwa raha za misaada. Hebu itizame tanganyika ukubwa wake baadaye iangalie zanzibari ukubwa wake , kuna nini hata tanganyika isiiwachie zanzibar.
Hivi kweli wewe ni wa kuandika maneno hayo hapo juu, ???

Umepata za baridi nini mchana huu ???
 
Taratiibu jamani,

Ambao hawataki muungano no nani haswaa? Wapemba au Waunguja?, swala hili sio rahisi kama wengi wanavyodhani. Yasije yakatokea kama yale ya visiwa vya Comoro na kisa cha Anjouani...
 
Kweli nendeni hata mkiungana na Muscat kwa babu zenu hakuna shida. Tuachie Nyerere wetu!! Hatuwahitaji stupid!!

Tizama ulivyoandika ??? Nyerere huyo umpendaye kaifisidi nchi , inaendelea kuangamia katika umasikini mpaka wakati huu yuko kaburini. Alianza kupokea misaada mwisho ameitia kilema nchi haiendi ila misaada na hapo ndio akina Cameron wanataka kutoa misaada kwa misingi ya ushoga , kazi kweli kuwafanya watoto wa Nyerere wakuelewe
 
Hebu waambieni waache tamaa na upuuzi. Mnaowabeza wazanzibari kuwa wakijitenga watahamia bara mnajua kuwa ukanda wa pwani wa Tanzania na Kenya hadi Msumbiji ni eneo la zanzibar? Kenya wana mgogoro na wakenya waliopo ukanda wa pwana wanataka kujitenga na kurudi Zanzibar. Tanzania hakuna evidence kuwa eneo waliloazimwa wajerumani na sultani wamelinunua kihalali (10 Kilometer wide coastal strip from Tanga - Mozambique). Je wazanzibar wakiamua kudai eneo lao mtalitoa? Kuweni Great Thinker ni kuwaomba waache mpango wao kwani sasa hakuna mzanzibari tumechanganyika mno baina ya sisi watanganyika na wazanzibari .

Umefilisika kifikra. Tanganyika ilipata uhuru 1961 na eneo lake linajulikana fika. Unajua Ikulu ilipo, na hata Mwingereza alipokabidhi Uhuru unafahamu fika, inashangaza unaleta stori za ajabu ajabu hapa. Kama Pwani ya Kenya, Tanganyika na Msumbiji ilikuwa chini ya Sultan iweje mwingereza akabidhi uhuru katika nchi isiyohusika. Kwa upande mwingine baada ya Zanzibar kupata uhuru 1964 kwa nini hawakuchukua Pwani ya Kenya, Tanganyika na Msumbiji? Wakati tunaungana nao eneo lao ni Pemba na Unguja na si vinginevyo. Mapinduzi yaliyofanyika yalikomboa visiwa vya Unguja na Pemba pekee, eneo la Kenya, Tanganyika na Msumbiji unalolidai lilikuwa huru wakati wa mapinduzi.
 
Taratiibu jamani,

Ambao hawataki muungano no nani haswaa? Wapemba au Waunguja?, swala hili sio rahisi kama wengi wanavyodhani. Yasije yakatokea kama yale ya visiwa vya Comoro na kisa cha Anjouani...

kwani yakitokea si yao wenyewe?????PILIPILI USIOILA YAKUWASHIA NINI??????
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom