Muungano tunaweza kuuongelea kwa hisia tofauti na tukasema yote tunayotaka kusema. Lakini sasa naona kuna haya maneno maneno ya kusema Zanzibar si nchi. Je hii dhana ni sahihi ? kutoka kipengele kipi cha katiba? Ama ni kwa hisia hisia zetu tu? Iwapo ni hisia tu, ni haki kweli kuvua utambulisho wa eneo kikejeli kejeli kweli. Na kama sio nchi, Zanzibar ni nini sasa? Mkoa? wilaya ama ni kitu gani?